Shirika la DDC Kuchukua Ardhi huko Mbopo, Kinondo na Mabwepande kutoka kwa Wananchi ni Uporaji

Shirika la DDC Kuchukua Ardhi huko Mbopo, Kinondo na Mabwepande kutoka kwa Wananchi ni Uporaji

Ninajua vizuri sana hili sakata na kesho nitakuja na Uzi kuhusu eneo hili ambalo aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi Ridhiwan Kikwete aliwauzia wawekezaji kutoka Uturuki bila uhalali Sasa mwekezaji aliyeuziwa anadai eneo lake anataka kujenga malls. Ridhiwan aliwadanganya Waturuki eti eneo hilo ni pori na akaliondoa kwenye ramani ya google. Dogo jizi sana.
Bora hata Lukuvi! Japo na yeye ni mwana CCM yule yule lakini angalau mambl ya ardhi alikuwa anayaweka sawa kwa kiasi fulani

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Mleta mada anaelekea ni mmoja wa wavamizi huko. Ni hivi DDC wana hati ya miaka 99 tangu miaka ya 1970. Mmeenda huko kichwakichwa mkauziwa mkapigwa na madalali wezi . Sasa DDC wanataka eneo lao haki yao wengi humo wamekaa miaka 5 HADI 7 tu hawana haki ya adverse possesion . DDC wamewapa nafasi ya kukubaliana mlipe kidogo mnakataa. Kwanza mlitakiwa mnyongwe wezi wakubwa kama Magufuli.
Hata pale wazo kiwanda cha cement ni hivo hivo. LIPA AU ONDOKA BAAASI.
Hivi hao DDC wanakuwa ni wazalendo wanapigania ardhi ya serikali au watendaji wana lao jambo?

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Vingunguti ni eneo la Shirika la Reli la Tanzania
 
Maeneo kadhaa huko Mbopo, Kinondo na sehemu fulani huko Mabwepande shirika la DDC linadaiwa kuvamia raia na kuyapora maeneo wakidai ni ya kwao. Nyumba zinavunjwa viwanja walivyonunua wananchi kwa taratibu kabisa na uwepo wa wajumbe wa maeneo husika lakini wanakuja kuwapora huu ni uvunjifu wa HAKI za binadamu na haikubaliki kunyanyasa raia wa nchi hii.

Ombi kwa serikali kuu ingilieni mtafaruku huu utasababisha uvunjifu wa amani pasipo sababu zozote. Muda wote walikuwa wapi hao DDC wakavizia wananchi wameuziwa na kujenga nyumba kisha waende kupora ardhi na kuvunja nyumba zao bila fidia?

Mada iko mezani wadau na wanasheria jitokezeni kukomesha uonevu huu. Mbunge wa Kawe yuko wapi?
Tatizo letu wa Tanzania Tunapenda Mteremko! Eneo ni la DDC walipewa miaka ya 70, Serikali ikijuwa kuwa mji wa Dar utapanuka! Mfano pale palipojengwa Hosp ya Mlonga nzira Serikali ilipagawa kwa Muhimbili miaka mingi sana hiliyopita enzi ya Mwalimu Nyerere. Ukiwa smart unatakiwa nunua kiwanja kilichopimwa na sio skwata. Tuache kulia lia
 
Kirefu chake ni 'District Development Cooperation-DDC' likijumuisha wilaya zote za wakati huo za Dar Es Salaam ambalo lilianzishwa na serikali mnamo tarehe 18/5/1971 na miradi yake ilikuwa DDC Kariakoo, DDC Mlimani, DDC Magomeni, DDC Keko, Garage, Mashamba nk
Wee mtu DDC ni Dar es Salaam Development Corporation-Shirika la Maendeleo la Dar es Salaam
 
Hilo suala la Mbopo, Mabwepande, Kinondo, Malolo na maeneo ya karibu na huko ni mfupa mgumu ambao Lisu na CHADEMA wameamua kuutafuna. Tusubiri tuone mwisho wake maana ndani ya huu mgogoro kati ya DDC na hao wananchi wa huko kuna mambo mengi yenye utata sana na hayaelezeki kabisa katika hali ya kawaida:-

