Serikali yawatelekeza wanafunzi 29 Ukraine

Duh, mtanisamehe sana, nimechelewa kuisoma hii thread na sikujua kama kuna develpment kama hii. Hili ni jambo la dhararu, Mwanakijiji, naomba nami unitumie details kwenye mwanasiasa@jamboforums.com

Sasa, hii shida ndio ingekuwa mwanzo wa ku-consolidate lile wazo letu la kuanzisha scholarship program, huu ungekuwa mwanzo mzuri wa kutoka na mfuko huo. Will come back later with more ideas.

Mbarikiwe mlioanzisha wazo la kuwachangia hawa vijana.
 
Kiev:

Vijana bado wapi Ubalozini. Kutokana na hali ya hewa kubadilika (joto kali mchana na baridi kali usiku) baadhi yao wameanza kupata homa kidogo. Wamekubaliana kuwaruhusu dada zao (watatu) kurudi vyuoni (leo ikiwa ni siku ya mwisho) na vijana 17 wao hawaendi popote. Michango iliyotumwa jana imefika na wanashukuru (kwa machozi). Michango ambayo inakusanywa leo nitawapa habari zake kesho.

Ubalozi wa Uingereza Ukraine umeendelea kuwa na mawasiliano na Ubalozi wao TZ na walitarajia kupata majibu ya serikali jana. Leo hii (Jumamosi) hadi balozi anaondoka pale hakukuwa na majibu yoyote. Maelezo kuwa mama Kabaka yuko Ukraine hadi hivi sasa hakuna ushahidi kuwa anashughulikia jambo hilo (aidha Waziri Mkuu hakuwa na taarifa sahihi)

Dar:

Bado ni kimya Siku ya TATU
 
No problem KT, tangu niamke nimekuwa nikijitahidi kuwasiliana na Balozi Chokala bila ya mafanikio. Nimetuma email na pindi nikipata majibu nitawajulisha.
 
No problem KT, tangu niamke nimekuwa nikijitahidi kuwasiliana na Balozi Chokala bila ya mafanikio. Nimetuma email na pindi nikipata majibu nitawajulisha.
Mwanakijiji!
Nimefanya uchunguzi kuna wanafunzi kwenye Nchi zifuatazo Russia,Czhec Republic,Poland,China, Cuba ,Uingereza,Marekani,Uganda, Kenya ambao wanapata mikopo kutoka bodi ya mikopo pamoja na matatizo ya kuchelewa ,ufuatiliaji kwa wazazi kusainishwa huko nyumbani lakini wanapata.Sasa kulikoni hawa 29?Cha msingi wasaidiwe angalau kurudi nyumbani ili wasipate madhara zaidi ugenini kama wanaona hawawezi kuwapatia mikopo,Halafu waombe tena mikopo warudi shuleni popote watakapopata nafasi.
 
KNKCU, nimeshazungumza na wanafunzi wa Urusi ambao kesi yao ni tofauti kidogo lakini na wenyewe wanamatatizo hasa miezi hii inayokuja.. nimezungumza na wanafunzi wa Cuba ambao matatizo yao yalikuwa yanakaribiana na wa Ukraine. Ni kweli mengi yametetatuliwa, ila kama nilivyoeleza kwenye mada nyingine kesi ya Ukraine ni tofauti kidogo. Hata hivyo kumbuka pia kuwa kwa vijana hawa kuja hadharani na kusema hadharani na kutaja majina hadharani.. wamejijengea uadui mkubwa, hata kama wakirudi wanaweza kushindwa kabisa kusoma tena Tanzania!! na wakaoenekana ni maadui wa serikali!! mwisho tutaanza kuwashauri waombe political asylum kwani serikali haiwezi kuwatendea lolote jema baada ya haya yote.. I might be wrong.. lakini that option should be on the table now!

we'll take a notch higher next week..
 
Kama wataweza kuomba Assylum na kufanikiwa sioni ubaya wake ila itakapotokea wakakataliwa na kurudishwa Nyumbani huoni hapo watakuwa wamejiweka ktk kufunguliwa mashitaka kwani ndivyo wafanyavyo.Kama hao ubalozi walikubali waende Kiev Halafu walipofika wamewaacha nje huoni hilo nalo ni tatizo ,nilitegemea watawapokea na kuwapatia mahitaji ya muhimu ya kijamii wakati wanasubiri hatima au uamuzi kutoka serikali yetu Lakini kitendo cha kuwawacha Nje ya Balozi sioni Kama kinaleta picha nzuri ya kupata msaada hasa kwa maana ya msaada au cha hao ubalozi kutoa msaada kwa maana ya msada uliokamilika kwa watu wenye shida kama hao vijana wetu.
 
kwa vile sasa hivi hawajaomba Asylum ndio maana ubalozi unafungwa mikono kidogo. Na ubalozi huo uko tayari kuwasaidia endapo tu serikali ya Tanzania itakuwa tayari kurudisha hizo fedha kwa ubalozi. Nina uhakika endapo wataamua kujilipua basi ubalozi utaanza kushughulikia kama wakimbizi au asylum seekers..!
 
