Shemeji; Mimi naongea na Kaka yako nikiwa sina nguo, tuone atamsikiliza nani

Shemeji; Mimi naongea na Kaka yako nikiwa sina nguo, tuone atamsikiliza nani

Kweli maisha ni safari ndefu sana......

Nimekumbuka kisa kimoja miongo kadhaa nyuma.....wakati najitafuta nilijikuta nimepata hifadhi kwa Kaka yangu( Mola amrehemu).........Shemeji ilionekana hakuridhia uwepo wangu pale ingawa nilikuwa muda mwingi sipo nyumbani.....

Niliyajua hayo kupitia matendo yake maovu dhidi yangu kama vile kuninyima chakula....na kunifungia mlango ili nilale nje kipindi ambacho kaka amesafiri kikazi.......

Nikavunja ukimya na kumwambia kaka baada ya kuona mambo yanazidi kuwa magumu.....hapo ndio nilijua nguvu ya Shem kwenye nyumba ile.......

Sikujua kaka alifikisha ujumbe wangu kwa njia ipi lakini asubuhi baada ya kaka kwenda kazini... Shem alinifata na kuniambia kuwa..."Wewe unaongea na kaka yako mkiwa mmevaa nguo....mimi naongea na kaka yako nikiwa UCHI...je atamsikiliza nani..."

Nashukuru Mungu baada ya siku kadha kaka alinipangishia chumba cha bei chee maeneo ya manzese na kunihudumia hela ya matumizi mpaka nilipoweza kusimama mwenyewe kimaisha......


NILICHOJIFUNZA......
KUISHI KWENYE FAMILIA ZA WATU UNATAKIWA UWE MPOLE HUKU UKIPAMBANA UONDOKE HAPO HARAKA IWEZEKANAYO ILI AMANI IWEPO KATI YAKO WEWE NA NDUGUYO.....
Pamoja na kuongea kwake bila nguo lkn ulisikilizwa na ulishinda na kaka Yako hongera zake, hao ni wanawake wa mjini na wenye malengo yao japo si wote, take care asije kuwa na mke wako kama huyo, na ukisikia kushikwa ndo huko.
 
Kweli maisha ni safari ndefu sana......

Nimekumbuka kisa kimoja miongo kadhaa nyuma.....wakati najitafuta nilijikuta nimepata hifadhi kwa Kaka yangu( Mola amrehemu).........Shemeji ilionekana hakuridhia uwepo wangu pale ingawa nilikuwa muda mwingi sipo nyumbani.....

Niliyajua hayo kupitia matendo yake maovu dhidi yangu kama vile kuninyima chakula....na kunifungia mlango ili nilale nje kipindi ambacho kaka amesafiri kikazi.......

Nikavunja ukimya na kumwambia kaka baada ya kuona mambo yanazidi kuwa magumu.....hapo ndio nilijua nguvu ya Shem kwenye nyumba ile.......

Sikujua kaka alifikisha ujumbe wangu kwa njia ipi lakini asubuhi baada ya kaka kwenda kazini... Shem alinifata na kuniambia kuwa..."Wewe unaongea na kaka yako mkiwa mmevaa nguo....mimi naongea na kaka yako nikiwa UCHI...je atamsikiliza nani..."

Nashukuru Mungu baada ya siku kadha kaka alinipangishia chumba cha bei chee maeneo ya manzese na kunihudumia hela ya matumizi mpaka nilipoweza kusimama mwenyewe kimaisha......


NILICHOJIFUNZA......
KUISHI KWENYE FAMILIA ZA WATU UNATAKIWA UWE MPOLE HUKU UKIPAMBANA UONDOKE HAPO HARAKA IWEZEKANAYO ILI AMANI IWEPO KATI YAKO WEWE NA NDUGUYO.....
Huyo mke wa kakaako yuko wapi saivi na mmewe kafariki!!?
 
Wanawake wanataka wakae ndugu zao kwake ila sio ndugu wa mwanaume sijui wana shida gani
Tatizo sio wanawake, tatizo huwa ni ndugu wa mme hujiona wao ndiyo wamuhimu kuliko mke aliyepo hapo nakuona anamnyoja ndugu yao, wengine hata uwafanyie nini watakusema tu.
 
