Serikali yaunda Kamati kuchunguza chanzo cha moto Soko Kuu Kariakoo. Waziri Mkuu asema hatua zitachukuliwa moja kwa moja ikijulikana kuna mkono wa mtu

Ule mkataba ulikuwa unaleta Dron hapo sokon ingefanyaje kazi? Lakini ata hivo huwezi kufanya mipango ya kusaini mkono wa takriban Trilion 1 huku baraza la waziri halijui chochote
Kwamba hiyo Trilion 1 ilikua ya kuleta drone tu hakuna vifaa vingine?
 
Hivi ile migari miingi ya washa washa waliyonunua wakati wa uchaguzi mkuu 2015 yanafanya kazi gani? Mengi naona yanaoza kwenye vituo vya polisi bora yangegeuzwa mabasi au zimamoto
 
Miaka yote hii hakuna mikakati ya kukabiliana na majanga? Kama kujaza maji kwenye magari kumeshindikana ndiyo wataweza kutengeneza mkakati?
Inshu ya zimamoto inahitaji preparation kubwa unaweza kwenda na maji yamejaa kumbe Moto unahitaji dry chemical Powder , au sand au carbon , Moto hauzimwi tu unazimwa kutokana na chanzo cha Moto , zaidi ukijua fire classes itakusaidia kwamba sio kila kitu ni zima Moto Bali watoa taarifa kuhusu chanzo cha moto
 
Kamishna Mkuu wa Zimamoto aliwahi kutumbuliwa enzi za JPM kwa tuhuma za kusaini mkataba aghali wa vifaa vya Zimamoto
Yule ni haki kabisa kutumbuliwa.
Unakwenda kununua drone hata nchi tajiri za Europe bado awajaweza kununua.
Magari ya kuzima moto tunayo lakini maji tu yametushinda.
Kwa nini asingewekeza kwenye water supplies kwenye sehemu kama hizi ambazo ni very risk!! Mambo madogo tu yanatushinda tunakimbikilia makubwa!!
 
Ule mkataba ulikuwa unaleta Dron hapo sokon ingefanyaje kazi? Lakini ata hivo huwezi kufanya mipango ya kusaini mkono wa takriban Trilion 1 huku baraza la waziri halijui chochote
Yule aliyetaka kununu drone ambazo ni bei kubwa ni mpuuzi sana!!
Hata water supplies ilimshinda ndio aliona drone ndio solution!
Angalia hata majengo yaliyojengwa sasa hivi kama yalijengwa kukabikiana na matatizo ya moto kama yakitokea. Mfano milango, window materials na hata kama ya hydrant karibu!!
Yeye badala ya kuboresha fire safety regulations alikimbilia mambo makubwa…bure kabisa!
 
Serikali pia inunue magari ya Zimamoto yenye maji.

Inasikitisha sana Waziri Mkuu anakuja na kauli kama ile eti kama Kuna mkono wa mtu.

Unasemaje namna hiyo, how do you lead a country ufikiri Kuna hujuma??

How long this administration itakua inalilia hujuma tu,

Hujuma ni kuficha madhaifu.

Lazima tupambane na madhaifu yetu na sio kulia lia kuhujumiwa.
 
Acha ramli. Na maeneo mengine ambako kila mara kunatokea ajali za moto, wanaosababisha ni iliyokuwa board ya soko la Kariakoo?

Nchi hii mambo mengi ni ovyo karibia kila sehemu. Hatuna uwezo wa kupambana na matukio ya dharula na ajali kwa sababu watawala hawajui vipaumbele.

Fikiria watu walivyokufa kwenye ajali ya meli pale Mwanza, ndipo utajua kuwa nchi hii hatuna serikali kwaajili ya watu bali ipo serikali dhidi ya watu.
 
Mombasa soko pia limeungua ... na kuna shule ya imeungua we unaonaje
 
Mombasa soko pia limeungua ... na kuna shule ya imeungua we unaonaje
Kule Arusha Kuna wakati shule ziliungua mfululizo walikua wanamhujumu Magufuli au??

Mimi nadhani serikali inapaswa kutathmini uwezo wake wa kukabiliana na majanga ya aina mbali mbali na sio kukimbilia tu kusema Kuna mkono wa mtu.

Tunapaswa kuwa na uwezo na utayari wa kukabiliana na dharura za aina mbali mbali.
 
je kama ni hitilafu ya umeme,
 
Shule zote za mlengo flani wa dini? Hakuna kitu kama hicho kwenye intelligensia labda tu useme sababu na motives behind hazikuwekwa public
 
Tunapowaambia nchi inahitaji mabadiliko mnaanza kusema chokochoko tunahitaji fikira pevu sio hizi za kinyerere pumzikeni hata hao munaowaita wapinzani ni watanzania wote mmetuletea mpaka wahutu na wametuongoza pumzikeni mmechoka nyie ma Ccm
 
Siku zote tunaambiwa na vyombo vya usalama chanzo cha moto hakijulikani, sasa wananchi wa kawaida watajuaje kama wataalamu hawajui
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…