Shilingi ya Tanzania inaporomoka kwa kasi kubwa

Shilingi ya Tanzania inaporomoka kwa kasi kubwa

Wew umeongea ukweli ..blaa blaa za export ni kwa watu waliokosa hoja ..huweiz kuwaambia watu wale kwa urefu wa kamba zao halafu utegemee moujiza ufisadi ni wa kiwango cha juu sana
Kazi kwao mimi na wewe ipo siku tutakufa, kama Ilivyo watu ambao leo ni mamlaka ya teuzi na wao ni wafu watarajiwa.

Tanzania itakuwepo mpaka siku jua litakapoishiwa hydrogen, hiyo siku hakuna anaeijua.

Sasa katika muda huo wakati tunasubiri jua kumaliza hydrogen fuel (only god knows when) ni jukumu letu watanzania wa kuwaachia watanzania wa kesho maisha bora na uwezo wa kuilinda Tanzania ya kesho mpaka hapo jua litakapo maliza hydrogen fuel.

Who knows by that time jua likiishiwa hydrogen fuel kama tumewajenga sahihi na wao kuwajenga wafuatao sahihi huko mbele kutakuwa na watu wenye uwezo wa kuunda vyombo vya kupaa sayari nyingine mambo yakienda mrama duniani.

That is to say kwa sasa nchi inaongozwa na watu wapumbavu wanaofikiria leo idara zote, uwezi kuzuia kila mtu kufikiria tumbo lake. Lakini kama kila mtu anafikiria tumbo lake from civil services to politicians you are doomed.

Bila ya watu wakutabudili fikra we are doomed, maendeleo hayana maajabu; Iła yana discipline tu na kanuni zake.

Na kwa sasa Tanzania aina watu wa kuongoza nchi

Ukienda ulaya ukapanda underground train. design engineer wa mwanzo wengi walijua hizo train awatopanda.

Ukiona Disney park leo, kama unajua historia ya ‘Walt Disney’ hakuna theme Park ata moja aliyoiona.

Siku ‘Walt Disney Park’ ya kwanza inafunguliwa California; Walt Disney alikuwa kafariki miezi michache kabla. Kaka yake ‘Roy Disney’ alipoulizwa inasikitisha ‘Walt Disney’ kafariki bila ya kuona uzuri wa hii theme park.

Jibu la Roy Disney kwa mwandishi lilikuwa wala hakuna cha kusikitisha ‘Walt Disney’ kufa siku chache kabla ya park kufunguliwa. Kwa sababu tunachokiona mimi na wewe leo kwenye hii park nzuri na ya maajabu ‘Walt Disney’ amekiona kwa miaka mingi sana kwenye kichwa chake ndio maana akatenga hela ya kuitengeneza hata kama hayupo leo.

Sasa jiulize hawa wapuuzi waliopo I leo Tanzania ya kesho wanaionaje.
 
Mpango alikuwa chini ya kiongozi imara ..sasa wa kwetu anarembu na kusema mkalitizama ..basi unategemea miujiza gani
Ufisadi, rushwa, ubinafsi, kutowajibika na kutowajibishwa, teuzi, tenguzi za hovyo,undugu, udini,ushikaji kwenye serikali unaliangamiza taifa. Sijawahi kumsikia SSH akikemea ufisadi, rushwa au kufukuza mawaziri kwa kutowajibika kubadili kauli yake wale kwa urefu wa kamba zao.

Yeye ni safari kila mwezi nje, seminar, warsha, kukaribisha viongozi, kuomba mikopo. Vitu vya msingi kama ukaguzi wa miradi nchi nzima, kusikiliza kero za wananchi, hana habari, alimwachia Makonda kwa miezi kadhaa kazi iliyotakiwa aifanye yeye. Hata hivyo akamtoa alipoona anapata umaarufu mkubwa, kama alivyomfunga mikono Majaliwa na kufukuza Lukuvi, Kabudi, Polepole. SSH ni janga kubwa sana kwa nchinya Tanzania.

Urais akipewa hata Majaliwa Kassim Majaliwa tutaona maendeleo haraka, kupungua vitendo vya ufisadi, rushwa na uhuni mwingine pamaja na uwajibikaji kuongezeka.
 
