Shangazi Fatma Karume afika mbele ya kikosi kazi kutoa maoni yake kuhusu mambo ya katiba na mengineyo

Shangazi Fatma Karume afika mbele ya kikosi kazi kutoa maoni yake kuhusu mambo ya katiba na mengineyo

Wanachokifanya Zitto na Fatma Karume ni kitu kisicho na mantiki

Niweke wazi, kwenda kutoa maoni, aina ya maoni ni haki yao na isihojiwe na mtu yoyote

Tatizo ni hili, walitakiwa wajiulize;
Maoni ya Wananchi kupitia tume ya Mzee Warioba yanamatatizo gani?
Kikosi kazi kimeundwa kwa utaratibu gani wa katiba?
Tatu, nani anahakiki maoni yanayotolewa yapo kwenye rekodi?

Kikosi kazi kilisema katiba isubiri.2025. kwa Mujibu wa Prof Lipumba aliyekuwa ndani kama Zitto hayakujadiliwa.

Mwisho wa siku 'uzushi' ukaingizwa katika ripoti na kujenga uhalali, vyama vimesema hadi 2025
Zitto anajua huu ni uharamia kwasababu hakuweza kudhibiti wala kukemea uongo huo.

Fatma anakwenda kujenga uhalali akijua maoni yake hayawezi kuwekwa katika mizani sawa na maoni yaliyotengenezwa tayari yanayotafutiwa majibu

Mwisho Fatma atajikuta analalama kama ambavyo Lipumba analalama lakini bila kufanya lolote

Kuwemo katika kikosi kazi au kutoa maoni katika kikosi kazi ni kujenga ''legitimacy' ya kikozi kazi ambayo ni utapeli tu wakati huo huo waki deligitimize maoni ya Wananchi kupitia Warioba

Nitashangaa sana nitakapomsikia Fatma akizungumzia tena Katiba! yeye keshaungana na wasiotaka kwa kuwajengea uhalali na uwezo wa kuendelea. Fatma , Zitto katika boti moja

Jiulize kwanini Msajili anatoa hiyo picha! kuna hoja hapo itakayotumiwa na Fatma ni sehemu yake

JokaKuu Tindo
1.Kwa mujibu wa katiba Rais ana uwezo wa kuunda ofisi/Taasisi yoyote katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania atakayoona inafaa

2.Rasimu ya Warioba ilishauawa na rasimu ya katiba pendekezwa ya Chenge/Samwel Sitta, na ni rasimu ambayo iko kwa mujibu wa sheria kama kweli tukiamua kufuata hiyo sheria unayoisema wewe Kwa hiyo lazima tuanze tena somewhere na kama busara za rais zimemtuma twende na kikosi kazi so be it, kama humtaki rais subiri 2025 umpigie kura ya kumtoa madarakani uweke mwingine atakayerudisha mchakato kwa staili unayoitaka wewe.

3.Nchi lazima isonge mbele, Warioba alikusanya mawazo ya watu laki 3, huenda kikosi kazi kikakusanya mawazo ya watu milioni, who knows?

4. Huenda kikosi kazi kikachukua mawazo mazuri ya tume ya warioba, mawazo mazuri yaliyomo kwenye rasimu pendekezwa ya chenge, mawazo mazuri yaliyomo kwenye katiba ya mwaka 1977, Na mawazo MAPYA na kusaidia kupata katiba bora zaidi

5. Kikosi kazi hakihusu ishu ta katiba mpya peke yake bali kina mandate ya mambo mengi sana, ikiwemo kutoa mapendekezo ya namna ya kurekebisha sheria za chaguzi, etc
 
1.Kwa mujibu wa katiba Rais ana uwezo wa kuunda ofisi/Taasisi yoyote katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania atakayoona inafaa

2.Rasimu ya Warioba ilishauawa na Katiba pendekezwa ya Chenge/Samwel Sitta, na ni katiba ambayo iko kwa mujibu wa sheria kama kweli tukiamua kufuata hiyo sheria unayoisema wewe Kwa hiyo lazima tuanze tena somewhere na kama busara za rais zimemtuma twende na kikosi kazi so be it, kama humtaki rais subiri 2025 umpigie kura ya kumtoa madarakani uweke mwingine atakayerudisha mchakato kwa staili unayoitaka wewe.

