Shura ya Maimamu Tanzania: Mlinzi Mwanamume wa Rais kuvaa Hijabu na kuingia Msikitini

Shura ya Maimamu Tanzania: Mlinzi Mwanamume wa Rais kuvaa Hijabu na kuingia Msikitini

Bismillahir Rahmanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

KAMATI YA MAADILI

WARAKA WA WAZI KWA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI

JUNI 18, 2024.

‘MLINZI MWANAMUME WA RAIS KUVAA HIJABU NA KUINGIA MSIKITINI’

Shura ya Maimamu imeona malumbano yanayoendelea katika Mitandao ya Kijamii kuhusiana na picha inayomuonesha mtu anayekisiwa kuwa ni mwanamume akiwa amevaa mavazi ya kike ya Kiislamu.

Picha hiyo inamuonesha mtu huyo akiwa pamoja na wanawake wa Kiislamu akiwa nyuma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Msikitini

Picha hiyo inasemekana ilichukuliwa katika Swala ya Idd Adh-Ha iliyo swaliwa juamatatu Juni 17, 2024, katika Msikiti wa Mikocheni (kwa Warioba), jijini Dar es Salaam.

Katika malumbano hayo inaelezwa kuwa mtu huyo ni miongoni mwa timu ya walinzi wa mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na alikuwa Msikitini hapo kikazi.

MAKOSA MAKUBWA
Shura ya Maimamu imo katika juhudi ya kupata hakika ya mtu huyo kama ni sehemu ya ulinzi wa Rais Samia Suluhu Hassan au laa. Hata hivyo ikiwa tukio kama hilo litaihusisha serikali yoyote ile tunasema ifuatavyo:

Ifahamike kuwa Wanawake wa Kiislamu huvaa mavazi ya stara kusitiri aura zao mbele ya wanaume wasio waume zao.
Lakini wanapokuwa sehemu ya wanawake Msikitini huwa huru kupunguza stara zao kwa kuamini kuwa hakuna mwanamume atakaye waumbua.

Kwa hiyo mwanamume kuingia sehemu hiyo tena kwa kificho, ni kudhamiria kuwaona utupu wanawake hao wachamungu wenye tabia ya kujistiri. Na hiicho ni kitendo kibaya cha kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wanawake wachamungu.

Vilevile Wanawake wa Kiislamu wanapo swali hujipanga katika safu peke yao mbali na wanamume. Kitendo cha kumuweka mwanamume miongoni mwao kisha wakagusana tena ndani ya swala kinaharibu swala zao.
Pia ni kutendo cha kukiuka sheria zinazolinda uhuru wao wa kuabudu. Kitendo hicho pia kinavunja utukufu na heshma ya nyumba takatifu ya Mwenyezi Mungu, Msikiti.

Turejee kusema iwapo mwanamume atajitanda kwa mavazi ya wanawake kisha akaingia Msikitini upande wa wanawake basi hicho ni kitendo kibaya kabisa kinachofedhehesha dini na hata usalama wa taifa.

Shura ya Maimamu inakemea vikali kitendo hicho kisifanywe na ikiwa kimefanywa mfanyaji, na walioidhinisha wanapaswa kuwaomba radhi Waislamu.

Iwapo wahusika hao ni Waislam, wanapaswa kutubu kwa Allah (SW) kwa kutothamini dini yao.

WITO KWA SERIKALI
Shura ya Maimamu inatoa wito kwa vyombo husika vya Dola Tanzania kutoa ufafanuzi iwapo ni kweli kwamba msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan ulijumuisha mlinzi mwanamume aliyeingia Msikitini sehemu ya wanawake na kwamba alifanya hivyo akiwa amefichama kwa kuvaa hijab, vazi la stara la wanawake wa Kiislamu.

Shura inasisitiza kuwa ufafanuzi huo ni muhimu sana kupatikana kwa haraka kwa sababu zifuatazo:

1. Kuondoa taharuki miongoni mwa jamii, na hususan wanawake wa Kiislamu.

2. Ikiwa serika ya Tanzania imehusika, ni muhimu Umma ufahamishwe tukio hilo ni la mara ya kwanza au ndiyo utaratibu wa kiulinzi toka Rais mwanamke alipokuwa Makamu wa Rais na sasa Rais.

3. Umma ufahamishwe iwapo mlinzi huyo ni yeye pekee au wapo wengine wanaume wanaoingia na Rais Msikitini upande wa wanawake wakiwa wamevaa hijabu.

