umeandika nini hapo?Kwa nn sheria na malezi ya mtoto hutoa hualari wa mtoto baada ya mzazi kuto mazazi kutojili baada ya miezi 24 na ustawi wa jamii hawakubali kiualaka kwenda kupima vina sana msaada plz
Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa mfano wanandoa ni wakristo. Mme amepoteza maisha na hajaacha wosia wowote juu ya Mali hizo. Na watoto wa nje wamejitokeza wanataka Mali. Hyu mjane c ana haki ya kuwanyima hata mia?Mkuu Victoire, kwanza yategemea namna ya ndoa iliyofungwa baina yenu.Kama ni ya kiislam,kwa mfano,watoto wa nje ya ndoa hawawezi kurithi. Kama ni ndoa ya kimila,yategemea mila za kabila lenu husika. Kama ni ndoa ya Bomani, yategemea na makubaliano yenu katika ndoa yenu.Hii ni kwakuwa,kifungu cha 58 cha Sheria ya Ndoa kinaruhusu uwepo wa Makubaliano juu ya umiliki wa mali za ndoa.Umiliki ndio unaelekeza urithi hapo baadaye.
Nataka nieleweke kuwa, kama mali ni binafsi kama inavyoruhusiwa chini ya vifungu vya 56 na 57,urithi waweza kufuata sheria,mila au Wosia.Lakini,kama ni mali ya pamoja watoto wa nje ya ndoa (kwa ndoa za bomani na za kikristo) hurithi kutokana na matakwa ya wanandoa tu na si vinginevyo.
Mkuu, mjane au ndugu yeyote hana haki ya kugawa au kunyima mirathi. Msimamizi wa Mirathi huteuliwa na Mahakama baada ya taratibu za kisheria kufuatwa. Mabishano ya nani ni mrithi na arithi nini yatamalizwa mahakamani.Sasa mfano wanandoa ni wakristo. Mme amepoteza maisha na hajaacha wosia wowote juu ya Mali hizo. Na watoto wa nje wamejitokeza wanataka Mali. Hyu mjane c ana haki ya kuwanyima hata mia?
Mkuu, swali lako hilo liliulizwa na Mkuu Nyani Ngabu na nilishalijibu. Tazama ukurasa wa kwanza.boss je sheria yetu inaruhusu 'pre-nups'??
shukrani mkuuMkuu, swali lako hilo liliulizwa na Mkuu Nyani Ngabu na nilishalijibu. Tazama ukurasa wa kwanza.
Aisee!!!! Lakin kwa uonavyo wewe kisheria hao watoto ambao hawajawah kuonekana nyumbani kwa marehem hta siku moja wanafaa kupata Mali yoyote???Mkuu, mjane au ndugu yeyote hana haki ya kugawa au kunyima mirathi. Msimamizi wa Mirathi huteuliwa na Mahakama baada ya taratibu za kisheria kufuatwa. Mabishano ya nani ni mrithi na arithi nini yatamalizwa mahakamani.
Hiyo inaitwa presumption of marriage yaani dhana ya ndoa.Mnatakiwa kuishi miaka miwili mfululizo kama mke na mume .Asiwepo mwenye ndoa nyingine kati yenu,jamii inayowazunguka iwatambue kama mke na mume.Kinyume na hapo hakuna ndoa.ni jinsi ipi ndoa inakuwa halali kisheria mkipitisha miezi mitatu mnaishi tuu?naisikiasikia lakini cna elimu kuhusu hili
Hakuna ndoa hapo,hiyo inaitwa cohabitation ,aina mojawapo ya uchumba.Kama kuna vijizawadi labda bi dada alimpatia kwa ahadi fulani fulani aweza kumrudishia ila hakuna cha kugawana,sheria ya ndoa haitambui hayo.Hata Diamond na Zari bado hawana ndoa maana hawajakaa miaka miwili mfululizo.Zari muda mwingi yuko South Africa na Jamaa yuko madale.okk,maana kuna kesi watu wameishi miezi mitano mwanamme kamfukuza hawara yake na kipigo juu.hawara anataka wagawane mali