Should Maximo stay and enjoy the money 4 nothing? - Contract to be renewed?

Should Maximo stay and enjoy the money 4 nothing? - Contract to be renewed?

Unaposema Kaseja ni kipa mzuri unamaanisha nini?

Hapa Tanzania ni kipa gani bora kuliko Kaseja? Yaani unataka kutuambia kuwa hata kama kuna kipa ambaye sio mzuri kama Kaseja basi aitwe timu ya taifa kwa kuwa ni mrefu kushinda Kaseja?
Kipa kuwa mzuri kwenye ligi au hata kwenye mashindano mengine haina maana basi ndio moja kwa moja aitwe timu ya taifa, kila cku huwa tunasema kuitwa kwa mchezaji kwenye timu huwa ni kwa mujibu wa mtazamo wa kocha wa timu husika kwamba ni yeye ndie anaamua nani anafaa kwenye timu yake na nani hafai, so hata wewe mkuu ukipewa ukocha leo unaweza ukaita kikosi ambacho kuna watu watasema umekosea na kuna watu watakukubali, so taifa stars suruhisho sio Kaseja coz hata kaseja nae alishawahi kudakia stars na akawa anakunywa magoli kama kawaida
 
Mziray needs to shut up. Yeye alikuwa kocha wa timu ya Taifa si mara moja na si mara 2, na mara zote hakuna lolote substantial alilofanya, zaidi ya kulalamikia wengine. Kila mara anakuwa wa kwanza kunyanyua mdomo wake na kukosoa makocha wenzake wakati yeye akipewa nafasi anakuwa wa kwanza kunyooshea vidole wengine kuwa hawamuungi mkono. Yeye kwake makocha, marefa, wachezaji na wengine wengi anaona useless.

Ameivuruga Yanga, ameivuruga Simba na alivuruga timu ya taifa na sasa anaanza kuvuruga media.

yeye professionalism yake iko kwenye Physical education, kama akiiongelea timu ya taifa on that side, i can buy his words.

Hakuna asiyejua kuwa Maximo is not a super coach, he has his own weaknesses but we need to be honest with ourselves and at least aprreciate what he has brought to the Taifa stars. Timu yetu sasa si kichwa cha mwendawazimu, although bado si faru dume kama ambavyo tungependa iwe. Lakini ameleta mabadiliko, tunatakiwa kwenda mbele na kuuenga kuanzia alipofikia, na sio kuwapa timu yetu watu wanaoitumia kujitafutia ujiko tu.

Where was Mziray timu yetu ilipokuwa kichwa cha mwendawazimu, was he in the country or somewhere else? Alipokuwa Kocha kilikuwa kichwa hichohicho cha mwendawazimu.

Kama ni mtu anayekaribia kufanana na wasomi, alitakiwa kuonesha tofauti kati yake na makocha uchwara. Anatakiwa kuongea na maximo mwenyewe na sio kwenda kumdhalilisha kwenye media, na kujitafutia umaarufu kwa wanawake, this is very low of him.
 


Juma Kaseja ni kipa mzuri lakini ufupi wake unachagia kwa kiasi kikubwa kuachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa.Najua wako mashabiki wengi wa Juma Kaseja wanatumia vyombo vya habari kushinikiza aingizwe timu ya taifa,naomba kuwauliza ni timu gani kubwa dunia yenye kipa andunje kama Juma kaseja ?.Nitajieni walau makipa watatu tu !!!!.

Mkuu Mbona Washambuliaji wa Kibongo wameshindwa kutumia Ufupi wa Kaseja Katika Premium League?

Simba waliwatoa Zamalek iliyosheheni nyota kibao wa The Pharaos mlangoni akiwa Kaseja

Hilo la Ufupi sio hoja, Mbona Kado aliitwa?
 
