Serikali yazuia vifaranga 62,730 vilivyoingizwa nchini kutoka Ubelgiji

Serikali yazuia vifaranga 62,730 vilivyoingizwa nchini kutoka Ubelgiji

Sasa huyu aliyeingiza hivyo vifaranga si wangemuacha tu ili apate hasara? Maana soko la vifaranga hakuna kwa mujibu wa yule mzungu wa Arusha
Labda hukumuelewa yule Mama !! Kuhusu hili la sasa; sheria ifuate mkondo wake.
 
Mkuu naomba unisaidie. Yule mama alivichoma vifaranga vyake kwa sabb gani haswa?
Sababu kubwa ni gharama kutoendana na bei ya soko ikiwa ni pamoja na uingizwaji wa vifaranga kutoka nje. Na sio ajabu uingizaji huu wenye ukwepaji kodi ni sababu mojawapo ya wafugaji wa ndani kushindwa kuendana na biashara hii na hivyo baadhi yao kuamua kuachana nayo.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Dar es Salaam, Desemba 24, 2022

KUZUILIWA KUINGIA NCHINI KWA VIFARANGA 62,730 VYA KAMPUNI YA PHOENIX FARMS LIMITED VILIVYOFIKISHWA AIRPORT KUTOKA NCHI YA UBELIGIJI
Ndugu wanahabari,

Tarehe 22/12/2022 saa nne usiku Wakaguzi wa Mifugo na Mazao yake walio katika kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) walikamata vifaranga wa kuku wa mayai 62,730 mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited ya Mkuranga, Pwani vilivyofikishwa uwanjani hapo vikitokea nchini Ubeligiji bila ya kuwa na vibali vya kuingiza nchini vifaranga (Import permit) pamoja na cheti cha afya (animal health certificate). Vifaranga hivyo viko kwenye makasha (crates) 697 na stakabadhi ya mauziano (Invoice) ya mzigo inaonesha vina gharama ya shilingi 200,262,706 ambayo ni sawa na Euro 80,828.80 (Cost Insurance and Freight – CIF). Mkurugenzi wa Kampuni pamoja na Wakala wa Mmiliki wa vifaranga (clearing agent) hivyo walikiri kutokuwa na kibali hivyo kuwa amevunja Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Sura ya 156 na Kanuni za Udhibiti wa Usafirishaji wa Wanyama na Mazao yake ya GN. Na. 28/2007.

Ndugu wanahabari,

Kulingana na kifungu cha 54(2) cha Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Sura ya 156 kinakataza kuingiza nchini mifugo na mazao yake bila kuwa na kibali nanukuu; “No person shall bring or cause or permit allow to be brought into the country any animal product, contrary to any order or regulation prescribing the introduction of animal products into the country or without animal products inspected and certified in the prescribed manner.” Hivyo kwa kitendo cha Kampuni ya Phoenix Farms kutaka kuingiza nchini vifaranga wa kuku wa mayai 62,730 ni kukiuka Sheria hii.
Ndugu wanahabari,

Aidha, Kanuni ya 26 ya Kanuni za Udhibiti wa Usafirishaji wa Wanyama na Mazao yake ya GN. Na. 28/2007 inabainisha kuwa, “Ikiwa wanyama au mazao ya wanyama yatafika nchini bila kibali na cheti cha afya ya wanyama au mazao ya wanyama, Mkaguzi aliyeko kwenye kituo cha ukaguzi azuie uingizaji wa wanyama au mazao ya wanyama husika nchini. In the event, of any animal or animal products intended for importation arriving without the certificate required as aforesaid, an Inspector shall refuse to allow such animal or animal products to enter Tanzania ….”.

Ndugu wanahabari,

Hivyo, kutokana na tafsiri ya vifungu hivyo viwili hapo juu, vifaranga wa kuku wa mayai 62,730 walioletwa na Kampuni ya Phoenix Farms Limited waliopo katika Uwanja wa Julius Nyerere International Airport (JNIA) upande wa mizigo (cargo) wamezuiliwa kuingizwa nchini kwa kuwa ni mzigo hatarishi. Aidha, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeutaka uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Tawi la Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kuielekeza Kampuni ya Phoenix Farms Limited kuvirudisha vifaranga hivyo nchini Ubeligiji kwa sababu wanaweza kuhatarisha usalama wa kuku nchini. Vilevile, Mkurugenzi wa Kampuni ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited ameelekezwa kuviondosha vifaranga hivyo katika maeneo ya uwanja wa ndege na kuvirudisha alikovitoa.

