Shuhuda za waliofanikiwa kupunguza uzito kwa mazoezi na lishe

Shuhuda za waliofanikiwa kupunguza uzito kwa mazoezi na lishe

Watu wengi tunapenda kupungua na kula tunapenda na mazoezi hatuwezi.

Mimi sipendi kitambi kwahiyo I watch what I eat mpaka watu wananishangaa kama mko kwenye ki-function vile nakuwa selective kwenye kuweka chakula. Na kama haya maharusi ya kulishana saa tano usiku nitaweka zangu salad na kuku au samaki nimemaliza.

Nikifanya mazoezi labda sit-ups. Sili kubwa ya kupungua ni kwenye kile unakula.

Nilipokua mjamzito nilifika kilo 89. Baada ya kujifungua nikawa nimebaki nazo kama 80 hivi ila sasa hivi niko kwenye kilo zangu za miaka yote. Na sijawahi fanya mazoezi ya aina yoyote.

Kwa yeyote anaetaka kupungua pangilia mlo wako vizuri lazima utapungua.
 
Watu wengi tunapenda kupungua na kula tunapenda na mazoezi hatuwezi.

Mimi sipendi kitambi kwahiyo I watch what I eat mpaka watu wananishangaa kama mko kwenye ki-function vile nakuwa selective kwenye kuweka chakula. Na kama haya maharusi ya kulishana saa tano usiku nitaweka zangu salad na kuku au samaki nimemaliza.

Nikifanya mazoezi labda sit-ups. Sili kubwa ya kupungua ni kwenye kile unakula.

Nilipokua mjamzito nilifika kilo 89. Baada ya kujifungua nikawa nimebaki nazo kama 80 hivi ila sasa hivi niko kwenye kilo zangu za miaka yote. Na sijawahi fanya mazoezi ya aina yoyote.

Kwa yeyote anaetaka kupungua pangilia mlo wako vizuri lazima utapungua.
Yap hakika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Don255,
Hongera sana.Umeandika vizuri na kutia hamasa.

Binafsi nilikuwa na kilo 92 wakati kwa mujibu wa BMI yangu nilirakiwa kuwa na kilo 81.

Nilianza kuitwa bonge.Na nilianza kupata matairi tumboni.

Kilichonisaidia ni mazoezi ya kukimbia.Nilikuwa nakimbia dakika 30 walau mara nne kwa wili.Pia nilikuwa naingia kufanya weight lifting na sit ups.Nilipunguza kabisa ulaji wa chips.Nilipunguza pia unywaji bia isipokuwa weekend.

Ndani ya miezi mitano nilifikia lengo la kuwa na kilo 81.Size ya kiuno ilipungua kutoka futi 36 mpaka 34.Sasa ivi nina six packs.Shinikizo la damu lilianza kuninyemelea ila kwa sasa halipo tena.

Mazoezi ni njia pekee.

Kweli mkuu...ahsante kwa kuliona hilo...nafurahi pia niliwasaidia na wenzangu kupunguza unene...kwa mazoez kuna jamaa angu alikuwa aenda gym miezi sita...kuna siku nilimuuliza unahitaji kupungua?...akanambia ndio...nkamuambia tukutane kiwanjani saa 12 asubuhi...leo hii kawa kimodo[emoji23]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umenipa hamasa...naanza ss na Mimi,,,hapa nilipo Niko na 95 kgs,...ila ukiniangalia sio bonge kiivyo,,,na pia ni mwepesi sana,,,mazoezi nafanya sana ila sins ratiba wala muda maalum,,,mazoez nayopenda ni kunyanyua vyuma,kichura,squart na kukimbia kidogo ila ss baada ya zoezi huo msosi ninaogonga+nyama Choma na TBL kidogo ni balaa,

Sent using Jamii Forums mobile app

Unaweza mkuu...yaani unaweza utapata tabu siku tatu za kwanza...ukichanganya utakuja useme hapa


