Serikali yatangaza Amri ya Bei Elekezi za Sukari Tanzania Bara

Serikali yatangaza Amri ya Bei Elekezi za Sukari Tanzania Bara

View attachment 2881106
View attachment 2881107
Kufuatia malalamiko ya Wananchi juu ya kupanda kwa gharama za Sukari, Serikali imetangaza Amri ya Bei Elekezi iliyoanza kutumika Januari 23, 2024 katika Mikoa yote ya Tanzania Bara kwa lengo la kudhibiti Bei holela za Bidhaa hiyo

Kwa mujibu wa Tangazo la Serikali, Amri hiyo imesema Mtu yeyote anayeuza Sukari kinyume na Bei Elekezi zilizoainishwa atakuwa ametenda Kosa na akitiwa hatiani atawajibika kwa adhabu iliyoainishwa katika masharti ya Sheria ya Tasnia ya Sukari

Bei Elekezi za Rejareja kwa Kilo 1 Sukari ziko kama ifuatavyo: Dar, Morogoro, Pwani Tsh. 2,700 - 3,000, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe Tsh. 2,700 -3000, Dodoma, Singida, Tabora Tsh. 2,800 - 3,000, Lindi Mtwara, Ruvuma Tsh. 2,900 - 3,200

Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara Tsh. 2,800 - 3,000, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara Tsh. 2,700 - 3,000 na Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa Tsh. 2,800 - 3,200
Uchumi hauendi hivyo, Mambo ya bei elekezi ni Mambo ya Kijima ya miaka 1947!
Bidhaa zinatakiwa ziende kwa nguvu ya soko,demand and supply,
Low demand, high supply, bei zitaporomoka!
High demand, low supply, bei Zita panda tu, high demand, high supply, bei zinakuwa stabble, sio huu upuuzi unaoendelea,
Inawezekana vipi, watu wakaficha bidhaa, ili bei zipande, na serikali IPO, Waziri, katibu mkuu, maofisa ndani ya mkoa, wilaya, watu wa usalama, nk
 
Hapa ndo wameipeperusha sikari moja kwa moja,sukari haitapatikana kirahisi kabisa,hivi sasa maeneo mengi sukari inapatikana kwa shilingi 4500 hadi 5000,sasa hiyo 2800 sijui itawezekana vipi?leo hii watu wa sigara nao wamepandisha bei ya sigara mfano sm na spot bunda moja la paket 10 ni tsh 43000 toka bei ya zamani sh 34000,Wiston tsh 26000 toka tsh 17000.ukifikiri kwa makini utagundua tuendako sio
 
Hapa ndo wameipeperusha sikari moja kwa moja,sukari haitapatikana kirahisi kabisa,hivi sasa maeneo mengi sukari inapatikana kwa shilingi 4500 hadi 5000,sasa hiyo 2800 sijui itawezekana vipi?leo hii watu wa sigara nao wamepandisha bei ya sigara mfano sm na spot bunda moja la paket 10 ni tsh 43000 toka bei ya zamani sh 34000,Wiston tsh 26000 toka tsh 17000.ukifikiri kwa makini utagundua tuendako sio
Halafu watumiaji wa sigara nao wamekaa kimya tu
 
Nakuelewa sana Mkuu, mtu aliyekua anaziweza hizi mambo ni huyo kwenye avatar Yako.

Unakumbuka sakata la mafuta ya kula, na sukari enzi zake...
Upo sahihi kabisa nakumbuka wakati wa magufuli kulikuwa na uhaba wa sukari sasa magufuli akadai sukari imefichwa makusudi sasa akikukamata nayo inataifishwa,sasa hapa mtwara kuna mzee mmoja alishusha kama tani 40 hivi za sukari na ile siku inashushwa mimi niliona kwa kuwa ni jirani yangu, ila chakushangaza wateja wakija anawajibu hana aisee ilipotoka ile amri yenye lafudhi ya kisukuma yule mzee alifichua mwenyewe ,,sasa je unadhani mfanyabiashara ni wakumuonea huruma?
 
Afu haitapatikana kabisaa
You are absolutely right. Enzi zetu hali ilikuwa hivyo. Pamoja na kuwa na bei elekezi haikusaidia kitu. Ama bidhaa ilipotea ghafla toka madukani au iliuzwa kwa bei tuliyoiita ya magendo. Tulikuwa na msemo kwa wakati huo " the controlled price is a price at which the commodity in question is not available"
 
Back
Top Bottom