Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania

Senzighe nyumbani wapi, Chatto au usukuma?
Makubwa hayo ni kupi, Au kwenye lile chama?
Kipaumbele ni kipi, ndege au wakulima?
Haya ya vyuma kukaza, leo ndiyo kusikia?
Kwangu mimi ni Unguja,nyumbani kwao Hussein
Hata bara ninakuja,kuyajenga ya chamani
Mojamoja sitataja,nikukabidhi ilani ?
Siraaj ng'aza siraat,tuondokwe na ghururi.
 
Kwangu mimi ni Unguja,nyumbani kwao Hussein
Hata bara ninakuja,kuyajenga ya chamani
Mojamoja sitataja,nikukabidhi ilani ?
Siraaj ng'aza siraat,tuondokwe na ghururi. I

Senzighe mnufaika, wa lile chama dhalimu!
Umekiri kwa hakika, kumbe kwako SiSi emu!
Kwenu kitu kusikika, hadi iwatoke damu!
Ama kweli mwenye shibe, ajuweje wenye njaa!
 
Senzighe mnufaika, wa lile chama dhalimu!
Umekiri kwa hakika, kumbe kwako SiSi emu!
Kwenu kitu kusikika, hadi iwatoke damu!
Ama kweli mwenye shibe, ajuweje

Senzighe mnufaika, wa lile chama dhalimu!
Umekiri kwa hakika, kumbe kwako SiSi emu!
Kwenu kitu kusikika, hadi iwatoke damu!
Ama kweli mwenye shibe, ajuweje wenye njaa!
Sitaapa kwa mitini,wala kwa mizaituni
Manufaa ni ya nini,chama kwetu ni imani
Tajiri na masikini,wote sawa kwa mizani
Ni mlezi wa wanyonge,ng'ara CCM ng'ara.
 
Alijikwaa malenga, uzuri hakuanguka,
Kwamba hakuweza lenga, ni gwiji huyu kumbuka!
Beti saba kazipanga, kwa hakika mtukuka,
Mizani iliyo paa, haimkwepi kombora!

Cc: missile-of-the-nation
Unaipenda na unaijua, professional yako, I like it! Ongeza ubeti wa pili sasa unisifu na mimi kwa kukuonyesha mahali ambapo wewe hukuwa umepaona, nimepaona mimi wakati mimi ni layman
 
Unaipenda na unaijua, professional yako, I like it! Ongeza ubeti wa pili sasa unisifu na mimi kwa kukuonyesha mahali ambapo wewe hukuwa umepaona, nimepaona mimi wakati mimi ni layman

Ewe bwana Makanyaga, wewe ni mmoja wetu,
Kupaona palolega, wewe ni gwiji mwenzetu!
Kwamba hukuja kuiga, ulicheki kila kitu,
Mwunge mkono kombora, kwa kuleta beti zako.

Missile = Kombora

Cc: missile-of-the-nation
 
Sitaapa kwa mitini,wala kwa mizaituni
Manufaa ni ya nini,chama kwetu ni imani
Tajiri na masikini,wote sawa kwa mizani
Ni mlezi wa wanyonge,ng'ara CCM ng'ara.

Chama hiki SiSi emu, ndicho kile cha Nyerere?
Au mnacheza gemu, kwani bora cha Mkwere!
Hiki cha hii awamu, madereva ni ngedere?
Kutwa kucha kukwapua, mkitaka mnauwa!
 
Nawashukuru malenga, nyote mliochangia
Mmesema ya kujenga, kukanya na kuusia
Hakika mmejipanga, Fani maudhui pia
Asante sana vipanga, Saluti nawapigia

Nyundo mmegongelea, kulinda demokrasia
Usaliti kuulea, si nzuri hiyo tabia
Kama msingeongea, Chadema ingejifia
Asante sana vipanga, saluti nawapigia

Tusisahau Mnyika, Na kamati kuu pia
Msimamo walishika, kuuondoa udhia
Wasaliti walitaka, kuipenyeza rupia
Asante sana vipanga, Saluti nawapigia

Ninaitua kalamu, wino umeniishia
Si kwa mwisho umuhimu, mkono kuwapungia
Mabingwa wataalamu, kofia nawavulia
Asante sana vipanga, saluti nawapigia
 
