Hili silioni kama jambo geni. Nani asiyemjua Paul! Hakuanza kutoa maagizo leo. Ni Paul huyu aliyelitukana 'Bunge' , Waziri mkuu akiwemo. Nini kilifanyika? Ni impunity. Si huyu paul alikuwa anatoa maagizo kila siku wakati wa JPM, wote wakiwemo PM walikuwa kimya. Jambo zuri la Paul ni kuwa consistent na utendaji wake, habadiliki.
Kwahiyo Waziri mkuu ni sehemu ya watu waliokubali uteuzi wa Paul. Si kukubali gizani, bali walikubali wakimjua.
Hapa kuna tatizo la ''ego' . Viongozi wanaogopa nafasi zao binafsi na si heshima na hadhi za nafasi zao.
Usingeweza kumtweza Kawawa, Malecela, Salim , Warioba, Msuya kireja reja namna hiyo. Ni hawa wasakatonge
Kwanza, anapaswa alinde heshima yake halafu tutmheshimu. Mzee Warioba aliwahi kwenda kwa Nyerere na kumwambia kama abcd inafanyika mimi najiuzulu.. Tena hiyo ilikuwa siri ya serikali lakini hakujali nafasi yake, alijali heshima ya nafasi na heshima yake. Mzee Warioba yupo anadunda heshima zinamfuata!
Narudia tena, lazima kwanza aheshimu nafasi yake halafu sisi tutamheshimu. Juzi alikuwa na chaguo, kumkaripia Paul au kumwambia Mwenyekiti kama humkemei hadharani naachia ngazi, hakufanya anaogopa asijekatwa jina wakati wa kinyang'anyiro cha Urais.
Ukimsikiliza Paul, kuna kauli anayotumia '' anamshukuru Rais SSH kwa kubeba jina lake hadi Kamati kuu''
Hii ni kuwaambia watu uwepo wake si wa kubahatisha, yeye ni mteule wa Mwenyekiti wa CCM na RASI kama wao
Juzi kasema ni maagizo ya chama, sasa unajiuliza Waziri mkuu hakuwepo kwenye vikao vya chama!
Paul atawasumbua sana kwasababu hawana mtima, wanaogopa vyeo na wanavizia teuzi. Huko ndiko uwanja wa 'nyumbani' wa Paul.