Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Ukimsikiliza Paul, kuna kauli anayotumia '' anamshukuru Rais SSH kwa kubeba jina lake hadi Kamati kuu''
Hii ni kuwaambia watu uwepo wake si wa kubahatisha, yeye ni mteule wa Mwenyekiti wa CCM na RASI kama wao
Umechambua vizuri sana.
 
Hili silioni kama jambo geni. Nani asiyemjua Paul! Hakuanza kutoa maagizo leo. Ni Paul huyu aliyelitukana 'Bunge' , Waziri mkuu akiwemo. Nini kilifanyika? Ni impunity. Si huyu paul alikuwa anatoa maagizo kila siku wakati wa JPM, wote wakiwemo PM walikuwa kimya. Jambo zuri la Paul ni kuwa consistent na utendaji wake, habadiliki.

Kwahiyo Waziri mkuu ni sehemu ya watu waliokubali uteuzi wa Paul. Si kukubali gizani, bali walikubali wakimjua.
Hapa kuna tatizo la ''ego' . Viongozi wanaogopa nafasi zao binafsi na si heshima na hadhi za nafasi zao.
Usingeweza kumtweza Kawawa, Malecela, Salim , Warioba, Msuya kireja reja namna hiyo. Ni hawa wasakatonge

Kwanza, anapaswa alinde heshima yake halafu tutmheshimu. Mzee Warioba aliwahi kwenda kwa Nyerere na kumwambia kama abcd inafanyika mimi najiuzulu.. Tena hiyo ilikuwa siri ya serikali lakini hakujali nafasi yake, alijali heshima ya nafasi na heshima yake. Mzee Warioba yupo anadunda heshima zinamfuata!

Narudia tena, lazima kwanza aheshimu nafasi yake halafu sisi tutamheshimu. Juzi alikuwa na chaguo, kumkaripia Paul au kumwambia Mwenyekiti kama humkemei hadharani naachia ngazi, hakufanya anaogopa asijekatwa jina wakati wa kinyang'anyiro cha Urais.

Ukimsikiliza Paul, kuna kauli anayotumia '' anamshukuru Rais SSH kwa kubeba jina lake hadi Kamati kuu''
Hii ni kuwaambia watu uwepo wake si wa kubahatisha, yeye ni mteule wa Mwenyekiti wa CCM na RASI kama wao

Juzi kasema ni maagizo ya chama, sasa unajiuliza Waziri mkuu hakuwepo kwenye vikao vya chama!

Paul atawasumbua sana kwasababu hawana mtima, wanaogopa vyeo na wanavizia teuzi. Huko ndiko uwanja wa 'nyumbani' wa Paul.
Paul atawapeleka Mzobe mzobe wachumia tumbo woote na hawana cha kumfanya
 
Hili silioni kama jambo geni. Nani asiyemjua Paul! Hakuanza kutoa maagizo leo. Ni Paul huyu aliyelitukana 'Bunge' , Waziri mkuu akiwemo. Nini kilifanyika? Ni impunity. Si huyu paul alikuwa anatoa maagizo kila siku wakati wa JPM, wote wakiwemo PM walikuwa kimya. Jambo zuri la Paul ni kuwa consistent na utendaji wake, habadiliki.

Kwahiyo Waziri mkuu ni sehemu ya watu waliokubali uteuzi wa Paul. Si kukubali gizani, bali walikubali wakimjua.
Hapa kuna tatizo la ''ego' . Viongozi wanaogopa nafasi zao binafsi na si heshima na hadhi za nafasi zao.
Usingeweza kumtweza Kawawa, Malecela, Salim , Warioba, Msuya kireja reja namna hiyo. Ni hawa wasakatonge

Kwanza, anapaswa alinde heshima yake halafu tutmheshimu. Mzee Warioba aliwahi kwenda kwa Nyerere na kumwambia kama abcd inafanyika mimi najiuzulu.. Tena hiyo ilikuwa siri ya serikali lakini hakujali nafasi yake, alijali heshima ya nafasi na heshima yake. Mzee Warioba yupo anadunda heshima zinamfuata!

Narudia tena, lazima kwanza aheshimu nafasi yake halafu sisi tutamheshimu. Juzi alikuwa na chaguo, kumkaripia Paul au kumwambia Mwenyekiti kama humkemei hadharani naachia ngazi, hakufanya anaogopa asijekatwa jina wakati wa kinyang'anyiro cha Urais.

Ukimsikiliza Paul, kuna kauli anayotumia '' anamshukuru Rais SSH kwa kubeba jina lake hadi Kamati kuu''
Hii ni kuwaambia watu uwepo wake si wa kubahatisha, yeye ni mteule wa Mwenyekiti wa CCM na Rais kama wao

Juzi kasema ni maagizo ya chama, sasa unajiuliza Waziri mkuu hakuwepo kwenye vikao vya chama!

Paul atawasumbua sana kwasababu hawana mtima, wanaogopa vyeo na wanavizia teuzi. Huko ndiko uwanja wa 'nyumbani' wa Paul.
Nimekuelewa sana Mkuu
 
R

Mwenyekiti wa chama mwenyewe amekuwa wa hovyo kuteua jitu la hovyo km lile. Makonda ana mtindio wa akili, hana akili hata kidogo. Sijawahi kusikia hata rais akimwita mkuu wa mkoa, eti njoo hapa tena kimbia, na mama mtu mzima mwenye watoto wakubwa na mme, Makonda lenyewe toto la juzi. Samia atapata anachokitafuta, anafikiri CCM ya leo ni ile ya enzi za mwl. Nyerere, km anataka usalama wake na usalama wa nchi aondoe ile takataka.

we kenge kasome katiba ya CCM kujua majukumu ya ile nafasi, na ukumbuke yeye siyo wa kwanza. Yule mshamba ni lofa, kwanza linapenda sana sifa mbele ya kadamnasi hasa kwa kuwadhalilisha wenzake. Yule fala alitakiwa gerezani, aliyemshauri Samia hakuwa na nia nzuri
Watu mbaujasiri sana kwenye keyboard nenda ista yake au facebook kaandike haya. uone nchi yetu ilivyo .
 
Chama kimempa maagizo waziri mkuu hadharani, sio Makonda, imeisha hiyo, endeleeni kujitekenya na hizo tafsiri zenu butu
Hivi muda ambao Makonda alimpa Waziri Mkuu kumaliza tatizo la migogoro ya ardhi umewadia? Kama bado je kuna dalili za migogoto hiuo kwisha. Je muda ukifika na migogoro hiyo bado iko pale pale je Makonda anawezak kuchukua hatua dhidi ya Waziri Mkuu?
 
Hivi muda ambao Makonda alimpa Waziri Mkuu kumaliza tatizo la migogoro ya ardhi umewadia? Kama bado je kuna dalili za migogoto hiuo kwisha. Je muda ukifika na migogoro hiyo bado iko pale pale je Makonda anawezak kuchukua hatua dhidi ya Waziri Mkuu?
Yes, kama wanavyosema Tanzania ni Channel ya Vichekesho huko Mbinguni, basi wale waliokuwa wanangali hivyo vichekesho wamuulize hatua atakayochukuliwa huyo waziri mkuu baada ya kushindwa kazi.
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
😂😂
 
Back
Top Bottom