Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Status
Not open for further replies.
Kumbuka jpm alisisitiza kujenga bandari hiyo ya bagamoyo wakati wa kampeni. Nakumbuka lowassa ndiye aliyekua mbele kupinga na kusema atasitisha ujenzi huo. Leo kimewakuta nn wanasitisha wakati ilikua ni moja ya ahadi yao kwa wananchi wa bagamoyo?
 
Hivi Tanzania inajenga huo mradi au ni wahisani? serikali iendelee na plan zake za kujega sijui ku upgrade bandari za tanga na mtwara, sio busara kufuta bandari ya bagamoyo, ni bora waseme ihamishiwe tanga au mtwara, sio kufuta kwa sababu ya vimapato walivyokusaya siku tatu nne ktk bandari ya dar. Mji mmoja wa Shenzhen una zaidi ya port mbili, namely Shekou, Yantian. Chiwan. Mawan. Tung Tau Kok, leo Dar kuwa na port mbili sio ubaya. Kama ni kugawanya basi ipelekwe huko kwingine na wala sio kufuta mradi.
 
Hii Bandari sikuona mantiki yake ukitegemea tuna tatu tayari Dsm Mtwara na Tanga ambazo hizi mbili zikiimarishwa tukaweka sawa miundombinu ya reli na barabara tutatosheka nazo sana kuliko kuingia madeni ya miaka zaidi ya hamsini bila sababu za msingi kwa porojo za kisiasa tu.
viva JPM
Kwa nini ujenge bandari mpya Bagamoyo, kilometa chache toka bandari ya Dar es Salaam, badala ya kuboresha bandari tatu tulizonazo za Tanga (Kask.), Dar (Kati), na Mtwara (Kus.)? Maamuzi ya kijinga-jinga kama hayo ndiyo yamezidi kutufanya maskini.
 
Hivi Tanzania inajenga huo mradi au ni wahisani? serikali iendelee na plan zake za kujega sijui ku upgrade bandari za tanga na mtwara, sio busara kufuta bandari ya bagamoyo, ni bora waseme ihamishiwe tanga au mtwara, sio kufuta kwa sababu ya vimapato walivyokusaya siku tatu nne ktk bandari ya dar. Mji mmoja wa Shenzhen una zaidi ya port mbili, namely Shekou, Yantian. Chiwan. Mawan. Tung Tau Kok, leo Dar kuwa na port mbili sio ubaya. Kama ni kugawanya basi ipelekwe huko kwingine na wala sio kufuta mradi.
Ndiyo maana wamesema inatakiwa kwanza zilizopo ziboreshwe. Ni sawa kujenga bandari mbili jirani kabisa, lakini kwa hali ya sasa zile za Mtwara na Tanga ziko dhaifu zinahitaji kuongezewa nguvu. Kujenga bandari kubwa Bagamoyo ni sawa na mtu mwenye shilingi elfu 20 kuamua kununua kilo mbili za nyama kwa pesa yote akasahau kuwa atahitaji ugali au mchele pia.
 
Its
Mkuu mimi nashangaa watu wanashingilia mradi kusitishwa. Eti tukarabati Dar na Mtwara.

Wameshindwa kabisa kuona umuhimu wa bandari kubwa na ya kisasa.
it's not true kwamba watu hawajaona umuhimu wa bandari kubwa na ya kisasa. .priority kwanza ni kujenga bandari Tanga kubwa na ya kisasa na kui link na reli mpaka musoma au mpaka reli ya kati kupitia arusha mpaka singida. .sioni umuhimu wowote wa kujenga bandari kabla haujajenga reli ya kisasa (standard gauge ) kuhudumia iyo bandari. .priority iwe reli kwanza..reli ya kisasa na yenye ubora wa kimataifa.
 
mkuu mambo yetu mengi yamejaa usiri unafiki na kutoaminiana,sasa waweza kuta kulikuwa na maslahi binafsi kwa baadhi ya watu na ndio maana unaona jambo muhimu kama hili linasumbua watu vichwa.vinginevyo sisi ni wakupuuza ila najua lazima kuna tatizo tena kubwa kuliko tunavyojua au kuhisi.
Nafikili kuna bandari ya Tanga eneo kubwa tu,mtwara vilevile haina haja kwa sasa kujenga bandari mpya.
 
