Serikali yasalimu amri mgomo wa wafanyabiashara Kariakoo, yakubali kusitisha kamatakamata ya TRA na kuleta mfumo mpya wa kodi

Serikali yasalimu amri mgomo wa wafanyabiashara Kariakoo, yakubali kusitisha kamatakamata ya TRA na kuleta mfumo mpya wa kodi

Hiyo damu ilimwagika wapi? Nani alimwagwa damu? Nani alinyang'anywa fedha zake? Unaweza kunitajia hao watu na walinyang'anywa kiasi gani?
Aliwaua watu zaidi ya 300 huko MKIRU, kuna wale wa kwenye viroba waliokuwa wakitupwa baharini. Aliua Ben Saanane, Azory Gwanda, Kanguye na alimshambulia kwa risasi Lissu kupitia kundi la wasiojulikana.

Aliwateka akina Mohamed Dewji, Roma Mkatoliki na Zakaria Trans. Ila Zakaria akakiwasha akawajeruhi watu wasiojulikana
 
Wajinga kama hao uliotaja huwa hawachelewi kupigwa pini na wajeda wenyewe. Unakumbuka ile kauli ya kihuni kuwa watafanya usafi wa kudumu kuzuia maandamano, kwamba wamekosa kazi za maana za kufanya?!!

Kwenye utawala enzi za sasa, ukitumia ubabe na udikteta hutoboi
Wengi wanatumia na wanatoboa,kuliko fedheha ya serikali kudhalilishwa.
 
Ukisikiliza malamimiko ya kodi sehemu kubwa ni kutoka kwa wafanyabiashara wadogo ambao hawana access za accountants au wataalamu wa kodi.

Shida sio waziri (labda mitizo yake kwa wananchi), Iła kwenye biashara 90% ya malalamiko ni uelewa mdogo wa maswala ya tax administration.
Hakuna swala la uelewa kuna faida gani kubwa inayoonekana wazi wazi ni matokeo ya kulipa kodi.
 
Ilikuwa zamani enzi za giza, siyo sasa.
Kukaa kwenye meza ya mazungumzo na kufikia muafaka ndiyo uongozi.

Ubabe na udikteta wa kulazimisha mambo yasiyowezekana hauna tija na ndo hupelekea nchi kuwa "a failed state"
Shukiruni ni mwaka wa Uchaguzi,huko Kenya wameuwa 3 ndio wanaojifanya kuwasikiliza.

Na nyie mlitakiwa mfinywe kwanza ndio msikilizwe.

Viva Chalamila.
 
Labda nikukumbushe tu kuwa tax system lazima iendane na jamii.Income tax yetu ni copy and paste ya India,Uk na ilikuwepo toka ukoloni hivyo inakubali kwenye jamij ambavyo mifumo ya Kodi Iko well organized.Africa mkulima au mtu anadeal agricultural sometimes anapata hela nyingi na faida kubwa kuliko mchuuzi wa nguo lakini mkulima hayuko rasmi na Wala hasumbuliwi.Tunahitaji kulea biashara huku tukitengeneza mifumo ya watu kujulikana income bila kutumia nguvu.
Tax rates anapanga waziri kila mwaka kupitia ‘finance act’ hiyo ndio inaamua rates za income tax, VAT na import duties; pamoja na misamaa au nafuu za biashara serikali inazitoa.

Sasa humo waziri na team yake ya mipango wao ndio wanajua wanalenga nini kwenye fiscal policies zao, targets za uchumi, social policies, kuondoa inequality kwenye jamii, public goods and so on kilicho important kama kipaumbele chao huko serikalini na kwenye chama chao.

Maana yake ni you can’t ‘copy and paste’ finance act ya nchi nyingine (ambayo inapanga kodi) kkwa vipaumbele vya nchi tofauti havifanani wala mtazamo wa kugawana keki ya taifa aufanani.

