Sheikh Farid: Tunashukuru tumeachiwa ni mwanzo mwema wa Rais Mwinyi na Samia

Sheikh Farid: Tunashukuru tumeachiwa ni mwanzo mwema wa Rais Mwinyi na Samia

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Sheikh Farid: Tunamshukuru Mwenyezi Mungu, kiufupi tunashukuru sisi tumeachiwa lakini huu ni mwanzo mwema ya busara ya marais wetu, Rais wa Zanzibar na Rais wa Tanzania, Amiri Jeshi mkuu, mama Samia Suluhu. Wamefanya busara kubwa sana kuondoa hii hali ya mtanziko ya muda mrefu sana wa hii Kesi.

Sheikh Mselem: Tumechukuliwa Gerezani jana Usiku, Maghrib na Insha tumeswali palepale gerezani, tumechanganywa na baada ya kuswali Maghribi tumetoka zetu tukaja Airport.

Airport tumeingia kwenye ndege ilikuwa iko faragha, tumefika zetu hapa tumefikia VIP ya zamani, ndege imekaa peke yake, hakuna mtu zaidi ya wenyewe na tulivyotoka pale kila mtu akaingia kwenye gari lake, akaulizwa nikupeleke wapi?

Mzee Mselem nikupeleke kwa mke wa kwanza, wa pili, wa tatu? Nikawaambia kwanza naenda kwetu, muda mrefu sijafika, nikayasome matatizo, ya kutatua nitatue na mengine alafu ndio nitaanza tena kwenda.

Hatukupewa waraka wowote.

 
Wavunje hata kesho! Sina cha kupoteza. Ila sitawaunga mkono kamwe hao Masheikh kuhubiri chuki na mwisho wa siku baadhi ya Watanzania wenzetu kumwagiwa tindikali, kisa wanataka kujitenga na Tanganyika!
Hivi kweli kama wanahusika na jinai hizo serikali ilishindwa kuwafungulia mashtaka wahukumiwe? Mbona walishikiliwa gerezani kwa tuhuma za ugaidi?

Bila shaka serikali ilitunga tuhuma za uongo na hata tuhuma za kuwamwagia watu tindikali ilifanywa na ma-agent wa serikali wasiojulikana! Mambo mengi mabaya yamefanywa na serikali nyuma ya mgongo wa wasiojulikana!
 
Back
Top Bottom