4. Umma ufahamu mlinzi huyo kuvaa hijabu na kuingia kwa kificho Msikitini kwa wanawake ni utashi wake au ni utaratibu wa kazi aliopangiwa.

5. Wananchi wana haki ya kupata ufafanuzi kwa serikali yao pindi linapotokea jambo lenye kutatiza katika jamii.

Katika kuhitimisha, Shura ya Maimamu inarejea wito wake kwa kuhimiza vyombo husika kitoa ufafanuzi wa suala hili kwa muktadha wa nukta tulizoainishwa hapo juu .

Imetolewa Dar es Salaam leo tarehe 18 mwezi wa 6 mwaka 2024.

USTADHI MUSTAFA M. ABEID
KATIBU KAMATI YA MAADILI
Kwanza tujue hiyo shura ya maimamu ni kikundi au mamlaka rasmi iliyokua na usajili au ni hivi vikundi vya kiislam vinazukaga kama uyoga na kujipa uwezo mbele ya jamii huku havipo kisheria. Tukimaliza hapo tuangalie hili jambo.
Kwa maoni yangu sio sahihi kabisa ulinzi wa rais kumuingiza mwanamume sehemu ya wanawake kwenye msikiti kwa hivyo yeyote aliyefanya hivyo inabidi achukuliwe hatua. Japo binafsi sio muislaam najua namna na desturi za waislaam kuheshimu ibada na kuna kitu wanaita udhu nadhani usafi. Kama kulikua na udharura inabidi kuomba radhi na hata kama ni dharura naona ingebidi walinzi wabaki nje ya msikiti au rais asishiriki kabisa ibada.
 
Yap.

Masista kutokuolewa si sawa na hoja ya kusema hairuhusiwi kuingia mwanaume upande wa wanawake wakati wa kuswali.

Kuwa sista si shuruti bali ni hiyari na ndiyo maana sista akivunja kiapo chake huondolewa kwenye usista. Na siyo Kila mwanamke wa kikristo ni sista.

La wanaume kutokuingia Kwa wanawake linasemwa kama sharti. Na kama sharti ni lazima kuwe na chanzo kilichoandikwa mahali.
Okay. Vipi mwanaume akiingia tu kawaida msikitini akaenda upande wa wanawake. Je ibada itasitishwa? Je kuna kifungu ambacho wata refer to?
 
Mihemko tu. Rais alindwe.
Sahihi alindwe, ila sema wewe hii siyo dini yako hivyo hujui UTARATIBU na MIIKO yake. Na kitu usichokijua siyo vizuri kukishangilia maana utazidi kupotosha na wengine.

Hapa watu hawaangalii nafasi ya mtu ktk serikali, wanaangalia UTARATIBU na MIIKO ya dini husika inasemaj. Km wangekuwa wanaangalia nafasi ya mtu basi Rais huyo angeingia msikitini na mabunduki yamemzunguka km anapokuwa kwenye mazingira mengine ya kawaida.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo basi asingevua viatu nje na kuingia peku msikitini na wasaidizi wake.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo asingefuata maagizo ya IMAMU wakati wa kuswali. Imam akielekeza kuwa "sasa ni muda wa swala kila mtu azime SIMU yake lazima azime". Unajua ni kwa nini.

Tusipende kudakia na kushadadia mambo tusiyoyafahamu. Madaraka ya duniani mwisho ni mlangoni mwa mlango wa nyumba ya ibada. Nyie ndo mnakuwa viongozi tayari unachukuwa na nafasi ya Mungu, unaanza kudharau watu, kuwatusi, na kuwatisha ili wakunyenyekee.

Kumbuka wanaoona km jambo lilofanyika halikuwa sawa ni ndugu zake wenyewe (WAISLAM WENZAKE). Sasa wewe wa upande wa pili unapata wapi nguvu ya kusema alikuwa sahihi lazima alindwe. Km kulikuwa na tishio la usalama asingetoka hata kwake. "Ulinzi pekee wa uhakika unatoka kwa Mungu, Unaweza kuwa na mabunduki yako na mapanga lakini ukauwawa na MANATI."
 
Bismillahir Rahmanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

KAMATI YA MAADILI

WARAKA WA WAZI KWA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI

JUNI 18, 2024.

‘MLINZI MWANAMUME WA RAIS KUVAA HIJABU NA KUINGIA MSIKITINI’

Shura ya Maimamu imeona malumbano yanayoendelea katika Mitandao ya Kijamii kuhusiana na picha inayomuonesha mtu anayekisiwa kuwa ni mwanamume akiwa amevaa mavazi ya kike ya Kiislamu.

