Si busara kumruhusu mtoto aanze kujitegemea wakati hana chochote

Si busara kumruhusu mtoto aanze kujitegemea wakati hana chochote

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
Kuna dhana imezoeleka na wazazi ambao vijana wao wamefikia umri wa kujitegemea kuwaruhu ama kuwataka waondoke nyumbani ili hali hawana chochote na inawezekana hata kazi hana inayoeleweka.

Hii hali ina athari nyingi sana kwa vijana wa jinsia zote ila kwa wakike ndio zaidi. Kijana kuhitimu chuo haimaanishi kwamba sasa anaweza kumudu kila kitu,bado anakuwa na changamoto za kutqfuta kibarua ili aweze kujikimu.

Kwa upande wangu mimi nitafanya hivi ,wanangu kutoka nyumbani itakuwa ni option,na anapotoka nilazoma nijue kwa uyakinifu anaenda wapi na kwanini? Akinipa hoja yakinifu na nikazikunali basi nitagharamia kila kitu,kodi ya nyumba miezi 6, pesa yakujikimu miezi 6( hata kama anamshahara) kama amepata kazi,!,nitam unulia kila kitu ambacho ni hitaji muhimu kwa kuanza maisha ikiwemo kitanda, na godoro na mengineyo.

Kama ameamua kufanya biashara basi nitampatia mtaji,na nitaifuatilia mpaka pale jitakapo ona imesimama,na katika kipindi hicho chote nitampatia mahitaji muhimu mpaka pale biashara itakapo shinda kipindi cha mpito.

Unamruhusu mtoto aondoke halafu mkononi hana kitu wala hana kitu cha maana, matokeo yake kama ni wa kike anashawishika kujiuza.

Hakikisha mtoto kasimama na unauhakika kasimama kikamilifu ndio umuache.
 
Mimi ni mmojawapo nilivyomaliza chuo niliambiwa nisirudi home. Nikakomaa hapa mjini mpaka nikatoboa acheni kuwalegeza watoto wa kiume kwa mtoto wa kike sawa, kama hana kazi akae home.

Mzee alinambia kama unafungua biashara niione hapo nitakupa pesa ya kukuza biashara. Acheni kuwalemaza watoto wa kiume, unampa mtaji anakwenda kidimbwi kula bata ananunua na macho 3.

Akimaliza chuo fukuza akatafute maisha hapo atapata akili ya maisha.
 
Mimi ni mmojawapo nilivyomaliza chuo niliambiwa nisirudi home. Nikakomaa hapa mjini mpaka nikatoboa acheni kuwalegeza watoto wa kiume kwa mtoto wa kike sawa, kama hana kazi akae home.
wewe ulinyanyaswa kisaikolojia na wazazi wako ila kwa kukuwa Mungu amejaalia umefanikiwa imekuwa bahati kwako ila usingefanikiwa ndio ungejua hujui.

mtoto lazima aandaliwe kisaikolojia na kimaisha na wazazi au walezi wake ili pindi anapoanza kujitegemea iwerahisi kukabiliana na mazingira na hatakiwi kutelekezwa mbali mfana angalia wanyama na ndege waanza kutengena taratibu na vifaranga vyao au vindama vyao hata simba uanza taratibu kuwatenga madume na baadae kuwafukuza kabisa. sio jambo la kukurupuka tu tuna mengi ya kujifunza hata wanyama pia wanatufunza sana.
 
Mimi ni mmojawapo nilivyomaliza chuo niliambiwa nisirudi home. Nikakomaa hapa mjini mpaka nikatoboa acheni kuwalegeza watoto wa kiume kwa mtoto wa kike sawa, kama hana kazi akae home.

Mzee alinambia kama unafungua biashara niione hapo nitakupa pesa ya kukuza biashara. Acheni kuwalemaza watoto wa kiume, unampa mtaji anakwenda kidimbwi kula bata ananunua na macho 3.

Akimaliza chuo fukuza akatafute maisha hapo atapata akili ya maisha.
Mzee wako ni Magufuli mwingine
 
Mimi baada ya kuingia kidato cha tano shule ya boarding chumba changu kilipangishwa, ilikua ni alama ya sasa sina makazi ya kudumu nyumbani ilimaanisha natakiwa nianze kujitegemea. Toka wakati huo nilijitegemea rasmi.
That's good.
 
Mimi ni mmojawapo nilivyomaliza chuo niliambiwa nisirudi home. Nikakomaa hapa mjini mpaka nikatoboa acheni kuwalegeza watoto wa kiume kwa mtoto wa kike sawa, kama hana kazi akae home.