Mfano mdogo tu ni:-
1. Juu ya hati ya hilo eneo ambalo DDC wanasema wanalimiliki kuna wananchi zaidi ya 100 wana hati halali. Hati juu ya hati tena 100 ni Mabwe pande, Mbopo, Malolo, Kinondo na meneo ya karibu na huko ndio pekee yake duniani unaweza
kukuta hili jambo.
2. DDC wanasema ni eneo lao lakini wakifika kwa watu ambao wanafanya kazi kwenye vyombo vya dola, wastaafu waliokuwa na dhamana serikalini na matajiri wanawaruka hawagusi ardhi zao badala yake wanaenda kupora ardhi ya wasio na uwezo.
3. DDC sio kampuni ya upimaji ardhi na hakuna sehemu popote inayoonyesha kuwa wao ni wataalamu wa mipango miji lakini inasemekana wao ndio wanapima ardhi na kupanga mji - kuna nini hapa?
4. DDC wanapima viwanja vya 20 X 20 ambavyo serikali kupitia waziri Mabula alikataa ukubwa huo wa viwanja wao wamepata wapi hayo mamlaka kwenda kinyume na waziri? Na ardhi iliyobaki wanaichukua wao baada ya kumuachia 20 x 20 waliyemkuta kwenyeneneo hilo. Kwa wale ambao hawajajenga wantwaa ardhi yote.

Hayo ni machache tu yapo mengi kwenye huo mgogoro na kubwa zaidi wale wote wenye dhamana wanauogopa huo mgogoro labda tungojee Mheshimiwa raisi Samia mwenyewe aje aingilie kati na kuutatua kwa kuwa wasaidizi wake wote wanauogopa. Na mbaya zaidi hata Gwajima na ujanja wake wote na ambaye ndiye mbunge wa hilo eneo japo aliingilia kati kwa mbwembwe baada ya kupewa vielelezo na kujiridhisha kuwa wananchi wana haki na yeye katulizwa ghafla.
 
Nimepata taarifa hapa kuwa mkuu wa mkoa anaenda huko ijumaa hii saa nne asubuhi. Kama amepata taarifa sahihi na anakwenda kuumaliza huo mgogoro litakuwa jambo jema sana kwa wakazi wa huko hasa ukizingatia wao wapo hapo zaidi ya miaka 40 (tangu 1970). Je DDC alikuwa wapi muda wote huo zaidi ya miaka 40 mpaka aibuke sasa hivi?
 
Bora hata Lukuvi! Japo na yeye ni mwana CCM yule yule lakini angalau mambl ya ardhi alikuwa anayaweka sawa kwa kiasi fulani

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app



Ingawa hili hakutaka kulitatua mpaka akatumbuliwa.

Serikali Kwanini kwa miaka mingi mgogoro wa ardhi Mbopo hautatuliwi na kuisha ibaki historia?
 
Hilo suala la Mbopo, Mabwepande, Kinondo, Malolo na maeneo ya karibu na huko ni mfupa mgumu ambao Lisu na CHADEMA wameamua kuutafuna. Tusubiri tuone mwisho wake maana ndani ya huu mgogoro kati ya DDC na hao wananchi wa huko kuna mambo mengi yenye utata sana na hayaelezeki kabisa katika hali ya kawaida:-

Mfano mdogo tu ni:-
1. Juu ya hati ya hilo eneo ambalo DDC wanasema wanalimiliki kuna wananchi zaidi ya 100 wana hati halali. Hati juu ya hati tena 100 ni Mabwe pande, Mbopo, Malolo, Kinondo na meneo ya karibu na huko ndio pekee yake duniani unaweza
kukuta hili jambo.
2. DDC wanasema ni eneo lao lakini wakifika kwa watu ambao wanafanya kazi kwenye vyombo vya dola, wastaafu waliokuwa na dhamana serikalini na matajiri wanawaruka hawagusi ardhi zao badala yake wanaenda kupora ardhi ya wasio na uwezo.
3. DDC sio kampuni ya upimaji ardhi na hakuna sehemu popote inayoonyesha kuwa wao ni wataalamu wa mipango miji lakini inasemekana wao ndio wanapima ardhi na kupanga mji - kuna nini hapa?
4. DDC wanapima viwanja vya 20 X 20 ambavyo serikali kupitia waziri Mabula alikataa ukubwa huo wa viwanja wao wamepata wapi hayo mamlaka kwenda kinyume na waziri? Na ardhi iliyobaki wanaichukua wao baada ya kumuachia 20 x 20 waliyemkuta kwenyeneneo hilo. Kwa wale ambao hawajajenga wantwaa ardhi yote.

Hayo ni machache tu yapo mengi kwenye huo mgogoro na kubwa zaidi wale wote wenye dhamana wanauogopa huo mgogoro labda tungojee Mheshimiwa raisi Samia mwenyewe aje aingilie kati na kuutatua kwa kuwa wasaidizi wake wote wanauogopa. Na mbaya zaidi hata Gwajima na ujanja wake wote na ambaye ndiye mbunge wa hilo eneo japo aliingilia kati kwa mbwembwe baada ya kupewa vielelezo na kujiridhisha kuwa wananchi wana haki na yeye katulizwa ghafla.

Poleni sana ,uvamizi wa rdhi upo maeneo mengi sana ,hata Efatha naye hayupo nyuma kwenye uvamizi.
 