Hivi tatizo lililopo ni lipi hasa kwa i.e. balozi wetu anayeshughulikia Ukraine au yeyote yule ambaye Ubalozi wa UK ulim-contact kutoa assurance kwamba Serikali ya Tanzania itawalipia hao vijana waliofika hapo ubalozi wa UK kule Ukraine na kuwaomba waangalie hati zao za usafiri kwa kuhakiki na kuwatatulia matatizo yao. MAMBO MENGINE YOTE YAFUATE BAADAYE. WE NEED TO SEE SOME HEADS ROLE INCLUDING THOSE WHO ARE CONTACTED BY THE BRITISH HIGH COMMISSION FOR INDECISION

MBONA BALOZI NYINGI TU WAMEWEZA KUTUMIA FEDHA ZA WALIPA KODI VIBAYA BILA RIDHAA YA BUNGE NA WIZI WA KIMACHO MACHO TU. JE UNAPOPEWA DHAMANA YA KUONGOZA MAANA YAKE NI NINI? HAWA VIONGOZI MBONA WANAKUWA WEPESI KUSAINI MIKATABA MABOMU LAKINI KWA JAMBO KAMA HILI WANASUASUA?
 
dua.. right on.. viongozi hawafuati!! ninaposema Msolla ajiuzulu ni kwa sababu hii ameshindwa kuongoza!!
 
Sasa huyo Mh. Chokala anafanya nini Kama hawezi kukubali ktk mambo ya shule kwavile hana mamlaka nayo kwanini asikubali tu kusaidiwa na huo ubalozi wa uingereza kwa kukubali wakatiwe angalau tiketi warudi nyumbani.Nafikiri tunamatatizo ya decision making Kama ni mimi ningekubali msaada wa hao vijana kukatiwa tiketi warudi nyumbani ,Halafu nione kama hao mabosi huko nyumbani ktk hali kama hiyo wangenifukuza kazi kwani ushahidi wa fedha zilivyotumika ungekuwepo tena kuna Organization inaitwa IMO(INTERNATIONAL MIGRATION ORGANIZATION) Ni kiasi tu cha balozi kuwaandikia tu nina wananchi wenzagu ninaomba wasafirishwe kurudishwa Tanzania kwani hatuna uwezo kwasasa.Hao jamaa wakipata hiyo barua wanawaandalia walengwa usafiri na fedha za matumizi hadi kwao.Wana ofisi pale moscow inayoshughulikia Nchi zote zilizokuwa chini ya Jamhuri ya Kisoviet ya Urusi ikiwemo hiyo Ukraine.
 
Kazi, naona umeona tatizo lilipo sasa..
Unajua kadiri unavyotafuta habari kupitia vyanzo mbali mbali ndiyo unavyoelewa zaidi na unapopata majibu ya uhakika kutokana na kile unachokifuatilia,Baada ya kutafuta habari na kuona kuna wanafunzi wanalipiwa tena Nchi nyingi tu na bodi ya mikopo na maelezo yako amabayo umeyapata moja kwa moja kutoka kwa hao vijana nimeona tatizo ni hilo,Inanisikitisha sana na ninatamani kuona ufumbuzi wa haraka unafanyika ili kuwatoa hawa vijana kwenye hiyo adha wanayopambana nayo.Unajua nimewahi kutembelea Ukraine mara kadhaa ninaelewa nini kinachowakabili hao vijana ktk mazingira ya NCHI ILE.Kinachonisikitisha ni kwamba pamoja na majukumu yetu tuliyonayo sisi kama wanadaamu tunawezaje kutafuta habari na kujaribu kutafuta ufumbuzi wa tatizo lakini wale wenye Jukumu hilo ambao ni watumishi wa umma na wanalipwa kwa kazi hiyo washindwe?
 
ukipata jibu la swali hilo Kazi, unaweza kujishindia milioni! wenyewe wanasema "that is a million dollar question"!
 
Mzee Mwanakijiji,

Ile mada inayoomba Msolla ajiuzuru iko wapi?.. nafikiri inatakiwa kichwa chake kabisa...
 
Mkandara, I'm working on a revised argument.. kama kuna kiongozi katika awamu hii ambaye anastahili kufutwa kazi, au kujiuzulu yeye mwenyewe ni Prof. Msolla, najaribu kupata habari nyingine sahihi kutia nguvu hoja yangu. wish me luck!
 
Kiev: Vijana bado wapo. Wamewaruhusu dada zao (3) kurudi vyuoni kwani hali ya hewa si nzuri. Usiku wa kuamkia leo wamenyeshewa na mvua lakini bado wapo nje ya Ubalozi wakisubiri majibu labda kesho asubuhi.

Moskow: Ubalozi bado haujasema lolote na jitihada za kuwapata hazikuzaa matunda.