3.Nchi lazima isonge mbele, Warioba alikusanya mawazo ya watu laki 3, huenda kikosi kazi kikakusanya mawazo ya watu milioni, who knows?

4. Huenda kikosi kazi kikachukua mawazo mazuri ya tume ya warioba, mawazo mazuri yaliyomo kwenye rasimu pendekezwa ya chenge, mawazo mazuri yaliyomo kwenye katiba ya mwaka 1977, Na mawazo MAPYA na kusaidia kupata katiba bora zaidi

5. Kikosi kazi hakihusu ishu ta katiba mpya peke yake bali kina mandate ya mambo mengi sana, ikiwemo kutoa mapendekezo ya namna ya kurekebisha sheria za chaguzi, etc
Nadhani wale wanaodai katiba mpya wanajaribu kuliepusha Taifa na Mambo Kama hayo ya kufanya Mambo makubwa ya Nchi kwa utashi wa mtu mmoja.

1;-kamati zile za akina mzee Warioba zilipoundwa kwa msingi wa sheria iliyotokana na Bunge, Rais wa kipindi hicho hakuwa na mamlaka hayo ya kuiunda ile tume Kama ofisi tu?

2:-unasema hicho kikosi kazi kina fanya kazi ya kurekebisha sheria zingine, je sheria zingine zote zimekuwa zikirekebishwa kwa mtindo gani? Hapakuwa na idara yoyote kwa mwanasheria mkuu wa serikali inayohusika na Hilo?

3:- umemjibu mdau kuwa asubiri 2025 amtoe Rais madarakani ili amuweke Rais mwingine ili afanye marekebisho kwa njia aitakayo mdau hapo juu,vipi nae Rais atakae kuja akifanya kwa utashi wake tofauti kabisa na huyu wa Sasa na ikawa tofauti na utaratibu wa kisheria anaopendekeza mdau.kwanini katika Jambo kubwa Kama hili isiwepo sheria inayoongoza Jambo Hilo ili ajaye yeyote afuate sheria itakavyo?

4:-unasema mzee Warioba na tume yake walihoji watu laki 3, who knows hii yaweza hoji watu milioni?.. kwa msingi huo waweza kuwa unamaanisha kuwa maoni Yale mengine yaweza kuwa yamepitwa na wakati,ok fine.kumbuka kikosi kazi hiki kimepewa miaka 9 kifanye kazi yake,baada ya hapo tunaamini mheshiwa Rais atakuwa keshamaliza mhula wake wa pili,aweza kuwepo Rais mwingine,na yeye asipopendezwa na mchakato wa mwenzake,ataanzisha wa kwake wa miaka 10,hatutamaliza Jambo Hilo kamwe

5 :- Ni maoni yangu kuwa Bunge halitakiwi kukaa kimya juu ya Jambo hili kubwa linalofanyika bila lenyewe kujua.maana hiki kikosi kazi kimeundwa kuwatuliza wale wanaonadi maridhiano (TCD ya zito kipindi hicho) ili wasiendelee kupiga kelele lakini hakuna Nia ya dhati ndani ya kikosi hicho
 
1.Kwa mujibu wa katiba Rais ana uwezo wa kuunda ofisi/Taasisi yoyote katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania atakayoona inafaa

2.Rasimu ya Warioba ilishauawa na Katiba pendekezwa ya Chenge/Samwel Sitta, na ni katiba ambayo iko kwa mujibu wa sheria kama kweli tukiamua kufuata hiyo sheria unayoisema wewe Kwa hiyo lazima tuanze tena somewhere na kama busara za rais zimemtuma twende na kikosi kazi so be it, kama humtaki rais subiri 2025 umpigie kura ya kumtoa madarakani uweke mwingine atakayerudisha mchakato kwa staili unayoitaka wewe.

3.Nchi lazima isonge mbele, Warioba alikusanya mawazo ya watu laki 3, huenda kikosi kazi kikakusanya mawazo ya watu milioni, who knows?

4. Huenda kikosi kazi kikachukua mawazo mazuri ya tume ya warioba, mawazo mazuri yaliyomo kwenye rasimu pendekezwa ya chenge, mawazo mazuri yaliyomo kwenye katiba ya mwaka 1977, Na mawazo MAPYA na kusaidia kupata katiba bora zaidi

5. Kikosi kazi hakihusu ishu ta katiba mpya peke yake bali kina mandate ya mambo mengi sana, ikiwemo kutoa mapendekezo ya namna ya kurekebisha sheria za chaguzi, etc
Siku njema huonekana asubuhi.