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahyo mchana wote natumia maji tu au haata maji NO!..
Kunywa maji ili mwili uwe hydrate. Usipokunywa maji utachoka sana. Na kama unataka kula mara moja kwa siku na vile sio mwezi wa Ramadan basi kula mchana. Jioni ule matunda pendelea yenye maji kama watermelon na tango. Maji unywe maji ndio utaweza kukaa na njaa
 
nina kilo 57 mwili wa kawaida urefu 5'5 shida kakitumbo ka chini hakatoki natamani flat, mazoezi huwa naruka kamba kiasi na kutembea.
Tumbo la chini kulitoa linahitaji uvumilivu mno....Yan kwa hizo kilo zako na height tumbo la chini hukupaswa kuwa nalo..

Fanya mazoezi ya tumbo kwa muda mrefu takribani mwezi mzima hvi..asubuhi na jioni kila siku..

Kazania hayo mazoezi kwa muda mrefu kama ukiweza kimbia ama ruka kamba kwa uchache ili usipungue kilo sana,Lengo liwe tu kutoa tumbo la chini...

Pale utakapoona maumivu endelea usiache mazoezi ya tumbo japo ukweli yanahitaji uvumilivu..

Usile sana vyakula vya mafuta kila siku...kula tu mara moja moja inapobidi...

Thank me later!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo sio kila mtu ni mtu wa mazoezi....mie kukimbia sipendi na huwa sikimbii,kutembea umbali mrefu ndio nilishashindwa
Kiufupi siwezi mazoezi

Nafikiri watu wanene wazingatie vyakula,japo kuna wale wanene wa kurithi
Fanya hata aerobics
 
Mkuu uzito unaenda sambambs na tumbo.sidhani kama kunajitu nene lenye tumbo flat.

Watu wafocus kwenye kuondoa tumbo mana linabeba mikilo mingi
Tumbo la chini kulitoa linahitaji uvumilivu mno....Yan kwa hizo kilo zako na height tumbo la chini hukupaswa kuwa nalo..

Fanya mazoezi ya tumbo kwa muda mrefu takribani mwezi mzima hvi..asubuhi na jioni kila siku..

Kazania hayo mazoezi kwa muda mrefu kama ukiweza kimbia ama ruka kamba kwa uchache ili usipungue kilo sana,Lengo liwe tu kutoa tumbo la chini...

Pale utakapoona maumivu endelea usiache mazoezi ya tumbo japo ukweli yanahitaji uvumilivu..

Usile sana vyakula vya mafuta kila siku...kula tu mara moja moja inapobidi...

