Na Mwandishi wetu.
Mwenyekiti Jumuiya na Taasisi za Kiislaam nchini Tanzania, Shekhe Mussa Kundecha amefunguka na kukemea wazi wazi kitendo cha Mwanaharakati wa mitandaoni Maria Sarungi kuweka chapisho la Picha za Kumdhihaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu na kusema picha hizo sio tu zinamdhihaki Rais bali zinadhihaki Vazi la kislaam na Waislam wote.
Ambapo katika Chapisho hilo Maria Sarungi alituma picha ya Chura akiwa amevaa vazi la Hijab, jambo ambalo ni sawa na kuikashifu na kutukana jamii ya Waislamu Tanzania na Duniani kiujumla.
Shekh Mussa Kundecha amemtaka Maria Sarungi afute chapisho hilo haraka sana kabla wauumini wa dini ya kislamu hawajaungana kwa pamoja kushitaki kwa MwenyeziMungu juu ya jambo hilo ambalo halina taswira nzuri kwa waumini wa Dini ya Kiislamu.
View attachment 3017478