Lipumba amesema kuwa hawakuwahi kukubaliana kuwa mchakato wa Katiba Mpya uanze 2025. Naamini alisema ukweli kwa sababu hamna aliyejitokeza kumpinga. Tutawaaminije kama waliweza kukaa kimya wakati wamewekewa maneno kinywani katika jambo la msingi kama hilo? Inavyoelekea hawa hawana nia ya dhati ya kutilia maanani mawazo ya wadau bali wako kuhalilisha msimamo wa aliyewateua ambae amesema bayana kuwa huu sio wakati wa kujadili Katiba Mpya.

Kama wameweza kusema uongo kwenye hoja ya msingi ya Katiba Mpya tutawaamini vipi kwenye hizo nyingine unazosema na zenyewe watazijadili? Mpaka sasa hivi mawingu yametanda na hamna dalili kuwa siku itakuwa njema.

Fatma amewapa uhalali ambao mwenzake amekataa.

Hivi kweli unaamini kuwa raia hana haki ya kumkosoa rais wake baada ya uchaguzi kupita? Uchaguzi ambao ukifanyika chini ya hii Katiba iliyopo utakuwa wa haki au la kutegemea utashi wa Rais!

Amandla...
 
Siku njema huonekana asubuhi.

Lipumba amesema kuwa hawakuwahi kukubaliana kuwa mchakato wa Katiba Mpya uanze 2025. Naamini alisema ukweli kwa sababu hamna aliyejitokeza kumpinga. Tutawaaminije kama waliweza kukaa kimya wakati wamewekewa maneno kinywani katika jambo la msingi kama hilo? Inavyoelekea hawa hawana nia ya dhati ya kutilia maanani mawazo ya wadau bali wako kuhalilisha msimamo wa aliyewateua ambae amesema bayana kuwa huu sio wakati wa kujadili Katiba Mpya.

Kama wameweza kusema uongo kwenye hoja ya msingi ya Katiba Mpya tutawaamini vipi kwenye hizo nyingine unazosema na zenyewe watazijadili? Mpaka sasa hivi mawingu yametanda na hamna dalili kuwa siku itakuwa njema.

Fatma amewapa uhalali ambao mwenzake amekataa.

Amandla...
Sasa wewe unamuamini Lipumba mtu aliyeacha uenyekiti wa CUF huku dunia nzima ikimuona ila baadae akaja na kudai kuwa yeye bado ni mwenyekiti halali?
Asiye na credibility si wa kumuamini katika mambo makubwa huenda anacheza trick zilezile alizozizoea
 
Sasa wewe unamuamini Lipumba mtu aliyeacha uenyekiti wa CUF huku dunia nzima ikimuona ila baadae akaja na kudai kuwa yeye bado ni mwenyekiti halali?
Asiye na credibility si wa kumuamini katika mambo makubwa huenda anacheza trick zilezile alizozizoea
Wasio na credibility ni wale walioshindwa kumsahihisha kama alisema uongo. Hata saa mbovu hupatia muda mara mbili kwa siku.

Amandla ...
 
Nadhani wale wanaodai katiba mpya wanajaribu kuliepusha Taifa na Mambo Kama hayo ya kufanya Mambo makubwa ya Nchi kwa utashi wa mtu mmoja.

1;-kamati zile za akina mzee Warioba zilipoundwa kwa msingi wa sheria iliyotokana na Bunge, Rais wa kipindi hicho hakuwa na mamlaka hayo ya kuiunda ile tume Kama ofisi tu?

2:-unasema hicho kikosi kazi kina fanya kazi ya kurekebisha sheria zingine, je sheria zingine zote zimekuwa zikirekebishwa kwa mtindo gani? Hapakuwa na idara yoyote kwa mwanasheria mkuu wa serikali inayohusika na Hilo?

3:- umemjibu mdau kuwa asubiri 2025 amtoe Rais madarakani ili amuweke Rais mwingine ili afanye marekebisho kwa njia aitakayo mdau hapo juu,vipi nae Rais atakae kuja akifanya kwa utashi wake tofauti kabisa na huyu wa Sasa na ikawa tofauti na utaratibu wa kisheria anaopendekeza mdau.kwanini katika Jambo kubwa Kama hili isiwepo sheria inayoongoza Jambo Hilo ili ajaye yeyote afuate sheria itakavyo?

