#COVID19 Shirika la Afya Duniani (WHO) laitaka Tanzania kujiandaa kupokea chanjo ya Corona

#COVID19 Shirika la Afya Duniani (WHO) laitaka Tanzania kujiandaa kupokea chanjo ya Corona

Kuhusu Chanjo, ni kweli Tanzania sio kisiwa hivyo kwa niaba ya wananchi, serikali Ina wajibu wa kukubaliana na suala la Chanjo kwa raia wake.
Lakini suala la kutangaza taarifa sidhani Kama linaathiri mapambano dhida ya janga Hilo.
Mkuu kuna sehemu jpm alisema kuwa hatapokea au hataki chanjo ya corona?

Mimi ninachojua kilichosemwa na jpm ni kuwa wizara ya afya iwe makini katika upokeaji Wa chanjo

Tuache kumlisha rais wetu maneno ambayo hana uhusiano nayo.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Serikali lazima ikubali kupokea chanjo na kama inakataa lazima kuwa na hoja za msingi sana za kushawishi kuwa sio chanjo bora au ina shida. lakini kuikataa tuu haitawezekana kwa sababu uchumi wetu na kila kitu kinategemea muingiliano wa watu ni lazima chanjo tukubali kwani hili ni jambo jema kwani tuna chanjo nyingi sana tumezikubali na zimeonesha ufanisi mkubwa. Serikali kukataa chanjo ni kuua watu wasio na hatia.

Tumesaini mikataba mingi ya kimataifa lazima tukubali chanjo hii.
Swala la chanjo ni lazima.
Hatutaki chanjo sisi!

Una uhakika kama hiyo chanjo ndiyo aliyopigwa biden na kutumika nchi za Ulaya

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Wahenga walisema usipo sikia la Mkuu Utavujika mguu!

EEH MWENYEZI MUNGU TUFUNIKE CHINI YA MBAWA ZAKO!

KWA AKILI ZETU NA NGUVU ZETU HATUYAWEZI!

HIVYO TUNAJISALIMISHA CHINI YA ULINZI WA MKONO WAKO THABITI!

UTAKALO WEWE LIFANYIKE!
A M E N[emoji120]
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mwisho wa siku hii chanjo tutapewa bure huku wengine wakiinunua kwa gharama mara mbili!

Saa nyingine mikwara ya JPM inasaidia sana.
Hahahaaaaa 😅😅😅😅😅
 
Mkuu kuna sehemu jpm alisema kuwa hatapokea au hataki chanjo ya corona?

Mimi ninachojua kilichosemwa na jpm ni kuwa wizara ya afya iwe makini katika upokeaji Wa chanjo

Tuache kumlisha rais wetu maneno ambayo hana uhusiano nayo.


Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Kuhusu watu walioenda nje wakachanjwa huko na kutuletea korona za ajabu ajabu ulimsikia akisema?au masikio yako yanachagua cha kusikia?
 
Ila Hawa wazungu, mambo ya chanjo tena aaaaagh[emoji21]
 
Nimekagua maktaba ya Taifa kuona kama kuna Rais yeyote wa Afrika aliyewahi kupambana na the so called mabeberu akashinda. Aibu inamnyemelea Jiwe.
Ulipo kagua, kwani uliwahi kusikia au kuona aliyekuwa anapambana nao alikuwa ni Magufuli au tu anakaribiana na 'calliber' ya Magufuli akiwa na Mungu na watz wakim'back-up'!?

Record nyingine inakwenda kuwekwa duniani na jembe letu kwa neema ya Mungu! Tuombe uzima tu!

Hawa mabwana zenu wanaoharakisha kuwachanja watu watafute pa kuchificha 'very soon' pale wachanjwaji kutoka kote duniani watakapo lipuka kutokana na madhara yatokanayo na michanjo uchwara hii! Just wait and see 😳🙄🤫!
 
Kwa hivyo tutachanjwa kwa lazima whether we like it or not!

