Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Hata hapo Malawi ilifanyika hivyo !
Rais alianzisha Chama chake akiwa Ikulu !
kwa hapa nchini wanasema sekretarieti ya chama cha mapinduzi ina nguvu kubwa kuliko kiongozi yeyote wa serikali isipokuwa rais. Wanahalisha katibu wa uenezi wake ana mamlaka ya kum command kiongozi yeyote wa serikali isipokuwa rais. Tuseme tu huo ni mfumo wa chama chao kutawala, haiwezekani katibu wa itikadi na uenezi kumsulubu waziri mkuu au makamu wa rais huo ni utovu wa nidhamu na ni utawala mbovu (regime)
 
Mi naona kama utovu wa nidhamu. Waziri mkuu ni kiongozi mkubwa hapaswi kuagizwa kufanya jambo fulani na katibu muenezi wa chama. Serikali ni kubwa kuliko chama. Kuna nchi rais wake anaweza kuachana na chama chake kilichomuingiza ikulu na akaanzisha chama kingine huku akiendelea na urais wake
Jidanganye....siku anaacha uanachama..na urais unasepa hapohapo
 
Umeongea point sana watu hawajui kazi ya makonda yupo kwa ajili ya kuludisha chama matumaini kwa wananchi watu mnamuona kama vile anamsema waziri mkuu ila nikama maigizo hayo wanafanya wana ccm ili muone kama chama hakiwaogopi viongozi ili wananchi muludishe Imani kwa chama
Kweli watu Wanasemaga SiHasa ni uongo uongo tu unaokubalika !
Ngoja tuone !!
 
Umeongea point sana watu hawajui kazi ya makonda yupo kwa ajili ya kuludisha chama matumaini kwa wananchi watu mnamuona kama vile anamsema waziri mkuu ila nikama maigizo hayo wanafanya wana ccm ili muone kama chama hakiwaogopi viongozi ili wananchi muludishe Imani kwa chama
Mwamba alisemaga Mtanikumbuka !
Umagufulication katika kuongoza Nchi hakukwepeki !
Ndio maana Makonda alipokelewa pale Lumumba kwa kibwagizo cha -
Magufuli Magufuli Magufuli !! Everything was planned !

“Mtanikumbuka kwa yale mazuri sio kwa yale mabaya “ By Mwamba !
 
Maagizo yakitolewa ndan mnakimbilia space mnasema watu dhaifu,wengine lugha za kejeli "hili nalo mkalitizame" au hii sio kejel huko twita au mnafikiri hatuoni? Maagizo yanatolewa live live bila chenga napo mmekuja kuanza kulia sasa wakil msom mbona space kule tunakuaga wote hamuelewek.au ndio nasikia mnatumia kero za wananch kama kete.zikishughulikiwa tutakosa ajenda
 
Jidanganye....siku anaacha uanachama..na urais unasepa hapohapo
Rais wa Nchi ni mkubwa sana kuliko chochote kile katika Nchi !!
Na wengine wakaongeza na cheo cha Mwenyekiti wa Chama ambaye pia kwa kanuni zilizopo Chamani Mwenyekiti hawezi kutikiswa na yeyote pale Chamani 😅😅😅🙏🙏🙏 !
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Anayetoa maagizo anatumwa na mwenyekiti ambaye ndiye boss wa huyo waziri mkuu. Samia ni rais mpole na pia hana uwezo wa kurumbana hadharani na wasaidizi wake ambao wote ni wanaume waliomzunguka.

Ujumbe anaoutoa Makonda moja kwa moja una akisi kile ambacho boss anafikiria muda huo huo. Huyo ni mjumbe tu hauawi hata siku moja.

SSH anachukuliwa kama Mama na ni hulka inayompa aina fulani ya udogo mbele ya wasaidizi wake tofauti na JPM aliyewavaa uso kwa uso wote waliomkera na kumkwaza katika kufanikisha mipango ya kimaendeleo.

Kawapelekea Makonda waumane wao kwa wao, huo ndio ujumbe wa Samia ndani ya CCM na ndani ya serikali kuu.
 