4:-unasema mzee Warioba na tume yake walihoji watu laki 3, who knows hii yaweza hoji watu milioni?.. kwa msingi huo waweza kuwa unamaanisha kuwa maoni Yale mengine yaweza kuwa yamepitwa na wakati,ok fine.kumbuka kikosi kazi hiki kimepewa miaka 9 kifanye kazi yake,baada ya hapo tunaamini mheshiwa Rais atakuwa keshamaliza mhula wake wa pili,aweza kuwepo Rais mwingine,na yeye asipopendezwa na mchakato wa mwenzake,ataanzisha wa kwake wa miaka 10,hatutamaliza Jambo Hilo kamwe

5 :- Ni maoni yangu kuwa Bunge halitakiwi kukaa kimya juu ya Jambo hili kubwa linalofanyika bila lenyewe kujua.maana hiki kikosi kazi kimeundwa kuwatuliza wale wanaonadi maridhiano (TCD ya zito kipindi hicho) ili wasiendelee kupiga kelele lakini hakuna Nia ya dhati ndani ya kikosi hicho
Rais anaweza kuunda taasisi yoyote ya kumshauri chochote kwa mujibu wa sheria ila kuupokea au kuukataa ushauri ni haki yake pia.

Kikosi kazi kitamsaidia rais ushauri ambao utaisaidia serikali yake kuboresha sheria mbalimbali za mambo nyeti ya nchi ikiwemo hiyo sheria ya mabadiliko ya katiba. Kama hutakibaliana na rais basi
1. Subiri 2025 upige kura ya kumtoa Madarakani au labda nature ichukue nafasi yake

2. Unaweza kuikataa rasimu atakayokuja nayo kwenye kura za maoni
 
Tena haraka sana maana wanatumia kodi tulizolipa , zoezi hili linatakiwa kuwa live mubashara TBC na vituo vingine vya televisheni vya binafsi pia online tujue zoezi hili muonendo wake ni kwa manufaa ya wananchi wote au ni kwa ajili ya kakikundi cha watu wachache wa chama fulani na siyo kwa manufaa ya taifa letu na raia wote bila kujali vyama vya siasa.
Nafikiri ipo haja ya kuangalia mienendo ya namna wananchi wanavyoreact kulingana na dhamira njema ya serikali katika kutuletea maendeleo endelevu, ili kila mtu aonje keki tamu ya Taifa, zoezi haliwezi kuwa mubashara kulingana na katiba iliyopo, wale wengine walisusa wakatoka bungeni je waliwaacha watu wengine kwenye kile chama kilichoshika hatamu waendeleze agenda yao? Jibu ni no, kwna hiyo tuiachie serikali iliyopo madarakani itupe directions, our GOD IS ORGANISED,
(UKIONA MTU NYUMA YAKO MSITUNI PEKE YAKO AMESHIKA PANGA,MUNDU,KOLEO,BISIBISI,KISU,BUNDUKI, NA MBELE YAKO AMESHIKA PANGA,MUNDU,KOLEO,BISIBISI,KISU,BUNDUKI Utafanya nini?
Mshirikishe Mungu,tafakari, omba hekima kwa Mungu na Mungu aonae sirini atatubariki kama Taifa
KOTAPINI, KUINGIA KWA NYUNDO KUTOKA KWA NYUNDO!!!
 
