Sheikh wa Wilaya ya Tanga awaomba waumini kutotumia Sanitizer kabla ya swala maana ina kilevi

Sheikh wa Wilaya ya Tanga awaomba waumini kutotumia Sanitizer kabla ya swala maana ina kilevi

Sheikh hayupo sahihi. Alcohol ni "pure" siyo najisi na haitengui udhu wala swala labda uwe umeinywa kwa kuelewa kuwa unainywa ili ulewe. Hakuna anaekunywa sanitizer, unajipa au kujipulizia tu na si kwa sababu ya kulewa.

Huyu ndiyo wale wanaoharamisha ambavyo havijaharamishwa na Allah.
Namfahamu vizuri huyu mzee, nishekh watanga mjini sahare msikit wa ibnu abas, nikada wa ccm na alikua diwani wasahare majengo mapya kwazaid ya miaka 10 kupitia ccm.
Najiuliza nanialiewapeleka eatv kwa huyo mzee na sijui walitarajia nin

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Masheikh na wachungaji wanapigana vikumbo fools avenue.
 
View attachment 1439997

Sheikh Mohamed Kombora amewaasa waumini wa Kiislam wa wilaya ya Tanga kuacha matumizi ya vitakasa mikono (Sanitizer) kabla ya swala maana vina kilevi kwa zaidi ya 60% na kwamba wakitumia watanajisi swala zao.

Chanzo : EATV

Nakala : FaizaFoxy
Pombe sio najisi.

Kwa hiyo ukisali nayo hibatilishi sala kabisa kwa sababu haukusali na najisi.

Hapo shekhe kachemka.

Najisi ndo ukisali nayo inabatilisha sala.

Sio kila haramu ni najisi.

Pombe ni haramu lakini sio najisi.

Kama ambavyo nguruwe ni haramu lakini sio najisi.
 
Ukiumia ukaweka spirit kwenye kidonda huwezi kuswali pia? Nadhani kaichukua kwa wepesi sana hiyo hoja.
 
Pombe sio najisi.

Kwa hiyo ukisali nayo hibatilishi sala kabisa kwa sababu haukusali na najisi.

Hapo shekhe kachemka.

Najisi ndo ukisali nayo inabatilisha sala.

Sio kila haramu ni najisi.

Pombe ni haramu lakini sio najisi.

Kama ambavyo nguruwe ni haramu lakini sio najisi.

Uko sahihi kabisa akhiy Maa sha Allaah.
 
Bakwata mnaambiwa kila siku someni dini mnabaki kufanya maulidi na kula ubwabwa tu, ndio haya sasa mnatudhalilisha waislam, ni wapi ulipoambiwa alcohol ni najisi ikiwa katika hali yake ya kawaida? Mtihani sana
 
Back
Top Bottom