SGR Dodoma -Dar yaanza rasmi leo 25 July 2024 usiku huu

Mbeba maono ni Ben Mkapa.

Mchochea maono ni JK wa Msoga.

Mtekeleza maono ni Mwendazake Magufuli

Mtimiliza maono ni yeye Suluhu

Kila mmoja kwa nafasi yake ametenda kwa kiwango fulani.

Tupia picha!
Umemwamini mzee wa Msoga? Hahaha
 
Ukitaja Magufuli kuna watu wanatamani wakutangulize mbele za Muumba lakini ukweli utabaki kuwa ukweli bila uthubutu wake mengi tunayoyaona yasingekuwepo.
Hivi yale makontena ya Makinikia bado yapo pale?
 
Naona Kikwete anapambana sana kwa kucha na meno kuzima uthubutu wa Magufuli wa kuanza ujenzi wa SGR_TZ.
Hata kama maono yalikuwa ya Ben Mkapa, Magufuli alianzisha ujenzi pale ambapo Kikwete alishindwa kuanza. Magufuli anasistahili sifa zote hata kama hampendi.
 
R.I.P CHUMAJPMA
Naamini ungekua hai mpka sasa, tungekua na SGR ya kwenda Kigoma/Kilimanjaro/Mwanza na Mbeya
 
Ukitaja Magufuli kuna watu wanatamani wakutangulize mbele za Muumba lakini ukweli utabaki kuwa ukweli bila uthubutu wake mengi tunayoyaona yasingekuwepo.
Hivi yale makontena ya Makinikia bado yapo pale?
wapuuzi tu
 
nia ni kufuta legacy ya #CHUMAJPM#
 
Maombi yangu kwa watanzania haswaa waliopewa dhamana ya kusimamia huu mradi, kuhakiksiha wanasimamia kwa weledi!mambo yaliyotokea kwenye mradi wa mwendokasi tusingependa kuyaona huku!train zifanyiwe service kwa wakati, majengo yatunzwe, reli zitunzwe!etc
 
Maombi yako ni sahihi
 
Mbeba maono ni Ben Mkapa.

Mchochea maono ni JK wa Msoga.

Mtekeleza maono ni Mwendazake Magufuli

Mtimiliza maono ni yeye Suluhu

Kila mmoja kwa nafasi yake ametenda kwa kiwango fulani.

Tupia picha!
Maono ya kuhamia Dodoma yaliasisiwa na nani? hapo katikati wamepita marais wangapi? uliona hata wamejitikisa kudhubutu? Kubali tu ukweli ulio wazi, bila Magufuli huo mradi mgeishia tu kuuona kwenye TV. usiwape watu sifa wasizostahili...hii pia ni aina flani ya roho ya chuki ulionayo.
 
Yote hii mnakwepa kuusema ukweli ilimradi tu sifa asipewe mwendazake, nikuulize, wazo la kuhamia dodoma liliasisiwa na nani? hapo katikati wamepita marais wangapi? A typical tanzanian ktk ubora wako na roho ya kwa nini?
Si ndo hapo yaani wanaumia kweli wakiona watanzania tunamvyokubali Magufuli
 
Nimepanda hiki chuma Leo siku ya uzinduzi dar Dodoma Express..kitu amaizing tumetoka saa kumi na mbili kamili asubuhi tumefika Dodoma saa nne kasoro , target ilikuwa kufika saa tatu na dk 25, lakini ilichelewa kama dk 20 hivi kutokana na kusubiria treni ya morogoro kupishana. Nadhani huo mpishano ukitatuliwa itatumia masaa matatu na dk 25....
 
Viva Samia, uliikuta reli haijafika hata kilometa 40, sasa mpaka mabehewa yapo, yanatembea
Dooh huu ni zaidi ya unaa jamaa.....mama kakuta mradi upo zaidi ya 60% acha uchawa usio na tija....... magu anafariki almost tuta lilikuwa bahi kipande kidogo tu kilibaki kukamilika......mataluma yalifika kilosa au zaidi.......
 
Upuuzi wa SGR ni ukataji wa tiketi. Wameshindwa nini kufanya watu wanaokata tiketi online waweze ku print tiketi zao huko huko au ziwe kwenye simu na ziwe na QR code? Wanaocheki tiketi kwenye treni wawe ni code reader basi. Mtu unalipia tiketi online bado unalazimika kukaa kwenye mstari ili tiketi yako iwe printed. Sasa kulipia online kunasaidia nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…