Jumuiya ya kimataifa ina iangalia na kufuatilia mwenendo wa Tanzania chini ya awamu 6 kwa karibu sana kuona kama utawala wa sasa una hila na hadaa au inasema na kutenda vile ilivyoridhia masuala 252 mbele ya wadau wa maendeleo Geneva Uswisi kuhusu haki.
Ndugu yangu Bagamoyo,sisi Watanzania tunapenda sana kupuuzia mambo/kusahau haraka sana.Hii yote ni kwa sababu watu wote wamekubali kuimbishwa nyimbo hata wasizozifahamu na CCM tangia Uhuru wa Tanganyika chini ya TANU.
Tuliaminishwa kuwa fikra za mtawala ndiyo zidumu badala ya kuongozwa na malengo mapana ya Ustawi wa Raia kupitia raslimali zilizopo.
Badala ya kuwa na Dira ya Taifa tukaanza kuunganishwa na Zanzibar kinadharia na hadi leo tunataabishana juu ya muungano huo.Gharama ya kuulinda wamebebeshwa wananchi ambao hawafaidiki moja kwa moja na muunganiko uliopo.Tunapoteza raslimali nyingi kwenye mambo ya kinadharia mengi tu.Mara watu wanalinda legacy huku wakilia vyuma vimekaza.
Haya yanayotokea yote,rushwa,uonevu,uvunjifu wa Haki za binadamu yanafanyika kwa maelekezo ya wasiojulikana ili watawala wasihojiwe hojiwe mambo ya msingi.Unatengeneza tatizo halafu unajitokeza kutatua-sielewi tunamdanganya nani na kwa faida ya nani hasa.Nguvu kubwa inatumika watu kubaki madarakani.Baada tu ya uchafuzi mkuu kampeni za uchafuzi ujao zinaanza.Hatuna raslimali za kuendesha nchi lakini huduma kwa watawala ni 100%.
Duh.Naomba niishie hapo kwa kusisitiza kuhusu dai la Katiba Mpya.
 
Rais anaweza kuunda taasisi yoyote ya kumshauri chochote kwa mujibu wa sheria ila kuupokea au kuukataa ushauri ni haki yake pia.

Kikosi kazi kitamsaidia rais ushauri ambao utaisaidia serikali yake kuboresha sheria mbalimbali za mambo nyeti ya nchi ikiwemo hiyo sheria ya mabadiliko ya katiba. Kama hutakibaliana na rais basi
1. Subiri 2025 upige kura ya kumtoa Madarakani au labda nature ichukue nafasi yake

2. Unaweza kuikataa rasimu atakayokuja nayo kwenye kura za maoni
Mimi naona mama kuna kitu anawapiga chenga sukuma Gang hapa🤣🤣🤣
 
Wanachokifanya Zitto na Fatma Karume ni kitu kisicho na mantiki

Niweke wazi, kwenda kutoa maoni, aina ya maoni ni haki yao na isihojiwe na mtu yoyote

Tatizo ni hili, walitakiwa wajiulize;
Maoni ya Wananchi kupitia tume ya Mzee Warioba yanamatatizo gani?
Kikosi kazi kimeundwa kwa utaratibu gani wa katiba?
Tatu, nani anahakiki maoni yanayotolewa yapo kwenye rekodi?

Kikosi kazi kilisema katiba isubiri.2025. kwa Mujibu wa Prof Lipumba aliyekuwa ndani kama Zitto hayakujadiliwa.

Mwisho wa siku 'uzushi' ukaingizwa katika ripoti na kujenga uhalali, vyama vimesema hadi 2025
Zitto anajua huu ni uharamia kwasababu hakuweza kudhibiti wala kukemea uongo huo.

Fatma anakwenda kujenga uhalali akijua maoni yake hayawezi kuwekwa katika mizani sawa na maoni yaliyotengenezwa tayari yanayotafutiwa majibu

Mwisho Fatma atajikuta analalama kama ambavyo Lipumba analalama lakini bila kufanya lolote

Kuwemo katika kikosi kazi au kutoa maoni katika kikosi kazi ni kujenga ''legitimacy' ya kikozi kazi ambayo ni utapeli tu wakati huo huo waki deligitimize maoni ya Wananchi kupitia Warioba

Nitashangaa sana nitakapomsikia Fatma akizungumzia tena Katiba! yeye keshaungana na wasiotaka kwa kuwajengea uhalali na uwezo wa kuendelea. Fatma , Zitto katika boti moja

Jiulize kwanini Msajili anatoa hiyo picha! kuna hoja hapo itakayotumiwa na Fatma ni sehemu yake

JokaKuu Tindo
Mimi nadhani Fatuma kama nguri wa sheria na haki za binadamu atawapa nondo za kutosha.

Si vizuri kuwasusia hao watu na genge lao. Bora kuwafata huko.huko.
 
Nadhani wale wanaodai katiba mpya wanajaribu kuliepusha Taifa na Mambo Kama hayo ya kufanya Mambo makubwa ya Nchi kwa utashi wa mtu mmoja.

