Shukrani ya Wapigania Uhuru ni kuacha watoto wasiojua baba zao Maeneo ya karibu yaliyokuwa makambi yao

MakinikiA

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2017
Posts
5,104
Reaction score
6,827
Salaam,

Kwa kweli sijapenda hawa wapigania uhuru kutoka Namibia, Msumbiji, Zimbabwe kutuachia watoto wasiojua baba zao, leo siku ya mashujaa kuna kambi kule Mtwara ni huruma.

Mama mmoja anajieleza walivyokuwa wanatongozwa na kuvalishwa magwanda ili waingie makambini.

NB: Tunaomba zoezi la sensa lituletee data kamili tuwatafutie ndugu zao.
 
1. Msaada wa masikini hauna nguvu kama mchango wa mwenye nacho.
2. Mwanzoni nilidhani na niliamini Tanzania ndio ilikua alfa na omega kwenye hili swala la wokozi kwa nchi nyingi za Afrika lakini baada ya kutembea kumbe nchi nyingi sana zilichangia na zilitoa michango mikubwa tu kuwezesha hizo nchi zilizokua zinapigania uhuru kupata uhuru wao. Hapa naweza kusema serikali huamua watu wake wasome nini na nini wasisome kwa wakati upi.
3. Vizazi vinakuja na mazingira na changamoto zao za wakati huo, kizazi cha miaka ya 1995s SA, Namibia Angola au Zimbabwe si rahisi kukuelewa kuhusu Tanzania ila ni rahisi kumuelewa labda mchina mchango wake kwa sasa
 
So tulikuwa tulalishwa matango pori sie wana TANU yajenga Nchi
 
Umejibu kiutopolo sana mkuu....Tanzania kuna makambi kibao ya wapigania uhuru nchi mbali mbali za afrika.Sema tu sisi historia ndio inatuhukumu tulikuwa mlengo wa kisosholisti ili hali huyo mkoloni na ambaye ndio ana nguvu mpaka sasa ndiye alikuwa beberu mwenyewe.
 
Ni kweli ila Jina la Nyerere linajulikana ila kama nchi mmmmm bado maana ni rahisi mtu kujua Jina la Nyerere kuliko nchi, ila ni kweli sio mchango wetu tu ndio uliokomboa hizi nchi nyingi za kusini, kuna factors zilizotia uzito zaidi kuliko mchango
 
Ungenisaidia ku-highlight wapi nimejibu “kiupotolo”!!!
 
Yawezekana tulipewachumvi nyingi😅😅😅
Yes chumvi nyingi mno mkuu, hivi vyama vya ukombozi navyo vilikuwa vya kinyama sana,zanu p ilishot ndege ya kiraia iliyobeba watoto kutoka Victoria falls, anc wameuana sana pale angola etc etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…