Kwa kweli shillingi ya Tanzania inaporomoka kwa kasi ya kutisha dhidi ya sarafu nyingine. Ukitaka kujua kuwa shillingi yetu inaporomoka kwa kasi linganisha bei ya bidhaa kwa leo na ulinganishe na miaka mitatu, miwili na hata mwaka mmoja.

Chukua mfano wa nishati ya mafuta. Miaka mitatu iliyopita bei ya dizeli kwa lita moja ilikuwa wastani wa Tshs.1,500 leo hii lita moja ya dizeli ni wastani wa Tshs.3,300. Mfano mwingine chukua sukari. Miaka mitatu iliyopita sukari kilo moja ilikuwa Tshs. 1,300 leo hii kilo moja ya sukari ni Tshs.3,500.

Sasa tuje kwenye kichekesho. Jana nilikuwa kwenye mwalo moja hapo Ziwa Victoria na sikuamini macho yangu nilipoambiwa kuwa samaki moja aina ya sato ni Tshs. 30,000 karibia bei ya mbuzi wakati miaka mitatu iliyopita samaki wa uzito huo alikuwa akiuzwa kwa Tshs.8,000.

Tuna wachumi, tunaelezwa uchumi kwa Mama umepaa na mbona sisi wananchi hatuoni badiliko lolote. Huku kijijini kuna umaskini wa kutisha. Mtu kujaliwa kula balanced diet labda kuwe na harusi au sherehe fulani.

Tuwaulize wachumi wetu, Je uchumi umepaa kwa vigezo gani?.
Unaonaee !,Eti Lipumba hawezi kuwa Waziri wa mipango kisa yeye ni CUF,
 
Kuishi Tz ni Kama drama hivi yaani sisi wananchi ndio mtaji wa serikali kwa sehemu fulani hivi yaani pamoja na kuwa na
Mbuga
Migodi
Bahari/Bandari
Lakini bado wananchi ndio pato lenyewe. Wananchi wanahela.
Mtumishi wa umma Tz analipa kodi kubwa wakati mwingine Sawa na wafanyabiashara wakubwa wakubwa. Hii yote ni katika kuimarisha uchumi wa nchi
Mshahara wa laki nane unalipa kodi 98100

Ambayo ni Sawa na 1,177,200 kwa mwaka
Kodi ya nyumba 100,000 hadi 200,000
Nauli zimepanda utoke tegeta au kimara 3000 kwa siku

Haya una kausafiri kaka utalipa ada ya maegesho mafuta nayo juu

Haya bei za vyakula sasa

Then serikali ikijiskia itatoa ongezeko la 2% kwenye mshahara while inflation ni almost 100% kwa miaka 10

Yaani bei ya cement 2016 miaka nane ilio pita ilikua 10,000 mwaka jana 15,200 leo 18,500
Haya twende taratibu 18,500-10,000=8,500
Hili ni ongezeko la 85%

Haya tufanye ulikua unapata ongezeko la 2% kwa miaka nane hii na mshahara wako ulikua ni 800,000
kwahiyo mwaka wa kwanza 16000
Mwaka wa pili 16320😅
"" tatu 16640
"""Nne 16979
""" tano 17300
"""Sita. 17630
""" saba 17950
""" nane 17270

Inamaana kwa muda huu mtumishi anachukua 918,440/= baada ya kua na ongezeko la 2% ya basic salary kila mwaka

Haya turudi sasa ile 800,000=80 bags of cement kwa bei ya 10,000 mwaka 2016

918,440=49 bags of cement kwa bei ya cement sasa mikoa mingine 20k....kumbuka haya ni malipo kwa mwezi mzima wa mtumishi


(Kumbuka pia waajiliwa wengi hawakupanda madaraja wala kuongezewa mishahara kipindi hiki)
 
Haa hiyo awamu ya 5 inaonyesha ulikuwa umeipania kweli ya 6..naona umeitetea kweli kwa external factor. Lakini amna awam ya hivyo kama hii 6
Nakubaliana nawe mkuu
Kwa kweli amechambua kwa kufuata matamanio na hisia zake na siyo takwimu


