Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Ameunguruma Simba, Nchi imetetemeka
Manyang'au yamevimba, Aibu imewashika
Yalijiona miamba, Ile isiyovunjika
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Hawa watu waonevu, Ni watu waso na soni
Matendo yao uovu, Na ghiliba za shetani
Mipango yao mibovu, Kaivunja Freemani
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Nchi imekuwa dampo, La uchafu wa wahuni!
Mambo wayafanya simpo, Kiburi cha Firauni
Wamejifanya madompo, hawamuogopi nani!
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Aibu yetu au yao?, Huu ni msala wao!
Wasaliti wana chao?, Chao ni ujinga wao!
Wameuza utu wao, Kwa uchu tamaa zao!
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Wananchi tunaona, Wananchi tunajua!
Hadaa tumeziona, Inda tunaitambua!
Mambo yao konakona, Akili zao vibua
Hongera sana Mbowe, wewe ni mtu makini!

Wewe umeona wapi, Dhulma ishinde haki?
Kwenye mwanga saa ngapi, Giza likatamalaki?
Maono yao mafupi, Kama yale mafataki.
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Hima sasa wananchi, Kamanda kaweka sawa
Hila zote kazipanchi, mambo sasa sawasawa
Hadaa kapiga tochi, wamebaki kupagawa
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini!
 
Jana Imenifanya Nianze Kufikiria Kujiunga Na CHADEMA, Maamuzi Aliyoyafanya Mbowe Ni Ya Kiume. Barua Walizoandika Kina MDEE ni Ushahidi Tosha Kwamba MWENYEKITI WA TUME TA TAIFA YA UCHAGUZI alitudanganya Watanzania

Kama Kweli Akina Mdee Waliteuliwa Na Chama Chao Isingekuwa Tabu Kufika Mbele Ya Kamati Kuu Na Kujieleza.

Halafu Sikufikiria Hivi Ni Kweli Pale Walipo Apishiwa Sio Bungeni [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
 
Jana Imenifanya Nianze Kufikiria Kujiunga Na CHADEMA, Maamuzi Aliyoyafanya Mbowe Ni Ya Kiume. Barua Walizoandika Kina MDEE ni Ushahidi Tosha Kwamba MWENYEKITI WA TUME TA TAIFA YA UCHAGUZI alitudanganya Watanzania...
Jana endapo mbowe asingewafukuza akina covid 19 wanandungai lazima chadema ingefariki ghafra na kuwa kama TLP NCCR na CUF ya Lipumba, wanachama wa chadema walipanga kuondoka chadema kwa mpigo, lakini kwa Akili kubwa mbowe ameirejeshea heshima zaidi chadema itakuwa imara zaidi na zaidi
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
Maneno haya yalikuwa wakati ule wa slaa yakambuma , yakatokea mengine kuwa wa mzee ndio wapiga kura lakini ukiwaambia tuweke tume huru wanarukaruka kama kitenesi.

Haya wameshinda majimbo yote wamefurahi , fanyeni kazi mnataka chokochoko kwenye vyama vya wenzenu jamni nini tatizo?

Kama wakimama ndio wapiga kura sawa si ndio maana mmeshinda kwanini mnatumia nguvu katika watu mlilowashinda pigeni kazi acheni umama
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
Waende tu wabaki kuwa wanachama wa mahakama, ila Chadema imeshafanikiwa kuwajulisha wananchi na jumuia za kimataifa kuwa haitambui uchafuzi uliofanywa october 28
 
Nlitegemea jana angavamiwa na "POLISISIEMU" na kumzuia asiongee na vyombo vya habari.

CCM wanateseka sana na hivo viti maalum 19 vya chadema, si wangewapa Polisi na TISS hizo nafasi bungeni.
Umaja wa Ulaya huchangia Bajeti ya Tanzania na moja ya mashariti yao makubwa ni razima bunge liwe na vyama vya upinzani ndiyo maana Ndungai kuwanunua covid 19 kienyeji kwa njia haramu za kishetani akiamini uwepo wao Bungeni utawasaidia kupata pesa za misaada toka ulaya
 
Maneno haya yalikuwa wakati ule wa slaa yakambuma , yakatokea mengine kuwa wa mzee ndio wapiga kura lakini ukiwaambia tuweke tume huru wanarukaruka kama kitenesi...
CCM wanatumia pesa za walipa kodi kuwanunua covid 19 wanandungai kwa gharama kubwa badala ya maendeleo ni matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
Who cares hata wawe wabunge hadi 2050, what matters most ni kuwa sio wanachama wa Chadema tena na hawatatumia jina la Chadema bungeni na chochote watakachofanya bungeni Chadema haitakuwa answerable.
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
Wakina mama wapi? Unadhani wangekuwa na hiyo influence wakina mama wasingeandamana kuwaunga mkono? Badala yake wameandamana na kutoa matamko ya kushinikiza wafukuzwe.

Ni kweli uwezekano mkubwa ni kuwa wataendelea kuwa wabunge. Bila shaka watajitahidi kuonyesha kuwa hawajabadilika kwa kuikemea sana serikali na kuzungumzia adha waliyopata mikononi mwake. Watasikilizwa, watapigiwa makofi na wabunge wenzao halafu watapuuzwa.

Mwaka 2025 watahamia CCM lakini uwezekano mkubwa ni kuwa wengi wao hawatapata kitu. Kumbuka wako zaidi ya Halima na wakina Esther. Changamoto kwa wakina Halima ni kuhakikisha 19 wanabaki 19 maana unaweza kukuta wengine waliaminishwa kuwa Mbowe yuko nao.

Amandla...
 
Back
Top Bottom