Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Naliona la muhimu, Hili letu kuridhia,
Kapambana Maalimu, Zenji kaipigania,
Akamwage yake damu, ndicho kilichobakia?
Sefu kawapigania, nyie mmemsaliti!

Akapumzike Sefu, ale sasa kuku wake,
Huyu bwana si dhaifu, alipenda nchi yake,
Kwa hakika amekifu, kuwa wewe naye wake?!
Kwa nini alipigana, eti kuwa hamjui!

Aliye wapigania, kaachwa kwenye mataa,
Wengine mwamchukia, Hamjui yuafaa,
Mawaziri ulizia, nyote amewakataa,
Mtamkumbuka Sefu, Gwiji lile la Zanzibar!

Leo Zanzibar mkoa, macho mmeyatumbua,
Mawaziri mmenoa, Hivi mnajitambua?
Sefu angewaokoa, nchi wakaitambua,
Ilikuwa yarejee, ya wasisi wa Mwungano!
Seif tutamkumbuka,kwa tabia ya uongo
Anapenda kucharuka,wakati moyoni fyongo
Siyo wa kuaminika,fitina mwenye mipango
Cheo alikitamani,kwa nadhiri ya mandevu.
 
Lile Moja saba moja, bandiko lilikuhusu,
Ajabu moja kwa moja, macho hukuyaruhusu,
Ukafanya huna haja, ya kusoma hata nusu,
Unapojitafakari, liko hapa chini tena.

----------------------

View attachment 1643292

Asante sana mkuu, kwa yote na uzi huu,
Umedhihiri ukuu, pasipo hata makuu,
Penye moto wa vifuu, umeileta nafuu,
Wanapokwenda yajenga, tuwape moyo wadada!

Tuwape moyo wadada, wanapokwenda yajenga,
Tukizingatia mada, wizi ule wa kijinga,
Kwa zipi hizo faida, juhudi zipi kuunga?
Wale ni wezi vibaka, wa pet(i)roli na moto!

-----------------------
Kwako wewe m-Senzige, wasalimie Dodoma,
Kwetu bado tuna Ruge, Si peke yake Halima,
Ukawafunde waige, si kwa kupora wa mama,
Kupora pora wa mama, hizo siasa uchwara!

Hizo siasa uchwara, uporaji wa wamama,
Mmefanya biashara,haramu isiyo dhima,
Hii ni kama ya kura, mlizokwiba kigoma!

Kupora pora wa mama, hizo siasa uchwara!
Utampora mmoja,ila si kumi na tisa,
Walikaa kwa pomoja,wakaifanya siasa
Wakaenda kwa umoja,kujiapia vipusa
Hakuna aliyeporwa,wenyewe waliridhia
 
Seif tutamkumbuka,kwa tabia ya uongo
Anapenda kucharuka,wakati moyoni fyongo
Siyo wa kuaminika,fitina mwenye mipango
Cheo alikitamani,kwa nadhiri ya mandevu.


Huku nilikukaribisha. Hata hivyo nisiache kukupa vidonge vyako hapa pia:

Vita sasa mumo mumo, hongera bwana Hamadi,
Walidhani huna kimo, wakuchomeshe mahindi,
Itahitajika Omo, kuusafisha ushindi,
Ndani sasa yuko Sefu, pa kuficha pawe papya!
 

Huku nilikukaribisha. Hata hivyo nisiache kukupa vidonge vyako hapa pia:

Vita sasa mumo mumo, hongera bwana Hamadi,
Walidhani huna kimo, wakuchomeshe mahindi,
Itahitajika Omo, kuusafisha ushindi,
Ndani sasa yuko Sefu, pa kuficha pawe papya!
Hakuna haja ya vita,akae na kutulia
Atakunywa sunvita,hawezi tena fulia
Ya kwake yatamsuta,fujo alitarajia,
Katulizwa kama boli,adunde aende wapi ?

Katulizwa kama boli ,adunde aende wapi ?
Atalishwa na kacholi,tende halua na pipi
Hata akitaka mwali,mrefu hata mfupi
Ndani sasa yupo Sefu,lakini hafurukuti.
 
Hakuna haja ya vita,akae na kutulia
Atakunywa sunvita,hawezi tena fulia
Ya kwake yatamsuta,fujo alitarajia,
Katulizwa kama boli,adunde aende wapi ?

Katulizwa kama boli ,adunde aende wapi ?
Atalishwa na kacholi,tende halua na pipi
Hata akitaka mwali,mrefu hata mfupi
Ndani sasa yupo Sefu,lakini hafurukuti.

Kama we Mzanzibari, basi Sefu hana chake,
Vipi wewe lile gari, Dar siyo Chake chake?
Wamekupiga kabari, ulipe faini yake,
Wajifanya Mtunguja, Kumbe Matumbi wa Bara?

Kuwasemea wa Zenji, wewe nani kakutuma,
Makazi mnayafoji, Hali nyie wa Musoma!
Kuwa we si mkaaji, Mwayajengea Dodoma?
Sefu jembe la Zanziba, mmekwisha poteana

Sasa mwajifanya wao, kuwasemea wa Zenji,
Sefu ni mcheza kwao, atunzwa na wakijiji,
Sefu Yule mtu wao, Siyo wa kwenu Kimbiji,
Senzige wewe ni popo, kumbukumbu ni muhimu!

Linganisha:

Kwangu mimi ni Unguja,Nyumbani kwao Hussein
Hata bara ninakuja,kuongea ya chamani
Tunapanga yenye tija,vyote ndani ya ilani
Siraaj ng'aza siraati,tuondokwe na ghururi.


Pia hapa:

 
Back
Top Bottom