Shemeji; Mimi naongea na Kaka yako nikiwa sina nguo, tuone atamsikiliza nani

Shemeji; Mimi naongea na Kaka yako nikiwa sina nguo, tuone atamsikiliza nani

Kweli maisha ni safari ndefu sana......

Nimekumbuka kisa kimoja miongo kadhaa nyuma.....wakati najitafuta nilijikuta nimepata hifadhi kwa Kaka yangu( Mola amrehemu).........Shemeji ilionekana hakuridhia uwepo wangu pale ingawa nilikuwa muda mwingi sipo nyumbani.....

Niliyajua hayo kupitia matendo yake maovu dhidi yangu kama vile kuninyima chakula....na kunifungia mlango ili nilale nje kipindi ambacho kaka amesafiri kikazi.......

Nikavunja ukimya na kumwambia kaka baada ya kuona mambo yanazidi kuwa magumu.....hapo ndio nilijua nguvu ya Shem kwenye nyumba ile.......

Sikujua kaka alifikisha ujumbe wangu kwa njia ipi lakini asubuhi baada ya kaka kwenda kazini... Shem alinifata na kuniambia kuwa..."Wewe unaongea na kaka yako mkiwa mmevaa nguo....mimi naongea na kaka yako nikiwa UCHI...je atamsikiliza nani..."

Nashukuru Mungu baada ya siku kadha kaka alinipangishia chumba cha bei chee maeneo ya manzese na kunihudumia hela ya matumizi mpaka nilipoweza kusimama mwenyewe kimaisha......


NILICHOJIFUNZA......
KUISHI KWENYE FAMILIA ZA WATU UNATAKIWA UWE MPOLE HUKU UKIPAMBANA UONDOKE HAPO HARAKA IWEZEKANAYO ILI AMANI IWEPO KATI YAKO WEWE NA NDUGUYO.....
Rafiki yangu aliambiwa hivi;
Shemeji, tutakusaidia mpaka lini? Jiongeze basi utoke!
 
Nje ya mada kidogo:
Hivi huwa inakuwaje mwanaume timamu anatawaliwa na mke wake wandugu?.

Ila kaka yako alikuheshimisha sana Mkuu, hakutaka mambo yawe mengi.
Mara nyingi inakuwa sio mtu katawaliwa bali anaepuka matatizo ili kuinusuru familia maana anajua hawa wenzetu huwa wanafanya maamuzi kwa mihemko lakini baadae hujutia....maamuzi magumu hufanyika kama wakivuka mipaka......

Kaka alikuwa anamuelewa mkewe roho yake na hakutaka kuongeza mgogoro.....alifanya maamuzi ya kiume Sana.....
 
Kaka Yako licha ya kufikisha ujumbe,alifanya jambo la maana kukupangishia chumba kwani aliona mbele mambo yataharibika
Alifanya jambo la maana na nilikuja kumuelewa baadae sana.....

Kuna umri ukifikia automatically unahitaji amani na utulivu ili kuijenga kesho njema ya familia yako......

Ni wakati ambao mwanaume anaonekana kuyapuuzia mambo mengi sana na wakati mwingine kuonekana mjinga.....lakini akivuka hali hiyo ndio huwa yanapita maamuzi magumu ili kudumisha amani ya moyo wake...
 
Shemeji yako alikua ana tabia za kibinadamu za kawaida tu!

Bro wako alikua na akili kubwa sana, ila binafsi naona angekufanyia maarifa ya room kimya kimya bila kumdokeza chochote mke wake

Kuna mashemu ni mashetani
Suala la yeye kunitafutia chumba nadhani hakumuambia mkewe alifanya kimya kimya....hata mimi aliniambia baada ya kuwa ameshalipa Kodi na kuweka fenicha kadhaa za kuanzia maisha.....nadhani ulikuwa mpango wake tangu nafika pale
 
Back
Top Bottom