Picha hiyo inamuonesha mtu huyo akiwa pamoja na wanawake wa Kiislamu akiwa nyuma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Msikitini

Picha hiyo inasemekana ilichukuliwa katika Swala ya Idd Adh-Ha iliyo swaliwa juamatatu Juni 17, 2024, katika Msikiti wa Mikocheni (kwa Warioba), jijini Dar es Salaam.

Katika malumbano hayo inaelezwa kuwa mtu huyo ni miongoni mwa timu ya walinzi wa mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na alikuwa Msikitini hapo kikazi.

MAKOSA MAKUBWA
Shura ya Maimamu imo katika juhudi ya kupata hakika ya mtu huyo kama ni sehemu ya ulinzi wa Rais Samia Suluhu Hassan au laa. Hata hivyo ikiwa tukio kama hilo litaihusisha serikali yoyote ile tunasema ifuatavyo:

Ifahamike kuwa Wanawake wa Kiislamu huvaa mavazi ya stara kusitiri aura zao mbele ya wanaume wasio waume zao.
Lakini wanapokuwa sehemu ya wanawake Msikitini huwa huru kupunguza stara zao kwa kuamini kuwa hakuna mwanamume atakaye waumbua.

Kwa hiyo mwanamume kuingia sehemu hiyo tena kwa kificho, ni kudhamiria kuwaona utupu wanawake hao wachamungu wenye tabia ya kujistiri. Na hiicho ni kitendo kibaya cha kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wanawake wachamungu.

Vilevile Wanawake wa Kiislamu wanapo swali hujipanga katika safu peke yao mbali na wanamume. Kitendo cha kumuweka mwanamume miongoni mwao kisha wakagusana tena ndani ya swala kinaharibu swala zao.
Pia ni kutendo cha kukiuka sheria zinazolinda uhuru wao wa kuabudu. Kitendo hicho pia kinavunja utukufu na heshma ya nyumba takatifu ya Mwenyezi Mungu, Msikiti.

Turejee kusema iwapo mwanamume atajitanda kwa mavazi ya wanawake kisha akaingia Msikitini upande wa wanawake basi hicho ni kitendo kibaya kabisa kinachofedhehesha dini na hata usalama wa taifa.

Shura ya Maimamu inakemea vikali kitendo hicho kisifanywe na ikiwa kimefanywa mfanyaji, na walioidhinisha wanapaswa kuwaomba radhi Waislamu.

Iwapo wahusika hao ni Waislam, wanapaswa kutubu kwa Allah (SW) kwa kutothamini dini yao.

WITO KWA SERIKALI
Shura ya Maimamu inatoa wito kwa vyombo husika vya Dola Tanzania kutoa ufafanuzi iwapo ni kweli kwamba msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan ulijumuisha mlinzi mwanamume aliyeingia Msikitini sehemu ya wanawake na kwamba alifanya hivyo akiwa amefichama kwa kuvaa hijab, vazi la stara la wanawake wa Kiislamu.

Shura inasisitiza kuwa ufafanuzi huo ni muhimu sana kupatikana kwa haraka kwa sababu zifuatazo:

1. Kuondoa taharuki miongoni mwa jamii, na hususan wanawake wa Kiislamu.

2. Ikiwa serika ya Tanzania imehusika, ni muhimu Umma ufahamishwe tukio hilo ni la mara ya kwanza au ndiyo utaratibu wa kiulinzi toka Rais mwanamke alipokuwa Makamu wa Rais na sasa Rais.

3. Umma ufahamishwe iwapo mlinzi huyo ni yeye pekee au wapo wengine wanaume wanaoingia na Rais Msikitini upande wa wanawake wakiwa wamevaa hijabu.

4. Umma ufahamu mlinzi huyo kuvaa hijabu na kuingia kwa kificho Msikitini kwa wanawake ni utashi wake au ni utaratibu wa kazi aliopangiwa.

5. Wananchi wana haki ya kupata ufafanuzi kwa serikali yao pindi linapotokea jambo lenye kutatiza katika jamii.

Katika kuhitimisha, Shura ya Maimamu inarejea wito wake kwa kuhimiza vyombo husika kitoa ufafanuzi wa suala hili kwa muktadha wa nukta tulizoainishwa hapo juu .

Imetolewa Dar es Salaam leo tarehe 18 mwezi wa 6 mwaka 2024.

USTADHI MUSTAFA M. ABEID
KATIBU KAMATI YA MAADILI
Picha iko wapi
 
Sahihi alindwe, ila sema wewe hii siyo dini yako hivyo hujui UTARATIBU na MIIKO yake. Na kitu usichokijua siyo vizuri kukishangilia maana utazidi kupotosha na wengine.