Mzee alinambia kama unafungua biashara niione hapo nitakupa pesa ya kukuza biashara. Acheni kuwalemaza watoto wa kiume, unampa mtaji anakwenda kidimbwi kula bata ananunua na macho 3.

Akimaliza chuo fukuza akatafute maisha hapo atapata akili ya maisha.

Siku hizi common sense imeanguka sana.

Sijui ndio haki za binadamu. Sijui.
 
Mtoto kwanzia akiwa mdogo mjenge ajue thamani ya pesa ,na jinsi ya kupata kipato na kukitunza , then kama una nia ya kuja kumpa mtaji au kumwacha ajitegemee itakua poa sna , usije ukampa mtaji au kumwacha ajitegemee mtoto ambae haujamfundisha vzuri.
 
Kuna dhana imezoeleka na wazazi ambao vijana wao wamefikia umri wa kujitegemea kuwaruhu ama kuwataka waondoke nyumbani ili hali hawana chochote na inawezekana hata kazi hana inayoeleweka.

Hii hali ina athari nyingi sana kwa vijana wa jinsia zote ila kwa wakike ndio zaidi. Kijana kuhitimu chuo haimaanishi kwamba sasa anaweza kumudu kila kitu,bado anakuwa na changamoto za kutqfuta kibarua ili aweze kujikimu.

Kwa upande wangu mimi nitafanya hivi ,wanangu kutoka nyumbani itakuwa ni option,na anapotoka nilazoma nijue kwa uyakinifu anaenda wapi na kwanini? Akinipa hoja yakinifu na nikazikunali basi nitagharamia kila kitu,kodi ya nyumba miezi 6, pesa yakujikimu miezi 6( hata kama anamshahara) kama amepata kazi,!,nitam unulia kila kitu ambacho ni hitaji muhimu kwa kuanza maisha ikiwemo kitanda, na godoro na mengineyo.

Kama ameamua kufanya biashara basi nitampatia mtaji,na nitaifuatilia mpaka pale jitakapo ona imesimama,na katika kipindi hicho chote nitampatia mahitaji muhimu mpaka pale biashara itakapo shinda kipindi cha mpito.

Unamruhusu mtoto aondoke halafu mkononi hana kitu wala hana kitu cha maana, matokeo yake kama ni wa kike anashawishika kujiuza.

Hakikisha mtoto kasimama na unauhakika kasimama kikamilifu ndio umuache.
Akili za kibabe. Only the fittest of the fittest sHall survive
 
Unataka uondoke na chochote Cha nani. Mali za baba yako siyo zako ni zake na mkewe.Watoto acheni kilialia ndio maana mnawachuria wazazi wenu wafe ili mbaki na mali. Kwani yeye hizo mali alipewa na baba yake. Pambana na hali Yako.
Hii nyuzi ni muendelezo wa uzi wangu wa jana nilioupa jina "MALI ZANGU JI KWA AJILI YA WANANGU" kaa kwa kutulia
 
Mimi ni mmojawapo nilivyomaliza chuo niliambiwa nisirudi home. Nikakomaa hapa mjini mpaka nikatoboa acheni kuwalegeza watoto wa kiume kwa mtoto wa kike sawa, kama hana kazi akae home.

Mzee alinambia kama unafungua biashara niione hapo nitakupa pesa ya kukuza biashara. Acheni kuwalemaza watoto wa kiume, unampa mtaji anakwenda kidimbwi kula bata ananunua na macho 3.

Akimaliza chuo fukuza akatafute maisha hapo atapata akili ya maisha.
Lengo sio kulemaza lengo nikufanya aishi bila stress na kukwepa vishawishi,siwezi kufukuza mwanangu wa kumzaa mwenyewe mkuu
 
Siku hizi common sense imeanguka sana.

Sijui ndio haki za binadamu. Sijui.

wewe ulinyanyaswa kisaikolojia na wazazi wako ila kwa kukuwa Mungu amejaalia umefanikiwa imekuwa bahati kwako ila usingefanikiwa ndio ungejua hujui.

mtoto lazima aandaliwe kisaikolojia na kimaisha na wazazi au walezi wake ili pindi anapoanza kujitegemea iwerahisi kukabiliana na mazingira na hatakiwi kutelekezwa mbali mfana angalia wanyama na ndege waanza kutengena taratibu na vifaranga vyao au vindama vyao hata simba uanza taratibu kuwatenga madume na baadae kuwafukuza kabisa. sio jambo la kukurupuka tu tuna mengi ya kujifunza hata wanyama pia wanatufunza sana.
Mpigieni makofi tafadhali😅😅
 
Back
Top Bottom