Mimi nasimama na Jiwe hachanjwi mtu hapa hahaa!
Shitholes hakuna openness kama huko walikostaarabika ambako tuliona viongozi mbalimbali wakipata chanjo (tulivyo wazushi hatukawii kusema changa la macho); huku kwetu mambo ni sirini sio ajabu huyo unayesimama naye alishachanjwa siku nyingi sirini endelea kuwa mjinga.
 
Mwanzo baada ya serikali kuacha kutoa takwimu tuliambiwa tutatengwa hadi na majirani ila naona lilipita hilo,sasa hivi limekuja la chanjo hebu tuone nalo litaishiaje.
 
It is a small World after all. Kama Dunia ilivyopambana na magonjwa ya kutisha polio, kifua kikuu, Ebola (ambayo bado inasumbua) Surua n.k. ndiyo hivyo hivyo juhudi ya Dunia yote kwa kushirikiana na WHO inahitajika ili kupambana na COVID-19. Huyo anayejiita mwendawazimu hana ubavu wowote wa kushindana na Dunia.
Mpaka kitaeleweka tu. Meko kama kawaida aliropoka tu bila kujua kwamba anabanwa na makubaliano ya Kiafya ya WHO.
 
Siku moja baada ya Rais wa Tanzania, John Magufuli kutaka wizara ya afya kutokukimbilia chanjo ya Corona, Shirika la Afya Duniani WHO imeitaka nchi hiyo kujiandaa na chanjo ya Corona kama mataifa mengine duniani.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao, mkuu wa WHO kanda ya Afrika Dkt. Matshdiso Moeti amesema kuwa Tanzania inatakiwa kutumia mwanya wa upatikanaji wa chanjo kwa faida ya wananchi na kanda ya Afrika Mashariki kwa ujumla.

''Tumeanza kuwasiliana upya na ngazi za juu za uongozi, na tunatoa mchango wetu kama ilivyokua hapo mwanzo, na tunataka kushirikiana na Tanzania, kwa niaba ya watu wa Tanzania, nchi jirani na dunia kwa ujumla. Sehemu ya mawasiliano yetu na Tanzania ni kukumbusha serikali kuwa, hii ni sehemu ya makubaliano ya kanuni za afya za kimataifa ambapo nchi wanachama wamekubali kwa pamoja kuzuia kusambaa kwa magonjwa'' anasema Dkt. Moeti.

WHO inasema kuwa imekua ikitoa mchango na kuwasiliana na serikali ya Tanzania kuanzia mwanzo wa janga hili la Corona.
Shirika hilo pia limesisita Tanzania kutoa takwimu za mwenendo wa Corona nchini Tanzania ili iwe rahisi katika kupambana na kuzuia maambukizi mapya.

Naye katibu mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Ghebreyesus anasema anaunga mkono alichosema @MoetiTshidi, anatoa rai hatua dhabiti za kiafya kukabiliana dhidi ya corona zinapaswa kufuatwa na kujiandaa kupokea chanjo.

Takwimu ni suala la muhimu pia kwa Tanzania kuzitoa, tena baada ya kesi za miongoni mwa wasafiri na wageni katika miezi ya hivi karibuni.

Chanzo: BBC SWAHILI

Si inauzwa mbona wanalazimisha kutupa wana nini hawa
 
Serikali lazima ikubali kupokea chanjo na kama inakataa lazima kuwa na hoja za msingi sana za kushawishi kuwa sio chanjo bora au ina shida. lakini kuikataa tuu haitawezekana kwa sababu uchumi wetu na kila kitu kinategemea muingiliano wa watu ni lazima chanjo tukubali kwani hili ni jambo jema kwani tuna chanjo nyingi sana tumezikubali na zimeonesha ufanisi mkubwa..... Serikali kukataa chanjo ni kuua watu wasio na hatia...

Tumesaini mikataba mingi ya kimataifa lazima tukubali chanjo hii....
Swala la chanjo ni lazima.
mkiambiwa mnaburuzwa na ZWAZWA wenu matokeo ndio haya
 
wakati wenzangu mnawaza hayo ya chanjo mi nawaza kama ningemjua aliyetenegeneza hicho kirusi ningemng'ang'ania koromero na kulinyofoa😳
 
Back
Top Bottom