Ni nyakatib hizi tu za Paul Makonda ambazo waziri mkuu anapewa maelekezo hadharani na kiongozi wa chama chake
 
Nilifikiri mada imeambatana na vifungu vya sheria kumbe hisia tu.

Hili agizo lingetolewa na mtu mwingine si ajabu isingekuwa topic!

Ndiyo maana mmeletewa Makonda wanajua kila atakachoongea ni mjadala.
 
Ila PM naye ana moyo! Ingekuwa Mimi ningekuwa nikishaniuzuru siku nyingi sana. Sio kwa movie hizi
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
sasa nimeelewa kwann aliteuliwa makamo waziri mkuu
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Wameshawekana sawa ili lionekane si tatizo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapi na nani kasema kashindwa kazi? PM atakuwepo Kila Kona ya Tzn? Kwa hiyo Wananchi wakiibua shida asielekezwe au? Acha ujinga
Najaribu kutafuta mjinga ni nani nashindwa.
Yaani PM kapelekewa Dotto ambaye ana ulinzi/sauti kuliko manaibu wote hujiulizi!??
Haya PM anaagizwa agizwa tu kama mtendaji wa kitongoji bado tu hushtuki!!?
Ngoja niwaachie ulimwengu watajibu.
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Acha wavuane nguo tu maana sisi wananchi wenye njaa na maisha magumu hayatuhusu
 
Acha wavuane nguo tu maana sisi wananchi wenye njaa na maisha magumu hayatuhusu
Usiseme hivi... Nchi inaenda inavoenda kwa sababu washajua wananchi wengi hawana interest na siasa za nchi!
Hivyo viongozi wanaiba tu na kuwasababishia ugumu wa maisha
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Ndo yametokea tufanyeje Sasa ?Yesu macho na masikio!
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.
Hili silioni kama jambo geni. Nani asiyemjua Paul! Hakuanza kutoa maagizo leo. Ni Paul huyu aliyelitukana 'Bunge' , Waziri mkuu akiwemo. Nini kilifanyika? Ni impunity. Si huyu paul alikuwa anatoa maagizo kila siku wakati wa JPM, wote wakiwemo PM walikuwa kimya. Jambo zuri la Paul ni kuwa consistent na utendaji wake, habadiliki.
Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.
Kwahiyo Waziri mkuu ni sehemu ya watu waliokubali uteuzi wa Paul. Si kukubali gizani, bali walikubali wakimjua.
Hapa kuna tatizo la ''ego' . Viongozi wanaogopa nafasi zao binafsi na si heshima na hadhi za nafasi zao.
Usingeweza kumtweza Kawawa, Malecela, Salim , Warioba, Msuya kireja reja namna hiyo. Ni hawa wasakatonge
Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.
Kwanza, anapaswa alinde heshima yake halafu tutmheshimu. Mzee Warioba aliwahi kwenda kwa Nyerere na kumwambia kama abcd inafanyika mimi najiuzulu.. Tena hiyo ilikuwa siri ya serikali lakini hakujali nafasi yake, alijali heshima ya nafasi na heshima yake. Mzee Warioba yupo anadunda heshima zinamfuata!
Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Narudia tena, lazima kwanza aheshimu nafasi yake halafu sisi tutamheshimu. Juzi alikuwa na chaguo, kumkaripia Paul au kumwambia Mwenyekiti kama humkemei hadharani naachia ngazi, hakufanya anaogopa asijekatwa jina wakati wa kinyang'anyiro cha Urais.

Ukimsikiliza Paul, kuna kauli anayotumia '' anamshukuru Rais SSH kwa kubeba jina lake hadi Kamati kuu''
Hii ni kuwaambia watu uwepo wake si wa kubahatisha, yeye ni mteule wa Mwenyekiti wa CCM na Rais kama wao

Juzi kasema ni maagizo ya chama, sasa unajiuliza Waziri mkuu hakuwepo kwenye vikao vya chama!

Paul atawasumbua sana kwasababu hawana mtima, wanaogopa vyeo na wanavizia teuzi. Huko ndiko uwanja wa 'nyumbani' wa Paul.
 
Back
Top Bottom