Si kwa ajili ya ubaguzi, bali namshauri Rais Samia aepuke kufanya maamuzi makubwa ya muda mrefu yanayohusu upande wa Tanzania bara peke yake

Si kwa ajili ya ubaguzi, bali namshauri Rais Samia aepuke kufanya maamuzi makubwa ya muda mrefu yanayohusu upande wa Tanzania bara peke yake

..serikali zinazopaswa kurudishwa ni zile zilizokuwepo 1964 kabla ya muungano.
Serikali iliyotuwekea misingi mibovu mpaka tukawa masikini wa mwisho duniani?

"Kazi ya Mungu haina makosa".
 
..sasa hivi Maraisi wote wanatoka Zanzibar. Kama wako serious huu ndio muda muafaka wa kuvunja muungano.

..ningekuelewa kama ungesema CCM ndio wanang'ang'ania muungano. Na humo wako Watanganyika na Wazanzibari.
Najua umeshaelewa, ila kukubali mbele ya watoto ndio shida, halafu sasa hivi wamebadilishana mtanganyika anatawala zenji na mzenji anatawala bara

Ccm wapo makini sana, haiwezi kutokea hata mara moja marais wote wakatoka upande mmoja wala dini moja, wala makamu na rais wakafanane, katu haitatokea tena
*
Kama ulikua hufahamu, Huseni ni mbara tena mtanganyika original
 
Najua kwamba Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama Rais wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Rais Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Rais Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Rais Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na matokeo ya maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Rais Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Rais Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
inakwaza kuona nchi yenye raia zaidi ya 58m inashindanishwa waajiriwa/wateuliwa na kawilaya kenye watu hata 2m hawafiki, kazanzibar. Tanganyika ipo mioyoni mwa wengi na kuna siku itafufuka kwa nguvu kubwa sana, na wale walioibeza watatafuta kwa kwenda.
 
Najua kwamba Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama Rais wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Rais Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Rais Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Rais Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na matokeo ya maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Rais Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Rais Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
Unapoteza muda wako bure kushauri wapumbavuu
 
Najua umeshaelewa, ila kukubali mbele ya watoto ndio shida, halafu sasa hivi wamebadilishana mtanganyika anatawala zenji na mzenji anatawala bara

Ccm wapo makini sana, haiwezi kutokea hata mara moja marais wote wakatoka upande mmoja wala dini moja, wala makamu na rais wakafanane, katu haitatokea tena
*
Kama ulijua hufahamu, Huseni ni mbara tena mtanganyika original

..Watanganyika wengi huwa hawana habari na muungano mpaka pale Wazanzibari wanapoanza kulalamika.

..Vilevile Watanganyika hawana muamko wa siasa kulinganisha na Wazanzibari kwa hiyo sio rahisi kuanza kuudadisi muungano.

..Watanganyika wanaopinga muungano ni wale wanaofuatilia historia na siasa kwa ukaribu, na tena wako ktk vyama vya upinzani.

..Kwa upande mwingine, muungano unalindwa na kutetewa na genge la Watanganyika na Wazanzibari walioko ndani ya CCM.

..Wazanzibari walioko CCM wanategemea majeshi ya muungano kutwaa madaraka ya Zanzibar. Hivyo wanatetea muungano kwasababu unawasaidia kubaki madarakani.

..Watanganyika walioko CCM hawataki muungano uguswe, kwasababu hauwezi kuguswa bila kugusa na mengine kama Tume ya Uchaguzi, mamlaka ya Raisi, etc etc. Mabadiliko yoyote ktk muungano yanatishia madaraka yao.

..Huo ndio mtizamo wangu kuhusu kinachoendelea ktk muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 
Najua kwamba Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama Rais wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Rais Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Rais Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Rais Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na matokeo ya maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Rais Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Rais Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
Una hoja Mkuu.
 
Huyu mama kazungukwa na watu ambao sio wazuri na wanamdanganya na kwa bahati mbaya mno ni watu ambao anawaamini.
 
Labda Watoto wa Waasisi ni special 😂😂

Ulale Unono 😃

Mtoto akirithi kazi za wazazi wake kuna ubaya? Tena huyo anakuwa mzuri zaidi.

Tazama wahindi na Waarabu wanavyotesa watoto zao kwa kazi za kurithi
kwa wazazi wao.

Unataka mtu katoka maporini huko mjini kaja kwa kusoma tu akihitimu anapewa shirika la umma la usafirishaji?

Matokeo; DMT chali, UDA chali, KAMATA chali. hatujakoma, sasa BRT chali.

Tunaisubiri na ATC na SGR, kama hatua za haraka hazitachukuliwa, na zenyewe chali.

Januari alitakiwa aishie jeshini na kwenye chama tu, kama baba'ke.

Nape, mwisho kabisa ukuu wa mkoa tu.
 
Mtoto akirithi kazi za wazazi wake kuna ubaya? Tena huyo anakuwa mzuri zaidi.

Tazama wahindi na Waarabu wanavyotesa watoto zao kwa kazi za kurithi
kwa wazazi wao.