1;-kamati zile za akina mzee Warioba zilipoundwa kwa msingi wa sheria iliyotokana na Bunge, Rais wa kipindi hicho hakuwa na mamlaka hayo ya kuiunda ile tume Kama ofisi tu?

2:-unasema hicho kikosi kazi kina fanya kazi ya kurekebisha sheria zingine, je sheria zingine zote zimekuwa zikirekebishwa kwa mtindo gani? Hapakuwa na idara yoyote kwa mwanasheria mkuu wa serikali inayohusika na Hilo?

3:- umemjibu mdau kuwa asubiri 2025 amtoe Rais madarakani ili amuweke Rais mwingine ili afanye marekebisho kwa njia aitakayo mdau hapo juu,vipi nae Rais atakae kuja akifanya kwa utashi wake tofauti kabisa na huyu wa Sasa na ikawa tofauti na utaratibu wa kisheria anaopendekeza mdau.kwanini katika Jambo kubwa Kama hili isiwepo sheria inayoongoza Jambo Hilo ili ajaye yeyote afuate sheria itakavyo?

4:-unasema mzee Warioba na tume yake walihoji watu laki 3, who knows hii yaweza hoji watu milioni?.. kwa msingi huo waweza kuwa unamaanisha kuwa maoni Yale mengine yaweza kuwa yamepitwa na wakati,ok fine.kumbuka kikosi kazi hiki kimepewa miaka 9 kifanye kazi yake,baada ya hapo tunaamini mheshiwa Rais atakuwa keshamaliza mhula wake wa pili,aweza kuwepo Rais mwingine,na yeye asipopendezwa na mchakato wa mwenzake,ataanzisha wa kwake wa miaka 10,hatutamaliza Jambo Hilo kamwe

5 :- Ni maoni yangu kuwa Bunge halitakiwi kukaa kimya juu ya Jambo hili kubwa linalofanyika bila lenyewe kujua.maana hiki kikosi kazi kimeundwa kuwatuliza wale wanaonadi maridhiano (TCD ya zito kipindi hicho) ili wasiendelee kupiga kelele lakini hakuna Nia ya dhati ndani ya kikosi hicho
Ahsante sana kwanza kwa majibu yenye mantiki na pili kwa kurahisishia kazi ya kutomjibu Missile of the Nation bandiko#44

Sitaki ku-'quote' chochote nisije nikachenjua hoja tena zenye nguvu. Nitupie senti sumuni

Missile of the Nation anasema ''Rais atapokea ushauri lakini hatalazimika kuufuta'
Kikosi kazi kinaweza kumpa ushauri kama hautaki hataufuata. Upo Missile of the Nation !

Pili, Missile anasema Raisa ana mamlaka ya kuunda ofisi/taasisi.
Kwa mtazamo wake Rais anaweza kuunda taasisi na kuiita Bunge kwasababu tu ana mamlaka.

Haya ndiyo tunayotaka yarekebishwe katika katiba. kumpa rais 'blank cheque' kunaweza kutumiwa vibaya kama missile of Nationa anavyosema

Tatu, Rais alisema suala la katiba pembeni kwanza tujenge uchumi.
Baada ya pressure akakutana na vyama vya siasa kutaka wajadili demokrasia n.k.

Hii ilikuwa gia ya kuunda kikosi kazi
Hakukuwepo na tatizo la demokrasia, kulikuwa na tatizo la kukiukwa kwa sheria kama vile marufuku ya mikutano . Mkuatano wa Zitto huo ndio ulizaa kikosi kazi

Kikosi kazi kinakusanya maoni sijui ni yapi kwasababu ya tume ya Warioba yapo.

Yote aliyoagiza Rais katika kuunda kikosi kazi ndiyo yalikuwa taarifa ya kikosi kazi

Lipumba kasema wamechomeka UONGO, hakuna hata mmoja akiwemo Zitto aliyesema 'sikweli'.

Tuhuma za Lipumba zinaondoa credibility na hazikupaswa kukaliwa kimya, lakini kama ndio ukweli kuna jibu gani mbadala!