Dar: Msimamo wa serikali wa kutowatambua na kushindwa kutafuta utatuzi wa suala hili bado ni ule ule. Hakuna kiongozi anayejisikia haja ya kulizungumzia jambo hilo. Vyombo vya habari vya nyumbani licha ya kujua kuhusu suala hili bado wako kimya na hawajaanza kulifanyia kazi.

Michango:

Hadi hivi sasa ni watu wanne tu wamechanga karibu dola 300 hivi ambazo zimetumwa na zimepokelewa leo. Nashukuru wote mliojitokeza kusaidia na kwa niaba yao Mnyezi Mungu awabariki na kuwazidishia.
 
Watu tuna majukumu mengi sana ya kifedha; ila nadhani mojawapo kati ya mambo ya maana sana tunayoweza kufanya ni hili kuwasaidia watoto hawa walioko ugenini. Nimesikia kuwa baadhi yao wanatoka kwenye familia ambazo zinakabiliwa na tatizo la asilimia 40 pale mlimani. Wahenga walisema tenda wema wende zao; kama kweli huwa tunachangia harusi hadi zile harusi ambazo muoaji anakuwa anaoa mke wa pili, nadhani kama Jamboforums tungejitosa kama jumuia moja na kutoa michango ya dola 10, pauni 5, yen 1000 EU 5 na vitu kama hivyo tungezeweza kufikisha angalu dola 1000 kuwasaidia watoto hawa katika kipindi hiki kigumu. Nina imani kuwa tatizo kwa wengi limekuwa ni ile haja ya kuwatumia watoto hawa moja kwa moja kwa westernunion ambapo gharama za utumaji ni kati ya dola 15 hadi 20: zaidi kiasi kinachoweza kutolewa na mchangiaji kwa kiwango nilichotaja hapo juu cha dola 10. Ninashauri kuwa watu wanaojua mambo ya biashara ya kimataifa watusaidie tena hapa kutafuta utaratibu wa kufanya michango ya haraka haraka kwa kiwango reasonable kwa kutumia jina la mtu mmoja na kuwatumia vijana hawa. Ikiwezekana tuchange kwa kutumia Paypal Account ya Jamboforums na kuwachia Admin jukumu la kuzifikisha kwa walengwa.

Kati ya wachangiaji wanne waliotajwa na MKJJ, utakuta kuwa kati ya $60 hadi $80 zimetumika kusafirishia hizo $300, which is more than 25%. Kama zote ningewafikia ingekuwa jambo la maana sana.
 

Kwa sababu ni vigumu kuamini kuwa nchi (taifa) linaweza kutowajali raia zake kiasi hiki.

Halafu, pamoja na yote hayo, ubalozi walikokimbilia wakidhani kuwa labda watapewa msaada, nao unakosa hata ule ubinaadam tu wa kawaida. Hivi kweli inawezekana, watu wakafika nyumbani kwako, hata kujikinga mvua tu, halafu wewe ukawaambia wakae huko nje kibarazani huku wewe ukiendelea kujitanua ndani? Ni ubinaadam gani huo?

Mkjj, tafadhari bwana tupe ukweli - hao vijana wamekaa nje ya ubalozi kwa siku hizi nne sasa, bila hata ya kupewa msaada hata wa chakula na maji? Ni kweli hiyo, au na wewe unatufumba macho kwa sababu unayoifahamu mwenyewe? Mbona ni vigumu hasa kuamini kuwa watu wanaojiita waliostaarabika kama hao Waingereza waweze kutenda hivyo? Mali zote zile walizosomba wakati walipotutawala, yaani hata kuwapa vijana hawa maji tu ya kunywa hakuna? Siamini.

Kioja kingine nisichokielewa kuhusu jambo hili ni ukimya wa vyombo vya habari, sio vile vya nyumbani tu pekee, lakini hata hivyo vya Uingereza na kwingineko. Watu zaidi ya ishirini wawe katika eneo la ubalozi hata pasiwe na habari yoyote iliyoandikwa au kutangazwa katika chombo chochote?

Nilisikiliza mahojiano yako (KHLNews) na hawa vijana na yale uliyowafanyia wazazi wao. Nadhani kuna jambo lililofichika kidogo, lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya serikali yetu kuwa na msimamo huu unaotutia aibu kama taifa.
 
Kalamu, nitawapa habari zaidi leo. Na kuhusu wao kuwa nje hapo, hata ofisa wa Ubalozi huo niliyezungumza naye Ijumaa alithibitisha hivyo. Sasa ukiniuliza kwanini watu "waliostaarabika" hawajali, jibu lake nitakuuliza kuhusu Darfur, Rwanda, na Somalia.... kama maslahi yao hayako matatani, they don't give a.. ... !! Na viongozi wetu wameanza kuwa na tabia hiyo, kama hakuna mtoto wa ndugu yao au watoto wao wenyewe.. hakuna haraka..!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…