Nimeguswa na hili la JUMA KASEJA, tuache chuki binafsi kaseja ni gorikipa pamoja na ufupi wake ila maximo ana chuki binafsi. nashangaa anamuita kipa namba 2 wa simba anayewekwa benchi na kaseja na kumkabidhi jukumu la kulinda milingo 3 katika mechi kubwa kama na misri unategemea nini? hata goli 5 zilikuwa chache. tatizo JK tungeshafukuza zamani kodi zetu zinatumika vibaya.
 
hivi watanzania tuna matatizo mangapi mpaka tunashindwa kuona mapungufu tele ya maximo? kocha gani duniani aliwahi kukaa na timu for such a long time bila kuleta hata kikombe cha kuku na hakutimuliwa???..huyu kocha anafaa sanna kuwa mwalimu wa nidhamu na sio mpira wa kuleta makombe nyumbani....hao wachezaji wake anaosema wana-nidhamu ndio hao vimeo wanachezea magoli hata kwa wachovu kama somalia...shame on maximo and his fanz...

Investment tulowekeza kwenye timu ya taifa kwa kipindi cha maximo ni zaidi ya mishahara ya waalimu yote kwa nchi nzima...timu inatumia 13b every year..na mafanikio bado hakuna..upuuzi huuu.

kipimo cha mafanikio ya kocha yeyeote wa footbal duniani hasa hizi national teams huwa ni VIKOMBE NA FAINALI AMBAZO TIMU YAKE ANAYOFUNDISHA HUPATA AU HUFIKIA...sio nidhamiu au hata kucheza pasi nyingi...LETS NOT LOSE OUR MAIN FOCUS....UBINGWA NA VIKOMBE..ndo maana kila siku makocha wa timu za wenye akili duniani wakichemsha tuuu...ajira hakuna..

NIDHAMU...ni nani alikuwa na nidhamu chafu kama ya paul gascoine gaza??...ila ilikuwa lazima aitwe timu ya taifa na anafanya kweli....nani kama romario, redondo..etc...hawakuwa na nidhamu lakini bila wao timu ilikuwa haishindi...

MAONI YANGU...maximo hatufai...hana jipya...mwisho wa upeo wake ushatimia...achape lapa tutafute makocha wengine wa ukweli....anyway kwa anayemjua vizuri maximo atupatie mafanikio aliyowahi kupata na timu yoyote ya taifa duniani..au hata klabu akiwa kama kocha mkuuu???
 
Kaseja ni kipa bora Tz, at least kwa hawa waliopo. Ni kipa pekee aliyefungwa magoli machache kwenye ligi ya bara mwaka huu. kuna mchangiaji mmoja alisema hapo juu, Zamalek ya Misri walishindwa kumtungua kaseja kwao na wakatolewa na simba. nakumbuka ilikuwa sare ya moja moja (kwa michezo yote miwili). na penalt akapangua.

Kuhusu mafanikio, Mzirai amepata mafanikio mengi kuliko Maximo...Aliiongoza Sigara vizuri, akaja Simba ikachukua Ubingwa wa bara na Yanga Pia. Na yeye ndio aliyetupatia Kombe la Challenge kwa mara ya mwisho mwaka 1994 akiwa Supercopach.

Ukiangalia makipa aliochagua Maximo, utaona kabisa kuna upungufu mkubwa wa kiufundi, hata kama si mtaalam wa mpira wa miguu. Barthez ni kipa namba mbili wa Simba, amesugua benchi kwa kaseja, eti anapangwa na ze pharaoh; Pia Dihile ndio yule aliyefungwa magoli ya aibu na Simba pale uwanja wa uhuru. Then, watu wakisema, eti wana chuki Binafsi. Hatuwezi kuendelea namna hii kwenye soka kama tunadhani Maximo bado ana uwezo wa kutuletea mana Tz. Kipimo cha kocha wa Soka ni ushindi. Kocha yeyote anayeleta longolongo kwa kufungwa, hafai. Raphael Benitez wa Liverpool, siku zake zinahesabika sasa baada ya Liver kuboronga siku za hivi karibuni. Na hicho ndicho kilichomkumba Santana wa bafana bafana kule Bondeni. Sisi timu inaboronga, lakini bado tunalea upumbavu. Haya, Jana tumebamizwa na Yemen bao mbili kwa moja. bado tunamlamba tu Maximo, puh!