Hapa watu hawaangalii nafasi ya mtu ktk serikali, wanaangalia UTARATIBU na MIIKO ya dini husika inasemaj. Km wangekuwa wanaangalia nafasi ya mtu basi Rais huyo angeingia msikitini na mabunduki yamemzunguka km anapokuwa kwenye mazingira mengine ya kawaida.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo basi asingevua viatu nje na kuingia peku msikitini na wasaidizi wake.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo asingefuata maagizo ya IMAMU wakati wa kuswali. Imam akielekeza kuwa "sasa ni muda wa swala kila mtu azime SIMU yake lazima azime". Unajua ni kwa nini.

Tusipende kudakia na kushadadia mambo tusiyoyafahamu. Madaraka ya duniani mwisho ni mlangoni mwa mlango wa nyumba ya ibada. Nyie ndo mnakuwa viongozi tayari unachukuwa na nafasi ya Mungu, unaanza kudharau watu, kuwatusi, na kuwatisha ili wakunyenyekee.

Kumbuka wanaoona km jambo lilofanyika halikuwa sawa ni ndugu zake wenyewe (WAISLAM WENZAKE). Sasa wewe wa upande wa pili unapata wapi nguvu ya kusema alikuwa sahihi lazima alindwe. Km kulikuwa na tishio la usalama asingetoka hata kwake. "Ulinzi pekee wa uhakika unatoka kwa Mungu, Unaweza kuwa na mabunduki yako na mapanga lakini ukauwawa na MANATI."
Manati ya Daudi 😂😂😂😂
 
Okay. Vipi mwanaume akiingia tu kawaida msikitini akaenda upande wa wanawake. Je ibada itasitishwa? Je kuna kifungu ambacho wata refer to?
Ahaa!!

Hilo swali lako ujumla wake ndiyo inatakiwa ijulikane kama ni mapokeo tu ama surah/aya inayokataza wanawake kuchanganyika na wanaume wakati wa kuswali ipo.

Maana wakatoliki wanapiga alama ya msalaba kabla ya kusali wakati wakristo wengine hawafanyi hivyo. Kwa ivo kupiga alama ya msalaba ni mapokeo tu ila yanayoheshimiwa.

Kwa ivo inawezekana pia kutochangamana wanawake na wanaume wakati wa kuswali inawezekana isiwe sharia ya kiislam ila ikawa ni mapokeo yanayoheshimiwa.

Siyo dhambi kuheshimu mapokeo(Sunnah).
 
Sahihi alindwe, ila sema wewe hii siyo dini yako hivyo hujui UTARATIBU na MIIKO yake. Na kitu usichokijua siyo vizuri kukishangilia maana utazidi kupotosha na wengine.

Hapa watu hawaangalii nafasi ya mtu ktk serikali, wanaangalia UTARATIBU na MIIKO ya dini husika inasemaj. Km wangekuwa wanaangalia nafasi ya mtu basi Rais huyo angeingia msikitini na mabunduki yamemzunguka km anapokuwa kwenye mazingira mengine ya kawaida.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo basi asingevua viatu nje na kuingia peku msikitini na wasaidizi wake.

Km ingekuwa inaangaliwa nafasi aliyonayo asingefuata maagizo ya IMAMU wakati wa kuswali. Imam akielekeza kuwa "sasa ni muda wa swala kila mtu azime SIMU yake lazima azime". Unajua ni kwa nini.

Tusipende kudakia na kushadadia mambo tusiyoyafahamu. Madaraka ya duniani mwisho ni mlangoni mwa mlango wa nyumba ya ibada. Nyie ndo mnakuwa viongozi tayari unachukuwa na nafasi ya Mungu, unaanza kudharau watu, kuwatusi, na kuwatisha ili wakunyenyekee.

Kumbuka wanaoona km jambo lilofanyika halikuwa sawa ni ndugu zake wenyewe (WAISLAM WENZAKE). Sasa wewe wa upande wa pili unapata wapi nguvu ya kusema alikuwa sahihi lazima alindwe. Km kulikuwa na tishio la usalama asingetoka hata kwake. "Ulinzi pekee wa uhakika unatoka kwa Mungu, Unaweza kuwa na mabunduki yako na mapanga lakini ukauwawa na MANATI."
Umesema Sana mkuu. Hapo umekua mtu na nusu. Hakuna mamlaka yazidiyo ukuu wa Mungu
 
Back
Top Bottom