Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Status
Not open for further replies.
Nilishangaa sana niliposikia inajengwa bandari nyingine Huko Msoga nikasema hivi viongozi wetu wanafikiria kweli vizuri, kwanza ukiangalia Bagamoyo na Dar ni pua na mdomo, pili Ukiangalia foleni za dar halafu ijengwe tena bandari nyingine ambayo inategemea barabara zile zile, binafsi niliwaza na kushauri kwa nn wasiboreshe bandari ya dar, tanga na mtwara coz ya mtwara ingeboreshwa kwa ajiri ya kuhudumia nchi za kusini mwa Afrika, halafu hii ya dar ibaki inahudumia nchi kama za Congo, Rwanda na Burundi.
 
Bandari ya Dar ina changamoto chungu nzima ni nifinyu sana, itatugharimu an arm and leg tukitaka kuipanua, kwa nini hatuendi kupanua Bandari ambazo zina a kina kirefu
Well said mkuu, mimi sidhani Serikali ina mpango wa kusitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, kama kuna mpango wa kujaribu kuweka spana kwenye Project hii nzuri basi Dunia itatushangaa, I hope hakuna external forces ambazo zina excert pressure kwa viongozi wetu ili wasitishe mpango huu mzima.

Wakati mwingine magazeti ya Citizen na Mwananchi yana kawaida ya exaggerate nambo madogo - wanakuza out of proportion 4 some reasons ambazo wanazijua wao, haingii akilini kwamba Serikali inaweza ku abandon Project kubwa ya ujenzi wa bandari ya kisasa na yenye manafaa makubwa kwa Taifa letu kwa kuendekeza ushauri ambao hauitakii mema Taifa letu - tukifanya mchezo washindani wetu watatuzidi kete,tutabaki tunajilahumu kwa ujinga wetu - si China wala Oman wataendelea ku entertain ujinga wetu, watakwenda kuwekeza kwingine.

Yap mkuu umejaribu kutokuwa mshabiki kama wengine humu,, hili suala watu wanarijadili kiushabiki sana mkuu..
tumeshaambiwa inaweza kuwa one of the big port in Africa, bila shaka mapato yake yangeweza kabisa kuzijenga Tanga na Mtwara kwa takribani kipindi cha miaka 20... Hii sio project yakuacha iende hivi hivi labda kama tuna solution inayofanana na hii project. Dar sio mji tena wakuutegemea kwa project yoyote kubwa baadala yake lazima tuwe na backup plan ya karibu na mji wa dar, bagamoyo port ingeamsha mji wa pwani, moro na tanga na kuunganisha dar,pwani,moro na tanga kimaendeleo, maana naona pia bandari ya tanga kutumika kama backup plan ya bandari ya bagamoyo kukiwa na congestation ya meli maana dar haitaweza tena, mtwara port itajijenga yenyewe maana tayari njia imeshaanza kufunguka kwenye oil na gas, lazima mapato yatapafikana tu maana hata makampuni ya mafuta na gas hayawezi kukubali kuteseka yatatujengea tu hii mtwara port kwa makubaliano fulani..
 
Wacha jipu litumbuliwe,huyu jamaa na mikataba yake feki ya kichina inabidi akalale lupango ili kurudisha heshima ya hii nchi
 
This is beyond my comprehension yaani bandari ambayo kwa sasa inatumiwa na mataifa jirani Congo, Rwanda, Burundi na mataifa mengine ya chini mwa Tanzania iwe katikati ya jiji.

Kwa sasa tu magari inabidi ya pakie usiku ambapo ni time consuming kwa wateja wengine kulaza magari ambayo yangekuwa yanawatengezea hela, port ya Bagamoyo si ndio ideal ipo nje ya mji kidogo na eneo linaweza wekewa mazingira tu suit entry and exit ya kumudu foleni za baadae ata mji ukikuwa na tena kuna investor ambaye yuko tayari, ajira ambazo zingepatikana kwa wadau maana dar is congested surely bagamoyo ingekuwa sababu ya kulitanua jij la Dar ambalo kwa sasa lipokea malaki ya economic migrants kila mwaka.

