Shule ya Kinondoni Muslim inawaka moto Kinondoni

Shule ya Kinondoni Muslim inawaka moto Kinondoni

mrangi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
88,759
Reaction score
123,368
Nimepewa code mitaa hiyo kuna moto.

Mwenye kujua zaidi atupe taarifa

Ova
======

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa Kinondoni Shamba amesema alipoongea na wanafunzi wamesema chanzo ni umeme lakini bado haijathibitishwa rasmi. Amesema moto unaendelea kusambaa kwa sababu baada ya kutoa taarifa limefika gari moja lakini wanaomba magari mawili kwa sababu shule ina mabweni makubwa na gari limeshaishiwa maji na moto unazidi kupamba kusambaa hivyo wanaomba msaada wa magari mengine ili msikiti mpya wa Bakwata usije nao ukaungua.

Amesema anashukuru Mungu wameokoa wanafunzi wote na wapo wawili wamewapeleka hospitali hivyo wanafunzi wote wako salama. Amesema kama wananchi wamejitahidi kuokoa vifaa kama computer na vinginevyo lakini juhudi zao zimegonga mwamba hivyo vilivyobaki wamewaachia Jeshi la zimamoto.

CHANZO: ITV

 
Shule ya secondari ya Kinondoni Muslim inateketea moto muda huu, ambapo chanzo chake hakijafahamika mara moja. Endelea kuwa nasi ili kufahamu kwa kina.
 
kino.png
 
Hizi shule 2 za secondary zimeteketea kwa moto kwa asilimia 75%+ nini kiko nyuma ya hii mioto. Turudi nyuma kwa nini hizi shule zilianzishwa? (Vision and mission of these schools) Je, wapi wamiliki wa hizi shule?

History ya walimu wa madrasa wa hizi shule zikoje? Kwa nini fire wanashindwa kufika katika eneo la tukio zaidi ya masaa 3? Na mwisho zinakuja Gari za zimamoto zaidi ya 2?
 
moto ni kitu hatari sana kwatuliowahi kupata ajali ya moto haswa nyumba tunajua taharuki yake.....moshi ongeza na moto na joto kali na kuchanganyikiwa.....Mungu awasaidie
 
Back
Top Bottom