Ndugu wanahabari,
  • Kama mtakumbuka, Mwaka 2006 Tanzania iliweka zuio (karantini) la uingizaji wa kuku na mazao yake kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Mafua Makali ya Ndege duniani (HPAI). Kutokana na zuio hilo (karantini), nchi yetu imeendelea kuwa salama dhidi ya ugonjwa huo ambao umeathiri nchi nyingi duniani. Ugonjwa wa Mafua Makali ya Ndege huambukiza wanyama na binadamu na hutokea kwa njia ya mlipuko na kusababisha madhara makubwa ikiwemo vifo vingi vya kuku na ndege wa porini. Njia za kudhibiti ugonjwa huu ni pamoja na kuzingatia usafi kwenye mabanda ya kuku (biosecurity measures) na karantini ya kuzuia kuingiza kuku, ndege wengine na mazao yao. Nitoe wito kwa watanzania wote hususan wadau wa kuku kuzingatia Sheria, Kanuni na Miongozo iliyopo ya kudhibiti kuingia na kuenea kwa magonjwa ya kuku nchini hususan Ugonjwa wa Mafua Makali ya Ndege ili kulinda usalama wa kuku, na ndege wengine pamoja na afya ya jamii ya watanzania kwa ujumla.
Asanteni kwa kunisikiliza
Imetolewa na
Profesa Hezron E. Nonga
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI
24 DESEMBA 2022
Hahahah rais Samia walindanganya afungue nchi, na kumdhihaki Dkt Magufuli, naona hivyo vifaranga ni moja ya big failure ya sera ya kufungua nchi ya rais Samia. Sisi wana CCM tunampenda sana, uzuri kila jambo tunamtonya kuwa anahujumiwa na wabaya wake. Swali hivyo vifaranga vitachomwa moto???
 
Sababu kubwa ni gharama kutoendana na bei ya soko ikiwa ni pamoja na uingizwaji wa vifaranga kutoka nje. Na sio ajabu uingizaji huu wenye ukwepaji kodi ni sababu mojawapo ya wafugaji wa ndani kushindwa kuendana na biashara hii na hivyo baadhi yao kuamua kuachana nayo.
Serikali ya awamu ya sita inafungua nchi
 
Labda hukumuelewa yule Mama !! Kuhusu hili la sasa; sheria ifuate mkondo wake.
No Rais Samia alisema ilikuwa makosa kuchoma vifaranga vya kenya, je vya hawa wazungu atavichoma??? Au vitarejeshwa??? Kwa ufupi nchi yetu imekosa dira na muelekeo. Tukiwaambia ni mtu asiyekuwa na info ndiye atakuja kuwekeza Tanzania, nwenye uelewa atachagua na kujiuliza sana kabla ya kuwekeza
 
Madam President akisema anaifungua nchi maana yake ni nini? Maana yake si ni kuwa na soko huria!?

Unampata wapi mwekezaji gani wa nje bila ya kumhakikishia ushindani huru na wenye haki sokoni!?
Hivi uwekezaji huwa unachagua soko la ushindani!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
No Rais Samia alisema ilikuwa makosa kuchoma vifaranga vya kenya, je vya hawa wazungu atavichoma??? Au vitarejeshwa??? Kwa ufupi nchi yetu imekosa dira na muelekeo. Tukiwaambia ni mtu asiyekuwa na info ndiye atakuja kuwekeza Tanzania, nwenye uelewa atachagua na kujiuliza sana kabla ya kuwekeza
Let's wait and see for a proper action to be taken.
 
Sheria haisemi hivyo... haitaki ilo unalo taka... tiisheria, fata sheria... kama tuna taka mabadiliko basi tufanye mabadiliko ya sheria na kanuni zake

Juzi yule mzungu mwenye kiwanda cha kuzalisha vifaranga vya kuku pale moshi alivitia moto au teketeza kwa moto vifaranga vingi sana kwa sababu ya kukosa soko

Leo nashangaa kuna mtu ana ingiza vifaranga takribani 60k, yani mwezi mmoja nazani baada ya yule mwanamama mzungu kuteketeza vifaranga vyake

Na alilalamikia kukosa soko na hasa uingizwaji wa vifaranga kutoka nje...

Hivi vifaranga vipatavyo 62,730 vina gharama ya Tsh. 200,262,706 ambapo kila kimoja ni Tsh. 3,192.4551

Wakati kwetu hapa tuna vifaranga vina uzwa mpaka 800/- na bei ya juu nazani ni 2,500/-

Uingizwaji wa hivyo vifaranga bago vina kodi zake hivyo tutegemee gharama zake kuongezeka kulingana na kodi atakayo chajiwa mnunuzi/muingizaji
Sheria inaweza kurekebishwa, yule bwana nilisoma habari yake, ni wazi hana connection/hajui biashara ya Tz, Mkuu unadhani biashara ya kuku imekuwa kwenye hali ile kweli ? Kila siku Bar kuku zinaliwa,Moshi pale mishikaki ya kuku wanauza mpaka buku

Ndio maana unaona huyu kaingiza kuku wote hawa anajua biashara ni nzuri , yule aliyechoma atakua hakuwa na pesa ya kuvilisha vile vifaranga labda, lakini angevifuga ilikuwa pesa ipo
 
Madam President akisema anaifungua nchi maana yake ni nini? Maana yake si ni kuwa na soko huria!?

