Miti7
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 1,081
- 1,958
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sijawahi ona huo mkataba mimi ila naamini Rais wetu ni mtu mzalendo Sana,Bondi mnaweka nn maana isije kua km uganda na je tumejipanga kupunguza mi kodi ya ajabu ili nchi jirani warudi kutumia bandari zetu ...maana tunaweza kujenga hiyo bandari ya bagamoyo harafu sera zikawa mbovu ikawa hasara tu kwetu .Hili swala inatakiwa utulivu sana tukikurupuka itakua km maswala ya gas tuliambiwa kua gas ya mtwara ikiianza kuchimbwa swala la umeme litabaki history je mpaka sasa ina faida gani hata hatujui.
Kwa Sasa Malori yanabeba mizigo mingi,Umeshajiuliza kuwa relu ya sasa ina uwezo wa kubeba mzigo kiasi gani na ni kiasi gani chazigo unapita kwenye reli as compared na kile kinachopita kwenye malori?
Kimsingi ulichokifanya ni kama kile kilimo cha matikiti kwenye karatasi.
Uhalisia hauko kama unavuo ongea. Shippers wana prefer malory kuliko train kwa sababu mbalimbali. Google ujielimishe
Khaaa mkuu, labda tutengeneze yetu sasaSiyo mbaya
Ila inafaa iwe dakika 20 hivi au 30
Utapiga je Pesa wakati mchina anakusanya mapato yote,pole pole alikuwa sawa tena sana.Mkuu hata kama Bandari ingekuwa ya Wachina bado SGR ni yetu tutapiga pesa tu,
Basi uwe makini sanaMimi sina mkuu kama unao lete tuujadili hapa,
Mimi nimeonesha analysis yangu hali itakuwaje hapo baadae nimeishia hapo,
Faida ya kusafirisha mizigo ndani na nje ya Tanzania ni kubwa kuliko ile kupakua mizigo,Utapiga je Pesa wakati mchina anakusanya mapato yote,pole pole alikuwa sawa tena sana.
Mkataba ni siri ya Serikali kwa masilahi ya nje mkuuBasi uwe makini sana
Kama hata wewe huo mkataba hujauona basi uwe makini sana hii nchi ni yetu mkileta uhuni tunawaloga tu mjifie huko
Akili kisoda sana hii===
SGR ikikamilika inaweza kubeba mizigo yote ya Bandari ya Dar es Salaam kwa siku 250 Tu,
Kama SGR itakamilika bila ya Bandari ya Bagamoyo kujengwa basi Malori yote ya mizigo mnayoyaona hapa nchini yatalazimika kupaki
Iko hivi,treni moja ya mizigo ya SGR inauwezo wa kubeba Jumla ya Tani elfu 10 karibu sawa na Malori 500 kwa Safari moja,
TRC ikiwa na Treni mbili tu za mizigo zinazopishana kwa kila siku basi tutasafirisha Jumla ya Tani elfu 20 kwa siku moja sawa na Malori 1,000.
Nimejaribu kutafuta wastani wa mizigo iliyopakuliwa pale bandari ya Dar es salaam kati ya mwaka 2016|2020 nimepata ni wastani wa Jumla ya Tani milioni tano ( 5M )
Kwamsiofahamu, 98% ya mizigo yote inayoingia na kutoka Tanzania na nchi jirani inapitia bandari ya Dar es Salaam,
Tujiulize, Kama tani elfu 20 kwa SGR zinaweza kubebwa kwa siku moja kwa kutumia treni mbili za SGR zinazopishana,
Je hizi tani 5M zinazopakuliwa pale bandari ya Dar es salaam kwa mwaka mzima zitabebwa kwa muda gan kwa kutumia hii SGR?
Fanya hivi,gawanya tani 5M kwa tani elfu 20 utapata Jumla ya siku 250 za kuisafirisha mizigo yote ya mwaka ya bandari ya Dar es salaam kwa kutumia SGR,
Mkumbuke kuwa, Safari ya Treni ya Mzigo toka Dar -Mwanza ni wastani wa masaa tisa ( 9 ) wakati Safari ya Lori ni zaidi ya masaa 48,
Lakini pia,bei ya kusafirisha mizigo kwa SGR ni ndogo kuliko ile ya Lori na Usalama wa mzigo kwenye SGR ni mkubwa kuliko ule wa kwenye Lori,
Sikia,Nimfanyabiashara mjinga tu ndio anaweza kuacha kupakia SGR yenye nafasi akapakia mzigo kwenye Lori
Sababu pekee inayoweza kuyanusuru haya Malori yetu ni kuwa na bandari nyingine kubwa itakayokuwa na uwezo mkubwa wa kushusha mizigo mingi zaidi ya ile ya Dar es salaam ili SGR ibebe na isaze na Malori ya bebe pia,
Kama hili halitafanyika kuna watu wengi mnakwenda kukosa ajira zenu hapo baadae kidogo,
Nadhani hii ni moja ya sababu ya kwanini Rais Samia anataka bandari hii ijengwe tena kwa haraka kabla ya kumalizika kwa SGR,
NB, Mnaolalamika kuhusu Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo rudieni tena kusoma andiko hili kwa makini
Ungefafanua kidogo mkuuAkili kisoda sana hii
Entebbe ipo chini ya nani Sasa hivi unajua?Faida ya kusafirisha mizigo ndani na nje ya Tanzania ni kubwa kuliko ile kupakua mizigo,
Wachina watapata nasisi tutapata pia,
Bandari hii mpya itakuwa yapili baada ya ile ya Durban SA,
Unajua mpango mikakati wa Reli?Ungefafanua kidogo mkuu
Entebbe ipo chini ya nani Sasa hivi unajua?
Licha ya tishio la ugaidi Uganda unajua kwann mpaka Sasa Museven yupo TZ?
Ukijua hilo utajua kwann bandari ya Bagamoyo ni upuuzi KWA sas
Sasa Yataendelea kubeba nini?Unajua mpango mikakati wa Reli?
Hivi huo uchumi mnasomeaga wapi nyinyi?
Kweli reli ikikamiliki ndo malori yatapaki?
Umewahi ona Dunia Gani hiyo,Acha mawazo ya kikoloni weweee
Kwani hizo contena zitabebwa na hiyo Reli mpaka mlangoni KWA tajiri?Sasa Yataendelea kubeba nini?
Kaja kuomba hela huyo akakwamue uwanja wa ndege huo,na ndo sababu ya kuja wangu wangu TZ.Hebu fafanua vizuri Mkuu
Mimi nilimaanisha Local & Transit, Haya Malori ya vichochoroni yanaishaje mkuu?Kwani hizo contena zitabebwa na hiyo Reli mpaka mlangoni KWA tajiri?
Je ni mikoa yote Reli imepita?
Endeleeni na hizo siri zenu na kuwaza maslahi ya nje kabla ya maslahi ya ndaniMkataba ni siri ya Serikali kwa masilahi ya nje mkuu
Daaah, Ila namwini sana Mama, Anawatu wazalendo sana, So relaxKaja kuomba hela huyo akakwamue uwanja wa ndege huo,na ndo sababu ya kuja wangu wangu TZ.
KWA tishio la ugaidi lilotokea,Museven asingeweza kuja haraka namna hii akaiacha nchi Zaid ya siku3