Mziray has all the rights to criticize (constructively) Maximo. kwanza ni mtaalam, na si mshabiki maandazi kama baadhi yetu humu.
 
bongo ni politiki plus plus. michezoni...politiki....uchumi....politiki...siasa...politiki...

nachelea kusema ndiyo sababu hii nchi imekwama katika nyanja zote ukiondoa ufisadi...na chembechembe zake...
 
Mkuu Malaria sugu tafadhali weka makala yote ya Mziray ili tuweze kuijadili vizuri.Kwa kuanzia tu tayari naona Mziray anachemka kwa kudhani taifa star imefanya vibaya kwasababu Kaseja akuchaguliwa.

Juma Kaseja ni kipa mzuri lakini ufupi wake unachagia kwa kiasi kikubwa kuachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa.Najua wako mashabiki wengi wa Juma Kaseja wanatumia vyombo vya habari kushinikiza aingizwe timu ya taifa,naomba kuwauliza ni timu gani kubwa dunia yenye kipa andunje kama Juma kaseja ?.Nitajieni walau makipa watatu tu !!!!.


Lakini Maximo hamwachi Kaseja kwa sababu ya kimo. Sababu zake ni za Kiswahili kweli. Eti aliambiwa Kaseja alifurahia Ivo Mapunda kufungwa bao 4-0 na Senegal! Hata hivyo suala la kimo kwenye mpira sio issue. Sasa mtu achaguliwe kwenye timu ya taifa eti kwa sababu tu ni mrefu! Ebo! Angalia hao makipa wenu warefu wanavyobugizwa magoli.
 
Mziray has all the rights to criticize (constructively) Maximo. kwanza ni mtaalam, na si mshabiki maandazi kama baadhi yetu humu.

Kocha huwa hachaguliwi wachezaji. Kana kweli wewe ni mpenda soka unaweza kujua issue ya kseja sio ya kwanza duniani. Ukimuuliza Romario atakwambia Scolari alivyomfanya, kisa kukosa nidhamu. Si kwamba hakuwa mchezaji mzuri. Uliza kilichomkuta Roy Keane alitimuliwa wakati mechi za kombe la dunia zikiendelea. Kocha hafundishi kupiga pasi tu, anahitaji timu yenye nidhamu pia.

Kwa taarifa yako Mziray si mtaalamu wa Soka, ni mtaalamu wa elimu ya viuongo. (Physical Education) hizo timu unazesema alizifikisha pazuri ni kwa kuwa zilikuwa physically fit, na hazikuwa technical na skillful. Na timu zote ziliishia pabaya. Mziray mwenyewe hana nidhamu ya kuweza kucha Kocha mzuri. Ukiwauliza wachezaji wengi aliowafundisha wengi walilalamika kuwa alikuwa anawachukulia wanawake zao.
 

Swali langu nimeomba nitajie makipa watatu andunje kama Juma Kaseja wewe umekimbilia kumtaja kipa mmoja tu hii pengine inathibitisha kile ninachokipigia kelele kwamba ni vigumu sana kukuta timu kubwa zinatumia makipa andunje.
Afadhali umeweka wazi kuwa huna uhakika na unachokisema, ndo maana umetumia neno 'pengine'.
 
Yale yaleee....hivi nchi hii hakuna kipa mwingine isipokuwa Kaseja?
 
wapo ila wachovu kaseja ndio kinara wao,aitwe kaseja kama kweli ni national team,au la basi tuahache,Mziray yupo sawa kabisa na anachokisema,wakati ule wa team ya Mziray siye wachezaji tunajua tulikuwa hakuna kitu chochote cha ziada kwenye team ya taifa tofauti na sasa hivi,kama hujui mpira ndio utaongea kama Bongolander,kuanzia lini team ya ilikuwa inaenda nje ya nchi kwa ajili ya friend match?au inaweka kambi Brazil?au inakuwa na wazamini kama sasa hivi?Maximo keshafikia mwisho mtake msitake na hatufai tena kwakweli.
 
Maximo Akiri Vipigo Vya Taifa Stars
3541738.jpg

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Marcio Maximo Friday, November 13, 2009 5:36 PM
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Marcio Maximo amekiri kwa kusema kuwa ,matokeo mbaya waliyoyapata katika mechi tatu za kirafiki za kimataifa katika nchi za Misri na Yemen yatachochea moyo wa kujituma kwa wachezaji wake.Maximo alisema watakuwa na hamu ya kufanya vema kwa timu ya Tanzania Bara itakayoshiriki michuano ya Chalenji itakayofanyika Kenya kuanzia mwishoni mwa mwezi huu.

