Sheria inasemaje kuhusu kuzaa na mke wa mtu?

Sheria inasemaje kuhusu kuzaa na mke wa mtu?

Usiibe, nenda kaombe mtoto. Unalindwa na mazingira ya kuishi mtoto siyo salama. Sheria inasema hata kama mtoto ni under 7yrs, anaweza kulelewa na baba au mtu mwingine ikiwa itathibitika mtoto atakuwa salama kuliko kuishi na mamaye.

Hapa mke na mume wanagombana kwa kuwa mtoto si wa baba mwenyenyumba. Kuna hatari ya mtoto kuuawa katika ugomvi au kupewa sumu na baba mwenyenyumba.

Kwa nafasi hii ustawi wa jamii wanaweza kumtenganisha mama na mtoto ili mtoto awe salama.

Nilifundishwa nikashinda na kumchukua mtoto wa mwaka na miezi mitatu nikalea mwenyewe.
sawa
 
Inawezekana mwanaume wenzio alimtelekeza mkewe.

Si mnajua mkishikwa na micheps mkashikika mnavyokuwa?

Sasa ndio kakumbuka ana mke, au kaona mke anaendelea na maisha yake bila yeye karudi kumvurugia.(ni tabia yenu wanaume)

Hebu mtafute mama mtoto kwanza mzungumze ujue situation ya mtoto kabla hujafanya maamuzi mengine.
Na huenda huko kwa mchepuko vimechachuka, na huyo mwanamke miaka 4 mtu kanitelekeza halafu aje kunisumbua? Weee hapatatosha siwezi kuwa mnyonge kabisa
 
Hiyo ni sababu ya kuvunjika kwa ndoa ya mtu endapo mmoja wapo atafanya kitendo cha uzinzi na ikathibitika. Na pia wewe unaweza kulipa fidia endapo mwenye mke ataamua kukushitaki.

Lakini pia kwenye hali ya kawaida ikitokea kwa upande wako mkeo azalishwe na mwanaume mwingine kwako utajiskiaje au kwenye hii dunia unajiona kidume ni wewe tu au unadhani utayemuoa ni mwanamke wa tofauti sana.
Hana kosa lolote maana alipata ushirikiano mkubwa toka kwa mwanamke...na pia ukiangalia mda aliokaa huyo mune wake miaka minne...mingi mno...hapa mwanamke ndo Mwenye makosa maana alidanganya!! Jamaa hana kosa,hapa aende tuu ustawi wa jamii...
 
Habari Wakuu,

Ninaomba kufahamishwa sheria ya ndoa Tanzania inasemaje ikiwa umezaa na mke wa mtu? nataka kujua kama unaweza endelea kutoa matunzo ya mtoto akiwa kwenye familia nyingine. Na unatakiwa kufata utaratibu gani kumchukua mtoto anapo fikisha umri wa kulelewa na baba.

Hii imenitokea kwa mwanamke ambae nilizaa nae mwaka 2017 kwa kipindi cha miaka minne nimekuwa nikitoa matunzo yote kama mzazi mpaka mwaka jana nilipo pokea simu kwa mtu ambae alijitambulisha kama mume halali wa mama mtoto.

Nilishangaa sababu mwanamke alinitambulisha kuwa yeye ni single mama nilipo muuliza jamaa alikuwa wapi kwa kipindi chote anasema alikuwa safarini. Na mwanamke anakiri kweli ni mume wake na waliishi pamoja ila mwanaume alimtelekeza akaenda kuishi na mwanamke mwingine.

Sasa baada ya malumbano ya muda mwanaume akachukua simu ya mama huyo akaiharibu ili nipoteze mawasiliano na mimi nikaamua kukaa kimya ili kuona nini huyo dada atafanya nini.

Baada ya miezi miwili nikapokea simu kutoka kwa jirani wa mama wa mtoto huyo akinijulisha hali ya mtoto sio nzuri hakuna uangalizi tena maana nyumba imekuwa uwanja wa vita. Nikajiskia vibaya sana mana kweli ni damu yangu ila watuwazima na makosa yetu ndio tunapelekea watoto kuwa na mazingira magumu.

Lengo la kuja hapa ni kutaka kujua uhalali wangu kwa mtoto huyo na si mwanamke ili tu mtoto apate haki yake ya malezi.
Huna kosa kwenye macho ya sheria..kwa sababu kama ungekuwa unajua kuwa yule mwanamke kwenli kaolewa ana mume wako Kabisa, hapo ungekuwa na kosa na ungeshitakiwa kwa kula mke wa mtu .lakin kwakuwa mwanamke alikataa kama kaole a badala yake ni single mother...hiyo sababu pekee inakuondolea kosa!