Serikali wananchi walovamiwa na kuchukuliwa maeneo yao kuwa imeshindikana kutatua huo mgogoro ili wenyewe wajue cha kufanya.
 
Wavamizi wanaendelea kufaidika kutumia maeneo ya watu wakati wamiliki halali wakiendelea kurejesha mikopo walokokopa kununua maeneo hayo.

Hii haikubaliki.
 
Nimepata taarifa hapa kuwa mkuu wa mkoa anaenda huko ijumaa hii saa nne asubuhi. Kama amepata taarifa sahihi na anakwenda kuumaliza huo mgogoro litakuwa jambo jema sana kwa wakazi wa huko hasa ukizingatia wao wapo hapo zaidi ya miaka 40 (tangu 1970). Je DDC alikuwa wapi muda wote huo zaidi ya miaka 40 mpaka aibuke sasa hivi?
DDC wana hati miliki hadi mwaka 2070 (miaka 99-1971 hadi 2070)na wanalipia,muda huu ndiyo wameamua kulitumia eneo lao suala la walikuwa wapi halihusiani.
 
*Excellent dedication to Hon. MP Halima Mdee for seriously speaking out for the voiceless citizens in the Kawe constituency whose land plots were recently looted by the so-called DDC at Mbopo Pande, Kinondo, Msumi Mabwe, Malolo, Nyakasangwa and Bunju. Ms. Halima Mdee (Esq) and Mr. Tundu A Lissu (Esq) have won a gold accolade for voicing the pinch the citizens are inflicted by irresponsible government officials. Hopefully, the robbed land shall be restored to the citizens or compensated for the multi-complex loss they sustained during the robbing and demolishing process in an injustice manner outrageously violating human rights with impunity that overrides natural justice.

Due diligence contending for the under-dogged citizens is the spirit of the committed and responsible leaders of the courageous leaders mentioned above

xxxxx
Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Mbunge Halima Mdee kwa kuwasemea kwa umakini wananchi wasio na sauti katika Jimbo la Kawe ambao viwanja vyao vya ardhi viliporwa hivi karibuni na wale wanaoitwa DDC katika maeneo ya Mbopo Pande, Kinondo, Msumi Mabwe, Malolo , Nyakasangwa na Bunju. Bi Halima Mdee (Esq) na Mhe. Tundu Lissu (Esq) wameshinda tuzo ya dhahabu kwa kukemea ubadhirifu ambao wanafanyiwa wananchi wasio na nafasi ya kujitetea dhidi ya viongozi wa serikali wasiowajibika. Ni matumaini yetu kuwa, ardhi iliyoprwa itarejeshwa kwa wananchi au kulipwa fidia kwa hasara nyingi walizopata wakati wa mchakato wa ukwapuaji na ubomoaji huo kwa njia ya dhuluma inayokiuka haki za binadamu bila kuzingatia haki ya asili.

Kwa sababu ya bidii ya kuwapigania wananchi wasio na sifa ni roho ya viongozi waliojitolea na kuwajibika wa wanandoa waliofukuzwa hapo juu.

Link:
 
Alikuwa mbunge kwa muda mrefu kule alishindwa kufuatilia na kutatua migogoro hiyo?

Tena huenda ilijitokeza akiwa yeye ni mbunge.

Leo anataka kusemaje Kwa mfano?

Imebaki siasa tu?!
 
Maeneo kadhaa huko Mbopo, Kinondo na sehemu fulani huko Mabwepande shirika la DDC linadaiwa kuvamia raia na kuyapora maeneo wakidai ni ya kwao. Nyumba zinavunjwa viwanja walivyonunua wananchi kwa taratibu kabisa na uwepo wa wajumbe wa maeneo husika lakini wanakuja kuwapora huu ni uvunjifu wa HAKI za binadamu na haikubaliki kunyanyasa raia wa nchi hii.

Ombi kwa serikali kuu ingilieni mtafaruku huu utasababisha uvunjifu wa amani pasipo sababu zozote. Muda wote walikuwa wapi hao DDC wakavizia wananchi wameuziwa na kujenga nyumba kisha waende kupora ardhi na kuvunja nyumba zao bila fidia?

