Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Ni Lowasa all the way, wewe baki na washirikina wa ccm, kwa sababu tunataka upinzani imara baki huko mtaunda kambi ya upinzani na Ayatola Zitto Kabwe ili Serikali mpya ya UKAWA isilale.

Aamen....
 
Ama kweli viongozi wetu hawatupendi wananchi hata kidogo
 
CBa3a8aUcAEqice.jpg:large


Sheria hii inatarajiwa kupitishwa Jumanne 31 March na Aprili 01, 2015 kwa hati ya dharura.




Wakuu,

Baada ya kuisoma sheria tarajiwa ya makosa ya jinai kwa watumiaji wa mitandao (Cybercrime) ambayo inapitishwa Bungeni kwa hati ya dharura, napata shaka juu ya uhuru wa watanzania watumiao mtandao.

Serikali yetu imeamua kutuumiza watanzania kwa mara nyingine. Inauma, inasikitisha na hatuna wa kututetea.

Wameona kupunguza vifurushi pekee hakutoshi, wameamua kutupangia nini tuongee, nani aongee na aongee vipi. Watoa huduma watalazimishwa kutoa taarifa zetu na wakikataa wataadhibiwa "kwa mujibu wa sheria".

Kwa ufupi, serikali inataka kuamua upi ukweli na upi uwongo. Huu ni ubakaji mkubwa wa Demokrasia. Wengi tutafungwa kwa uonevu wa kipengele hiki.


Napata shaka zaidi kwa watumiaji kutokujua hatari inayokuja mbele yao na hivyo kuchukua tahadhari.
Aidha, nina mashaka sana kama wabunge wetu wanaelewa athari yake kwao pia maana kama walidhani wanalengwa JF tu, basi hii ina upana zaidi ya hapo.

Kwa kiingereza:


Na pia, kipengele cha 21 kinaihusu JamiiForums au wengine wanaotoa huduma kama hizi. Serikali yetu tukufu inataka iwe ni lazima taarifa za watu zitolewe na watoa huduma ili iweze kufanya uchunguzi.

Wanaharakati, wapinzani na wengine ambao Serikali yenu Tukufu huenda inawahofia au kuwatilia shaka, itawalazimisha watoa huduma kutoa siri zenu. (Email zenu hupita kwa ISP na sio encrypted):



Soma pia kuhusiana na watoa huduma:

Aidha, serikali hii tukufu imeamua kutumia kifungu cha 22 kuonyesha dhamira yake si ya kutania endapo itataka kupata taarifa za mtu na mtoa huduma akataka kuua ushahidi kama inayosomeka:

Angalieni kipengele hiki pia:


Tupo salama?





Ni kutaka kudhibiti taarifa wakati wa uchaguzi? Ni kuwalinda kina nani?

Isomeni sheria nzima hapa - http://mst.go.tz/index.php/componen...wnloads?download=24:the-cybercrimes-bill-2015

Nimeambatanisha kipengele ninachoona ni tatizo zaidi.

CC EMT, Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mchambuzi na wengine mnaoweza kututoa wasiwasi
MPAngo mzima hapa ni Tuchague UKAWA kisha TUFUTE HII SHERIA..
 
MPAngo mzima hapa ni Tuchague UKAWA kisha TUFUTE HII SHERIA..

Kufuta hapana ila ni kuirekebisha ndio jambo la msingi kwani kuwa na hii sheria ni vyema sana kutokana na kukua kwa teknolojia hapa nchini
 
Katika jamii zetu za leo ambapo intaneti inasaidia kurasimisha kila hatua za maendeleo ya watu kiuchumi..kijamii na kisiasa. hakuna budi kwa serikali kuweka uangalizi na uhakiki wa taarifa.

Kuanzia banking system, education systems, social media and political struggles zote zinahusisha matumizi ya internet. Kuacha taarifa hizi bila kulindwa na kusimamiwa vema italeta madhara sana.

Internet usage kwa tanzania is now moving from a WANT to a NEED. there is a point to protect everything within.
 
nichekiii kwa hiii no +255 673 612 886 nitext kukuunge team lowassa whatsap group kwa updates za ukawa
 
Issue ni kwanini kipindi hiki hasa mambo haya yanapewa kipaombele zaidi. Nafikili democrasia sasa inakwenda kubakwa kwani lazima kutakuwa na watolewa kafara tu ili ieleweke.
 
Hii sasa hatari, Demokrasia ndo imewekwa pembeni. Nilitegemea nguvu hii ya kupitisha hii sheria ingetumika kupitisha sheria kali kwa wauaji Albino na mambo ya msingi yanayo hatarisha maisha. Kila chenye mwanzo kina mwisho pia, october sitafanya makosa.
 
Hii ndiyo ile sheria itakayokuja kutukandamiza wapenda mageuzi e mwenyezi Mungu utusaidie
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    35.4 KB · Views: 753
Ni muda wa kuchukua tahadhari kwa kila mmoja
 
Wana jf,sheria yoyote itungapwo uwa ina akisi hali ya kisiasa ya nchi husika pale itungwapo
na sheria hii maalumu kwa ajili ya kudhibiti kubadilishana habari kipindi hiki cha uchaguzi
NB:sipingi uwepo wa sheria hii na najua after november haitatumika tena kama ile ya gharama za uchaguzi au rushwa!
lengo ni kujaribu "kuipiga chenga ya mwili" sheria tunapo badilishana habari ambazo ni za ukweli ila "kitengo" akipendi zijulikane!
kwa hiyo naomba tusaidiane yafuatayo:
a)wanafasihi wa kiswahili na kiingeleza watuundie misemo mipya ya kutumia ambayo aidha haijawa "defined au implied" ndani ya sheria husika ambayo itarahisisha usambazaji wa habari za ukweli
b)wana lugha ya kiswahili na kiingeleza watufundishe na watumie lugha za mafumbo hili kuficha maudhui ya habari zijazo umu
c)wanasheria watueleze "loopholes" za sheria hii na jinsi ya kuzi tumia kujikinga
d)wana tehama watusaidie kujua ni apps zp zitaficha privacy ya watumiaji hasa umu ndani au kwenye mitandao mengine

kama una mengine ongezea
 
Tutapike tu hawana hiyo technologia kutengeza kibiriti hawawezi wataweza kutu trap ktk media technology wanatutisha tu si walituonyesha panya wakasema watatumika ktk kuwapata majambaz mbona kimya kila siku twaibiwa
 
Unaonekan unatumika sasa hii sheria lazima ikuweke ndani ww....
 
Back
Top Bottom