However Income Tax act na VAT acts (hizi zinaweza fanana na nchi nyingi, ni sheria lakini zipo sana kufuata accounting standards za dunia) na uwa azibadiliki sana ni kwa ajiri ya administration purposes za kodi, kikubwa zinaelezea taratibu za kukusanya kodi information ambazo TRA na person (hilo ndio jina la kikodi kwa biashara ndogo), biashara kikodi ni (usajili wa public or private listed companies).

Shida ya wafanyabiashara wengi hawajasoma hizo sheria za (VAT and Income tax acts) hapo ndipo wanaposhindwa kuelewa hatua za TRA na kudhani wanaonewa.

Moreover kila ‘finance act’ mpya inapoanza kazi, TRA kupitia site yao (ambayo design view yake ni mbaya with so much clustered information inahitaji maboresho) uwa wanaweka necessary info kwenye website yao. Kule unapata info kama za import duties ya bidhaa mbali mbali, VAT zote fully, reduced rates and zero rated products, kuna maelezo ya kupiga hesabu mbali mbali za kodi.

Wakija sasa kama ni hesabu za kodi unatakiwa kujua finance act inasemaje kuhusu hiyo bidhaa VAT rate gani, import duty ni kiasi gani etc. Same kama ni income tax unatakiwa kujua how they calculate turnover ya chini tsh 100 na what changes ukizidisha.

Routine zingine za kuandaa vitabu vya biashara na jinsi TRA watakavyodai (fanya kazi ya kukusanya kodi) soma sasa ‘VAT na Income tax’ acts. Wafanyabiashara wa Tanzania they don’t read those acts wakitoka hapo wanalaumu TRA kwa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria.
 
Kwa Mtazamo wangu

TATIZO LA KARIAKOO NI ZAIDI YA WAFANYABIASHARA,WACHUUZI..LETS BE SERIOUS.

Tatizo la kariakoo haliwezi Kwisha ikiwa total supply chain ya mizigo inayouzwa kariakoo isiporekebishwa au kudhibitiwa kupitia maamuzi magumu na kutooneana haya wala aibu..

Bidhaa nyingi zinazouzwa kkoo zinaingizwa (Imported) toka China,India,Uturuki,Thailand,Vietnam,Zambia,Uganda,etc..Mfumo wa uingizaji na ulipiaji kodi wa mizigo husika ndio mzizi wa shida na tatizo lililopo na litakalokuwepo..

Cartel inayoratibu Logistics na supply chain ya mizigo ya wafanyabiashara wa karikoo isipodhibitiwa kila nyakati tutaona fukuto na migomo isiyohitaji siasa Bali utashi wa maamuzi magumu kudhibiti wahujumu uchumi tunaowalinda..

Mathalani,Mfanyabiashara akiagiza mzigo wa viatu Kwa kontena na kulipa ushuru stahiki kisha kuwa na nyaraka zote Za kikodi (Import duties,Port charges,Wharfage,VAT) inamgharimu milioni 45….NOTE:- Ila akiagiza mzigo huo huo kwa kutumia Logistics Cartels inamgharimu Milioni 15 tu pasipo nyaraka zozote lakini Ana uhakika wa kufikishiwa mzigo dukani au warehouse kwake pasipo usumbufu..

Sasa wale wafanyabiashara waliokuwa wakikomaa na kufuata taratibu stahiki wamejikuta wakishindwa kushindana ktk soko na kufirisika ama kufa kibiashara sababu ya ughali wa bidhaa dhidi ya wale wanaotumia Logistics Mafia..

On the other hand wanaotumia huduma za logistics cartel au mafia inawawia Vigumu sana kufanya compliance za kikodi sababu ya kukosa nyaraka muhimu kussuport mapana ya stock zao..Mauzo yao,returns zao..Hapa ndio kwenye shidaa haswaa…Wengi wana stock kubwa kuliko vielelezo vya manunuzi ya stock husika..Wamegeuka wachuuzi..Wanaouza ambacho hawana nyaraka Za wametoa wapi..SHIDA.