1980-1996: Mambo yalikuwa yameharibika kabisa hasa 1987-1995 ambato Tz ilikuwa nchi masikini zaidi kuliko zote Duniani, tukatangazwa kuwa hatukopesheki, printing ikatamalaki na inflation ili hit 36% (ilikuwa a total economic failure)
!996-2005: Uchumi ulirudi kwenye mstari na inflation rate ika drop kutoka 35% hadi 5.2%
2006-2014: Uchumi uliyumba sana hasa 2011-15, Inflation ikapanda hadi 10%+
2016-2020: Uchumi ulitengemaa ambapo inflation ili drop had 3.2%. kabla ya covid gdp growth ilikuwa 5.5%+
2021-present: hali siyo mbaya kiivyo lakini inflation imeanza kupanda taratibu tupo 4%+
 
Hayo ndio matokeo ya kuongozwa na watu ambao wanasifa zifuatazo:

1. Hawana elimu ya uchumi hata ile ya msingi tu ili iwasaidie kujitathimini maamuzi yao ambayo in long-run yana impact mbaya sana kwenye uchumi na taifa.

2. Watu wanaodhania uongozi ni fursa ya utajiri hivyo wakiingia hawaheshimu kanuni za uongozi, sheria za inchi, mamlaka, taasisi na vyombo ambavyo vinasimamia ustawi wa uchumi, jamii na inchi kwa ujumla.

3. Wanaoishi kwa kufanya madili na ufisadi na kudhurumu raia wakiwamo wafanyabishara wakubwa kwa wadogo ili wapate maslahi binafsi.

4. Wanashirikiana na wageni kupurusa rasilimali za raia na inchi huku raia wakikosa fursa ya kutumia rasilimali zao kujiletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

5. Wanaona pesa kama bidhaa hadi wanashiriki kuingia mikopo isiyo na ulazima yenye masharti ya kinyonyaji matokeo yake taifa linakabwa na ubepari wa magharibi kufidia madeni.

6. Kutoheshimu sarafu ya inchi kwa kuruhusu manunuzi na malipo kufanyika kwa njia ya dola badala local currency itumike katika mauziano ya bidhaa za ndani ili kukuza matumizi na uhitaji wa pesa yetu.

Kuna haja ya somo la fedha kuingizwa katika mtaala wa sekondari kuwe na somo la uchumi ili kuanzia miaka 15 wanafunzi waanze kupata ufahamu juu ya thamani ya pesa na kuitunza thamani hiyo.
 
Sukari gani ambayo kilo ilikua 1300? Hata wakati wa Kikwete ilikua 1800, tatizo lenu wengi humu hamna majukumu ngumu hata kujua bidhaa zilikuwa zinauzwaje miaka kadhaa iliopita.
Watu wananunua sukari kutoka maeneo tofauti. Unadhani wewe uliyepo Dar unanunua sukari kwenye maduka ya Dar ni sawa na mtu wa Mbeya anayenunua kwa Vendors wanaopata sukari yao tunduma?

Kwasasa mafisadi ya serikalini yamekaza mianya ya sukari unaona na kubana wachuuzi ili wanunuzi wakose option wanunue tu sukari wanayouza wao.

Unajua sukari kutoka hapo Brazil ukiileta hapa bongo hadi inafika inauzika kiasi gani? Kilo ni 700 so tukiongeza na upuuzi wa tozo na kodi inaweza kuwa 1200 hadi 1300 kwa kilo.

Ila sijui tumefikaje hadi kilo 3,600. Hii inchi tunahitaji kusafisha damu chafu itolewe turejeshe uzalendo, huu mwendo hatutaishia pazuri hata kidogo.
 
Juzi tu toyota ist iliuzwa 12m, leo nasikia wananunua 17m. Yaani 2020 hadi leo, hii ni hatari.
Bajaji ya kununua milioni 10 kweli? Bajaji? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sisi tuna export malighafi tena kidogo, wao wana export finished product kwa wingi. Import/Export ratio. Wao wanatechnologia wanazalisha ndani zaidi, na ziada wanagawa nje, sisis technologia hatuna, tunazalisha kidogo, ili kukidhi mahitaji yetu ya ndani tunaagiza kutoka nje. Tunaponunua kutoka nje tunatumia pesa za kigeni.

