Should Maximo stay and enjoy the money 4 nothing? - Contract to be renewed?

Should Maximo stay and enjoy the money 4 nothing? - Contract to be renewed?

Tatizo mfumo hata angekuja Dunga au Arsen au hata Ferguson bila kuwa na mfumo kazi bure,lakini juu ya yote Maximo sio coach ni msanii aliyejaa kibri na uwezo wake ndio umefikia mwisho hana jipya na nibora awapishe wengine yeye abaki na kucheza filamu bana
 
Kwangu mimi sioni tatizo la Maximo. Bali naliona tatizo letu sisi kama watanzania, ambao kikweli hupenda kuvuna bila ya kupanda. Timu ya taifa ya taifa lolote sio mahali pa kukuza vipaji kama tunavyomtaraji Maximo afanye. Timu ya taifa iliyojengwa kwa misingi imara kutoka kwenye football academy ambako mtu akichaguliwa timu ya taifa kutokana na nidhamu ya kitaaluma aliyonayo ataona fahari na sio kufanya ubishoo kama wanavyofanya masupastaa wa bongo. Nakubaliana na msimamo wa Maximo ya kusisitiza nidhamu japokuwa sio kazi yake persee anajikuta analazimika kulifanya hilo kwa sababu halipo. Kiwango cha mchezaji wa team ya taifa hafundishiwi nidhamu katika timu ya taifa bali ni kwenye ngazi za chini alikotoka na mwisho kabisa ngazi ya vilabu.

Mziray ni lazima aseme kwa sababu mafanikio yoyote ya Maximo kwake kama kocha wa kitanzania ni mwiba. Mzirai sio mgana ni mtanzania tumekuwa naye hapa miaka dahari, amefundisha yanga ule mpira wa kesho mechi tukalale makaburini, mkienda Misri makaburi atawaonyesha nani?

Soka yetu kama walivyochangia wachangiaji wengine hapo juu inahitaji zaidi ya kocha mzuri. Tunahitaji maandalizi tuwe na vitalu kama mpango wa taifa wa namna ya kukuza vipaji na ajira, pili vilabu ama viwezeshwe au vione haja ya kuwa na yanga academy, simba academy, mtibwa nk.

Bila hivyo hata tukisubiri kocha bora ambaye timu ya taifa anayoiongoza ikimaliza kazi ya kuchukua kombe la dunia SA mwaka 2010 halafu tumchukue sisi tutaja mtusi hivihivi tunavyofanya kwa Maximo kwani hatuna maandalizi badala yake tunajiandaa kushangilia bila kuwa na mkakati wa ushindi.

Ili tuwe fair kama wananchi na wanamichezo, tumpongeze Maximo kwa hatua aliyotufikisha kwani hatukuwa hapa tulipo. Tujiulize kwanini hatutoki hapa tulipo mimi nina hakika kwamba tatizo letu ni kukosa mkakati wa maana kama taifa wa ushindi. Mambo mema hayataki haraka ati.
 
Tanzania inapoteza hela bure kutafuta makocha wa kigeni..fedha hizo zingetumika katika program nyingine za kukuza vipaji,kujenga vyuo vya soka,kuwafundisha wataalamu wetu wa kizalendo,ambao ndo wanajuwa mahitaji ya soka yetu na wanawajuwa vijana wetu,na wanaeleweka vizuri..tukakuza vijana tokea Juvenile...junior...central mpaka seniors...tukiwa na makocha hao hao akina Mashi na Mkwasa. Si tumeona Kombe la dunia la vijana U-17,Nigeria, watoto wa Kiswiss wanakanyaga gozi la ng'ombe kama watu wazima,wanasema watoto wale wamehamishwa makwao na wengi wapo katika vyuo vya soka wakikuzwa vipaji vyao...na U-swiss wanatarajia kuwa na timu tishio ya taifa kutoka na vijana wale muda si mrefu(wale wtoto si masikhara wanaujuwa hasa)..kwanini tusiwekeze kwenye program kama hizo...kama tumeweza kujenga uwanja kwanini tusijenge chuo cha michezo kukuza vipaji...wachezaji tulionao Stars wanacheza kama wamejifunza mpira ukubwani vile...hawana skills...hawafundishiki..ni aibu kusema timu ya taifa inafundishwa na kocha wa kigeni.
kwanza wawashe umeme nchi nzima na waweke kila mahali maji ya bomba ndio baadae waanze kujenga hayo mavyuo ya soka.
 
halafu mbona huyu mziray kamkomalia sana maximo???Mziray banaa namjua in out hana lolote hata mpira haujui than kubahatisha sana tu mambo yake mpaka hapo alipo....amshukuru mungu wake mbonaaaaa.
 
