Shindano la big brother lina maudhui gani?

Shindano la big brother lina maudhui gani?

Binafsi imenishinda hata nikijaribu kufit-in na wenzangu niingalie naona sitoboi naachana nayo.

Kuna show ya Netflix inaitwa The Circle…. Mi nimeifuatilia na kuipenda, inahusiana na namna ambavyo unaweza kumanipulate watu kupata influence ya mapenzi/urafiki/uongozi…….ukiwa nyuma ya keybord. Unachagua profile unaweka iwe ya uongo au ya ukweli.
Onhoo thank you hii nitaifatilia
 
Kuna mshikaji mmoja natamani nimtag aje atoe neno hapa maana kukiwa na BB siku hiyo mkizubaa hakuna kitakachoendelea kisa anaangalia show.

Maudhui yake nadhani, mbali na kuburudisha hasa katika kizazi hiki kinachoabudu celebrities hata kama hawana kipaji cho chote, ni kuonyesha ushindani; na hasa undumilakuwili na unafiki wa binadamu maana mule hakuna kuaminiana. Hata mtu mnayenyanduana naye anaweza kukugeuka wakati wo wote na kukuleftisha.

Ni show isiyoeleweka hasa katika uwasilishaji wake wa maudhui japo inapendwa sana na vijana wa kizazi kipya wanaotafuta mashujaa wapya na role models katika maisha yao.
Kama wale ni role models wa watoto wetu basi tumeishaaa
 
Mi nilipenda sana maisha plus ila hiyo big brother watu wanafanya vitu vya hovyo kabisa.

Wanapima vitu kibao kama sex intention yaani ile watu wanaoga pamoja wote wapo uchi ,lakini eti mwanaume asione tamaa ila wengine wananyanduana wanashindwa na wanakosa point za kuendelea yaani hovyo sielewi.
Hii imekaa kingono zaidi....na freemason
 
Wanasema ukiona Kipindi hukielewi, huenda haukuwa Mlengwa.

Kutokana na Umri, kwasasa nimekuwa sifatilii Big Brother tena, ingawa wakati nilipokuwa kwenye lika la adolescent nilikuwa muhanga wa kukitazama miaka ile ya Akina Mwisho Mwampamba, baadaye akina Richard n.k

==============
Kuna baadhi ya Filamu/Vipindi vya TV kutokana na maadili yetu havistahili kutazamwa.

Hiyo Program ya Big Brother na nyingine zenye mlengo huo, zimeanzishwa kwaajili ya ku-brainwash Vijana wetu ili waone mambo ya ngono na kukaa na vichupi chupi mbele ya Wazee wao ni jambo la kawaida.

Kama una vijana wako nyumbani, ni heri Remote ikafichwa chumbani kwa Baba.

Ni heri kuitwa Mzee Mnoko kuliko kuharibu kizazi chako kwa mikono yako.
 
Back
Top Bottom