#COVID19 Shirika la Afya Duniani (WHO) laitaka Tanzania kujiandaa kupokea chanjo ya Corona

#COVID19 Shirika la Afya Duniani (WHO) laitaka Tanzania kujiandaa kupokea chanjo ya Corona

Hivi huelewi! Dawa za malaria tunazijua mpaka na 'pharmacodynamic & kinetics! Hiyo chanjo walioikimbiza hatakaharaka baada ya kutengeza kirus ndio hatuielewi na hatuitaki! Na kukazia tu hatuhitaki kuielewa maana tumeshajua lengo lake!
Sasa kwa nini unataka wakuletee chanjo za malaria?
 
Sio tena kutunusuru maiti zetu zisizagae barabaran ifikapo May 2020… hakuna kazi ngumu kama kuulinda Uongo
Kwasababu Tz sio kisiwa kwamba mmejifungia. Wanataka mkienda kwao msiwe tishio kwao
 
Siku moja baada ya Rais wa Tanzania, John Magufuli kutaka wizara ya afya kutokukimbilia chanjo ya Corona, Shirika la Afya Duniani WHO imeitaka nchi hiyo kujiandaa na chanjo ya Corona kama mataifa mengine duniani.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao, mkuu wa WHO kanda ya Afrika Dkt. Matshdiso Moeti amesema kuwa Tanzania inatakiwa kutumia mwanya wa upatikanaji wa chanjo kwa faida ya wananchi na kanda ya Afrika Mashariki kwa ujumla.

''Tumeanza kuwasiliana upya na ngazi za juu za uongozi, na tunatoa mchango wetu kama ilivyokua hapo mwanzo, na tunataka kushirikiana na Tanzania, kwa niaba ya watu wa Tanzania, nchi jirani na dunia kwa ujumla. Sehemu ya mawasiliano yetu na Tanzania ni kukumbusha serikali kuwa, hii ni sehemu ya makubaliano ya kanuni za afya za kimataifa ambapo nchi wanachama wamekubali kwa pamoja kuzuia kusambaa kwa magonjwa'' anasema Dkt. Moeti.

WHO inasema kuwa imekua ikitoa mchango na kuwasiliana na serikali ya Tanzania kuanzia mwanzo wa janga hili la Corona. Shirika hilo pia limesisita Tanzania kutoa takwimu za mwenendo wa Corona nchini Tanzania ili iwe rahisi katika kupambana na kuzuia maambukizi mapya.

Naye katibu mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Ghebreyesus anasema anaunga mkono alichosema @MoetiTshidi, anatoa rai hatua dhabiti za kiafya kukabiliana dhidi ya corona zinapaswa kufuatwa na kujiandaa kupokea chanjo.

Takwimu ni suala la muhimu pia kwa Tanzania kuzitoa, tena baada ya kesi za miongoni mwa wasafiri na wageni katika miezi ya hivi karibuni.

Chanzo: BBC SWAHILI

Ishu ya chanjo hii ya COVID 19 inahusishwa na swala zima la IMANI kuwa chanjo hii ndani yake imebeba alama ya mpinga Kristo 666...

Mch. Josephat Gwajima ndiye mshauri mkuu wa Rais Magufuli kwa sasa kuhusu hili. Kwa lugha nyingine ni kuwa Rais Magufuli, ameamini na anafanya kila linalowezekana kwa kutumia mamlaka yake ya Urais kuwalinda watu wake na Mpinga Kristo na alama 666...

Anaihusisha chanjo ya COVID 19 na na alama ya mpinga Kristo 666 na kuwa yeyote anayeipokea chanjo hiyo anakuwa ameikubali namba na alama ya Mpinga Kristo 666 na kumkana Yesu Kristo...

Lakini swali kubwa ni hili: ATAWEZAJE? Na je, Biblia inasemaje?

Neno la Mungu liko wazi sana. Kwamba, wokovu unamfuata na kupokelewa na mtu mmoja mmoja kwa kadiri anavyosikia Neno la Mungu na kuliamini...

Kwa hiyo, Tanzania ina jumla ya watu wanaokaribia 60,000,000. Neno la Mungu linasema "....kila aaminie ataokoka...."