Tanzania inapoteza hela bure kutafuta makocha wa kigeni..fedha hizo zingetumika katika program nyingine za kukuza vipaji,kujenga vyuo vya soka,kuwafundisha wataalamu wetu wa kizalendo,ambao ndo wanajuwa mahitaji ya soka yetu na wanawajuwa vijana wetu,na wanaeleweka vizuri..tukakuza vijana tokea Juvenile...junior...central mpaka seniors...tukiwa na makocha hao hao akina Mashi na Mkwasa. Si tumeona Kombe la dunia la vijana U-17,Nigeria, watoto wa Kiswiss wanakanyaga gozi la ng'ombe kama watu wazima,wanasema watoto wale wamehamishwa makwao na wengi wapo katika vyuo vya soka wakikuzwa vipaji vyao...na U-swiss wanatarajia kuwa na timu tishio ya taifa kutoka na vijana wale muda si mrefu(wale wtoto si masikhara wanaujuwa hasa)..kwanini tusiwekeze kwenye program kama hizo...kama tumeweza kujenga uwanja kwanini tusijenge chuo cha michezo kukuza vipaji...wachezaji tulionao Stars wanacheza kama wamejifunza mpira ukubwani vile...hawana skills...hawafundishiki..ni aibu kusema timu ya taifa inafundishwa na kocha wa kigeni.
Junius ukiacha masuala ya Zanzibara na ud... unaongea pointi kwelikweli. Mafanikio yeyote yanaletwa na kuanzia chini kabisa.

maximo katumia cv ya nchi yake kupata kazi tanzania na sisi tulivyo wavivu wakumchambua mtu kabla hatujamuajili ndio maana tumeangukia kwake.
Point tupu

huyo Maximo anatugeuza sisi kuwa kichwa ya mwendazimu..hana jipya wala nini...kashatuchukua sehumu ambayo uwezo wake inamruhusu...hana first 11 mpaka leo anakula mshahara ya bure tuu..TFF nayo wajinga wanamuogopa....maximo atuachie timu yetu...Mpeni Timu Patrick Phiri tutaona mwanga and timu itakuwa tishio...angalia simba alivyogeuza mwaka jana and mwaka huu ni moto ya kuotea...go away maximo and leave our team to the ones who love it with their hearts....
Una hoja hapa mheshimiwa yaani umejenga hoja kwa mfano. Tena kuna mbabaishaji mmoja anapinga hilo.

Nakuunga mkono mkuuuulu

Mpira some times ni vichwa vya wachezaji tu kama kaujuzi ni mafundisho madogo sana kwa wachezaji wetu vinginevyo tuko poa tu na hiyo TFF nayo ifanyiwe reshuffle jamani wachezaji inao wachukuwa 100% ni simba na yanga au kwa kiswahili kingine ni wachezaji wa kutoka Dar tu,

Sijui tufanyenini hapo sasa. na tatizo sio kocha
sasa unataka uchukue wachezaji wa Toto Africans waliokataliwa na timu zote?

Kwangu mimi sioni tatizo la Maximo. Bali naliona tatizo letu sisi kama watanzania, ambao kikweli hupenda kuvuna bila ya kupanda. Timu ya taifa ya taifa lolote sio mahali pa kukuza vipaji kama tunavyomtaraji Maximo afanye. Timu ya taifa iliyojengwa kwa misingi imara kutoka kwenye football academy ambako mtu akichaguliwa timu ya taifa kutokana na nidhamu ya kitaaluma aliyonayo ataona fahari na sio kufanya ubishoo kama wanavyofanya masupastaa wa bongo. Nakubaliana na msimamo wa Maximo ya kusisitiza nidhamu japokuwa sio kazi yake persee anajikuta analazimika kulifanya hilo kwa sababu halipo. Kiwango cha mchezaji wa team ya taifa hafundishiwi nidhamu katika timu ya taifa bali ni kwenye ngazi za chini alikotoka na mwisho kabisa ngazi ya vilabu.

Mziray ni lazima aseme kwa sababu mafanikio yoyote ya Maximo kwake kama kocha wa kitanzania ni mwiba. Mzirai sio mgana ni mtanzania tumekuwa naye hapa miaka dahari, amefundisha yanga ule mpira wa kesho mechi tukalale makaburini, mkienda Misri makaburi atawaonyesha nani?