Kumbuka Dollar ni moja ya sarafu zinazutumika kama sarafu za biashara kimataifa, bila kusahau Swiss Franc, Japaneese YEN, British Pound, pesa ya kijerumani, kifaransa na Italiano.

Madafu yetu hayawezi kupanda thamani wakati hatuzalishi bidhaa zinazouzika kimataifa.

Factor ni nyingi wataalamu wasomi wa uchumi watasaidia mengine.
Comment ya maana kuliko zote so far. Umeongea vizuri nimependa.
 
Tatizo kubwa la Tanzania ni kutowekeza kwenye viwanda, Leo hii Tunapata shida ya sukari wakati tulipaswa kuwa na kiwanda Kila mkoa ama Kila Kanda. Viwanda vya nondo vilipaswa viwepo liganga lakini mnapeleka dar, uchumi umebase kwenye kilimo, wakati tuna Mali asili nyingi. Utalii haujatangazwa vyakutosha. Kila tunapotangaza tunaonyesha wanyama pekee, lakini Kuna utalii wa culture. Mfano sinema ingechezwa ya wahadizabe na maisha yao, ingevutia watalii wengi kuliko hata ya mbuga za wanyama. Tunauzaje ngano badala ya mikate na unga wa ngano, tunauzaje mahindi badala ya unga. Yaani kujikwamua hapa bidhaa za kilimo zinapaswa kuongezwa thamani kwa kufanyiwa packaging. Tanzania tunashida ya wasomi kuwa wanasiasa badala ya kuisaidia Nchi. Kila kitu siasa siasa na wasomi ndio wanaongoza kuididimiza hii Nchi.
 
Kwa kweli shillingi ya Tanzania inaporomoka kwa kasi ya kutisha dhidi ya sarafu nyingine. Ukitaka kujua kuwa shillingi yetu inaporomoka kwa kasi linganisha bei ya bidhaa kwa leo na ulinganishe na miaka mitatu, miwili na hata mwaka mmoja.

Chukua mfano wa nishati ya mafuta. Miaka mitatu iliyopita bei ya dizeli kwa lita moja ilikuwa wastani wa Tshs.1,500 leo hii lita moja ya dizeli ni wastani wa Tshs.3,300. Mfano mwingine chukua sukari. Miaka mitatu iliyopita sukari kilo moja ilikuwa Tshs. 1,300 leo hii kilo moja ya sukari ni Tshs.3,500.

Sasa tuje kwenye kichekesho. Jana nilikuwa kwenye mwalo moja hapo Ziwa Victoria na sikuamini macho yangu nilipoambiwa kuwa samaki moja aina ya sato ni Tshs. 30,000 karibia bei ya mbuzi wakati miaka mitatu iliyopita samaki wa uzito huo alikuwa akiuzwa kwa Tshs.8,000.

Tuna wachumi, tunaelezwa uchumi kwa Mama umepaa na mbona sisi wananchi hatuoni badiliko lolote. Huku kijijini kuna umaskini wa kutisha. Mtu kujaliwa kula balanced diet labda kuwe na harusi au sherehe fulani.

Tuwaulize wachumi wetu, Je uchumi umepaa kwa vigezo gani?.

Halafu Wachumi wa Tanzania wakiongozwa na Mchumi Mwigulu bado watakuambia kuwa inflation Tanzania iko chini ya 5 % ..... Huu Uchumi Mwigulu aliusomea wapi!?
 
Inflation (mfumuko wa bei) hili imekuwa global challenge

Hata ukienda Ulaya na Marekani nao wanakumbwa na changamoto hii

Sikatai kuwa shilingi inashuka thamani lakini sio sababu pekee ya ongezeko hilo kubwa la bei za bidhaa

Ndio maana BoT kwenye Q2 ya huu mwaka (Apr-June) wameongeza interest rate ili kupambana na inflation

Tunaimport vitu vingi sana, kama bidhaa huko ilipotoka imepanda bei basi tunapata kitu kinaitwa imported inflation
 
Hii Tanganyika ya KIZIMKAZI yy wala apagawi na hii changamoto.

KAZI ni kipimo cha UTU
 
Back
Top Bottom