Unampata wapi mwekezaji gani wa nje bila ya kumhakikishia ushindani huru na wenye haki sokoni!?
Hivi uwekezaji huwa unachagua soko la ushindani!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha wale viherehere wa kufungua nchi waje haraka sana hapa. Maana wengi comments zao eti aliyeingiza vifaranga aadhibiwe. Unajiuliza swali, je Rais si walimdanganya kuwa eti nchi ilikuwa imefungwa, na wakamuandalia safari na alivyorudi akaitisha vyombo vya habari akijisifia kusema eti nchi ilikuwa imefungwa enzi za Dkt Magufuli wakati yeye huyo huyo rais Samia alitumwa kwenda nje kumuwakilisha na mabalozi duniani kote walitumwa, then eti unakuja kusimama kuutamkia umma eti nchi ilikuwa imefungwa??? Hakika kazi iko kubwa mbeleni. Maana akija rais Mwingine atamwaga kejeli kibao kwa rais Samia. Rais Samia bado anaomuda, amuombe radhi Dkt Magufuli huko aliko amsamehe kwa dhambi ya kumdhihaki na kumdharau otherwise utawala wa rais Samia utaendelea kuonekana ni maigizo
 
Hebu kwanza:

Huyu Professa Hezron E Nonga ni Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, na wakati huo huo ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi?

Kuna maswali kadhaa ya kujiuliza hapa:

Hii Kampuni ya Phoenix hawajui sheria zilizopo zilizotajwa hapo, kiasi kwamba hawakufikiri kabisa kuwa wanaweza kuingia hasara kubwa, au walishajua namna ya kuzunguka hizo sheria, na kwa bahati mbaya sana safari hii ikawa tofauti?

Lakini ukweli ni kwamba, hivyo vifaranga vimekwishaingia Tanzania, hayo mengine yanayosemwa kuvirudisha UBelgiji ni stori tu za vijiweni.
Inawezekana kabisa mwekezaji mwenyewe alijua hivyo na hana mashaka yoyote juu ya vifaranga vyake. Hizo kelele ni kulaza tu akili za wajinga.

Ni hivi karibuni tu pametolewa taarifa za kuzuia uagiza wa vifaranga na mayai ya kutotolesha toka nje na wizara hiyo hiyo kwa sababu za kuwalinda tu wazalishaji wa ndani, ambao sasa bei zao zipo juu sana. Kuna umuhimu wa kuangalia upya zuio hilo lisilokuwa na manufaa kwa sekta hiyo.
 
Tukisema Nchi hii imeshakuwa shamba la Bibi watu wengine wanakataa.
Hivyo vimeshikwa, je, vingapi havijashikwa?
Hata hivi kushikwa kutakuwa na sababu zake ambazo hazielezwi.

Habari ilivyokaa ni kama alikuwa anajua analofanya toka mwanzo.

Hakuna mtu mwenye akili timamu achukue risk yote hiyo (hiyo ni hela ndefu hata kwa wenye ukwasi kupoteza tu hivi hivi).
Anajua vifaranga havirudi ubelgiji, na mambo yatakwisha kimya kimya.
 
Hivi wale wa kibaha walochoma vifaranga kukosa soko ndo Hawa hawa au wengine[emoji848]
 
Vifaranga wanatolew Belgium kuja Tanzania, duh!
 
Sheria haisemi hivyo... haitaki ilo unalo taka... tiisheria, fata sheria... kama tuna taka mabadiliko basi tufanye mabadiliko ya sheria na kanuni zake

Juzi yule mzungu mwenye kiwanda cha kuzalisha vifaranga vya kuku pale moshi alivitia moto au teketeza kwa moto vifaranga vingi sana kwa sababu ya kukosa soko

Leo nashangaa kuna mtu ana ingiza vifaranga takribani 60k, yani mwezi mmoja nazani baada ya yule mwanamama mzungu kuteketeza vifaranga vyake

Na alilalamikia kukosa soko na hasa uingizwaji wa vifaranga kutoka nje...

Hivi vifaranga vipatavyo 62,730 vina gharama ya Tsh. 200,262,706 ambapo kila kimoja ni Tsh. 3,192.4551

Wakati kwetu hapa tuna vifaranga vina uzwa mpaka 800/- na bei ya juu nazani ni 2,500/-

Uingizwaji wa hivyo vifaranga bago vina kodi zake hivyo tutegemee gharama zake kuongezeka kulingana na kodi atakayo chajiwa mnunuzi/muingizaji
Hawa ni Parents stock, nashangaa sana kwa nini anaingiza Parents stock bila kibali, ni uzembe wa kiwango cha mwisho kabisa, yaani wa kulaumu ni mwagizaji wa hao vifaranga
 
Sasa huyu aliyeingiza hivyo vifaranga si wangemuacha tu ili apate hasara? Maana soko la vifaranga hakuna kwa mujibu wa yule mzungu wa Arusha
Ni.mzembe sana huwezi ingiza mzigo huo mkubwa hivyo Bila vibali aisee
 
Back
Top Bottom