Neno la Mungu halisemi, "...amri au misimamo ya Rais wa nchi fulani itawaokoa watu wake..."

Rais naye ni mtu. Imani yake kwa Mungu aliye hai ktk Yesu Kristo ndiyo itakayomponya. Kwa hiyo kama anaamini, anafanya vyema sana, amechahua fungu sahihi na salama.

Anachotakiwa kufanya ni kutumia nafasi yake ya Urais kuihubiri injili ya Kristo ili watu waamini na kuchagua uhai badala ya kifo...

Aidha Neno la Mungu linasema, "... kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe. Baba hatachukua dhambi za mwanaye, vivyo hivyo mwana hatabeba dhambi ya wazazi wake...."

Ninachotaka kusema ni hili, kuwa, chanjo ya COVID 19 itaingia Tanzania. Rais Magufuli hawezi kuzuia hili...

Kama ni kweli, chanjo hiyo imebeba alama ya mpinga Kristo 666, basi uamuzi wa kuipokea au kuikataa unabaki wa mtu mmoja mmoja kwa kadiri ya imani yake...

Maana, Mungu anasema hivi; "....Tazama nimeweka LAANA/MAUTI na BARAKA/UZIMA mbele yako. Chagua uzima ili uishi..."

Uchaguzi (choice) uko kwa mtu mwenyewe binafsi kwa kadiri ya kuamini kwake...
 
Habari ya saa hizi waungwana.

Hapa tuache siasa pembeni tulikabili hili swala la Watanzania kulazimishwa chanjo ya Corona. Sitaki kusema au ku judge mengi wala sitaki kufika kwenye point kwamba wanaokufa wengi na mfululizo ni wazungu kuliko waafrika ila tunalazimishwa sana sisi. Wazungu watatuwekea vikwazo vya kijinga jinga na kututenga na nchi za wenzetu wa karibu. Mimi nina wazo moja!

Wazungu wakileta hizo dawa zao SHARTI LA KWANZA! TUNAANZA NA FAMILIA ZA MABALOZI WAO. Yani chanjo zinaingizwa kwenye godown moja. Zinapangwa randomly alafu WATOTO WA MABALOZI WA HUKO NCHI ZA HAO WANAOTUPENDA SANA WANAANZA KUCHOMWA WAO. Mwenye akili achambue asietaka aache. This is my country and I’ll stand by our safety before anything else. Tanzania First 🇹🇿

NB: KICHWA CHA HABARI NILITAKA KUANDIKA BBC YATANGAZA KUWA WHO YAITAKA TANZANIA KUJIANDAA NA CHANJO YA CORONA. Typing error.
 
Wazilete tu hawakumbuki yale mabarakoa tuliyafanza nini eh shenziii
 
Taarifa nilizonazo baada ya kukagua website ya WHO kwa haraka haraka sikuona mahali zilipo maabara za WHO za kuzalisha na kufanyia majaribio ya chanjo hizo wanazofekea watu!
Una busara sana, Mungu akubariki sana kwa mchango wako wenye mshiko - sema ni kweli by 100%, WHO hawana maabara za utafiti wala Viwanda vya kutengeneza dawa wala chanjo - wanategemea viwanda vya makampuni binafsi predominantly kutoka mataifa ya magharibi, madawa na chanjo zinazo zalishwa Uchina na Urusi vinatoka kwenye viwanda vya Serikali.

Asilimia kubwa ya mchango wa fedha zinazo tumika kuendesha W. H. O unatolewa na Serikali ya Merikani, hivyo asilimia kubwa ya vitengo nyeti kwenye taasisi ya WHO vinakuwa headed na wafanyakazi wenye asili ya USA - mwisho wa siku Big Pharma Companies za Merikani na washirika wake wa Ulaya ndio zinapewa kupa umbele kwenye masuala ya ku-supply madawa na Chanjo kwa WHO ili yasambazwe Duniani.

Hivyo ni wazi Amerika ina sauti na ushawishi mkubwa ndani ya WHO,hivyo Makampuni makubwa ya madawa kutoka USA ni rahisi ku-manipulate shirika linavyo endeshwa, kama ulivyo sema hii inatoa mwanya wa uwezekano mkubwa WHO kutumiwa vibaya na nchi zenye hila -na hicho ndicho kinacho endelea, once again be Blessed.
 