Soka yetu kama walivyochangia wachangiaji wengine hapo juu inahitaji zaidi ya kocha mzuri. Tunahitaji maandalizi tuwe na vitalu kama mpango wa taifa wa namna ya kukuza vipaji na ajira, pili vilabu ama viwezeshwe au vione haja ya kuwa na yanga academy, simba academy, mtibwa nk.

Bila hivyo hata tukisubiri kocha bora ambaye timu ya taifa anayoiongoza ikimaliza kazi ya kuchukua kombe la dunia SA mwaka 2010 halafu tumchukue sisi tutaja mtusi hivihivi tunavyofanya kwa Maximo kwani hatuna maandalizi badala yake tunajiandaa kushangilia bila kuwa na mkakati wa ushindi.

Ili tuwe fair kama wananchi na wanamichezo, tumpongeze Maximo kwa hatua aliyotufikisha kwani hatukuwa hapa tulipo. Tujiulize kwanini hatutoki hapa tulipo mimi nina hakika kwamba tatizo letu ni kukosa mkakati wa maana kama taifa wa ushindi. Mambo mema hayataki haraka ati.

Ulipokosea tu ni kumpamba Maximo na kumponda Mziray. Mziray hakupewa resource kama za alizopewa Maximo na bado alileta Challenge Cup 1994. Kuhusu nidhamu ni maneno ya mshindwaji hayo. Kama Boban hana nidhamu kiasi hicho iweje waalimu wa nidhamu wafikirie kumsajili? Mara aseme Kaseja mfupi mara alishangilia kufungwa kwa Ivo sasa tuchukue lipi? In short huyu jamaa si kocha.
 
yeah huyu maximo naona anatupanda kichwani, yani hamna mtu anaeweza kumkemea...yeye kila siku anasema hawana nidhamu lakini hatuambiwi kivipi, kwa sababu haohao wanaoonekana hawana nidhamu taifa stars vilabuni mwao wanapiga fresh tu pamoja na kwamba wanafundishwa na makocha wakigeni pia. yule jamaa analeta bifu zake binafsi. wameshindwana kwenye ma***u mmoja kamshinda mwenzake mashairi then ikawa bifu.
 
Wapenda soka wenzangu, dawa ya kuwaonyesha Bwana Tesha na wenzake huko serikalini kwamba tumemchoka Maximo ni kususia michezo yote itakayocheza na timu ya Taifa hapa nchini. Tesha sio mdau wa mpira wa miguu ndio maana haumii moyoni timu yetu inapogeuzwa kichwa cha mwenda wazimu. Kosa la Kaseja na Chuji ni kitu gani ambacho hawawezi kusamehewa? Ebu tumpe kocha Mzirai nusu ya huo mshahara wa Maximo halafu uone vitu vyake! Tesha acha siasa kwenye mambo haya!
 
Mziray ni mnafiki mkubwa! hatumuhitaji kwenye timu yetu ya taifa hata kama Maximo ataondoka leo. Hana la maana zaidi ya kuchonga saaaaana.
Mzirai toka maximo aingie hoja ni hiyo tu kumpinga basi
 
Yaleyale nchi hii bana ni shamba la bibi kwani wakati wa kuingia mkataba hakuna kipengere kilichowekwa kuwa serikali inaweza vunja mkataba kwa mfano kutokana na utendaji wa kazi(performance)kua mheshimiwa Maximo ni hivi ukifanya haya mkataba utaendelea na ukifanya haya na haya mkataba utavunjwa.Haya mambo ya kusema tukivunja mkataba serikali itaingia gharama kubwa ndio yaliyotufikisha hapa kwenye uozo uliopo kila kona,sasa mnatufanya tuanze kwanza kuichukia serikali kwa mambo ya hovyo sasa serikali inaleta uozo wake hata kwenye burudani ,hatuwezi kumwacha Maximo kwani sisi wananchi ndio tunamlipa hiyo hela ni yetu ati serikali haina hela bana hizo ni kodi zetu tuna haki ya kudai uwajibikaji wa Maximo,kila kitu hakiwezekani wapi tunaenda kama taifa,sasa pia nimeanza kuchukia taaluma ya sheria kwani kila sehemu ambayo mambo yameenda kombo ni mikataba mibovu hivi nyia wanasheria hamna uchungu na nchi yenu ?kwa kweli mnatia aibu na huo ndo ukweli wenyewe wanasheria kwa kutumia hizo sheria zenu mmetuangusha na si kuwa hamjui mfanyalo hapana mnajua sana tatizo mnapenda rushwa !fullstop otherwise hizo ngonjera za ajabu zingekuwa historia .kula kona mikataba mibovu inauzi kwelikweli
 
Huyo tesha na wenzake wana uhakika na fungu la kumi toka kwa pato la maximo ndio maana wanamtetea,hapa hatuna kocha hata kidogo,ni ufisadi mtupu!!
 
