Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Habari zenu wadau

Wahenga walisema kwenye wengi hapaharibiki jambo, natumai humu wapo watalamu wa sheria kuhusu ndoa naomba tupeane uelewa kuhusu mambo mbali mbali kuhusu sheria za ndoa mfano

1) ili ndoa iwe halali kipi kinaitajika kufanyika

2)Je serikali ya Tanzania ina tambua ndoa za aina ngapi

3) Kuna maneno mitaani kuwa ukiishi na mwanamke miezi mitatu ni mkeo kisheria je hapo ikoje?

4)Je mwanamke ambaye umeishi naye bila ndoa ana haki ipi mkiachana

Karibuni wadau


UPDATE

Hii ni kutoka humu humu JF

HAKI NA WAJIBU WA MUME NA MKE KATIKA NDOA KISHERIA SEHEMU YA 1

Maana ya ndoa
Ndoa maana yake ni muungano wa hiari kati ya mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu kwa muda wa maisha yao yote (Kifungu cha 9 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971). Ili ndoa hiyo iwe halali hapa nchini inapaswa kufuata matwaka ya Sheria za Tanzania kama:

Muungano lazima uwe wa hiari, muungano uwe ni kati ya mwanamke na mwanaume, muungano huo uwe unakusudiwa kuwa wa kudumu, wafunga ndoa wawe wametimiza umri unaokubalika kisheria, wafunga ndoa wasiwe maharimu (wasiwe watu wenye mahusiano ya karibu ya damu au kindugu), kusiwe na kipingamizi na mfungishaji ndoa awe na mamlaka ya kufungisha ndoa.

Aina za ndoa
Kulingana na Sheria ya Ndoa kuna aina kuu mbili za ndoa; ndoa ya mke mmoja na ndoa ya zaidi ya mke mmoja. (Ifahamike kwa Sheria ya Tanzania mke anapaswa kuwa na mme mmoja tu).

(a)Ndoa ya mke mmoja

Huu ni muungano unaoruhusu mwanamme kuoa si zaidi ya mke mmoja. Mfano, ndoa ya Kikristo.

(b) Ndoa ya zaidi ya mke mmoja
Huu ni muungano unaoruhusu mwanamume kuoa mke zaidi ya mmoja. Mfano, ndoa za Kiislamu na ndoa za kimila.

Sheria ya Ndoa inatambua aina tatu za ufungaji ndoa yaani kiserikali, kidini na kimila. Pamoja na aina za ndoa zilizotajwa hapo juu sheria ya ndoa inatambua dhana ya kuchukulia ndoa hii ni kwamba iwapo itathibitishwa kwamba mwanamume na mwanamke wameishi pamoja kwa muda wa miaka miwili au zaidi na kupata heshima ya mume na mke basi itakuwepo dhana inayokanushika kwamba watu hao walioana ipasavyo. Madhumuni ya dhana hii ni kumwezesha mwanamke na watoto kupata masurufu pale ambapo ndoa inavunjwa.

HAKI NA WAJIBU WA MUME AU MKE KATIKA NDOA
Baada ya kufunga ndoa na ikaonekana haina kasoro yoyote, mke na mume aana haki mbalimbali kisheria anazostahili kuzipata kisheria. Haki hizi ni kama;


Matunzo
Mke au wake wana haki ya kutunzwa na mume wao kwa kuwapatia mahitaji muhimu kama chakula, malazi, mavazi, matibabu, n.k kulingana na uwezo alionao mume. Hivyo katika ndoa mume anao wajibu wa kumkimu mkewe kwa kumpatia malazi, Nguo na chakula. Mke mwenye kipato vile vile anao wajibu wa kumkimu mumewe ikiwa tu mume huyo:
· Hajimudu kabisa.
· Hawezi kupata chumo la Maisha yake kwa sababu ya athari ya akili au afya mbaya
(hii ni kwa mujibu wa Sheria ya ndoaSura ya 29 ya sheria kifungu 63).