Gazeti moja la kila siku limeandika kuwa, Maximo alitarajia kupata matokeo mazuri katika michezo mitatu waliyocheza, lakini hali imekuwa tofauti kabisa kutokana na sababu tofauti ikiwemo kuzidiwa na hali mbaya ya hewa nchini Yemeni.

Stars ilifungwa na Misri 5-1, ikatoka sare ya 1-1 na Yemen katika mchezo wa kwanza na kupoteza mchezo wa pili baada ya kufungwa 2-1.

"Misri ni timu ya kiwango cha juu mno na ukitaka kucheza nayo lazima ujiandae, nilikubali kucheza mchezo huu kwa sababu tulikuwa tumewaomba muda mrefu kucheza nao bila mafaniko, niliona hii ilikuwa ni fursa nzuri kupima kikosi changu licha ya kufanya mazeozi siku mbili tu, lakini huu ndiyo mpira, tumejifunza mengi.

"Yemen ni timu ya kiwango cha chini ukilinganisha na Taifa Stars, tulijitahidi kuwabana katika michezo yote miwili na kumiliki mpira kwa asilimia kubwa, lakini nafasi tuilizotengeneza hatukuzitumia kupachika magoli, lazima tuichukue hali hii kama changamoto tunapokwenda kwenye Chalenji hakuna njia," alitanabaisha Maximo.

Kocha Maximo ambaye amekuwa akiinoa Stars kwa miezi 39 sasa amesema jambo lingine ambalo anaona ni la manufaa katika ziara hii ni kuwa ameweza kuwatumia wachezaji wake wote 19 aliokuwa nao safarini na hivyo kuweza kupima uwezo na maendeleo ya kila mchezaji kwani kila mmoja amepata nafasi ya kucheza walau mchezo mmoja.

"Matokeo si mazuri, lakini kuna mambo mengi ya manufaa, nataka kutumia siku tisa tutazokuwa kambini kurekebisha kasoro hizi kabla ya kwenda Nairobi," alifafanua.

Mbrazil huyo alisema makosa yaliyojitokeza katika safu ya kiungo na ushambuliaji yanahitaji ufumbuzi wa haraka.

"Lazima tumiliki mpira na kupunguza mianya sehemu ya kiungo huku tukiwabana vilivyo wapinzani wetu muda wote na baada ya hapo tulenge lango mara nyingi zaidi ili tupate magoli ya kutosha, nitajihidi kuyaweka sawa yote hayo na sina shaka tutafanikiwa."

Mashindano ya Chalenji yamepangwa kuanza Novemba 28 na kumalizika Desemba 13 mwaka huu na yatachezwa katika miji ya Nairobi na Mumias.

Tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo miaka 35 iliyopita Tanzania Bara imetwaa ubingwa mara mbili tu mwaka 1974 ilipokuwa mwenyeji na mwaka 1994 ilipofanyika Kenya.

Katika miaka ya 1975, 1980,1981, 1992 na 2002 Tanzania Bara ilifungwa katika michezo ya fainali na Uganda, mara mbili, Kenya, mara mbili na Sudan mara moja.
 
washabiki wana uwezo mkubwa sana wa kufanya huyu afukuzwe lakini ndio hivyo watanzania kila kitu kwetu kigumu.jamaa kuna kipindi nilikuwa na msupport lakini baada kuona kwamba analete beef za ajabu na wachezaji na kukosa muelekeo sidhani kama anaju anachokifanya.
 
Lazima aondoke,ngoja tumsikilize kesho anaongea nini-maana kesho anakutana na waandishi wa habari tff asubuhi.
 
maximo sasa nae anaboa, kila cku anasema tusubiri, sijui lini hizo ahadi zitatimia... ukichemka challenge uondoke hatukutaki
 
Hana jipya aende zake tu mshahara wake wa milioni 10 ungetumika kwa mambo mengine muhimu
 
Back
Top Bottom