Wazilete tu hawakumbuki yale mabarakoa tuliyafanza nini eh shenziii
Mi nakwambia yaani wakileta tu wasitupangie uchomaji. Sisi tutawachoma watoto wa mabalozi wao. Wao ndo watakua sampuli zetu. Wazungu wasitufanye sisi sokwe. Ubalozi wa marekani.

Sijui uingereza sijui takataka gani wote wajiandae hata kama ni kuwanywesha kwa nguvu. We are independent mkitaka kutulazimisha chanjo na sisi tutaweka utaratibu wetu ili wote turidhike
 
Kwahio mfano wa hii sumu ya Corona wakiwapa wananchi wao inakuwa pipi, ngozi nyeusi inakuwa sumu ? Na ungejua Capitalist Countries wanatuhitaji sisi tukiwa hai (as a market, labor force and source of raw materials) haya yote usingesema...
Unapokuwa na chuki juu ya mtu unapoteza uwezo wa muona wa mambo! Kama unataka kuwa panya wa maabara we nenda kadungwe tu!
 
Sio BBC bwana,ni WHO
Thanks kwa kunikumbusha ni typing error nlikua naandika kwa haraka maana kichwa kishawaka hapa kwa hasira😂😂 KICHWA CHA HABARI NILITAKA KUANDIKA BBC YATANGAZA KUWA WHO YAITAKA TANZANIA KUJIANDAA NA CHANJO YA CORONA. Typing error.
 
Mpaka kitaeleweka tu. Meko kama kawaida aliropoka tu bila kujua kwamba anabanwa na makubaliano ya Kiafya ya WHO.
Kwa hiyo unataka kuja kufanyiwa majaribio? Nchi za Nordic watu wamekufa baada ya kupewa hiyo chanjo, watu hamuoni?

Wailete tu na wawape mnaoitaka. Maana naona mnaipenda sana!
 
kwa hiyo unadhani hiyo chanjo inafanya kazi au, tumia akili China wanatumia chanjo yao, U. S wanatumia yao, na Ulaya nao Yao kwanini wasitumie chanjo moja endelea na ushakibi
Chanjo yetu iko wapi ndugu tuitumie?

Umesema China na USA wanachanjo zao, tuoneshe chanjo ya Tanzania tuitumie boss
 
Kwa hiyo unataka kuja kufanyiwa majaribio? Nchi za Nordic watu wamekufa baada ya kupewa hiyo chanjo, watu hamuoni?

Wailete tu na wawape mnaoitaka. Maana naona mnaipenda sana!
Hii chanjo jau, wailete tuje tuichome mbwa mm sitaenda kuchanjwa bora waniuwe
 
Dunia ni Kijiji, vyema tupate hizo chanjo ili kuruhusu watu waendelee na biashara zao hasa za kusafiri bila kuwekewa vikwazo vya kusafiri.

Tukikaidi kupewa chanjo hakuna Mtanzania ataruhusiwa kusafiri nje ya Mipaka.
Watu wengi hamna taarifa za kutosha. Unajua kwamba ukishapata chanjo bado utaendelea kuvaa barakoa na tahadhari zingine?

Ni vema mjitahidi kupata taarifa sahihi kabla ya kuweka ushabiki kwenye afya zenu. Kumbuka uhai hauna shamba kwamba utavuna tena. Ukiondoka haurudi. Nakuwekea hapo chini baadhi ya taarifa za CDC. Soma mwenyewe kama lugha ya wenyewe inapanda, amua mwenyewe kwa kuwa na taarifa sahihi.

1611860544261.jpg



1611860521855.jpg
 
Chanjo yetu iko wapi ndugu tuitumie?

Umesema China na USA wanachanjo zao, tuoneshe chanjo ya Tanzania tuitumie boss
natural immunity has already built in our body, ugonjwa umetokea mwaka jana mpaka leo tupo it's means our bodies are resistitive to that diseases.
 
Back
Top Bottom