Rudia tena kwanza!ndoa ya kanisani haifi hadi kifo au takala. kule kwa msajili majina yenu bado yanasomeka na hamtakiwi kufunga ndoa ingine kisheria hadi iyo ivunjwe. ukifunga ndoa wakati ipo inayoendelea ni kosa la jinai. be careful
Jamani, mkichokana mnafanyaje sasa?Ila pia, ni lazima ajue mambo mawili muhimu sana kisheria, kwanza ni mahakama pekee yenye mamlaka ya kutoa talaka, tena huzitoa kwa ndoa zote hata za kidini namaanisha hata za kikatoliki, pili ni sababu, kuna sababu spesho zilizoainishwa kisheria zinazoweza kupelekea mahakama kuitoa hiyo talaka, kuchokana haipo.
Ila pia, ni lazima ajue mambo mawili muhimu sana kisheria, kwanza ni mahakama pekee yenye mamlaka ya kutoa talaka, tena huzitoa kwa ndoa zote hata za kidini namaanisha hata za kikatoliki, pili ni sababu, kuna sababu spesho zilizoainishwa kisheria zinazoweza kupelekea mahakama kuitoa hiyo talaka, kuchokana haipo.
Hayo makubaliano yenu mwende nayo hivyohivyo tu, lakini siku mmoja akibadili gia angani na kwenda mahakamani, matokeo ndio haya unayopewa, ndoa bado ipo kisheria. Mahakama inazitambua ndoa za kimila na kidini lakini haitambui talaka zake, full stop.
nirudie nini, nimeandika kiswahili ujue.Rudia tena kwanza!
Hii stori ya kutunga. Hivi ni.mali gani walizochuma wakati ndoa yenyewe imetimiza miezi michache tu? I can't believe this story.Wananzengo!!
Tushauriane jinsi ya kumsaidia huyu dada, ameachwa. Scenario iko hivi:
Kuna scenario kwamba watu walioana kwa ndoa ya kanisani kisha wakaingia mgogoro ndani ya miezi michache tu, mke akatoroka, akarudi kwao. Kisha baada ya miezi kadhaa akafuata mali zake kwa mumewe (zake/walizochuma pamoja), mumewe akubali kumpa kwa sharti la kwamba pawepo na mashahidi. Mke akatafuta mashahidi na mume akatafta mashahidi pia (miongoni ni wazazi wa mume na mke). Aliitwa pia polisi na balozi wa mtaa kusimamia usalama kwakua palikua na tishio la kuibuka kwa ugomvi wakati wa kugawana vitu.
Mume akaweka sharti mbele ya mashahidi kwamba waandikishane kwanza kila mali atakayochukua mwanamke na ikadraftiwa "hati ya kugawana mali" pale nyumbani na hati ikaeleza wazi kwa maandishi kwamba mke kachukua chake kwasababu "ndoa imevunjika"....wanandoa na mashahidi, polisi na balozi wakaweka sahihi zao na kila mmoja (mme, mke na polisi) wakapata nakala.
Kisha mke akaondoka na vitu vyake akarudi kwao na mume nae akaendelea na maisha yake, hawakuwa na mawasiliano tena. Lakini talaka ya mahakama haijatolewa mpaka sasa na wala hawajafanya mchakato wa kwenda mahakamani, ni mwaka tangu wamegawana mali.
Maswali:
1. Je, ndoa bado ipo kisheria? Kwanini?
2. Je bado wanandoa wanayohaki ya kuenforce ndoa yao (eg. Kukamatana ugoni)
3. Nani anayohaki ya kufungua shauri lolote kuhusu status hii. (e.g mke kudai arudi/ mume kudai mkewe)
4. Kuna makosa yoyote kisheria?
Mhh!!Talaka ya Sunnah: Nayo ni mume kumuacha mkewe katika utwahara ambao hujawahi kukutana naye kimwili.