Huyo mke wa kakaako yuko wapi saivi na mmewe kafariki!!?
Bado wapo kwenye mji wao na familia yake kwani ni miaka mingi imepita kwa hivyo hata watoto wake ni vijana wakubwa wanaojitegemea na familia zao.....na yule Shemeji sasa hivi ameshakuwa mtu....kama unavyojua utu uzima unakuja na mambo yake..... sasa ni mpole na mwenye hekima sana
 
Kaka angeaua πŸ˜‚

Nguvu ya K ni hatari sana, kuna jamaa yangu kapoteza kibarua kisa mke wa bosi wake walipishana kidogo mno, mke kaenda mwambia boss kijana wako anasema unampa hela sana ananitaka.
Sasa unabishana vipi na mke wa boss wako?

Walisema mtumikie kafiri upate mradi wako unazani walikuwa wajinga?
 
Sasa unabishana vipi na mke wa boss wako?

Walisema mtumikie kafiri upate mradi wako unazani walikuwa wajinga?
Mapishano mengine ni ya kibinadamu tu na wala sio ya kiuadui kama unavyojua binadamu kupishana kauli ni vitu vya kawaida....
 
Boss hakosei unazani wale machawa wawatu wanafanyaje nikujitoa ufahamu, huko Kwa mkeo au mmeo ndiyo katambe.
Pia watu tumetofautiana kwenye kuyapokea na kuyachukulia mambo... unaweza ukaongea ukadhani ni masikhara kumbe kwa mwenzako ni mtihani
 
Tatizo sio wanawake, tatizo huwa ni ndugu wa mme hujiona wao ndiyo wamuhimu kuliko mke aliyepo hapo nakuona anamnyoja ndugu yao, wengine hata uwafanyie ninj watakusema tu.
Kabisa . Ndugu wengi mizinguo. Kitu kidogo tu tayari mke ashatangazwa kwa ndugu wengine ili
aonekane mbaya.

Kuna kipindi nilikosana na bro alipotaka kumtangazia sifa mbaya mke wangu mbele ya ndugu wengine.

Mke wangu alipishana kauli kidogo na dada yangu upande wa mama mdogo.Lilikuwa suala dogo tu lakini bro aliposikia akaitisha kikao na kuanza kumsema vibaya mke wangu, weweee niling`aka nikamwambia mbona mke wako hujawahi kumwitishia vikao je hajawahi kukosea? Wote kimya na baada ya kikao kuvunjika akaanza kusema pembeni mara ooh sijui fulani ukimgusa mke wake anakuwa mkali.

Ukikaa kiulegevu ndugu wanakuvurugia familia kwa jambo dogo tu.
 
Kabisa . Ndugu wengi mizinguo. Kitu kidogo tu tayari mke ashatangazwa kwa ndugu wengine ili
aonekane mbaya.

Kuna kipindi nilikosana na bro alipotaka kumtangazia sifa mbaya mke wangu mbele ya ndugu wengine.

Mke wangu alipishana kauli kidogo na dada yangu upande wa mama mdogo.Lilikuwa suala dogo tu lakini bro aliposikia akaitisha kikao na kuanza kumsema vibaya mke wangu, weweee niling`aka nikamwambia mbona mke wako hujawahi kumwitishia vikao je hajawahi kukosea? Wote kimya na baada ya kikao kuvunjika akaanza kusema pembeni mara ooh sijui fulani ukimgusa mke wake anakuwa mkali.

Ukikaa kiulegevu ndugu wanakuvurugia familia kwa jambo dogo tu.
Pamoja na hayo lakini ndugu ufanye ukali kwa kiasi ndugu usiongee ukamaliza.....hao unaowaona wanamsema vibaya wanaweza kuja msaada mkubwa kwako siku za usoni kipindi ambacho yule unamtetea kwa kugombana na ndugu ameshaondoka.......

Dunia ina mambo
 
Back
Top Bottom