Logistics Cartel/Supply chain Mafia:-Ni kundi hatari lenye nguvu kupitia wanasiasa wakubwa waliopo na wastaafu..Wana ukwasi mkubwa na umaarufu mkubwa ktk Kiwango cha kuogopeka na Wakubwa wa TRA,Polisi,Etc..Wana nguvu mnooo ya kufanya wakubwa ktk mamlaka Za kodi watumbuliwe,Wafanyakazi wahamishwe,Wawe demoted..Wapate Stroke..Nina hakika hata CG wa TRA anawaogopa..Hana la kuwafanya..Inasemekana baadhi ya viongozi ni marafiki wakubwa..

Cartels hizi zimehodhi Supply chain Za uagizaji bidhaa,usafirishaji,Ulipaji kodi,Udanganyifu (under declaration&Falsa Declarations),Uzungushaji mizigo (Taarifa Za kampuni Za tracking devices Za mizigo ya transit zina mengi)..Wanamiriki makampuni ya uagizaji,Usafirishaji,Bonded Warehouses,ICD’s,CFS..yaani acha tu..Nani wa kuwagusa?!

Kwa hakika tunapoteza kodi nyingi sana zinazoingia mifukoni mwa wachache tunaowaimbia mapambio ya utajiri na ubilionea huku wachache wakikamuliwa hata kuzirai kibiashara..Bila maamuzi magumu na dhabiti tutaendelea kukwama na kuumiza wasiostahili..

Tukiamua Tunaweza..Viongozi wenye dhamana Simameni kwenye haki na ukweli..
 
Hiyo ndio Taarifa ya sasa baada ya mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo unaoendelea

=======


Waziri wa Viwanda na Biashara, Kitila Mkumbo amesema wamekutana na wafanyabiashara wa Kariakoo na kutoka sehemu nyingine Tanzania wakiongozwa na mwenyekiti wa wafanyabiashara Kariakoo, Majid Mbwana baada ya mapema kutokea Mgomo wa Wafanyabiashara ambapo Biashara zilifungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024. Pamoja na Chalamila kuwasili Kariakoo katika jitihada za kutatua mgogoro huo jitihada zake ziligonga mwamba Baada ya Chalamila kuondoka Kariakoo, bado Wafanyabishara waliendeleza mgomo wa kufunga maduka.

Waziri Kitila amesema changamoto zilizofanya wafanyabiashara kutaka kufunga biashara zao zipo katika maeneo matano ambayo ni:-
  1. Changamoto ya ukosefu wa nyaraka hususan bandarini inayosababisha makadirio ya kodi yasiyo sahihi.
  2. Changamoto ya ukokotoaji ya kiwango cha kodi ambacho wanalipa.
  3. Suala la uwepo wa machinga katika maduka ambayo wanauza
  4. Suala la kamatakamata ambalo limekuwa likiendeshwa na mamlaka ya mapato(TRA)
  5. Changamoto kwenye sheria ya muswada wa fedha(Finance Bill)
Baada ya majadiliano ya kina Serikali imekubaliana mambo yafuatayo
  1. Kuanzia Julai 1, 2024 mamlaka ya mapato Tanzania itakuwa na mfumo mpya wa nyaraka ambao utatumika vizuri zaidi katika kuhakikisha wafanyabiashara wanapata makadirio ambayo ni sahihi.
  2. Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) inasitisha operesheni zake maarufu kama kamatakamata mpaka itakapokamilisha utaratibu huu ili kuweka mfumo mzuri zaidi wa kukusanya mapato.
  3. Suala la ukokotoaji wa kodi ni suala la kisheria, Serikali imelichukua na inaendelea kuliangalia ili kuboresha zaidi mfumo wa ukokotoaji wa kodi hususani bandarini.
  4. Kuendelea kuwapanga wamachinga kama ambavyo Rais aliagiza ili wakae katika maendeo sahihi ambayo hayaingilii biashara za watu wenye maduka ili kila mtu aweze kufaidika, wamachinga na wenye maduka katika eneo la Kariakoo.
  5. Serikali imewataarifu wafanyabiashara kuwa muswada wa sheria ya fedha(Finance Bill) ya mwaka 2024 bado haujapitishwa na sasa uko katika majadiliano bungeni na kamati ya bunge la bajeti imeita wananchi wote waweze kutoa maoni ikiwemo wafanyabiashara hivyo imewaalika yale maoni ambayo wanayo wayapeleke kwenye kamati ya Bunge na wabunge watazingatia maoni yao kabla sheria haijapitishwa.