Talaka Bid‘ah (Uzushi): Ni mume kumuacha mkewe akiwa katika siku zake za ada, au katika kipindi cha damu ya uzazi, au katika twahara aliyomuungilia au kumuacha talaka tatu kwa mpigo mmoja. Mwenye kutoa talaka aina hii huwa ana madhambi lakini talaka yenyewe huwa imepita ila ile ya tatu huhesabiwa kuwa ni moja tu.
Talaka Baain: Ni ile ambayo mume anamuacha mkewe akakosa haki ya kumrejea kwa kuwa eda imekwisha. Hivyo, mume huyo akawa ni mposaji kama waposaji wengine na mke akikubali inabidi mume apose, atoe mahari na ifungwe ndoa upya.
Talaka Rejea: Hii ni ile ambayo mume anamiliki haki ya kumrejea mtalaka wake. Huku ni mume kumrejea mkewe katika kipindi cha eda la kuachwa talaka ya kwanza au ya pili.
Talaka Bayana: Hii ni talaka iliyo wazi kabisa isiyo na utata aina yoyote. Nayo ni kamakusema: “Nimekuacha”. Na talaka hii si lazima ukusudie kwani tamko lako linatosha.
Talaka Kinaya (isiyo bayana): Hii ni lazima ukusudie talaka kwa kuwa tamko lako si bayana kama kusema: “Nenda kwa ndugu zako” au “Usiseme na mimi” na yanayofanana na hayo. Ikiwa talaka imenuiwa basi itakuwa imetuka.
Talaka ya hapo kwa hapo: Ni ile ambayo inapotolewa mke huachika hapo hapo bila kuchelewa. Hiyo ni kusema: “Wewe umeachika” baada ya mume kutamka hayo mke atakuwa ameachika.
Talaka ya Kutungika: Ni ambayo mume ameitungika juu ya kitu kingine kuwa kitu hicho akikifanya au akikiacha atakuwa ameachika. Mfano ni mume kusema: ukitoka hapa nyumbani utakuwa umeachika” na mfano kama huo.
Talaka ya Khiyari: Hii ni mume kumwambia mkewe nimekupatia khiyari kutengana nami au kubaki nami. Akichagua kutengana talaka itakuwa imepita. Hii ni kama Anavyotueleza Allaah Aliyetukuka kuhusu uteuzi waliopatiwa wakeze Mtume na Mtume mwenyewe (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyo katika Suratul Ahzaab (33), Aayah ya 28.
Talaka kwa Uwakala au Maandishi: Mume kama atamuwakilisha mtu mwingine kumuacha mkewe au akamuandikia mkewe talaka akimuarifu katika maandishi hayo kuwa amemuacha, mke atakuwa ameachika.
Talaka kwa Kuharamisha: Hii ni kusema kwa mume kumwambia mkewe: Wewe ni haramu kwangu au unakuwa haramu, kama atakusudia kwa tamko hilo talaka itakuwa talaka, na kama atakusudia dhihari itakuwa dhihari naye atawajibika kwa tamko hilo kafara la dhihari.
Asallaam alaikum.Nauliza hivi
Kuna binti rafiki angu antaka kumuoa alitengana na mumewe tangu 2015 akarudi kwao baada ya kutokea ugomvi na familia ya mumewe wa zamani
Sasa baada ya rafiki kuonyesha nia ya kumuoa binti
Mumewe ndo kaja jana kwao na binti kutaka suluhu je sharia inasema vipi kuhusu hili maana toka 2015 january mpk 2018 juni
You are a real talentboy1)Talaka Moja, ni talaka rejea
2) Talaka ya Pili, talaka rejea
3) Talaka ya Tatu, hauwezi kumrudia mkeo tena,na kama utataka kurejea ni lazima kwanza aolewe na mwanaume mwengine aachike ndio unaweza kumuoa tena...na itabidi uanze utaratibu upya kama ule wa mwanzo wakati unataka kuoa kwa mara ya kwanza.
