Serikali yasitisha ujenzi wa vituo vya mafuta

Serikali yasitisha ujenzi wa vituo vya mafuta

Dk Angeline Kusimamisha ujenzi wa vituo vya mafuta inaonyesha umeichoka wizara ya ardhi.

Sasa unatafuta kushika simba masharibu au ndevu na dawa utaipata.

Sasa wengi wataanza na kufuatilia hiyo Phd yako ulivyoipata iwapo wengi walikuwa wamepiga kimya.

Visima vya mafuta vingi na vinavyojengwa ni vya naibu wako na mtoto wa mtu mkubwa.

Baraza la mawaziri linasukwa upya utajikuta kukipigwa chini kama Mulamula
Hilo baraza linasukwa kila uchao?
 
Huu ni usanii, nani asiyejua kuwa ridhiwani alipelekwa ardhi kufanikisha upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya vituo vya lake oil ambavyo vimechipuka kama uyoga baada ya pesa fulani kupigwa...
Wee akili huna hivi nchi hii kupata vibali vya ardhi kujenga shell mpaka ridhiwani awe naibu waziri wa ardhi?naibu waziri kwaza Hana uwezo wa kutoa kibali
 
Huu ni usanii, nani asiyejua kuwa ridhiwani alipelekwa ardhi kufanikisha upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya vituo vya lake oil ambavyo vimechipuka kama uyoga baada ya pesa fulani kupigwa...
Hivi unamjua mwenye lake oil au unataka kuleta story za kwenye kahawa
 
Yaan ilikuwa hadi kero hadi unashangaa
Mfan Ukianza kwa tumbo tandare mpk darajani sinza kuna vituo vya mafuta 7 vinne vishakamilika vitatu vipo ongoing kwa maana vibari vishatoka au vinasikiliziwa maana maeneo yapo wazi kwa ujenz
Yaan hapo kutoka kwa Tumbo mpaka darajani ni ndani ya kilomitaa kama 1.5 au 1.7
Lkn pana utitili wa vituo vya mafuta
Ambavyo vinaibuka kama UYOGA
Watu wanaangalia fursa wewe huoni ongezeko kubwa la watu kununua magari ongezeko la pikipiki bajaji vituo vikiwa vichache kwa hali ilivyo mtapanga foleni
 
Hilo baraza linasukwa kila uchao?
Wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi imemshinda, wakulima na wafugaji wanauana anapiga kimya, ujenzi holela mijini unakua kwa kasi ya 5G, mahakama Za ardhi rushwa umefikia 100%, mahakama hiyo ilitakiwa kutumia lugha ya Kiswahili Ili kutenda haki ila hakumbuki kufuatilia .

Leo anaibuka na vituo vya kuweka mafuta?

Aondolewe tu na jimboni kwake aliwahi kusema maji sio kipaumbele chake.

Hii Phd yake tunaifuatilia tutawapa majibu.
 
Mkuu mkoa mzima? Sidhani
Ndio ukweli mnapoongea vitu mzunguke nchi nzima mjiridhishe dio kuandika tu mnatenda dhambi kwa kuongea uongo Nina ushahidi wa mikoa kadhaa lake oil haipo usione vinajengwa dar ukadhani ni nchi nzima?
 
Hii ni serikali ya kipumbavu sana. Sasa mtu amekopa hela benki ajenge kituo cha mafuta aanze kurudisha mkopo, wao wanamzuia? Watamlipia mkopo? Nonsense!
Wamezuia vibali vipya
 
Ukija pale jkt mlalakuwa kuelekea kawe kuna kituo,na pale paliwa makazi,ukija maringo njia panda kawe kna kituo...
Kino studio kituo ....
Ila hawa wafanyabiashara wana nguvu lazima watakuja na plan B [emoji1]

Ova
Kama pale JKT wamevunja vile vigorofa mshenzi, afu kituo kimesimama

Kile cha Kituo cha Kawe ni kama vile hakitaanza kazi, pamoja na cha Feza
 
Watanzania wengine wana roho ya kichawi

Mimi sioni shida hata hiyo kampuni ikimilikiwa na mtanzania ngozi nyeusi mwenzetu yeyote awe Ridhiwani au yeyote

Watanzania ngozi nyeusi baadhi hawataki kuona wenzao ngozi nyeusi wanamiliki kampuni kubwa za mafuta wanataka ngozi nyeupe tu hivi shida nini?
Shida ni kupora pesa za umma kufanikisha hayo.., ni hayo tu
 
Ndio ukweli mnapoongea vitu mzunguke nchi nzima mjiridhishe dio kuandika tu mnatenda dhambi kwa kuongea uongo Nina ushahidi wa mikoa kadhaa lake oil haipo usione vinajengwa dar ukadhani ni nchi nzima?
Ok, ila wamewekeza sana mikoa mingi
 
Serikali imesitisha utoaji wa vibali vipya vya ujenzi wa vituo vya mafuta na mabadiliko ya matumizi ya ardhi kwa ajili ya vituo vya mafuta kwa muda wa miezi mitatu kuanzia leo.

Uamuzi huo umetangazwa leo Alhamisi Novemba 10, 2022 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula.

"Lengo ni kutoa nafasi kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wizara zinazohusika na utoaji wa vibali kufanya tathmini ya kina kuhusu ujenzi wa vituo vya
mafuta nchini," amesema.


=====

Serikali imesitisha utoaji wa vibali vipya vya ujenzi wa vituo vya mafuta na mabadiliko ya matumizi ya ardhi kwa ajili ya vituo vya mafuta kwa muda wa miezi mitatu kuanzia leo.

Uamuzi huo umetangazwa leo Alhamisi Novemba 10, 2022 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula.

“Lengo ni kutoa nafasi kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wizara zinazohusika na utoaji wa vibali kufanya tathmini ya kina kuhusu ujenzi wa vituo vya mafuta nchini,” amesema.

Aidha, Dk Angeline ameagiza kusitishwa kutolewa kwa vibali vipya vya ujenzi vinavyokiuka mipango kabambe ya majiji, manispaa, miji na kusitisha ugawaji wa viwanja kiholela unaosababisha taswira za miji kuharibika.

Ametoa mfano wa eneo lililopangwa kuendeleza ujenzi wa maghorofa vibali vifuate mpango.

Source: Mwananchi.
WIZARA YA ARDHI NDIO CHANZO KIKUBWA CHA UHARIBIFU WA MIJI YETU NCHI WATENDAJI WAKE WANAHUSIKA KWA ASILIMIA 100
 
Back
Top Bottom