Pia, Soma=> Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024

Sijasikia issue ya wafanyabiashara wa kichina ambayo wafanyabiashara wa kitanzania walilalamika,inaongelewa😱
 
Hiyo ndio Taarifa ya sasa baada ya mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo unaoendelea

=======


Waziri wa Viwanda na Biashara, Kitila Mkumbo amesema wamekutana na wafanyabiashara wa Kariakoo na kutoka sehemu nyingine Tanzania wakiongozwa na mwenyekiti wa wafanyabiashara Kariakoo, Majid Mbwana baada ya mapema kutokea Mgomo wa Wafanyabiashara ambapo Biashara zilifungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024. Pamoja na Chalamila kuwasili Kariakoo katika jitihada za kutatua mgogoro huo jitihada zake ziligonga mwamba Baada ya Chalamila kuondoka Kariakoo, bado Wafanyabishara waliendeleza mgomo wa kufunga maduka.

Waziri Kitila amesema changamoto zilizofanya wafanyabiashara kutaka kufunga biashara zao zipo katika maeneo matano ambayo ni:-
  1. Changamoto ya ukosefu wa nyaraka hususan bandarini inayosababisha makadirio ya kodi yasiyo sahihi.
  2. Changamoto ya ukokotoaji ya kiwango cha kodi ambacho wanalipa.
  3. Suala la uwepo wa machinga katika maduka ambayo wanauza
  4. Suala la kamatakamata ambalo limekuwa likiendeshwa na mamlaka ya mapato(TRA)
  5. Changamoto kwenye sheria ya muswada wa fedha(Finance Bill)
Baada ya majadiliano ya kina Serikali imekubaliana mambo yafuatayo
  1. Kuanzia Julai 1, 2024 mamlaka ya mapato Tanzania itakuwa na mfumo mpya wa nyaraka ambao utatumika vizuri zaidi katika kuhakikisha wafanyabiashara wanapata makadirio ambayo ni sahihi.
  2. Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) inasitisha operesheni zake maarufu kama kamatakamata mpaka itakapokamilisha utaratibu huu ili kuweka mfumo mzuri zaidi wa kukusanya mapato.
  3. Suala la ukokotoaji wa kodi ni suala la kisheria, Serikali imelichukua na inaendelea kuliangalia ili kuboresha zaidi mfumo wa ukokotoaji wa kodi hususani bandarini.
  4. Kuendelea kuwapanga wamachinga kama ambavyo Rais aliagiza ili wakae katika maendeo sahihi ambayo hayaingilii biashara za watu wenye maduka ili kila mtu aweze kufaidika, wamachinga na wenye maduka katika eneo la Kariakoo.
  5. Serikali imewataarifu wafanyabiashara kuwa muswada wa sheria ya fedha(Finance Bill) ya mwaka 2024 bado haujapitishwa na sasa uko katika majadiliano bungeni na kamati ya bunge la bajeti imeita wananchi wote waweze kutoa maoni ikiwemo wafanyabiashara hivyo imewaalika yale maoni ambayo wanayo wayapeleke kwenye kamati ya Bunge na wabunge watazingatia maoni yao kabla sheria haijapitishwa.

Pia, Soma=> Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024
Sijasikia issue ya wafanyabiashara wa kichina ambayo wafanyabiashara wa kitanzania walilalamika, inaongelewa
 
Wafanyabiashara have not gained much. Walichofanya ni ku delay makali . Serikali wa ache unafiki. Wanategemea TRA wataweza ku meet targets zao za tax collection kama the government does support them. I believe wako watu wanaweza ku replace hao wafanyabiashara.
 
Back
Top Bottom