Wabunge wa upinzani walilipinga sana suala bungeni lakini ilishindikana kutokana na kuwa na wabunge wengi wa ndiooooo! tuangalie kwenye hili bunge linalokuja kama bado tutakuwa na wabunge wengi wa Ndiooooo!
 
Last edited by a moderator:
Ngoja niwaite rafiki zangu Nguruvi3 Pasco JokaKuu Kichuguu naomba maoni yenu.
Wataalamu wanasema kupanga ni kuchagua!, kupanua bandari zilizopo ni nafuu zaidi kuliko kujenga mpya as long as huo upanuzi utahusisha kuongeza kina cha maji ili ile mimeli mikubwa ya 3G na 4G iweze ku dock!. Lengo ni kutoa kipaumbale cha kuhudumia kilichopo mkononi Darisalama na kile cha gesi ya Mtwara!. Kwa vile lengo la bandari ya Bagamoyo ni kujenga kipya ambacho hakipo na kuhudumia ukanda wa viwanda vya EPZA ya Bagamoyo ambavyo navyo bado havipo, then, moja shika sii kumi nenda rudi!.

Kama ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ulikuwa na motive behind ya muwamba ngoma, then kuusimamisha ni halali kabisa!, lakini kama unasimamishwa kwa hoja ya kwa nini Bagamoyo!, basi mtashangazwa sana na ujenzi wa ICD mpya ya Chato!.

Pasco
 
Nafikili kuna bandari ya Tanga eneo kubwa tu,mtwara vilevile haina haja kwa sasa kujenga bandari mpya.
kwa tanga naunga mkono kwani si mbali sana na bagamoyo ila mtwara si nzuri sana.la msingi ni tuipende nchi na tuache unafiki.tukiweza hilo tutaweza kila kitu.
 
Tunatakiwa kujenga bandari ya kisasa sio kuboresha wala kukarabati, tunatakiwa tuweke misingi ya maendeleo na plan za muda mrefu zaidi ya miaka 100, siio kila ya baada ya miaka 10 tunakarabati , tuamue moja, sio kuachana na bandari ya bagamoyo eti tunakwenda kukarabati mtwara na tanga, kwa hiyo magufuli aseme bandari ya bagamoyo kuhamishiwa tanga au mtwara na ujenzi wake kuanza ifikapo june. Tunakarabati nini, mabanda ya dar, mtwara na tanga na kuziita bandari?, tunakataa bagamoyo port , bandari ya kisasa tunakibmilia kukarabati?
 
Mkuu hoja ni utata wa mkataba?
Nayo inachangia kwa asilimia kubwa.
Tungelikuwa na uwazi wa kuijadili mikataba (sio hapa JF, japo Bungeni) basi nakuhakikishia mikataba tata isingelifika hata 5% ambacho ki kiwango kinachokubalika kimahesabu. Hebu angalia sasa hivi, hao internal auditors wanaibua madudu kwenye kila mkataba na hapo ukiweka external auditors ndio itakuwa balaa. Mfano ZZK alivyopiga kelele kwenye ujenzi wa bomba la gesi na hata kuweka wazi kuwa kuna nchi zaidi ya mbili zimejenga bomba lenye kipenyo hicho hicho, ulefu huo huo na tena kwenye ardhi isiyo salama na miamba kwa ghrama ya US $600m lakini sisi limetugharimu US $1.3b. Akitokea mtu kuvunja mkataba kama huu utamlaumu, au kwa vile huu ulijengwa haraka na kwa lazima ili wenyewe wachukue chao mapema!?
 
@FiazaFoxy Kimweri mlikuwa mnatoa povu sana kuitetea hii Bandari...