Unataka mtu katoka maporini huko mjini kaja kwa kusoma tu akihiytimu anapewa shirika la umma ya usafirishaji?

Matokeo; DMT chali, UDA chali, KAMATA chali. hatujakoma, sasa BRT chali.

Tunaisubiri na ATC na SGR, kama hatua za haraka hazitachukuliwa, na zenyewe chali.
Akina Maharagwe ni WA hapa hapa town kama Pedeshee Amos Makala na Mongela 😂
 
Mtoto akirithi kazi za wazazi wake kuna ubaya? Tena huyo anakuwa mzuri zaidi.

Tazama wahindi na Waarabu wanavyotesa watoto zao kwa kazi za kurithi
kwa wazazi wao.

Unataka mtu katoka maporini huko mjini kaja kwa kusoma tu akihitimu anapewa shirika la umma la usafirishaji?

Matokeo; DMT chali, UDA chali, KAMATA chali. hatujakoma, sasa BRT chali.

Tunaisubiri na ATC na SGR, kama hatua za haraka hazitachukuliwa, na zenyewe chali.

Januari alitakiwa aishie jeshini na kwenye chama tu, kama baba'ke.

Nape, mwisho kabisa ukuu wa mkoa tu.

..Je, Mama Abduli naye alitakiwa aishie kwenye ualimu, kwasababu ilikuwa kazi ya Mzee wake?
 
Linatekelezeka kwa kuirudisha nchi ya Tanganyika.
Kwanini iwe dhambi kuirudisha hiyo nchi?
Mkuu ni lazima wakubaliane na Nchi ya Zanzibar. Kwenye makubaliano ni budi kuwe na time mbili, moja ya Nchi ya Zanzibar na ingine ya Nchi gani (Tanganyika)? maana Tanganyika sio nchi, watu gani wataiwakilisha wenye hadhi ya Nchi.
 
Mkuu umenena vyema kabisa, kifo cha Hayati Rais Magufuli kimetoa somo kubwa sana juu ya mapungufu yaliyomo ndani ya KATIBA yetu. Kuna utata wingi kwenye Katiba iliyopo. Rasimu ya Katiba ya Mzee Warioba ilikuwa ndio Katiba sahihi na iliyo endana na wakati tulio nao, ila Bunge chini ya maelekezo ya wajumbe wachache ndani na nje ya Bunge waliifuta Rasimu hiyo na kutoa maelekezo ya aina ya Katiba waitakayo na kuliagiza BUNGE kutengua RASIMU hiyo kwa manufaa yao
Kumbe unaelewa bali unajitoa akili kimakusudi?

Mambo ya muungano yanajulikana, na japo Tanzania bara haina serikali yake, mambo yaliyofanywa kuwa ya Zanzibar yanafanya mambo yale yale yakiwa kwenye muungano yasiwe tena ya muungano bali ya Tanzania bara.

Kwa mfano, huwezi kusema mafuta yaliyoko Zanzibar ni suala la Zanzibar, na mafuta yaliyoko bara ni ya muungano. Ukishafanya mafuta yaliyoko visiwani ni ya Zanzibar, inference ni kwamba mafuta yaliyoko bara hayapaswi tena kuonwa kama ni mafuta ya muungano.

Kumbuka kwamba, kimsingi, iwe imeandikwa kwenye katiba au la, mteule wa kugombea uraisi wa Tanzania siku zote atatoka bara, na mgombea mwenza kutoka Zanzibar. Yote haya ni kutambua kwamba siku hizi raisi wa Tanzania kimsingi ni raisi wa Tanzania bara kwa sababu Zanzibar inajitegema kiserikali. Kuna kama 2% ya mambo atakayofanya kama raisi yataihusu Zanzibar, na sana sana ni mambo ya nchi za nje.

Katika mpangilio huu, hawakuona mbali na walisahau kusema raisi akifa makamu wa raisi hapaswi kuwa raisi kwa sababu siku zote makamu wa raisi wa kupigiwa kura atakuwa ni kutoka Tanzania bara, na akiwa raisi wa Tanzania ndio atakuwa raisi wa Tanzania bara, bila serikali ya Tanzania bara kuwapo rasmi. Raisi akifa na makamu wa Raisi toka Zanzibar akawa raisi basi awe acting president kwa maximum mwaka mmoja tu ili ndani ya muda huo uchaguzi mpya wa raisi ufanyike kisha arudie kuwa makamu wa raisi.

Theoretically, ukitaka kusawazisha hali iliyopo, ya Samia kuwa raisi wa Tanzania kutoka Zanzibar, inabidi mtu kutoka bara aende akawe raisi wa serikali ya mapinduzi Zanzibar. Tumpeleke Mwigulu akawe raisi kule, mweupe kama wao.

Ndio maana nikasema, kwa kuwa Samia anatoka Zanzibar kutokana na jambo lisilotazamiwa, ni busara kwamba asifanye maamuzi kuhusu mambo makubwa ya bara yenye long term lock-in effect, na kusubiri hadi raisi kutoka bara akiwa madarakani ndio afanye hayo maamuzi.
 
Back
Top Bottom