Thank me later!!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja niwaambie kitu kuhusiana na Diet na kupunguza mwili...watu wengi wana amini ku acha kula mlo mmoja kunaweza kukakufanya upungue SIO KWELI
...Kama unaamua kufanya diet kwa ajili ya kupungua mwili fanya yafuatayo
...Punguza kula vyakula vyenye asili ya wanga na sukari...tumia kipimo cha ngumi yako(yaani kula ugali au wali saiz ya ngumi yako)...unatakiwa ule sana mboga za majani na samaki(nyama nyeupe)
...mboga za majani hazina madhara kula kwa wingi uwezavyo...kula sana matuda yatakusaidia kupata nyuzi nyuzi(fibers)...hizi husaidia kusaga chakula kwa haraka
Hujaelewa?...Fanya hivi
Asubuhi ukiamka jitahid upate grass moja ya maji ya uvugu vugu(ukiitia ndimi au tangawizi ni bora zaid)
...Chai yako unaweza kula siles ya mkate moja au chapat moja au andazi 1(shughuli enhee[emoji23] ndo unapunguza wanga hivo)
...Mchana kula ugali saiz ya ngumi yako na mboga za kutosha pamoja na matunda...ukijisikia njaa kila tena ,ukijisikia tena njaa kula(kula saizi ndogo ya chakula utakapojisikia njaa...usile mpaka ukashiba sna
...Sema hapana kwa chips
....sema hapana kwa soda
.....Sema hapana kwa nyama nyekundu(ya ng'ombe,mbuzi
.....Kunywa maji mengi
.....kula kuku(bila ya ngozi yale)
FANYA MAZOEZI ...narudia tena FANYA MAZOEZ
...Kwa wale ambao wanasema wanafunga kupunguz uzito ni kweli kufunga kunapunguza mafuta mwilini....kivip? Kipi unatakiwa ufanya check hpa[emoji1484]
...Kwa kawaida mwilinwa binaadam huchukua masaa 8 kumaliza chakula kilichopo tumboni na kuanza kutumia mafuta yaliyo mwilini(kwenye cell)....hivo kama unataka utumie funga kumaliza mafuta mwilini hakikisha unafungulia na vyakula vyenye virutubisho na si wanga
Kivip? MFano umekula daku saa 8 usiku....uka kaa na njaa mpaka saa 12 jioni maana ake kuna mafuta yashatumika mwilini hivo basi jitahid hiyo saa kumi na mbili jioni ufungua kwa maji ya uvuguvugu(umeona enhee huwa tunafakamia ya baridi hapa[emoji23])...futari yako iwe nyepesi kama ni viazi viwe viwili mboga za majani na matunda kwa wingi
Kwa nini watu wanafeli?...watu wengi wanafunga lakini wanafungua kwa futari nzito na soda mpaka tumbo lina jaa...huwezi KUPUNGUA...kwa leo ni hayo(unaweza nirekebisha pia maana mimi sio mtaalamu wa rishe) nimeshea tu uzoefu maana nilikuwa mnene wazee[emoji23][emoji23]...nkitembea hatua mbili tu jasho naweza hata mwagilia mchicha
...Nikipata mda ntakuja niwaambie kuhusu Supu ya kabichi na kupunguza unene(japo mm ilinishinda[emoji23][emoji23][emoji23])...wewe sikukatish tamaa....jambo la kuzingaitia USITUMIE MADAWA YA KUPUNGUZA UNENE....ntakuja hapa kuelezea madhara yake


Sent using Jamii Forums mobile app
 
nina kilo 57 mwili wa kawaida urefu 5'5 shida kakitumbo ka chini hakatoki natamani flat, mazoezi huwa naruka kamba kiasi na kutembea.

Tafuta roller...
IMG_0022.JPG



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika. Mimi nimeweza kudumu kwenye kg 60 kwa muda mrefu sana. Nakula pale ambapo nasikia njaa sio vingenevyo. Siku inaweza ikapita nikala mara moja kama sitasikia njaa siku imeisha. Zikipungua 58 zikizidi 62
Una urefu gani!??

Hujawahi kuwa na kilo nyingi zaidi ya hzo!??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kula menyu msiogope ukitaka kupungua wewe vuta bangi hali itakaa vizuri tu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu uzito unaenda sambambs na tumbo.sidhani kama kunajitu nene lenye tumbo flat.

Watu wafocus kwenye kuondoa tumbo mana linabeba mikilo mingi

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilivyomsoma anasema ana Kilo 57 ambazo kiukweli si nyingi japo sijajua urefu wake ila kama tukimkadiria kuwa na cm 155 kwenda juu itakuwa ameenda sawa kuwa na uzito huo!!!

Kuna muda mafuta yanarundikana tumboni hivyo solution inakuwa kulifanyia mazoezi tumbo bila kujihusisha sana na Kukimbia ama mazoezi mengine ambayo kiukweli ukifanya kwa muda mrefu hupunguza sana mwili...

Hivyo ili kubakiza na kilo zake halisi na kuondoa kilo chache tu anapaswa kujikita zaidi kwenye mazoezi ya tumbo kuliko kufanya mengine yatakayopunguza mwili kwa ujumla

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom