Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Shirika la reli nchini, Tanzania Railways Corp limefanya kweli kwa kutoa ratiba ya safari za treni Dar-Dom zitakazoanza Julai 25 na sasa kwa treni ya mwendokasi utaweza kusafiri kwa masaa 3.25 kutoka Stesheni, Dar es Salaam mpaka Dom. Usafiri wa mabasi ya mikoani kawaida hutumia masaa nane.
Nawaona wafanyabiashara wanavyoenda kupunguza gharama za hoteli na Lodge, saa nne anaingia zake Kariakoo na kusubiri treni ya 11 jioni arudi Dom. Nawaona pia wale ndugu zetu waliohamishwa na Magu wakirudi kutembelea familia Ijumaa jioni🙂
Ukipiga hesabu za muda wa check in na umbali wa Airport ya Dar kutoka centre ya mji, kimahesabu ya rasilimali muda na fedha inaweza kuwa ahueni kwenda kukwea treni kuliko pipa..
Nawaona wafanyabiashara wanavyoenda kupunguza gharama za hoteli na Lodge, saa nne anaingia zake Kariakoo na kusubiri treni ya 11 jioni arudi Dom. Nawaona pia wale ndugu zetu waliohamishwa na Magu wakirudi kutembelea familia Ijumaa jioni🙂
Ukipiga hesabu za muda wa check in na umbali wa Airport ya Dar kutoka centre ya mji, kimahesabu ya rasilimali muda na fedha inaweza kuwa ahueni kwenda kukwea treni kuliko pipa..