Hivyo basi kisheria mume ndio mwenye wajibu wa kwanza wa kumtunza mkewe. Mke anaweza kumtunza/kumkimu mume ikiwa mume hajimudu i.e hawezi kufanya kazi au shughuli kwa sababu mbalimbali kutokana na athari ya akili au akiwa na afya mbaya. Ikumbukwe mke anaweza kudai kwenye vyombo vya kisheria ikiwemo mahakama kama mume hatampa matunzo.


kutunza watoto
Mume na mke wana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mtoto wao na kumpatia mahitaji muhimu kama chakula, nguo, malazi, elimu na mahitaji muhimu. Ni kosa kisheria kutokumuhudumia mtoto wakati ukiwa na uwezo wa kumhudumia. Makosa hayo ni:

Kutelekeza Watoto
Kwamba mtu yeyote ambaye, ni mzazi au mlezi au mtu mwingine mwenye uangalizi au utunzaji halali wa mtoto yeyote mwenye umri usiozidi miaka kumi na nane, hali ana uwezo, wa kumuhudumia mtoto, kwa kuamua au kinyume cha sheria, au bila ya sababu za msingi atakataa kumhudumia, na akamtelekeza mtoto bila msaada, atakuwa ametenda kosa. Kifungu cha 166 cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya sheria za Tanzania pamoja na kifungu cha 188 cha Sheria ya Mtoto ya 2009.

Kosa la Kupuuza kumpa chakula mtoto n.k
Mtu yeyote ambaye, ni mzazi au mlezi au mtu mwingine mwenye uangalizi au utunzaji halali wa mtoto yeyote mwenye umri usiozidi miaka kumi na nne na asiyejiweza, akakataa au kupuuza (hali ya kuwa anaweza kufanya) kumpa chakula cha kutosha, nguo, malazi na mahitaji mengine ya lazima kwa maisha ya mtoto kiasi cha kumdhuru kiafya mtoto huyo, atakuwa ametenda kosa. Kifungu cha 167 cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya sheria za Tanzania pamoja na kifungu cha 189 cha Sheria ya Mtoto ya 2009.

Umiliki wa pamoja wa mali na mahusiano baina ya wanandoa
Mali ya mke au mume iliyopatik
 
Umeona uzi unaeleweka vzr tu wala haihtaj kurudia ila Kuna mishthole itakurupuka huko kukimbilia ku quote tena uzi, ni mda wa nissan nyeupe kurud tena mtaani
 
Habari zenu wadau

Wahenga walisema kwenye wengi hapaharibiki jambo, natumai humu wapo watalamu wa sheria kuhusu ndoa naomba tupeane uelewa kuhusu mambo mbali mbali kuhusu sheria za ndoa mfano

1) ili ndoa iwe halali kipi kinaitajika kufanyika

2)Je serikali ya Tanzania ina tambua ndoa za aina ngapi

3) Kuna maneno mitaani kuwa ukiishi na mwanamke miezi mitatu ni mkeo kisheria je hapo ikoje?

4)Je mwanamke ambaye umeishi naye bila ndoa ana haki ipi mkiachana

Karibuni wadau

Samahani kama huna cha kuchangia pita kimya kimya

Mimi najua tu kwamba moja ya Sheria au Kanuni Kuu ya Ndoa ni kwamba Wewe Mwanamke / Mke endapo Mumeo siku yoyote ikitokea tu akaomba ' Kuzibua Choo ' cha ndani basi yakupasa umpe ushirikiano wako wote ili asije akavutiwa kwenda ' Kuzibua ' vya Majirani au wa mbali kabisa kisha akabobea / akatukuka huko na ukaja Kujuta na Kulaumu.
 
Wewe subilia watuja na majibu ,ila hawachelewi kusema maswali hayo ynajibiwa kwa malipo
 
Vipi kuhusu kampuni, ikiwa mmoja awa wanandoa alikuwa na kampuni anayoiendesha, katika kugawana mali kulingana na mchango wa kila mmoja inakuwaje kuhusu kampuni au biashara ambayo alikuwa nayo mmoja wa wanandoa kabla hawajaoana ikizingatiwa kuwa hakuna kilichoongezeka katika kampuni au biashara hiyo?
 
Mkuu Victoire, kwanza yategemea namna ya ndoa iliyofungwa baina yenu.Kama ni ya kiislam,kwa mfano,watoto wa nje ya ndoa hawawezi kurithi. Kama ni ndoa ya kimila,yategemea mila za kabila lenu husika. Kama ni ndoa ya Bomani, yategemea na makubaliano yenu katika ndoa yenu.Hii ni kwakuwa,kifungu cha 58 cha Sheria ya Ndoa kinaruhusu uwepo wa Makubaliano juu ya umiliki wa mali za ndoa.Umiliki ndio unaelekeza urithi hapo baadaye.