Ndiyo maana tunasema tayari kuna maoni ya kikosi kazi, kinachofanyika ni kuhalalisha kwa kutumia mikutano. Hakuna anayejua nini kinaongelewa kwahiyo kikosi kazi kitafanya kinavyojua

Kwa Fatma na Zitto kuwemo katika kikosi kazi au kutoa maoni ni kuhalalisha 'maoni yaliyopo' tayari (legitimize). Kama ingalikuwa mtaani tungesema wanashiriki kutakasa pesa

Mtu yoyote anayekwenda mbele ya kikosi kazi asitegemee maoni yake kuwa na maana, anachokifanya awaye ni kutoa uhalali wa kikosi kazi kutengeneza maoni na kuyafanya ya Umma.

Wanaweza kufanikiwa kwa muda lakini in long run itakuwa tatizo kubwa sana, umma haupo nao
 
Mimi nadhani Fatuma kama nguri wa sheria na haki za binadamu atawapa nondo za kutosha.

Si vizuri kuwasusia hao watu na genge lao. Bora kuwafata huko.huko.
Sijua kama watu wanaelewa hoja

Fatma anaweza kutoa nondo, je, nondo hizo zitasaidia nini ikiwa hazitafanyiwa kazi au zitabadilishwa? Lipumba yumo kasema kilichosemwa ni UONGO.
Kwamaneno mengine Mkandala alitengeneza maneno yake akayafanya kikosi kazi

Sasa haya ya Fatma nguli watashindwa vipi kuyapuuza au kuyabadilisha
Hakuna sheria inayowafunga , hakuna chombo kinacho wa monitor

Mwisho, hivi Rais akikataa maoni ya kikosi kazi kama sheria inavyomruhusu haya maoni ya akina Fatma yana maana gani?

Kwenda mbele ya kikosi kazi ni kukijengea uhalali. Kikosi kazi tayari kina maoni, sasa kinatafuta uhalali. Ni pale mtu anapokuwa na mipesa haramu akaisafisha!
 
Sasa wewe unamuamini Lipumba mtu aliyeacha uenyekiti wa CUF huku dunia nzima ikimuona ila baadae akaja na kudai kuwa yeye bado ni mwenyekiti halali?
Asiye na credibility si wa kumuamini katika mambo makubwa huenda anacheza trick zilezile alizozizoea
OK hapa unatusaidia kwamba Lipumba hana credibility na yupo katika kikosi kazi.
Unatueleza kikosi kazi kilivyokosa credibility siyo Lipumba tena

Lakini basi nani alisimama na kusema alichosema si kweli?
 
Rais anaweza kuunda taasisi yoyote ya kumshauri chochote kwa mujibu wa sheria ila kuupokea au kuukataa ushauri ni haki yake pia.
Kwahiyo anaweza kukataa maoni ya kikosi kazi kama hayampendezi!
Ndiyo maana tunasema kila kitu hapa ni usanii. Kwanini wasikae na Rais na kupanga wanachotaka ? Kuchukua maoni ni kupoteza pesa za Umma. Rais anaweza kukubali au kukataa! Unaelewa?
Kikosi kazi kitamsaidia rais ushauri ambao utaisaidia serikali yake kuboresha sheria mbalimbali za mambo nyeti ya nchi ikiwemo hiyo sheria ya mabadiliko ya katiba. Kama hutakibaliana na rais basi
1. Subiri 2025 upige kura ya kumtoa Madarakani au labda nature ichukue nafasi yake
Yes kikosikazi hakina maana! kwasababu moja, lazima kitengeneze kitu ambacho Rais atakubaliana nacho kama mtu na si Wananchi. Haya ndiyo matatizo tuliyo nayo yanyohitaji katiba mpya

Hapa pia unatusaidia kutueleza kuwa Fatuma Karume na akina Zitto wanapoteza muda na kutumika tu kuhalalisha uovu. Ikiwa Rais anaweza kusema yes or no kuna haja gani ya maoni?
Kwenda mbele ya kikosi kazi ni kuhalalisha kisicho halali. Ni kutakasa mchakato si kutoa maoni
Mtu mwenye akili na anayefaya uchambuzi ataliona hilo , si kwamba hata enda bali atakemea matumizi mabaya ya pesa za umma na madaraka
2. Unaweza kuikataa rasimu atakayokuja nayo kwenye kura za maoni
Aha! kumbe kuna rasimu inaandaliwa! hii ni news. OK
Kwa muda mfupi mkakati utafanikiwa, kwa muda mrefu ni tatizo kubwa sana. Kenya walianza hivi
 
Back
Top Bottom