Kuna vitu vingine maamuzi anayaelewa anaenua mwenyewe lakini sio duniani nzima hili ni moja wapo ina maana awaoni location wise tu bandari ya Dar sio sawa kwa volume inazobeba sehemu na sio sahihi kwa jiji leo.
Ngoja niwaite rafiki zangu Nguruvi3 Pasco JokaKuu Kichuguu naomba maoni yenu.
Eric, kwa hili kuna mengi sana ya kujifunza.

Moja, kama Taifa hatuna dira. Mtu mmoja anaweza kuamka na dira yake na ikawa ya Taifa. Dira ya JK imefeli tunasubiri ingine ifeli kwasababu zote zinaongozwa na dira ile ile iliyoshindwa miaka mingi

Pili. inaeleza tusivyoweza kusimama na kupanga mipango yetu kwa kutumia wataalam na utaalam bali wanasiasa

Tatu, inatukumbusha hakuna kilichobadilika, CCM ni ile ile. Hawa akina Magufuli, Mbarawa n.k. walikuwemo katika cabinet.
Hakuna hata mmoja aliyeoonyesha kutoridhishwa na madudu. Leo awanatuaminisha wana maono zaidi. T

Nne, tuliandika sana hapa JF na kuishauri serikali kuimarisha bandari zilizopo kwanza. Tulisema ile ya Tanga ina infrastructure nzuri kwanini haiiimarishwi sambamba na ya Mtwara?

Kwanini hatuimarishi ya Dar ikafanya kazi at capacity? Tulichoona miaka 10 uongozi uliachia watu wagawana magati.
Uongozi uliwaacha wahuni waliosaidia kampeni kuendesha bandari. Wao walikuwa angani

Tano, uamuzi wa kujenga bandari ya Bagamoyo ilikuwa knee jerk reaction baada ya CoW kujenga ya Malindi.
Tofauti na Kenya wenye dira, sisi tulikuwa na wapiga soga na bla bla, ujanja ujanja wa kariakoo, maneno maneno tuu n.k.

Wakasema wamepata pesa n.k. leo tunagundua ulikuwa ni udanganyifu tu

Sita, inaonekana kuliwa hakuna pesa, sasa mradi ulipangwaje kukiwa hakuna resource? Tunarudi pale pale bla bla, projo porojo

Saba. huu mradi ulipelekwa Bagamoyo kwasababu za kisiasa tu. Ni kama ule wa chuo cha IFM Msata.
Yote hayo nikukosekana kwa vision, tukaishi kwa hadithi na maneno neno porojo porojo na uzururaji ilimradi siku zinakwenda

Hawa wanaokataa mradi wa Bagamoyo ni CCM ile ile walioshindwa kusema hapana.

Ndio maana tunasema felia ipo pale pale tunabadilisha bega.

Hakuna sababu zilizoelezwa na kwamba nini kitafanyika tofauti kukabiliana na changamoto zilizopo bandari ya Dar.
Ni maamuzi yale yale yalifeli na sasa tunasubiri felia nyingine. Hakuna vision kwanini tusifeli? Felia ipo pale pale
 
Kimweri,

Kuhusu possibility ya Magufuli kuja ku-ruin uchumi wetu endapo ataendelea hivi nakubaliana na wewe na kuna mtu nilishawahi kumwambia all you need to agree with everything kwa haya yanayoendelea ni your preferred management style. Kama management style yako ni ile ya kuhakikisha mtu yupo kwenye kiti chake ofisini na hata akienda kunywa maji anaenda kwa kukimbia basi lazima leo hii aone Magufuli anatupeleka nchi ya Ahadi!

Yaani kabisa kuna wengine wanasema eti bandari zote hizo za nini huku akisahau kwamba moja ya sababu ya kwanini Dar inapokea mzigo mdogo kuliko Mombasa ni kwa sababu hata hao walaji na wauzaji wa ku-attract mzigo mkubwa Dar es salaam hawapo!! Yaani watu hawafahamu kwamba ni umasikini wetu ndio unaofanya bandari ya Dar es salaam ionekane inatosha!



Tatizo kubwa la sisi Waafrika ni kwamba hatuna akili na ndiyo maana ni ngumu sana kuendelea ingawaje tuna kila kitu!
Nchi yenye uchumi mdogo kama Tanzania hahitaji Bandari kubwa kama hiyo ya Bagamoyo sijui ya kuchukuwa mega ships hizo, hiyo Bandari ya Bagamoyo mnaing'ang'ania ili isafirishe nini?

