Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

Mwaka juzi nilifanya utalii wa ndani mbuga ya Saadani, ilikuwa shida kuwaona wanyama! Wanyama ni wachache sana.

Kingine kinachokwaza utalii ni tabia ya company za utalii kutumia local tour guide ili mradi anajua kuongea tu kiingereza kibovu na ujanja ujanja anaenda na mtalii.. akigingwa na swali kuhusu nature hajui, aina za miti na scintif name hajui, anajua kuelezea wanyama tu huku scientic name zake hajui. Kwa mtalii ana boreka.
 
Pamoja na gharama za viingilio, hizi zipo rasmi na mtalii huwa amejiandaa navyo... lakini pia kwa raia 'uchawa' ni mwingi na kero kubwa.

Tunawaombaomba sana, tukiona mzungu tu ni fursa... hata embe tu tutamuuzia 5000/- lengo ni kumpiga tu.

Wale vijana wa kupandisha watalii mlimani ni hatari tupu, mzungu ananyonyolewa kila kona na hana cha kufanya.
 

 
Hata kama sijui hapana aisee , kupanda mlima milioni 300 huu utakuwa ni uongo brother

unashangaa mil 300, the latest i know even hio ela ni ndogo saaahv!
mskilize aliepanda mlima mwenyewe, be sure that hio hela saaahv ni more than mil 300 atleast 400M for now or 500M
 

sawa sawa kabisa
 
Kama kawaida Mabongoman hawana ufahamu mwingi>>Mtalii siyo mtu tajiri kama mnavyofikiri. Watalii wengi wanafunzi na wafanyakazi wa kawaida sana ili wao wafike huku wamejidunduliza vidola kwa kusave hata miaka miwili sasa Mabongoman wakiwaona watalii wanawaona matajiri kweli wakizani jamaa wanamipesa ,huwa inatokea kama Abramovich, Will smith mara chache kuja kutalii

ubunifu,ubunifu ubunifu Mabongoman hata bonus hakuna
 
yes na lengo lisiwe kurudisha watalii waliokwishakuja.

bali kuongeza wengine zaidi.
Tunaweza pia kuwarudisha kwa kuwaonyesha bado kuna vivutio vingine hawajatembelea, au kuwapa motisha ya kuongeza muda wa kuwa nchini. Kila siku wanayoongeza wanafanya matumizi nchini. Unatakiwa uwape motisha ya kuendelea kufanya matumizi, aidha kwa kulipia huduma au kufanya manunuzi.
 
yah,maana ukiishaboresha kila kitu ni wao ndio watahitaji kubaki au kurudi kwa mara nyingine.
 
Mimi nafikiri tungetoa unafuu kwa vifaa hivi ili kusudi wajasiriamali wengi wajitokeze wanunue yale macamping equipment. Magari ili utalii wa ndani ukue

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwetu sio hivyo hao wageni ndio walikuepo kwenye hiyo biashara wanashinikiza mazingira magumu kwa wanaoanza ili wabaki wenyewe kwenye soko hawajui kuwa ubora na ufanisi wa kazi unakua kwa kiwango cha chini mno...
 
NGOJA KWANZA WATUMISHI WA WIZARA WAMALIZE KUKARIRI KURASA 260 ZA ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA HA MAPINDUZI KISHA TUTAANGALIA NAMNA YA KUTATUA TATIZO
 
"..Nikitoa my personal experience, nilitembelea Kisiwa cha Saa Nane, Mwanza, tukakutana na tour guide wa kike, wote tuliofika pale siku hiyo hatuwezi kutamani kurudi tena, mimi na wenzangu siku hiyo tulikuwa disappointed, siwezi kutamani hata kwa bunduki kutembelea tena hiyo hifadhi..."

Mkuu hujatufafanulia hapa kulikuwa na tatizo gani au ni huyu tour guide wa kike ndo alikuwa tatizo au alikuwa peke yake tu hifadhi nzima au ilikuwa vipi hasa??!!
 
Huduma mbovu zinazotegemea maelekezo kutoka juu ni chanzo kikubwa cha kupoteza watalii.
 
Nashauri tujifunze kwa nchi zinazofanya vizuri kama Dubai, Malaysia, Misiri, Hongkong n.k. hata ikiwezekana waje watufundishe kwa muda ili na sisi kufikia pale walipofikia.
Hivi kweli matatizo hamuyajui? Gharama kubwa, standards za chini, huduma mbovu, barabara mbovu, waongozaji lugha gongana; kiwango chetu kiko chini sana, ukilinganisha hata na Kenya tu hapa jirani! Wahusika wawe na elimu ya kutosha, wapeleke nje waone wenzao wanafanyaje; punguza uswahili uswahili! Simpo!
 
yes na lengo lisiwe kurudisha watalii waliokwishakuja.

bali kuongeza wengine zaidi.
Wewe unaonekana bado una elimu ndogo juu ya biashara. Nakufunza jambo, nalo ni, katika biashara yoyote unafanya, wekeza akili yako, ufahamu wako, jitihada zako, na mbinu nyingi kwa mteja ambaye umeshamuhudumia sababu huyu atakupa mrejesho wa biashara yako na wapi unapowaya. Ila ukianza tabia ya kuwapuuza wateja wa awali sababu unatarajia wapya, hapo ndipo unaharibu biashara na kufeli mapema.
 
utalii sio duka la mchele mangi.

leo hii tuna mpango wa kuweka cable za kupandia kilimanjaro,unadhani target ni wale ambao wameshakuja tayari kwamba warudi!!!!sio hivyo.ndio maana tunatangaza pia utalii na mandege yananunuliwa,haina haja ya yote haya kama mtu aliishafika bongo na anapajua.

mtalii kurudi,inaweza changiwa na huduma na maandalizi ya mwenyeji,lakini bado kurudi kwake liko mikononi mwake zaidi yako wewe.
 
ili kuvutia watalii wa kigeni zaidi, nadhani tozo za kuingia hifadhi ingepunguzwa ili wengi wao waweze kumudu na kuongeza mapato ya nchi.
The lower the price at good service level, the higher the number of customers joining the service.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…