Sheria za TFF zisingegusa matokea ya mchezo uliokatiwa rufaa

Hahaha Ulaya ngumu kuchezesha mchezaji mwenye kadi Tatu za njano, na Kagera walichofanya walikuwa wanakijua na waliamini hawatotambiliwa
 
Real Madrid mwaka jana/juzi alitolewa kwenye cops delay na alikuwa kashinda kwa kuchezesha mchezaji mwenye kadi
 
Real Madrid mwaka jana/juzi alitolewa kwenye cops delay na alikuwa kashinda kwa kuchezesha mchezaji mwenye kadi
Alitolewa ok. Na vp opponent wake, alipewa points 3 + magoli ma3, labda?
 
Ungekuwa umecheza mpira ungeelewa hoja ya mtoa mada. Ukweli ni kwamba mtenda kosa wa kwanza kabisa ni TFF wenyewe.. Wao ndio wenye wajibu wa kutunza rekodi zote za mchezo wa soka hapa Nchini! Wao ndio wenye kusema nani atashiriki katika mchezo na nani hatoshiriki!
Kabla ya mchezo wowote kuna kikao kinaitwa Pri-match meeting! Kikao hiki hushirikisha wadau muhimu katika mchezo, marefa, viongozi wa timu, kamisaa na wengineo. Hapa ndipo kila mmoja hupewa utaratibu wa mchezo. Ni jezi gani timu zitavaa, ni wachezaji gani wenye kadi wasioruhusiwa kwenye mchezo, ni muda gani mchezo utaanza nk.
Lengo la kikao hiki huwa ni kuondoa sintofahamu za kipuuzi ili hatimaye matokeo ya uwanjani yabaki salama.
Swali la kujiuliza ni je, kikao hiki kilifanyika? Na kama kilifanyika, je kilitimiza wajibu wake?
Ukianzia hapa ndipo utakuwa na uelekeo sahihi wa kujua kosa liko wapi!
Jambo lingine muhimu ni kujua nani aliwataarifu Simba juu ya kasoro hiyo lkn akaona sio muhimu kuwataarifu Kagera Sugar.
Ninaamini Kagera sugar na hata vilabu vingine wanastahili haki ya kupewa takwimu mbali mbali zihusianazo na mchezo wa soka hapa Nchini, na chombo pekee chenye wajibu huu ni TFF. Je, wanafanya hivyo?
 
Mimi naona hili swala linatolewa maoni kwa hisia.... Swala la kusema anapewa mtu point za mezani sijui na ukalalamika ni ujinga, tunafahamu na kama ww ni shabiki wa mpira basi utafahamu kuwa League zote duniani zina kanuni mfano ni Premier league England wao kadi 5 za njano Mchezaji harusiwi kucheza mchezo unaofuata na kila League ina utaratibu wake.
Sasa suluhisho ni Club ziwe na mfumo wakutunza kumbukumbu, na swala lakupokwa points na hayo maamuzi ya point za mezani unazodai hajaanza kupewa Simba leo, lishamfadisha Yanga, Azam pia so embu acheni lawama zisizo na msingi! League bado iko wazi, kama Yanga atashinda mechi viporo bado ataweza kuongoza
 
Brother, TFF ni mratibu wa sheria na kanuni za League... Yy ataonekana pale sheria au kanuni zimezidi.
Tatizo kubwa ni professionalism kwenye kuendesha hizi Club zetu, swala lakurekodi matukio ya kila match na kuweka kumbukumbu ni tatizo, wenzetu Ulaya huo upumbavu hakuna sababu kuna mtu maalumu wakufanya hilo.... Hv kama Kagera au Club yoyote ingelikuwa imeajiri mtu wakurecord hata kwa camera 1 match nzima na matukio yake kwajili ya kumbukumbu unadhani leo ingelitokea mkanganyiko! Kwanza ingesaidia hata kufanya coaching kujua mapungufu ya wachezaji kila mechi
 
Real Madrid mwaka jana/juzi alitolewa kwenye cops delay na alikuwa kashinda kwa kuchezesha mchezaji mwenye kadi
Hapo ni kuiondoa ktk mashindano kabisa sio kubadili matokeo ya uwanjani na kuwapa wengine.
 
Unazungumziaje rufaa ya yanga kwa Lyon walofanya kosa ka la mazembe? Vp rufaa ya police Dom kwa simba kuhusu kumchezesha lufunga? Hvyo ndo vinavyoleta ukakasi mpaka kufikia watu kulaumu sana coz inauma unapoona Wenzako wanapata point mezani ambapo ata wewe ulipaswa kuzipata
 
Vita ni moja, ila kuna tofauti ya mbinu za kupigana vita, hapo ukiwa dhaifu siku zote utaangukia pua
 
Uhalisia ile kadi ya tatu imetengenezwa na ndiyo maana jumanne wanaitwa wadau wote na vielelezo na kwa taarifa tu ni kuwa point zinarudishwa kagera sugar
 
Jenga maisha yako acha kuwaza utahira, hukuzaliwa kuikosoa TFF ulizaliwa ili uwe mtawala katika dunia hii,

amka toka usingizini wewe
Wewe ndiyo zoba yaani unajiona wewe ndiyo pekee mwenye kuchangia mawazo yako hapa JF?
 
Hoja yako ni ipi? Sheria ziangaliwe upya au kagera arudishiwe points tatu??..we unataka nini kati ya hivyo hebu chagua moja uwe huru maana naona huelewi unataka nn mpaka sasa
Jumanne point 3 zinarudishiwa kagera sukari
 
Matokeo ya uwanjani yabaki kama yalivyo na kama kuna timu inafanya makosa then wapate adhabu kwa hayo makosa bila kuathiri matokeo ya mchezo.
Wazo zuri sana mkuu
 
ulitaka wapewe nn ? serengeti boys karudishwa mashindanoni kwa ajili ya hiyo, real madrid alitolewa mashindanoni kwa ajili ya hiyo msimu uliopita
 
Kwani suala la timu kunyang'anywa points kwa makosa yao yanafanyika Tanzania pekee?? Mbona hizi ni sheria za Fifa na zinatumiwa na nchi zote wanachama wa Fifa! Mcpende kuwachagulia TFF adhabu za kutoa wakati sheria na taratibu zipo wazi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…