Nawashukuru malenga, nyote mliochangia
Mmesema ya kujenga, kukanya na kuusia
Hakika mmejipanga, Fani maudhui pia
Asante sana vipanga, Saluti nawapigia

Nyundo mmegongelea, kulinda demokrasia
Usaliti kuulea, si nzuri hiyo tabia
Kama msingeongea, Chadema ingejifia
Asante sana vipanga, saluti nawapigia

Tusisahau Mnyika, Na kamati kuu pia
Msimamo walishika, kuuondoa udhia
Wasaliti walitaka, kuipenyeza rupia
Asante sana vipanga, Saluti nawapigia

Ninaitua kalamu, wino umeniishia
Si kwa mwisho umuhimu, mkono kuwapungia
Mabingwa wataalamu, kofia nawavulia
Asante sana vipanga, saluti nawapigia

Asante sana mkuu, kwa yote na uzi huu,
Umedhihiri ukuu, pasipo hata makuu,
Penye moto wa vifuu, umeileta nafuu,
Wanapokwenda yajenga, tuwape moyo wadada!

Tuwape moyo wadada, wanapokwenda yajenga,
Tukizingatia mada, wizi ule wa kijinga,
Kwa zipi hizo faida, juhudi zipi kuunga?
Wale ni wezi vibaka, wa pet(i)roli na moto!

-----------------------
Kwako wewe m-Senzige, wasalimie Dodoma,
Kwetu bado tuna Ruge, Si peke yake Halima,
Ukawafunde waige, si kwa kupora wa mama,
Kupora pora wa mama, hizo siasa uchwara!

Hizo siasa uchwara, uporaji wa wamama,
Mmefanya biashara,haramu isiyo dhima,
Hii ni kama ya kura, mlizokwiba kigoma!
Kupora pora wa mama, hizo siasa uchwara!

cc: senzighe , missile-of-the-nation .
 
Stori za mbowe nahao makamanda wake inanikumbusha zile stori za kibwetele nawaumini wake. Wote wanaakili zinazofanana
 
Stori za mbowe nahao makamanda wake inanikumbusha zile stori za kibwetele nawaumini wake. Wote wanaakili zinazofanana

Za jiwe na mataga au buku 7 zinakukumbusha lolote?

Au zinakukumbusha umburula tu?
 
Chama hiki SiSi emu, ndicho kile cha Nyerere?
Au mnacheza gemu, kwani bora cha Mkwere!
Hiki cha hii awamu, madereva ni ngedere?
Kutwa kucha kukwapua, mkitaka mnauwa!
Ndiyo chama kilekile,cha Nyerere juliasi
Sera zake zilezile,za kukataa uasi
Ngedere ni kwenu kule,Vibaraka majasusi
Kama hambadliki ,dola kwenu marufuku
 
Ndiyo chama kilekile,cha Nyerere juliasi
Sera zake zilezile,za kukataa uasi
Ngedere ni kwenu kule,Vibaraka majasusi
Kama hambadliki ,dola kwenu marufuku

CCM ya Nyerere, Siyo hii m-Senzige!
Hata ile ya Mkwere, haikuwa ya kis*nge!
CCM ya ngedere, ni hawa hiki kilinge!
Leo tuna matabaka, awali hayakuwapo!

Umeyasema mwenyewe, sisi daraja la pili,
Ati ili kuwa yawe, hadi nyie mkubali!
Kwani nyie ni wenyewe, au lau madalali?
Kwamba dola marufuku, dawa yenu yachemka!
 
CCM ya Nyerere, Siyo hii m-Senzige!
Hata ile ya Mkwere, haikuwa ya kis*nge!
CCM ya ngedere, ni hawa hiki kilinge!
Leo tuna matabaka, awali hayakuwapo!

Umeyasema mwenyewe, sisi daraja la pili,
Ati ili kuwa yawe, hadi nyie mkubali!
Kwani nyie ni wenyewe, au lau madalali?
Kwamba dola marufuku, dawa yenu yachemka!
Astaghfirullah laadhim,Ashakum vina vyako
Lugha stara muhim,tughani yenye mashiko
Mwajitoa ufaham,kwenu mmekosa miiko
Eti mnataka dola ,midomo yenu michafu.

