Muhsin Snr
JF-Expert Member
- May 8, 2020
- 515
- 806
wananchi wa ngorongoro walishahamishiwa msomera huko Tanga kitambo sana na maisha yao ni mazuri kweli kweli...hakuna watu tena wanaoishi hifadhini ngorongoro....“Hatua ya kufuta vijiji na vitongoji ni hatua inayoenda mbali sana. Maana yake ni kwamba wananchi wahusika hawatakuwa na serikali zao za mitaa vijijini na vitongojini. Hii ni kinyume cha ibara ya 145 na 146 ya Katiba ambayo inazungumzia Madaraka ya Umma na kuweka Serikali za Mitaa. Kuwa na madaraka ngazi ya vijiji ni mosi, kuimarisha demokrasia ngazi za chini; pili kuwezesha wananchi waishio vijijini kushiriki katika utawala ambayo ni haki yao kwa mujibu wa ibara 21(1); na tatu, waishio katika eneo hilo kupata haki ya kuchagua na kuchaguliwa katika Halmashauri zao kama wananchi wenzao waishio katika maeneo mengine. Kwa kuwa vijiji vimefutwa wananchi hao watakosa haki hizo. Kwa maneno mengine wamekuwa disenfranchised (Kuporwa haki). Jamani tunaelekea wapi? Nini lengo la kufanya hivyo? Je tuelewe vipi? Tuambiwe waziwazi kama jamii ya Kimaasai waishio Ngorongoro ni wananchi au wakimbizi wa ndani? Prof. Shivji
Maneno ya Mhadhiri Mwandamizi Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Profesa wa Sheria Profesa Issa Shivji kupitia mtandao wake wa X.View attachment 3074956
Kuna haja ya kuwaondoa wachaga wote nao wapelekwe msomera ili eneo lao lote hilo tufuge kima na tumbili kwa ajili ya watalii wa kiarabu.Masai kasomeni Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999. Tatizo mnajazwa upepo na wanasiasa uchwara wasioishi Ngorongoro
Wamebakia thimba fisi na tembo sio?wananchi wa ngorongoro walishahamishiwa msomera huko Tanga kitambo sana na maisha yao ni mazuri kweli kweli...hakuna watu tena wanaoishi hifadhini ngorongoro....
wananchi wa msomera sasa sasahivi,
wanashiriki zoezi la kujiandikisha na uchaguzi wa serikali za mitaa na kujipanga na uchaguzi mkuu mwaka ujao....
nadhani Prof.Shuvji yuko nyuma kidogo kwenye uelewa na ufahamu wa hatua za kisheria zilizofikiwa kuhusu jambo hili muhumu sana. huko mbona tulishatoka kitambo sana ndrugu zangu?
na sasa tuko mbele sana kimaendeleo huko msomera. ukimbizi ni dhana tu labda ya prof. kutaka kuonyesha upande wake kwenye jambo hili, ambalo limekwisha kwa amani
yamebaki mazingira halisi yasiyo hatarini kuharibiwa zaidi tena na kupoteza uasili wakeWamebakia thimba fisi na tembo sio?
Tuendelee kudanganyana kama ni kwa manufaa ya nani sijui.yamebaki mazingira halisi yasiyo hatarini kuharibiwa zaidi tena na kupoteza uasili wake
Hayana akili hayoNi wakoloni wapya wa zama hizi.Wanaigawa nchi upya kimipaka kama mwaka 1886 kule Berlin/scramble for Ngorongoro.
Kwahiyo Sasa hivi nikitaka kuenda wilaya ya ngorongoro nisema nataka kuenda wapi Ili nieleweke naenda wapi?Serikali kupitia kifungu cha 30 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287 kinachotoa ruhusa kwa mamlaka za Serikali kufanya mgawanyo wa Halmshauri za Wilaya;
Imetoa AMRI rasmi iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali namba 673 la tarehe 02 Agosti, 2024; ili kufuta baadhi ya maeneo ya kiutawala kwenye mamlaka za Serikali za Mitaa hapa nchini kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa tarehe 27 Novemba, 2024.
Amri hii rasmi sasa inafuta Kata, Vijiji na Vitongoji katika Halmashauri za Wilaya zifuatazo; Ngorongoro, Bahi, Chemba, Kasulu, Kakonko, Hai na Rombo.
Katika Halmshauri ya Wilaya ya Ngorongoro pekee, kupitia AMRI hii, Serikali imezifuta Kata 11, Vijiji 25 na Vitongoji 96.
Garatwa,
Dar es Salaam, Tanzania.
20 Agosti, 2024.
View attachment 3074791
AondoleweJe ni halali mbunge wa Ngorongoro kuendelea kuwepo bungeni? Anamwakilisha nani? Wanyama na misitu!
Ndio unaenda DubaiAu niseme nataka kuenda vitalu vya Dubai?
Nenda wewe haujakatazwa.Msomera mbona pazuri tu
Mashati au Tarakea ??Rombo ni kama iko Kenya 😄
nchi iko salama wala usiwe na shaka ndugu..Nilisema humu na bado naendelea kusema. Hii kasi aliyokuja nayo, iko siku itafika. Kila unapokanyaga unaambiwa hili eneo huruhusiwi kufika, ni la nchi/mtu fulani ndani ya TZ. Tuendelee kuwachekea tu, tutakuja kushtuka too late.
Tangazo batili! Serikali itajuta kumuachia Mwabukusi kuwa Rais wa TLS!zingatia tangazo la serikali gentleman, makasiriko wala mihemko haisaidii