Ngoja nikusaidie kidogo nchi yetu inamport na export bidhaa za thamani ya dola kama bilioni 16 (Na hapa ni jumuisho ya kila tunachoingiza na kutoa na kuna bidhaa nyingi hazisafirishwi kwa meli nyingine br. nyingine ndege hivyo Bandari peke yake ni chini ya hapo )na hii ni pamoja bidhaa zote za nchi zinazotumia Bandari yetu sasa uchumi kama huu wa dola bilioni 16 ni wa kujengea Bandari ya dola bilioni 10 kweli? hiyo ni economics ya wapi? Halafu hizo mega ships zitasafirisha nini?
Unaafifikri wamiliki wa Mega ships wataleta meli zao kwenye nchi inayosafirisha bidhaa za Dola bilioni 10?

Wachumi wote wa Dunia wanasema kwamba sababu kubwa ya nchi zetu za kiafrika kutokuendelea ni kwamba nchi wanafanya projects ambazo hazimake economic sense yaani wanatumia fedha nyingi sana kwenye white elephants projects kama hii la Bandari ya B'moyo badala ya kuwekeza fedha hizi kwenye mambo ambayo yangeweza kuzinufaisha nchi kwa haraka, kwa mfano kama ukichukuwa hizo bilioini 10 ukazigawa bilioni 2 ikaenda Tanga, Bilioni 2 ikaenda Mtwara, bilioni 3 ikaenda kwenye reli na barabara, biloni tatu zilizobaki zikaenda kujenga bandari ya Ziwa Tanganyika ambapo itahudumia Burundi, Kongo na Zambia na zingine zikapelekwa Ziwa Viktoria zikawekezwa kwenye bandari pia huoni kwamba kutaifungua nchi kwa kiasi kikubwa sana klk kuzitumia biloni 10 kwenye Bandari mpya ambayo wala kwanza haipo, na nchi wala haina uwezo wa kuitumia kwa maana ni kubwa sana ukilinganisha na Uchumi wetu?
 
The Construction of the 10 billion (about Sh22 trillion) Bagamoyo Port has been suspended, The Citizen has learnt. The government wants to focus instead, on improving the capacity, performance and efficiency of the Mtwara and Dar es Salaam ports.

The Minister for Works, Transport and Communications, Prof. Makame Mbarawa, confirmed yesterday that the construction of what would be the largest port in Africa has been suspended, not shelved to pave way for upgrading berths 13 and 14 as well as developing the Mtwara Port depending on the availability of Funds. The activities would take years to complete, the minister said because the process has to start from finding funding.


Source: THE CITIZEN
View attachment 315504
bila kuwa na uhakika wa sababu za kusimamisha ujenzi huu ni vigumu kuchangia. Serikali isifanye kazi kwa kusikiliza makelele ya siasa kama wachezaji wanaocheza kwa kusikiliza kelele za mashabiki.

wazo la kujenga bandari ya bagamoyo ambayo ni ya kwanza kwa afrika ikijengwa na wachina ni best proposal kwa Tanzania kwa maana kwa kuangalia jinsi wachina walivyotapakaa afrika nzima ingekuwa ni business opportunity ya kuifanya dar ikue sana kibiashara, ingekuwa rahisi wachina hawa kuvuta mizigo katika nchi nyingi za afrika magaribi, kati na kusini kupita bandari ya bagamoyo.

kwa mtizamo wa juu juu nadhani kulikuwa na uwezekano wa kukuza biashara katika nchi yetu na nchi nyingi za afrika na nje ya afrika na tungepata mapato mengi yasiyo ya moja kwa moja kutoka katika bandari.

baada ya hapo tuangalie katika business wanayofanya wachina sisi tunge pata nini kutoka bandarini moja kwa moja kwa kuangalia, kodi, au kama tuna asilimia katika mapato ya bandari, tuangalie kutengeneza ajira.

haya yote tulinganishe na kukumbatia bandari tulizonazo ambazo ni bandari holela kama yalivyo makazi yetu holela, hazina maeneo ya kutosha, hazina vitendea kazi, hazina wataalamu waliokaa kibiashara bali watu wa dili na mengine.
 