Nataka nieleweke kuwa, kama mali ni binafsi kama inavyoruhusiwa chini ya vifungu vya 56 na 57,urithi waweza kufuata sheria,mila au Wosia.Lakini,kama ni mali ya pamoja watoto wa nje ya ndoa (kwa ndoa za bomani na za kikristo) hurithi kutokana na matakwa ya wanandoa tu na si vinginevyo.
Mkuu Peter, nirleweshe vizuri hapo kama tumejebga nyumba 3 na Mzee alafu kwenye wosia akamuandika mwanae wa nje? He nitawezaje kupinga?
 
Mkuu Peter, nirleweshe vizuri hapo kama tumejebga nyumba 3 na Mzee alafu kwenye wosia akamuandika mwanae wa nje? He nitawezaje kupinga?
Mkuu, mimi naitwa Petro na wala si Peter. Wosia si jambo lisilopingwa. Utaupinga kama umejumuisha mali au warithi wasiotakiwa. Ni jambo la kuthibitisha tu. Kama unapinga kujumuishwa kwa mrithi fulani, utajenga hoja zako na kueleweka tu.
 
Mkuu, mimi naitwa Petro na wala si Peter. Wosia si jambo lisilopingwa. Utaupinga kama umejumuisha mali au warithi wasiotakiwa. Ni jambo la kuthibitisha tu. Kama unapinga kujumuishwa kwa mrithi fulani, utajenga hoja zako na kueleweka tu.
Sorry petro simu inajiedit. Asante!
 
Masoma maswali yanayo ulizwa na majibu yake
 
Mkuu Petro na wengine.
Ni kipindi gani ukiishi na mwanamke ambye hujamuoa ataesabika kuwa ni mkeo.
 
Mkuu Petro na wengine.
Ni kipindi gani ukiishi na mwanamke ambye hujamuoa ataesabika kuwa ni mkeo.
Presumption of marriage sec 160 of law of marriage act sheria imesema ni miaka 2 inakuwa ndoa na jamii inayo wazunguka itambue kuwa mnaishi km mke& Mme na hio ndoa haina taraka Ila INA mgao WA Mali na maintenance of children and custody km ikivunjika (broken down irreparably) obiter dictum#
 
Presumption of marriage sec 160 of law of marriage act sheria imesema ni miaka 2 inakuwa ndoa na jamii inayo wazunguka itambue kuwa mnaishi km mke& Mme na hio ndoa haina taraka Ila INA mgao WA Mali na maintenance of children and custody km ikivunjika (broken down irreparably) obiter dictum#
thanks
 
Kuna mwamke nimeishi naye miaka kumi na nina watoto wawili na yeye, huyo mwanamke amechepuka na mwaume mwingine na imedhibitika huyo mwanamke nimemwacha sasa anadai Mali tulizochuma naye. Kisheria hili lipoje mkuu. Ushauri wako ni muhimu sana
 
Mimi nimeoa kwa ndoa Kiisilam mke wangu nilivo muowa alikuwa na kiwanja na mm ninakiwanja baada ya miaka mitatu mm nikaamu kujenga kumbe mke wangu nae alikuwa anajenga kwa sili mwishowe nikaamua kumuacha je ninafaa ile nyumba kugawananae vp ile yeye aliyo ijenga kwasili yatupasa nayo kugawana.
 
Kwanza,talaka ni mwisho wa ndoa.Pili,talaka hutolewa na Mahakama tu na si vinginevyo.Tatu, talaka ina taratibu zake.Kwa mfano,ni lazima kwa mwombaji wa talaka apitie katika Baraza la Usuluhishi la Ndoa kabla ya kwenda Mahakamani kudai talaka. Pia,Baraza husika lazima litoe kibali cha kushindwa kuwasuluhisha wanandoa hao ambao mmoja wao anataka kutalikiwa. Nne, talaka hutolewa tu pale ambapo ndoa hiyo itaonekana kuwa haiwezi tena kubaki a kurekebishika.

Kimsingi,Mahakama hulenga hasa katika kuilinda ndoa.Ndiyo maana,mwombaji wa talaka lazima athibitishe uwepo wa sababu za talaka kwa mfano mateso,kutelekezwa na uasherati wa mwenza wake.Ieleweke kuwa talaka zitolewazo kiislam ni hatua tu.Hii ni kwakuwa ni Sheria ya Ndoa tu ndiyo inayotumika katika suala hilo.
Sema kwa upande wa ndoa ya Kiislam, Sheria itakayotumika mahakamani ni Sheria ya Kiislam. Kwao hakuna kupitia mabaraza ya usuluhishi.
 
Back
Top Bottom