NB: Hizo talaka rejea inabidi umrejee kabla ya kipindi cha eda hakijamalizika,kama kikiisha na haujamrudia inabidi ukaoe tena.
- Hakuna talaka tatu kwa mpigo,hata ukisema umemuacha mkeo talaka 3 basi kisheria inahesabika ni moja tu na unaweza kumrejea.
-Katika uislamu talaka si lazima iandikwe ndo iwe halali ila hata ukitamka tu japo kwa masikhara basi inahesabika kuwa umemuacha mkeo...Talaka ni katika jambo ambalo halina mzaha,yaani ukweli wake ni talaka na hata kama unatania bado itahesabika ni talaka eg ukasema "mke wangu nimekuacha" but hukumaanisha lbd ulikuwa unamfanyia mzaha tu basi kisheria tyr umeshamuacha kweli..so uchunge sana ulimi wako ktk hili.
-Talaka tatu ndo hatua ya mwisho na ndo hapo ndoa imevunjika na haiwezi kutengamaa tena isipokuwa kwa utaratibu maalum kama niliouleza hapo juu.
Kwanza lazima itambulike kuwa je Alimpa Talaka au walitengana pasina kupeana talaka? MosiNauliza hivi
Kuna binti rafiki angu antaka kumuoa alitengana na mumewe tangu 2015 akarudi kwao baada ya kutokea ugomvi na familia ya mumewe wa zamani
Sasa baada ya rafiki kuonyesha nia ya kumuoa binti
Mumewe ndo kaja jana kwao na binti kutaka suluhu je sharia inasema vipi kuhusu hili maana toka 2015 january mpk 2018 juni
Madam samahani hapo sentensi nanukuu " kwanza kukaa muda mrefu kwa mume bila kutimiza majukumu yako kwa mke tayari ni talaka" SI KWELI. Usipotoshe umma. IttaqillaahHuyo mwanaume ni shaitwani wa dunia (Shekhe kipoozeo) asitake kumrejea miaka yote hiyo arejee leo kisa kasikia kapata faraja? Kiufupi hakutaka huyo bibie awe na furaha.
Kwanza kukaa muda mrefu bila kutimiza majukumu kama mume kwa mkeo nu talaka tayari.
Asante madam kwa jibu lakoTatizo mnajitia dini mwaijua ninyi tu. Alikuwa anawasiliana na mkewe? Wajua kutokuwasiliana na mwenza kwa muda mrefu kwa makusudi hukumu yake ni nini?
Wajua kumtamkia mtu kuwa humtaki si mumeo/ mkeo ni talaka?? Ngoja niishie hapa baadae ntarudi.
talaka ni mahakamani, ila watu tunaachana huku mitaani kwa vile hakuna cha kupoteza.Nina swali la kisheria kuhusu talaka ya Kiislamu.
Kwa kuwa Tanzania haitambui dini yotote lakini wananchi wana uhuru wa kuabudu dini yoyote, Je, talaka ya maneno au ya kiandishi huwa inatambulika na serikali?
Kwa nchi kama Marekani, hata uwe na dini gani, lazima uende ofisi za serikali (city hall) kuapishwa na mke mtarajia, na kuomba leseni ya kuoa. Pia jaji au mtu mwenye leseni ya kukuoza ( justice of peace) lazima apige saini . Unarudisha fomu na kupewa cheti cha ndoa. Baada ya hapo, mnaenda kuoa kikabila au kidini.
Mkiachana, lazima muombe cheti cha kuachana. Bila hivyo, ndoa haitambuliki kuwa mumeachana.
Je, ndoa ya Kiislamu, mkiachana, lazima serikali ya Tanzania itambulishwe? Kuna " cheti cha kumwacha mume au mke"?
Ahsante kwa kujibu swali langu.talaka ni mahakamani, ila watu tunaachana huku mitaani kwa vile hakuna cha kupoteza.