....lkn, kuna suala la uwezo wa bandari zetu kuhudumia meli kubwa,zinazobeba mpaka kontena elfu kwa mkupuo(3G&4G sea vessels), ambazo lamu port itakuwa na uwezo wa kuzihudumia...tunatazamaje hilo? Au sisi tutabaki tunapokea meli ndogo tu na kuacha biashara kubwa ya bandari, kwa wakenya, djibout, na south afrika?
Twende Mtwara kuna bandari yenye kina kirefu ni namna tu ya kuimarisha si lazima ujenge mpya wakati tunayo ya kuboresha na gharama zake haziwezi kuwa kama kujenga upya kwa mkataba wa namna ile lazima tujionee huruma na tuonew huruma vizazi vyetu vijavyo dhidi ya mzigo wa madeni ambayo yanaepukika.
 
Ni kweli haukuwa na mantiki yoyote. Lakini mmeshasaini mtaweza kuwalipa hao wawekezaji fidia ya kuvunja mkataba?
ni kweli mkuu watu wana mikakati ndo maana jamaa aliandaa kabisa na kampuni yake ili bandari ikijengwa Msoga basi Home wawe wanapakua na kutoa mizigo yao bila kulipa kodi, ndio maana Mzee wa msoga alifanya kila linalo wezekana Mdogo wake apate uraisi lakini Mungu naye mkubwa akaharamisha mipango ya wezi.
 
Sijui watu huwa mnajengaje hoja? Hayo mabavu anayoyatumia Magufuli kufanya hayo anayoyafanya kayatoa wapi kama si kwenye katiba. Uchaguzi Mwaka Jana ulifanyika kwa sababu Magufuli alitaka ufanyike au kwa kuwa Kikwete alichoka kuwa Rais? Magufuli anapoteua watu au kuhamisha huwa anafanya hivyo kwa kutumia mamlaka ambayo kayapata toka wapi kama siyo kwenye Katiba? Kasome vizuri ujue ni kwa nini wanasema Uingereza haina Katiba iliyoandikwa.


Ninachotaka kukisema ni kwamba Katiba haimmzuii Raisi kuwa mbaya na mwizi na ushahidi uko wazi, bali kinachotofautisha nchi moja na nyingine ni Utamaduni wa jamii husika na kamwe siyo Katiba, kama Raisi akitaka kutumia madaraka yake vibaya atayatumia tu hata kama Katiba hairuhusu atakachokifanya ni kupeleka mswada Bungeni kubadilsha kipengele ambacho hakitaki Wabunge wa Chama chake wanapitisha na anafanya anayotaka kuyafanya!

Hivi sasa Uhuru Kenyata ameshabadilisha mambo mengi tu ambayo yalikatazwa kwenye Katiba original kwa kutumia hilo hilo Bunge lao hata Kagame amebadilisha Katiba na huwezi kumlaumu kwa maana watu wamepiga kura ya maoni zaidi ya 90% wamependa abadilishe Katiba na hilo likafanyika hivyo Katiba siyo suluhisho bali ni Jamii yenyewe na utamaduni wake, kwa mfano sisi kwetu ni nini kilimzuia Kikwete kama kweli angeamua kubakia kuwa raisi mpaka leo hii?

Lakini hajafanya hivyo ni kwanini? Siyo kwa sababu ya katiba tu bali ni Utamaduni wetu hasa wa CCM waliojiwekea hivyo automatic unajiona haupaswi kuukiuka, Katiba haiendelezi nchi hata siku Moja asikudanganye mtu!
 
Mkuu ukijenga bandari bagamoyo bado kutakuwa na mlundikano wa watu katika mikoa hii miwili ambayo kiuhalisia ishajaa, tuijenge kusini na mikoa ya pembeni ili nchi ipanukee
Yaani ningekuwa mods, ningesema the mada is closed. Jibu lako ni tosha kabisa. Watu lazima wajue dar na bagamoyo si zaidi ya miaka kumi itakuwa imeungana, hivyo msongamano utakuwa pale pale. Nchi itanuliwe kwa kujenga bandari mbali kabisa na dar, na hilo litapunguza watu kuhamia dar kwa kasi kama ilivyo sasa.
 
Wengine tulijiuliza huyu Rais wetu ni mikataba gani 17aliyoingia kwa siku moja?

Ni vyema sasa mikataba yote iwekwe wazi na iwe inajadiliwa bungeni.
 
Hii nchi tutasubiri sana, ni chi ambayo haina dira, kila raisi ana dira zake za miaka 10, 10 au 5, mradi kama huu nlifikiri ulipewa baraka kubwa na baraza la mawaziri wote waliopita, ok tusirudi nyuma, lakini hapa inaonyesha ni jinsi gani kila kiongozi anaamuka na kufanya analojisikia. Kuna vitu nadhani hasa vya maendeleo viwe either tuna debate bungeni, kwenye vyombo ya habari, mitandaoni au njia yeyote itumike kuhalalisha sera na dira za maendeleo ya Tanzania. Haiwezekani unaamuka na kufuta project ya bandari ya 10B usd ambayo ingeli serve the whole africa , hivyo kuiongezea mapato na ajira kwa vija bila sababu. Kwani uwezo wa kupanua bandari ya zingine upo na wakati ujenzi wa bandari hii ukiendelea.
 
Ikiwa uyasemayo ni kweli,kwanini sasa watake kuimiliki bandari kwa muda huo tajwa?wanapata nini hapo bandarini in return?
Nilichosema ndo kweli yenyewe kwani wewe hukufahamu kwamba bandari iwe ya Mchina au Mwarabu lakini kodi iko pale pale basing na mzigo unaopita? Labda jambo moja ckusema-- China, wanataka independent port badala ya sehemu kama Dar coz' lengo lao ni ku-establish langu lao la kibiashara kati ya China na East & Central Africa! Kama ujuavyo, China ndo largest exporter to Africa... sasa walichotaka wao ni kutumia bandari ya Bagamoyo kwa ajili ya kusambazia bidhaa zao East & Central Africa na vile vile wana similar project Djibouti kwa ajili ya nchi za horn of Africa!! Sasa kwa mtu anayetaka kuushika u kanda mzima huwezi kumpeleka Bandari ya Dar yenye uhaba wa maeneo ya kuweza ku-handle millions of containers.

Tukija wao watapata nini; cjasema hawatapata kitu bali nilichosema TRA itaongeza mapato maradufu kutokana na kuongezeka kwa mzigo maradufu! Aidha nimesema mapato watakayoingiza TRA ni makubwa zaidi kuliko watakayoingiza Wachina!

Why 40 years?! Hii ni grand project.... $10 Billion sio pesa ndogo kui-refund na wala tusione ajabu! Fuatilia contracts za NHC na private real estate developer uone ni mikataba ya miaka mingapi wakati ile ni mikataba of just some billions Tanzania Shillings... wewe unashangaa mradi wa trillion 20 kuendeshwa for 40 years wakati hata sheria yenu ya kumiliki ardhi tu ni miaka 99 na wala hakuna serikali inachopata cha maana ingawaje nackia hivi sasa ni miaka 33!!! Sasa nyinyi mnaona hatari kwenye active project worth $10 billion kuwa operated kwa miaka 40 huku mkiendelea kukamua kodi kama kawaida?!

Lakini vilevile ikiwa shida ni hiyo miaka 40; solution ni kurudi kwenye negotiation table co kuachana na mradi....

Hapa narudia tena, kama hizi taarifa ni kweli basi Kenya lazima wachangamkie hii fursa na yale mashindano yetu na Kenya yatakuwa yamekufa rasmi na kutuacha na uboya wetu huku wenyewe tukifurahia! I bet atachofanya Mchina ni kitu kimoja tu... kuboresha TAZARA kisha anatuacha na uzuzu wetu!
 
Yap mkuu umejaribu kutokuwa mshabiki kama wengine humu,, hili suala watu wanarijadili kiushabiki sana mkuu..
tumeshaambiwa inaweza kuwa one of the big port in Africa, bila shaka mapato yake yangeweza kabisa kuzijenga Tanga na Mtwara kwa takribani kipindi cha miaka 20... Hii sio project yakuacha iende hivi hivi labda kama tuna solution inayofanana na hii project. Dar sio mji tena wakuutegemea kwa project yoyote kubwa baadala yake lazima tuwe na backup plan ya karibu na mji wa dar, bagamoyo port ingeamsha mji wa pwani, moro na tanga na kuunganisha dar,pwani,moro na tanga kimaendeleo, maana naona pia bandari ya tanga kutumika kama backup plan ya bandari ya bagamoyo kukiwa na congestation ya meli maana dar haitaweza tena, mtwara port itajijenga yenyewe maana tayari njia imeshaanza kufunguka kwenye oil na gas, lazima mapato yatapafikana tu maana hata makampuni ya mafuta na gas hayawezi kukubali kuteseka yatatujengea tu hii mtwara port kwa makubaliano fulani..