Sasa naona mmeshasomeshwa namba...
 
Swala la Bandari ya
Tunatakiwa kujenga bandari ya kisasa sio kuboresha wala kukarabati, tunatakiwa tuweke misingi ya maendeleo na plan za muda mrefu zaidi ya miaka 100, siio kila ya baada ya miaka 10 tunakarabati , tuamue moja, sio kuachana na bandari ya bagamoyo eti tunakwenda kukarabati mtwara na tanga, kwa hiyo magufuli aseme bandari ya bagamoyo kuhamishiwa tanga au mtwara na ujenzi wake kuanza ifikapo june. Tunakarabati nini, mabanda ya dar, mtwara na tanga na kuziita bandari?, tunakataa bagamoyo port , bandari ya kisasa tunakibmilia kukarabati?
Tanga mpaka wana Nchi walisha lipwa mwaka 2013 ktkt wahame kupisha upanuzi wa Bandari Tanga,ambayo itakua Bandari kubwa na yakisasa kabisa. Hii Bandari ya Bagamoyo kuna ubinafsi humo ndani take it from me,mwambani Tanga ni eneo pana sana linatosha kabisa kua na Bandari ya ukweli kabisa.
 
The Construction of the 10 billion (about Sh22 trillion) Bagamoyo Port has been suspended, The Citizen has learnt. The government wants to focus instead, on improving the capacity, performance and efficiency of the Mtwara and Dar es Salaam ports.

The Minister for Works, Transport and Communications, Prof. Makame Mbarawa, confirmed yesterday that the construction of what would be the largest port in Africa has been suspended, not shelved to pave way for upgrading berths 13 and 14 as well as developing the Mtwara Port depending on the availability of Funds. The activities would take years to complete, the minister said because the process has to start from finding funding

Source: THE CITIZEN
View attachment 315504
Viva sana Magufuli...kujenga bandari mpya kwa pesa mingi kiasi hicho wakati hz tulizonazo tumeshindwa kuziutilize n jambo la kipuuzi kabisa..naona kuna halufu ya ufisad hpo hyo mikataba ichunguzwe...sasa Magu ahamie kwe gesi ile mikataba ilipitishwa kwa speed y radi pale mjengoni.
 
Huu ni mradi wa kihistoria na kimkakati kati ya China na Tanzania japo mkataba wake ni siri, ulitarajiwa kubadilisha uso wa Bagamoyo. Ni mradi mkubwa.
Serikali ya JPM imetangaza kusitisha kwa maradi huo kwa kile kinachoelezwa kuwa "uongezwaji wa kina cha bandari ya Dar" na "upanuzi wa bandari ya mtwara.
Kwa kuzingatia mazingira ya makubaliano ya ujenzi wa bandari hii kati ya China na Tanzania na utaratibu wa zabuni ya ujenzi kwa kampuni fulani maarufu, napata shida kuelewa kama usitishwaji huu ni wa kimkakati au ni muendelezo wa utumbuaji wa majipu.
TUJADILIANE.
 
Nionavyo mimi...hoja nyingi ni one way trafic....! Hebu tutumie two way trafic tuone inakuwaje hasa!


hapo umenena.....nadhani wengi tunachangia kwa hisia....lakini pia ni moja ya maana ya mjadala.....lets analyse......kuna aliyesema upembuzi ulibainisha kuwa hitaji la bandari kubwa na ya kisasa kwa karne hii isingiwezekana kwa kurekebisha tu zilizopo, je ni kweli au zilikuwa fact za kupikwa? kama ni kweli nini strenght za Bagamoyo kulinganisha na sehemu nyingine inapobidi kujenga bandari mpya ya kisasa?......nini mahitaji ya ujenzi huo kijografia (wapi katika bandari hizi ni rahisi kufanya upanuzi au kufikika kimiundo mbinu ),kimkakati wa kibishara? na je gharama za kupanua/kuboresha zilizopo ni za chini kulinganisha na ujenzi wa mpya?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom