Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Si sahihi kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani, si kila kiongozi anaweza kupewa maagizo hadharani

Anachofanya Makonda ni Kutoa ishara ya Ukubwa wa Cheo chake, na kweli mliokua hamjui cheo cha Makonda sasa mtakua mmeanza elewa bwa mkubwa kapewa Kitengo.
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Ukiona jambo hilo ndugu Pascal Mayalla kakaa kimya basi ujue kwa mujibu wa taratibu za chama, Mwenezi hajachemka🤣🤣
 

Nilisema hili na ninarudia tena, katika nchi yetu Waziri mkuu hapewi hashima anayostahili kupatiwa kutikana na mamlaka yake. Hii inatokana na wivu wa kiutawala, sina hakika sana kama marais wetu wamekuwa 'wakiwaacha' mawaziri wakuu waheshimiwe.
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Asante sana mkuu.
 
Naona unateseka tu makonda awezi kukurupuka kabla ajasema walishaonana kwa siri na mawaziri wote na kashaambiwa aongee vipi
 
Mi naona kama utovu wa nidhamu. Waziri mkuu ni kiongozi mkubwa hapaswi kuagizwa kufanya jambo fulani na katibu muenezi wa chama. Serikali ni kubwa kuliko chama. Kuna nchi rais wake anaweza kuachana na chama chake kilichomuingiza ikulu na akaanzisha chama kingine huku akiendelea na urais wake
Chama ndio kimeunda serikali na siyo serikali iliyounda chama,. serikali haiwezi kuwa kubwa kuliko chama hata siku moja.Nenda kasome katiba ujielimishe kidogo maana naona uelewa wako siyo mkubwa sana kwenye haya mambo. Huwezi kuwa Rais kama huna chama cha siasa au hujapendekezwa na chama cha siasa. Kwa hiyo chama kinachokupa ridhaa ya kugombea ni kikubwa kuliko serikali utakayo iunda wewe baada ya kuchaguliwa. Wakati wa uchaguzi chama ndicho hutafuta kura kwa wananchi kwa kunadi ilani yake ambayo ndio hutekelezwa baada ya kupewa ridhaa na wananchi kupitia sanduku la kura. Chama kinaweza iagiza serikali kufanya jambo lolote lile na kuhitaji mrejesho wa utekelezaji wake.
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.

View: https://www.instagram.com/reel/CzJfL93IbJU/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.

Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.

Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.

Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.

Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Aliyetoa maelekezo sio Makonda ni Chama.

PM akiagiza Huwa hawasemi Majaliwa kaagiza Bali Waziri Mkuu Kwa niaba ya Serikalini nk so Makonda Yuko sahihi kiitifaki.
 
Jiulize kwani kuna vikao vya ccm vimekaa vikatoa hizo kauli anazoeneza Bashite PM Albert?
Kama HAPANA basi fahamu kuwa hayo ni maagizo toka kwa alomteua!
Huyo Majaliwa... achague Moja... Apokee maagizo ayafanyie kazi au abwage manyanga!
Akikomaa watamuongezea Naibu mwingine
 
Wahenga wanasema kulikuwa na 'H' Sita
Tatu zomekufa na Tatu hazifi mpaka kiama
Haya, Huba na Huruma zimekufa
Zilizobaki tatu ni Hila, Hadaa na Husda
 
Hilo li jamaa sijui lina siri gani na mama mpaka halijafunguliwa mashitaka kama Sabaya na badala yake limeteuliwa.
WACHA LIKIGAWE CHAMA
 
Mpole kabisa pamoja na kuwa uwezekano wa dua zako kutimia ni 0p% katiba ya jmt haimpi makamu wa rais hayo meno uyawazayo, kazi kubwa ya makamu wa rais ni kukata utepe tena wa miradi midogo midogo na kukagua bei ya vyakula tandale.
 
Kwani Katibu Mkuu wa CCM yupo wapi,mpaka subordinate wake Makonda ndo ampe Prime Minister Maagizo ? Hapa kuna kitu hakijakaa sawa.
 
Back
Top Bottom