Mada iko mezani wadau na wanasheria jitokezeni kukomesha uonevu huu. Mbunge wa Kawe yuko wapi?
Mabwepande, Mbopo-Kawe

Jumamosi, 1/7/2023
Mkutano wa RC-DSM na wananchi
Ngoma nzito

Jumapili, 2/7/2023
Mkutano wa M/kiti CDM Tundu A. Lissu na wananchi
Maswali magumu yaibuliwa
1. 1981 uongozi wa Dar kipindi hicho ulikataa maombi ya DDC kupewa ekari 1,931 mabwepande
2. 1984 DDC walifanya namna wakapewa hizo ekari 1,931 ikijumuisha mtaa wa Mbopo

Maswali magumu

1. Serikali au DDC ilitoa taarifa kwa wakazi wa eneo hilo kabla halijatwaliwa?
2. Kuna mthamini wa ardhi kutoka katika taasisi ya serikali alitumwa kwenda kutathmini thamani ya ardhi ambayo ilitakiwa kupewa DDC na wakazi wake wakalipwa fidia?
3. Ni mkazi gani wa eneo la Mabwepande na Mbopo alilipwa fidia kwa kutwalia eneo lake?
4. Je, DDC walifuata taratibu za umiliki ardhi ya ekari 1,931?
5. Je, nyaraka walizonazo DDC kuhusu umiliki la eneo la Mbopo Mabwepande ni halali?
6. Je, kuna tangazo la serikali au tamko la Rais la kufuta kijiji cha Mbopo Mabwepande na kuwaa eneo lao kwa matumizi ya umma?
7. Je, DDC wana miliki ardhi ya ekari 1,931 kwa kuzingatia sheria na taratibu katika kijiji cha Mabwepande na mtaa wa Mbopo?

Kama maswali hayana majibu kwa ushaihidi usio na shaka basi DDC hawana ardhi Mabwepande na Mbopo.
 
RC Chalamila ameongea vizuri sana juzi Na wananchi wamemuelewa.

Sasa mgogoro unaenda kuisha itabaki historia tu.

RC Chalamila songa mbele ktk kutatua mgogoro huo.
 
Na swala la bei wazingatie bei ya soko ya serikali na sio binafsi.

Kwani leo serikali ikiamua kupima viwanja Na kuuza maeneo Ya Dar katika Wilaya zake wangeuza kwa bei gani kwa square meter moja Kwa mfano?
 
RC Chalamila ameongea vizuri sana juzi Na wananchi wamemuelewa.

Sasa mgogoro unaenda kuisha itabaki historia tu.

RC Chalamila songa mbele ktk kutatua mgogoro huo.
Ameongea vizuri kitu gani kwa kuanza kutoa vitisho badala ya busara za kiuongozi?
Kutaka wananchi walipishwe shilingi 6500/4000 kwa mraba wa mita analomiliki mwananchi?

DDC alimlipa fidia nani wakati anapewa kumiliki hekari 1,931?
 
Ameongea vizuri kitu gani kwa kuanza kutoa vitisho badala ya busara za kiuongozi?
Kutaka wananchi walipishwe shilingi 6500/4000 kwa mraba wa mita analomiliki mwananchi?

DDC alimlipa fidia nani wakati anapewa kumiliki hekari 1,931?



Ameshasema kila mtu anajua mwenyewe namna alivyopata eneo pale maana wengine waliuziwa kwa bei chee sawa na bure,

Wengine walifanya kuvamia maeneo ya watu ,

N.k.

Sasa kama mtu aliuziwa kwa bei sawa na bure inabidi anunue kwa bei halali awe mmiliki halali.

Ndiyo maana nikauliza hivi;

Je serikali ingeamua kupima na kuuza maeneo kule Mbopo kuuzia wananchi ingeuza kwa shilingi ngapi kwa SQM kwa bei ya soko ?
 
Ameshasema kila mtu anajua mwenyewe namna alivyopata eneo pale maana wengine waliuziwa kwa bei chee sawa na bure,

Wengine walifanya kuvamia maeneo ya watu ,

N.k.

Sasa kama mtu aliuziwa kwa bei sawa na bure inabidi anunue kwa bei halali awe mmiliki halali.

Ndiyo maana nikauliza hivi;

Je serikali ingeamua kupima na kuuza maeneo kule Mbopo kuuzia wananchi ingeuza kwa shilingi ngapi kwa SQM kwa bei ya soko ?
Kipi kilitangulia kuwepo maeneo ya Mabwepande na Mbopo na umiliki wa ardhi kwa hati yenye shaka.

Kama vijiji hivyo vilikuwepo kabla ya madai ya ya DDC kumiliki eneo hilo, je nani alifuta ahati ya kijiji na kubadilisha matumizi ya ardhi?
Je, wataalamu wa ardhi walitumwa kwenda kufanya tathimini ya thamani ya ardhi hiyo na fidia kulipwa kwa wanakijiji?

Je, kuna uthibitisho wowote kwamba serikali au sshirika la DDC lilipa fidia kutwaa eneo eneo la la Mabwepande an Mbopo?

Kutumia nguvu kunyanyasa wananchi kisa ni dola ni uharifu usiokubalika popote Tanzania.
 
Back
Top Bottom