Maximo ni professional coach. Mziray nakumbuka alichonga sana tulipofungwa na Senegal. Ila stars ilipocheza soka la kiwango pale kirumba Mwanza mpaka Senegal jasho likawatoka akawa kimya

Mziray anauza sura tuu hana lolote na yeye
 
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kocha wa timu ya taifa, Marcio Maximo, ataendelea kuwa mwalimu wa Taifa Stars mpaka mkataba wake utakapomalizika na serikali imewataka 'wanaopiga kelele' kutaka afukuzwe, wamuache afanye kazi yake kwani gharama za kuuvunja mkataba wake ni kubwa mno.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Kauli hiyo ya serikali ya kumtetea Maximo imekuja kufuatia shutuma mpya za mashabiki na wadau wengine wa soka kutaka kocha huyo Mbrazili ampishe mwalimu mwingine kwa madai kwamba uwezo wake 'umegota'. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Akizungumza na Nipashe jana, Msemaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Jacob Tesha, alisema kuwa hakuna sababu ya wadau kumponda Maximo wakati amejitahidi kwa kiasi kikubwa kufanya mapinduzi kwenye soka la Tanzania.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Tesha alisema kuwa ni jambo la busara kama wadau hao kumpa nafasi Maximo kutekeleza mikakati aliyojiwekea kabla ya kumaliza mkataba wake mwakani.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]"Jamani hebu tumuunge mkono Maximo, tunataka atufanyie nini? Amelikuta soka letu likiwa sehemu isiyo nzuri na ametufikisha hapa, tumpe nafasi ili akamilishe programu zake kabla ya kumaliza mkataba wake," alisema Tesha.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliongeza kuwa gharama za kuuvunja mkataba na kocha huyo kwa vigezo vya kutoridhishwa na uwezo wake ni kubwa kuliko inavyofikiriwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hata hivyo Tesha alieleza kuwa si vibaya kwa wadau wa soka kutoa maoni yao lakini wanapaswa pia kuyangalia na mazuri aliyoyafanya kocha huyo.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Shutuma mpya dhidi ya Maximo zimekuja kufuatia matokeo mabaya katika mechi tatu za kirafiki za kimataifa zilizofanyika nchini Yemen hivi karibuni ambapo Stars ilifungwa mechi mbili na kutoa sare moja.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Katika mechi ya kwanza dhidi ya mabingwa wa Afrika Misri, Stars ilizidiwa kila kitu na kulala kwa magoli 5-1, kabla kulazimisha sare 1-1 katika mechi ya pili dhidi ya Yemen. Katika mechi ya marudiano na Yemen Stars ililala 2-1, na kuamsha hasira za Watanzania.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Miongoni mwa shutuma zinazomkabili Maximo ni kuwaita kwenye kikosi cha taifa makipa ambao hukaa benchi kwenye timu zao na pia kuwaacha nyota wengine -- jambo ambalo mwenyewe ameshalitolea ufafanuzi mara kwa mara kwamba ni ukosefu wa nidhamu.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Wakati huo, Maximo amepata sapoti kutoka kwa Katibu Mkuu wa chama cha makocha nchini (TAFCA) Eugean Mwasamaki ambaye amesema kuwa makocha nchini wanatakiwa kujifunza kutoka kwa Maximo juu ya msimamo wake wa kutosikiliza maneno ya nje.[/FONT]
“[FONT=ArialMT, sans-serif]Kocha anatakiwa kuwa na misimamo yake hasa kwenye suala la ufundi, makocha hawatakiwi kusikiliza maneno kutoka nje kama wanataka mafanikio, wafanye kazi kwa misingi ya kazi na taratibu waliyojiwekea wao na si kusikiliza kele za mashabiki,” alisema Mwasamaki.[/FONT]


Serikali haina budi kujua kuwa kila kitu kina gharama zake. Hivyo kama inadhamira ya kuendeleza soka haihitaji kuogopa gharama. Sababu kubwa inayotolewa na serikali ni kuwa kocha kaleta mapinduzi, hata hivyo msemaji hajaelezea mapinduzi hayo katika soko ni yepi.

