Sheikh Mkuu Zuberi jenga shule kubwa badala ya misikiti mikubwa

Its too late jamaa yng we angalia km roma wale wanazuga tu eti shule walizonazo ni kwa ajili ya kuandaa mapadri lkn sio kweli lengo ni kuingiza watu wao kwenye system ya ajira serikalin na kupata mapadri pia
Acha kudanganya darasa linaweza kuwa na wanafunzi 40 lakini wakatoka mapadre 3 vipi useme ni kwa ajili ya mapadre na hizo ni zile maalumu kwa ajili hiyo lakini zipo nyingine wanatoa elimu tu yakawaida, sema elimu yao watoa iliyo bora.
 
Wakristo madhehebu ni mengi sana kwa Tanzania,kwa hiyo kila dhehebu linajenga shule zake na vyuo vyake,kwa vile wako tofauti kiimani,hata waajiria wa hizo shule na vyuo ni wa imani husika.Kwa upande wa uislamu dhehebu kubwa ni moja tu Tanzania,ni suni ni 99%,na madhebu mengine yaliyobakia,hawatofautiani na suni ,kiasi cha kuwa wawe na shule zao,na vyuo ,vyao,na wakiwa navyo,hawachagui katika ajira,awe wa dhehebu lolote,atafanyakazi na atasoma.
 
Sasa waislam mna chuo kikuu kimoja miaka 60 baada ya uhuru.

Wakristo wana vyuo vikuu 5 miaka 60 baada ya uhuru.

Bado huoni tatizo tu hapo?
Hivyo vyuo vya kikirsto sio vya dhehebu moja,kila dhehebu lina chuo chao,ajira za hapo ni za wa dhehebu husika.Wakati waislamu wa Tanzani ni Suni 99%,na hakuna ubaguzi wa dhehebu katika uislamu,hao madhehebu yenye wafuwasi kidogo,hawabaguliwi kwenye ajira,na wao pia wakiwa na shule au chuo,hawabagui wengine.
 
Sasa kama muislam mwenzako hapo juu kwenye comment yake anaita elimu ya darasani ni elimu ya Kikafir, si mtatawaliwa na wakristo milele? (ambao hiyo elimu ya darasani anayoiita ya Kikafir wakristo wanaipa kipaumbele kuliko kawaida)
Katika kutawala,hakuchagui dini,sio ibada hiyo.Kuwa na akili.
 
Mtaa Nina oisho Mimi pale Moro Kuna shule za kikristo kama 6 hivi na hakuna hata moja ya kiislamu

Huo mfano tosha

Angalia hapo ulipo Hali ikoje.

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Hizo shule ni za madhehebu tofauti ya kikristo,madhehebu ni mengi ya kikristo,na yanaabudu tofauti.Lakini katika uislamu ,Suni ni 99%,dhehebu ni moja lenye watu wengi,wakijenga shule au chuo,kitakuwa ni kimoja,na wamadhebu wengine,hawabaguliwi,kwasabanu ibada zao hazina tofauti.
 
Wewe labda mgeni Tanzania,BAKWATA wana shule nyingi tu,na ni nzuri,wapo wasomi wengi wamemaliza huko.Shule karibia 30 na vyuo vya dini zaidi 32.Na ndani ya BAKWATA wapo wasomi wengi tu.
Huu ni mjadala wenye Tija na sio mabishano.Waislam amkeni.
 
Usione wengi ukadhani ndio wana maana sana. Ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi.


Msikiti ni kitovu cha elimu zpte, kwa wale wenye kufikiri tu.
 
Hahaaa acha kubalance story, shule za kikristo ni nyingi na zinafanya vizuri pia karibu asilimia 80 ya vyuo vya private ni vya wakristo
 
Mleta mada ilibidi afikirie hili jambo kabla hajaleta hii mada.
Mleta mada hajaongelea shule za msingi na form one. Kwenye ngazi ya primary schools takwimu zinaonesha kuwa kuna uwiano mzuri wa dini hizi 2 kuu nchini. Lakini huu uwiano unachafuka kwa kadiri unavyoolekea vyuo vikuu na kwenye ajira za umma.
 
Huu ni mjadala wenye Tija na sio mabishano.Waislam amkeni.
Unapokutana na sheikh anakwenda kuchomwa sindano matakoni na binti mdogo wa kikiristo wakati mabinti wa kiislam walihimizwa kuolewa wakiwa na miaka 14 hilo sio kosa la wakristo bali ni kosa la Muft. Ukiona sheikh anakwenda chumba cha upasuaji kutolewa tezidume na Daktari Mkristo wakati vijana wa kiislam wako madrasa wanahifadhi Qur'an kifuani hili pia ni kosa la waislam wenyewe. Ukiona mahujaji wanakwenda Maka kwenye ndege ambayo rubani wake ni Captain Anthony hili pia sio kosa la wakristo.

Lakini kama ofisi ya umma imeajiri watumishi wengi wakristo hata wafanya usafi na madereva na kuwaacha waislam wenye sifa za kufanya Kazi pale, hilo sio kosa la moja kwa moja la mufti bali kosa la mfumo.

Kule marekani kama utaona MTU mweusi chuo kikuu basi wengi wao ni weusi kutoka Afrika waliopata scholarship mbalimbali kutoka mataifa yao au taasisi za marekani, na hapa Tanzania kama utakuta chuo kikuu kina waislam wengi basi hao wametoka Zanzibar wamelipiwa na serikali yao kuja kusoma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…