Shura ya Maimamu Tanzania: Mlinzi Mwanamume wa Rais kuvaa Hijabu na kuingia Msikitini

Naye si angenyoa hizo ndevu zake...!
Ila kwakuwa hakuna Aya inayo kataza wanawake kuswali peke yao basi shura ya Maimamu haikustahili kukosoa hilo jambo.
 
Mkuu Angalia (Dili) na Waumin wengine wadogo, Wadogo. Mambo ya Serikali na Safu ya Ulinzi wa Rais n siri nzito. Pia kumbuka serikali Haina Dini
Pamoja na kwamba serikali haina dini, huheshimu dini za raia wake.

Haya mambo naona kama ni kumtega Rais, kuchafua serikali na kuigombanisha na raia kupitia dini kwa makusudi.

Inashindikana vipi kudhibiti kusanyiko la wanawake lilopangwa mpaka mwanaume ajivalishe hijab?

Kama kulikuwa na viashiria vya hatari, Rais mwanamke angewakilishwa na mwanaume.

Pili, shura ya maimamu inatakiwa ifanye uchunguzi wake, ikemee na itoe ushauri namna ya kuhakikisha usalama wa Rais katika matukio kama hayo ikishirikiana na vyombo vya dola.

Isisubiri kuomba radhi, maji yakimwagika hayazoleki.
 
Kwani Papa aliporuhusu mashoga kubarikiwa vatican aliweka andiko?
Unachanganya mada.
Wewe hujui kua wanawake hawachanganyiki na wanaume kwenye misikiti?
Najua. Lakini ni utamaduni tu ama ni sharia ya dini!?
Kwahiyo hao watu wa ulinzi wameingia kwa wanawake coz hawajui hilo andiko?
Inawezekana...
Ingekua hawajui kua wanawake hawachanganyiki na wanaume,wasingejificha kwa kuvaa hijabu.
Hawakujificha ila mazingira yaliwataka iwe hivyo.

Rais ameingia sehemu wapo wanawake peke yao. Unataka na mtu wa PSU aingie kama mwanaume?

Hivi wangeingia kikawaida si ndiyo ingezua taharuki siku ile ile!!??
 
Nimetafuta kama kuna andiko limewekwa linalokataza wanaume kuswali na wanawake sijaona.

Wangeweka hilo andiko bila ya shaka lingeongezea uzito wa habari yenyewe
Wenzetu huwa kwao utaratibu wa dini ndio muhimu zaidi kuliko andiko la Mungu. Kwao mungu = dini
 
Mtu kama wewe hata kukujibu ni kazi bure tu,maswali yako ya kijinga yanaashiria kua uwezo wako wa uelewa na kuchanganua mambo ni mdogo sana,najua kua unateswa na udini,

Rudia tena kusoma hilo tamko aliloweka mleta mada,majibu yamo humo tayari.
 
Mkichunguza mkajiridhisha kuwa alikuwa mwanaume then mtuambie nani huyo aliachana na kuswali akabakia kupiga picha ya wanaoswali.
 
Asante sana kwa ufafanuzi.
Naomba kuuliza shura ya imam na bakwata wana kauli moja ama kila mmoja ana kuwa na kauli yake haswa kwa maswala tata kama haya.
Wameshakwambi ni shura ya maimam meaning watu wasiofata sheria za mwenyezi mungu bali za dini tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…