Kitu ambacho ni dhahiri ni kuwa soka iko hapa ilipo sio shauri ya kocha wetu bali ni sababu ya serikali kussupport kidogo mpira wa miguu, NMB na SERENGETI kumwaga mahela mengi kwa njia ya udhamini ( tuwapongeze hawa), FIFA kutoa fedha nyingi za maendeleo ya soka sisi wananchi kwa kuwa na moyo wa upendo na ushabiki kwa timu yetu ya taifa kitu ambacho hakikuwepo awali.

Serikali ikumbukuke kuwa maximo na Taifa stars yake hawawezi kucheze na kuaccomplish wananchotaka kama uwanjani hawatakuwa na washangiliaji ambao ndio wanaotoa maoni yao, mkizidi kumsikiliza maximo na kudharau watazamaji siku moja timu ya taifa itaweza kuzomewa toka mwanzo mpaka mwisho na kushangilia timu ngeni.

Serikali isidharau mchango wa wananchi kwenye timu ya taifa, kwa kifupi wananchi hawamtaki huyo kocha, hamuwezi kusoma alama za nyakati, kwani kocha mwingine hawezi kupatikana?????? Kwa nini awe yeye tu?????
 
Mkuu, Mzirai anataka ukocha wa stars, lakini ha-qualify. Katika historia ya ufundishaji wa Mzirai sijawahi kuona mafanikio ya kuweza kujisifu kuwa yeye ni bora kuliko Maximo, au hata kuliko makocha wengine walipo Tanzania. Naweza kusema wazi kabisa kuwa Zakaria Kinanda na hata Joel Bendera ni much better kuliko Mzirai. Toka ameanza kufindisha soka hajawahi kuwa na mafanikio substantial, yes amefundisha Simba na Yanga na kupata ubingwa na timu hizo uwezo wake umeishia hapo tu na kidogo Afrika Mashariki.
Yeye ni mtaalamu wa elimu ya viungo, kama aki-judge timu ya taifa kwa vigezo hivyo naweza kukubaliana naye. Analysis zake zote zimekaa kifitnafitna na sio kitaalamu. Udhaifu wa soka yetu hauko kwa mtu mmoja tu, it is a whole set of factors, from players themselves, clubs, FA, mentality and institutions, asilete upuuzi wa kulaumu mtu mmoja eti kisa ni mgeni, akiwa ni mtu ambaye walau ana elimu kidogo alitakiwa kutoa sababu ambazo ni a bit more scientific kuliko kuleta uswahili na wivu kwa Maximo. Yeye mwenyewe alitakiwa kuonesha uzalendo kwa kumpa Maximo uungaji mkono, na sio kumsema kwenye media.
Tanzania inatakiwa kwenda mbele, haitakiwi kurudi kwenye ujinga wa miaka mitano iliyopita.
Tulimchagua Maximo kati ya makocha wawili, sio kama mmoja tuliyemwacha hakuwa mzuri kuliko Maximo, na sio kama serikali au wadau wa Soka hawakuona makocha wa Tanzania. Mzirai ni mswahili tu, ambaye umaarufu wake unakuja kutokana na kufundisha soka na kuwapikia majungu wengine. Ni vizuri kama hatapewa nafasi hiyo ya kuleta fitna na chuki.
 
Mimi nadhani Mziray kelele zote hizo ni kutaka mabadiliko ya staz yapatikane, na sio kuwa ana chuki binafsi na Maximo.
 
inaonekana kuna siri kubwa kati ya kaseja na maximo kama hamjatukunia mamake hapo lazima mmoja amekula tunda la mwenzake si hiivi hivi tuake nao tuwaulize....
 
pia amesema wanamsubiri Tenga ktk uchaguzi awaeleze taifa Star chini ya Maximo imefanya nini huku ikiwaacha wachezaji ambao kimsingi TFF wanatakiwa wakae nao na wasikilize matatizo yao.


Jamani jaribuni kukumbuka jinsi Maximo alivyopata kazi Tanzani na kuwa mwalimu wa Taifa stars, TFF haina sauti juu yake kwani wao hawakumtafuta na sio wanaomplipa ( at least kwa kipindi cha kwanza) Maximo ni presidential appointee na hivyo kuondolewa kwake kutafuata utaratibu ule ule.

Mpende msipende ataendelea kuwa kocha Taifa stars.
 
hawana nidhamu lakini hatuambiwi kivipi, kwa sababu haohao wanaoonekana hawana nidhamu taifa stars vilabuni mwao wanapiga fresh tu pamoja na kwamba wanafundishwa na makocha wakigeni pia.

Vilabu vyenyewe vipi? Simba? mbona nao hawana nidhamu tu, kwa hiyo kwa wao inakuwa rahisi kuvumilia upuuzi.
 
Back
Top Bottom