Nenda ustawi wa jamii ukaeleze lengo na Nia y'ako....( Pia wape background) Hadi mfike hapo mlipo...simple mtoto utamchukua...maana tayar ushahidi wa majirani kama mtoto yupo kwenye hatare, na utambeba kikubwa tuh awe hanyonyi...., Ila kama mazingira yakiwa salama kwa mama yake huwezi kumchukua akiwa Mdogo
 
swa
Huna kosa kwenye macho ya sheria..kwa sababu kama ungekuwa unajua kuwa yule mwanamke kwenli kaolewa ana mume wako Kabisa, hapo ungekuwa na kosa na ungeshitakiwa kwa kula mke wa mtu .lakin kwakuwa mwanamke alikataa kama kaole a badala yake ni single mother...hiyo sababu pekee inakuondolea kosa!

Nenda ustawi wa jamii ukaeleze lengo na Nia y'ako....( Pia wape background) Hadi mfike hapo mlipo...simple mtoto utamchukua...maana tayar ushahidi wa majirani kama mtoto yupo kwenye hatare, na utambeba kikubwa tuh awe hanyonyi...., Ila kama mazingira yakiwa salama kwa mama yake huwezi kumchukua akiwa Mdog

Huna kosa kwenye macho ya sheria..kwa sababu kama ungekuwa unajua kuwa yule mwanamke kwenli kaolewa ana mume wako Kabisa, hapo ungekuwa na kosa na ungeshitakiwa kwa kula mke wa mtu .lakin kwakuwa mwanamke alikataa kama kaole a badala yake ni single mother...hiyo sababu pekee inakuondolea kosa!

Nenda ustawi wa jamii ukaeleze lengo na Nia y'ako....( Pia wape background) Hadi mfike hapo mlipo...simple mtoto utamchukua...maana tayar ushahidi wa majirani kama mtoto yupo kwenye hatare, na utambeba kikubwa tuh awe hanyonyi...., Ila kama mazingira yakiwa salama kwa mama yake huwezi kumchukua akiwa Mdogo
sawa mkuu tayari nimeanza utaratibu wa kumaliza hili nategemea jumanne nitaleta mrejesho hapa
 
Hiyo ni sababu ya kuvunjika kwa ndoa ya mtu endapo mmoja wapo atafanya kitendo cha uzinzi na ikathibitika. Na pia wewe unaweza kulipa fidia endapo mwenye mke ataamua kukushitaki.

Lakini pia kwenye hali ya kawaida ikitokea kwa upande wako mkeo azalishwe na mwanaume mwingine kwako utajiskiaje au kwenye hii dunia unajiona kidume ni wewe tu au unadhani utayemuoa ni mwanamke wa tofauti sana.
Hivi mkuu umesoma na kumuelewa metal mada? Au umekuja na makasiriko ya kuliwa huyo mke wa mtu bila kuzingatia content ya mleta uzi?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Habari Wakuu,

Ninaomba kufahamishwa sheria ya ndoa Tanzania inasemaje ikiwa umezaa na mke wa mtu? nataka kujua kama unaweza endelea kutoa matunzo ya mtoto akiwa kwenye familia nyingine. Na unatakiwa kufata utaratibu gani kumchukua mtoto anapo fikisha umri wa kulelewa na baba.

Hii imenitokea kwa mwanamke ambae nilizaa nae mwaka 2017 kwa kipindi cha miaka minne nimekuwa nikitoa matunzo yote kama mzazi mpaka mwaka jana nilipo pokea simu kwa mtu ambae alijitambulisha kama mume halali wa mama mtoto.

Nilishangaa sababu mwanamke alinitambulisha kuwa yeye ni single mama nilipo muuliza jamaa alikuwa wapi kwa kipindi chote anasema alikuwa safarini. Na mwanamke anakiri kweli ni mume wake na waliishi pamoja ila mwanaume alimtelekeza akaenda kuishi na mwanamke mwingine.

Sasa baada ya malumbano ya muda mwanaume akachukua simu ya mama huyo akaiharibu ili nipoteze mawasiliano na mimi nikaamua kukaa kimya ili kuona nini huyo dada atafanya nini.

Baada ya miezi miwili nikapokea simu kutoka kwa jirani wa mama wa mtoto huyo akinijulisha hali ya mtoto sio nzuri hakuna uangalizi tena maana nyumba imekuwa uwanja wa vita. Nikajiskia vibaya sana mana kweli ni damu yangu ila watuwazima na makosa yetu ndio tunapelekea watoto kuwa na mazingira magumu.

Lengo la kuja hapa ni kutaka kujua uhalali wangu kwa mtoto huyo na si mwanamke ili tu mtoto apate haki yake ya malezi.
1. Katazame kwanza DNA.

2. Pelka maombi Mahakamani (ya watoto), kuomba kulea na kumtunza mwanao.

Magomvi yao, waachie wenyewe.
 
Back
Top Bottom