Dola gani mnataka,kwanza nendeni jandoni
Wawatoe majitaka,adabu wakufunzeni
Mkirudi mnawaka,akili zimesheheni
Bado hamjakomaa,saizi yenu mitaa.
 
Wanaenda fungua kesi mahakama itazuia kufutwa kwao sababu kesi inasikilizwa na kesi itaenda mpaka 2025 na baada ya hapo wataenda sisiemu, loser ni chadema! Mdee, bulaya, matiko wana influence kubwa sana kwa kina mama, ambao ndio wapigaji kura wakubwa..
Watayamaliza. Mark my words
 
Astaghfirullah laadhim,Ashakum vina vyako
Lugha stara muhim,tughani yenye mashiko
Mwajitoa ufaham,kwenu mmekosa miiko
Eti mnata dola ,midomo yenu michafu.

Dola gani mnataka,kwanza nendeni jandoni
Wawatoe majitaka,adabu wakufunzeni
Mkirudi mnawaka,akili zimesheheni
Bado hamjakomaa,saizi yenu mitaa.

Ya Nyerere siyo hii, ati sisi au nyie,
Mnatutaka utii, hata mkatufukie?
Ya kuwa hatuingii, masikio msikie,
Sisi daraja la pili, staha ipi mwataka!

Staha ipi mwataka, sisi daraja la pili?
Haki zetu twazitaka, hili kwa hali na mali,
Ni ya umma madaraka, sote tunastahili,
Kenge kwenu kusikia, mtoke damu sikio!
 
Ya Nyerere siyo hii, ati sisi au nyie,
Mnatutaka utii, hata mkatufukie?
Ya kuwa hatuingii, masikio msikie,
Sisi daraja la pili, staha ipi mwataka!

Staha ipi mwataka, sisi daraja la pili?
Haki zetu twazitaka, hili kwa hali na mali,
Ni ya umma madaraka, sote tunastahili,
Kenge kwenu kusikia, mtoke damu sikio!
Haki hampati katu,kama hamna adabu
Akili zenu fyatu,kila siku majaribu
Mtavisaga viatu,Ufipa hadi bububu
Hamtapata kitu Ng'o,mtakaa msubiri.
 
Ameunguruma Simba, Nchi imetetemeka
Manyang'au yamevimba, Aibu imewashika
Yalijiona miamba, Ile isiyovunjika
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Hawa watu waonevu, Ni watu waso na soni
Matendo yao uovu, Na ghiliba za shetani
Mipango yao mibovu, Kaivunja Freemani
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Nchi imekuwa dampo, La uchafu wa wahuni!
Mambo wayafanya simpo, Kiburi cha Firauni
Wamejifanya madompo, hawamuogopi nani!
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Aibu yetu au yao?, Huu ni msala wao!
Wasaliti wana chao?, Chao ni ujinga wao!
Wameuza utu wao, Kwa uchu tamaa zao!
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Wananchi tunaona, Wananchi tunajua!
Hadaa tumeziona, Inda tunaitambua!
Mambo yao konakona, Akili zao vibua
Hongera sana Mbowe, wewe ni mtu makini!

Wewe umeona wapi, Dhulma ishinde haki?
Kwenye mwanga saa ngapi, Giza likatamalaki?
Maono yao mafupi, Kama yale mafataki.
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini

Hima sasa wananchi, Kamanda kaweka sawa
Hila zote kazipanchi, mambo sasa sawasawa
Hadaa kapiga tochi, wamebaki kupagawa
Hongera sana Mbowe, Wewe ni mtu makini!
ndan ya miaka 15 ntakua waziri mkuu
 
Haki hampati katu,kama hamna adabu
Akili zenu fyatu,kila siku majaribu
Mtavisaga viatu,Ufipa hadi bububu
Hamtapata kitu Ng'o,mtakaa msubiri.

Aliyasema kaburu, kule Afrika Kusini,
Kuja nyie kuwa huru, yafuteni akilini!
Hata nyie makimburu, makwenu ni jalalani!
Alikotoka Kabundi, hakika mtarajea!
 
Back
Top Bottom