Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Tutapike tu hawana hiyo technologia kutengeza kibiriti hawawezi wataweza kutu trap ktk media technology wanatutisha tu si walituonyesha panya wakasema watatumika ktk kuwapata majambaz mbona kimya kila siku twaibiwa

roger that!nimekusoma ila sio mbaya kuchukua tahadhari
 
kama mpaka tovuti za serikali zina ingiliwa na hawezi fanya chochote, we unategemea nini?
 
Jamani sheria imeshatungwa na kilichobaki ni kutumika tu...kiukweli itapunguza wale matapeli lakumi kwenye maswala ya uchaguzi hapo hayanihusub
 
Tatizo watanzania mlinyimwa elimu sasa hata mawazo yenu ni kama nguvu za giza hsmuamini kama mabadiliko ni muhim na yanawezekana mimi nimesoma kenya sikuwah kuona kenya wanafunz wanakaa chini hakuna madawati au walimu hakuna ila hapa tanzania mwaona jambo la kawaida
 
cba3a8aucaeqice.jpg:large





sheria hii inatarajiwa kupitishwa jumanne 31 machi na aprili 01, 2015 kwa hati ya dharura.




Wakuu,

baada ya kuisoma sheria tarajiwa ya makosa ya jinai kwa watumiaji wa mitandao (cybercrime) ambayo inapitishwa bungeni kwa hati ya dharura, napata shaka juu ya uhuru wa watanzania watumiao mtandao.

Serikali yetu imeamua kutuumiza watanzania kwa mara nyingine. Inauma, inasikitisha na hatuna wa kututetea.

Wameona kupunguza vifurushi pekee hakutoshi, wameamua kutupangia nini tuongee, nani aongee na aongee vipi. Watoa huduma watalazimishwa kutoa taarifa zetu na wakikataa wataadhibiwa "kwa mujibu wa sheria".

Kwa ufupi, serikali inataka kuamua upi ukweli na upi uwongo. Huu ni ubakaji mkubwa wa demokrasia. Wengi tutafungwa kwa uonevu wa kipengele hiki.


Napata shaka zaidi kwa watumiaji kutokujua hatari inayokuja mbele yao na hivyo kuchukua tahadhari.
Aidha, nina mashaka sana kama wabunge wetu wanaelewa athari yake kwao pia maana kama walidhani wanalengwa jf tu, basi hii ina upana zaidi ya hapo.

Kwa kiingereza:


Na pia, kipengele cha 21 kinaihusu jamiiforums au wengine wanaotoa huduma kama hizi. Serikali yetu tukufu inataka iwe ni lazima taarifa za watu zitolewe na watoa huduma ili iweze kufanya uchunguzi.

Wanaharakati, wapinzani na wengine ambao serikali yenu tukufu huenda inawahofia au kuwatilia shaka, itawalazimisha watoa huduma kutoa siri zenu. (email zenu hupita kwa isp na sio encrypted):



Soma pia kuhusiana na watoa huduma:

Aidha, serikali hii tukufu imeamua kutumia kifungu cha 22 kuonyesha dhamira yake si ya kutania endapo itataka kupata taarifa za mtu na mtoa huduma akataka kuua ushahidi kama inayosomeka:

Angalieni kipengele hiki pia:


Tupo salama?





Ni kutaka kudhibiti taarifa wakati wa uchaguzi? Ni kuwalinda kina nani?

Isomeni sheria nzima hapa - http://mst.go.tz/index.php/componen...wnloads?download=24:the-cybercrimes-bill-2015

nimeambatanisha kipengele ninachoona ni tatizo zaidi.

Cc emt, mzee mwanakijiji, nguruvi3, mchambuzi na wengine mnaoweza kututoa wasiwasi

i love you tanzania
 
Informer mbona unataka kushusha kiwango chako? Kama huoni mantic ya sheria hii basi kiwango chako cha kufikiri kitakuwa kipo chini sana mkuu.
 
Sisi huku Kimara tunataka maji hatuna cha ziada. Barbara za mitaani tunatengenezaga wenyewe kwa michango yetu.
 
Sheria hii isiyo na mipaka inayoeleweka imepoteza lengo zuri lililokusudiwa na pia limepoteza lengo la sheria yoyote nzuri. To every good law there is an exception. Ukiondoa kesi za madai na fidia, lengo kuu la adhabu katika sheria ni kwanza kumfanya mkosefu asirudie kosa na kwa mfano wa adhabu hiyo, kuogopesha au kuzuia watu wasifanye kosa kama hilo.

Sheria hii imeshindwa kutenganisha mkosefu kwa makusudi na mkosefu wa bila kukusudia kufanya kosa. Kama vile hiyo haitoshi, adhabu ni kali na kandamizi pindukia na mbali na haki ya kibinadamu ukizingatiwa kuwa sheria imepitishwa bila kuzingatia maoni ya raia,
 
Back
Top Bottom