Big Port Afrika itasafirisha bidhaa gani? hakuna Uchumi Tanzania wala nchi zinazotuzunguka za kuweza kuitumia Bandari kama hiyo, hiyo ingekuwa ni white elephant project!
 
Nakatishwa tamaa sana ninapoona hoja dhaifu kutoka kwa wasomi kama nyinyi,sasa hao wasiobahatika kwenda shule sijui wako ktk hali gani kiupeo?Dr Magufuli yupo sahihi kabisa kuusimamisha mradi wa bandari ya Bagamoyo,bandari ya Bagamoyo ikikamilika itakuwa chini ya China kwa miaka 40,ndani ya muda huu bandari zetu zitaathirika sana kimapato kwasababu nina uhakika wateja karibu wote wa bandari ya Dar watahamia Bagamoyo kwasababu ya ukubwa wake,mbaya zaidi mapato yote ya bandari ya Bagamoyo yataenda China, Sisi tutaambulia vijikodi tu, wakati bandari zetu wenyewe zinazotuingizia mapato kwa 100% zikijifia,huo mkataba wa ujenzi ya bandari ya Bagamoyo ni bomu linalosubiri kutulipukia,bora Magufuli ameanza kulishughulikia male a.
Asante ndugu yangu kuzidi kuwafafanulia. Haiingii akilini kwa ghafla tuache kupata mapato ya bandari ili tusubiri miaka hamsini ya mapato tusiyokua na uhakika nayo. Mchina wa leo si yule wa enzi ya Nyerere. Anajua Sifa kubwa ya Tanzania yetu ni shamba la bibi. Masharti ya kwanza atakayoweka ni kwamba kwa miaka 40 hiyo meli zote lazima ziweke nanga bagamoyo. Hivyo bandari ya dar ingekufa kifo cha mende. Kwa kweli sijui kwa nini imekua shida kwetu kuona hilo. Kuna mtu katoa mfano mzuri sana hapa wa migodi ya dhahabu. Awali Mwalimu alikataa yasichimbwe kwa hoja watanzania hawatafaidika nayo. Sasa kuna migodi imemaliza madini na imefungwa hali wananchi wa maeneo hayo bado wako hoi. Kwa hili nampongeza sana Mhe Magufuli ila aende polepole na la walala hoi wa mabondeni. Kwa maana awaondoe lakini yeye kama baba wa Watanzania awasaidie wapate makazi hata kama ya muda.
 
Hii nchi tutasubiri sana, ni chi ambayo haina dira, kila raisi ana dira zake za miaka 10, 10 au 5, mradi kama huu nlifikiri ulipewa baraka kubwa na baraza la mawaziri wote waliopita, ok tusirudi nyuma, lakini hapa inaonyesha ni jinsi gani kila kiongozi anaamuka na kufanya analojisikia. Kuna vitu nadhani hasa vya maendeleo viwe either tuna debate bungeni, kwenye vyombo ya habari, mitandaoni au njia yeyote itumike kuhalalisha sera na dira za maendeleo ya Tanzania. Haiwezekani unaamuka na kufuta project ya bandari ya 10B usd ambayo ingeli serve the whole africa , hivyo kuiongezea mapato na ajira kwa vija bila sababu. Kwani uwezo wa kupanua bandari ya zingine upo na wakati ujenzi wa bandari hii ukiendelea.



Hata wewe tatizo la uelewa pia! Unawezaje kujenga Bandari TanZania ikahudumia Afrika nzima? Kivipi unaweza kuniambia? Kwa taarifa yako tu wateja wanaotumia hata Bandari ya Mombasa Kenya huwezi kuwaleta kutumia Bandari yetu ni ngumu sana na hai make economic sense kwao kijiografia sasa iweje Bandari ijengwe Bagamoyo ihudumua Afrika nzima? Unawezaje kumfanya Muethiopia au Msufdani aje kutumia Bandari ya Bagamoyo badala ya Mombasa unaweza kuniambia hilo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom