nandembako
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 655
- 526
- Thread starter
- #61
Brother mimi naamini kwenye kukua....unaanza chini kabisa,ukiwa na uthubutu kila kitu kinawezekanaMnajua hili swala la kujiajiri sio rahisi kama tunavyofikiria na kuwaza,
Nimeona tunalalamikiana na kushangaana kwamba kwakuwa mtu anamiliki smartphone basi huyo hapaswi kusema hana mtaji...si sahihi,
Kwa ulimwengu wa sasa SMARTPHONE ni muhimu sana hasa kwa sisi wajasiriamali na hata wanaotaka kuwa wajasiriamali, najua wengi wanasema uza smartphone upate mtaji sasa smartphone nyingne watu wanamiliki akiuza hata laki.2 haifiki....huyo utamwambia afanye biashara ni biashara gani unaweza ukaiendesha kwa kiasi hicho ktk ulimwengu huu wa ss,
Zingatia kuna mambo mtu atahitaji kujifunza...kusoma vitabu, kusoma makala za wajasiriamali wengne mtandaon kama humu JF, na hata kujua dunia inaendaje ktk swala zima la uchumi,
Kwahyo kwenye swala la mtaji hapakwepeki kwakwer hili ni tatizo,
Mimi wakat nasoma nlikua nasema ntajiajiri ila lazima niajiliwe kwanza na nkajiwekea naziri kwamba sitakaa ktk ajira zaidi ya miaka 5,
Ndani ya miaka hiyo 5 ingetosha kabisa kunipa Starting Capital ya kujiajiri, so twende mbele turudi nyuma kuajiliwa mwanzoni kupo unless kama utapata kianzio either kwa wazazi au ndugu jamaa na marafiki.
Ni vema tukaelewana na kushauriana tuache kusemana na kusimangana vijana....tupo tofauti kiakili, kiumri na hata kimazingira,
Na kuhusu ishu ya kukopi mawazo ya biashara hilo ni kawaida...hakuna biashara mpya duniani zote zilikuwepo sema tu zinafanyiwa Modification/Innovation....ndio maana ya ujasiriamali,
by emma mjasiriamali