Si vibaya kuajiri akili kubwa kutoka nje!

Si vibaya kuajiri akili kubwa kutoka nje!

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Napenda tu kuwakumbusha watawala wa Tanzania kuwa mambo yanaposhinda si vibaya kutaka msaada wa kiakili kutoka nchi zilizofanya vizuri.

Nasema hivi kwa maana naona gap kubwa ya uongozi mzuri katika Wizara na sekta nyingi Tanzania. Ukichunguza vizuri utaona mapungufu hayo kwa kweli yanatokana na kutojua, ujinga na 'lack of exposure' (Sijui utaiitaje hii) ushamba?

Si haramu kuwaajiri watu kutoka nje wakaziba pengo hilo angalau kwa muda hadi hapo tutakapokuwa na weledi sisi wenyewe, badala ya kujifunza kutokana na makosa....hili huchukua muda mrefu na husabisha hasara kubwa.

Ni wazi kabisa katika elimu, fedha, ustawi wa jamii, mipango miji, biashara, ardhi, benki.....Tanzania inahitajia akili kubwa. Katika Wizara na sekta chini ya Wizara hizo mambo ni ovyo ovyo.

Nitakumbusha tu, hata nchi zilizoendelea sana kama Marekani huazima 'akili kubwa' katika sekta zake. Ukienda NASA huko kumejaa kila aina ya watu kutoka India, Misri, Urusi nk.
Sekta ya Afya Uingereza, NHS, ukiwafukuza madokta kutoka India, Sudan, Nigeria.....hii leo, sekta nzima itaanguka! Mfano wa karibu ni Rwanda.

Nani walioendeleza Rwanda hadi kuwa na satalaiti yake yenyewe (jambo ambalo viongozi tulio nao hata hawajui umuhimu wake!) na mipango miji mizuri ya kuvutia? Ni wataalamu ambao Rwanda iliwakusanya kutoka nchi mbali mbali kutoka Uganda, Kenya, DRC na hata Tanzania.

Vyuo vikuu vya Rwanda hata vinadiriki kuwaajiri Wazungu kuwa wakuu wa chuo. Sisi tumeshikilia uzalendo njaa, hata uraia pacha hatuutaki! Pum..fu kabisa.

Hebu waajirini Wanyarwanda wale wale walioweka plan za miji yao, muone. Hebu mwajiri Waziri wa elimu wa Botswana aliyestaafu uone elimu inakuwaje Tanzania?

Hebu mwajiri Waziiri wa zamani wa fedha wa Kenya aliyeufanya uchumi wa Kenya kuondoka kwenye GDP ya USD 80b mwaka 2015 wakati huo ukifukuzana na wa Tanzania GDP USD 65 b, hadi leo ambapo uchumi wa Kenya umeushinda hata ule wa Ethiopia kwa ku click GDP USD 120 b, katika kipindi cha miaka 10 tu!, Wakati ule wa Tanzania uko hapo hapo!

Tanzania haitaukaribia tena uchumi wa Kenya, kama tuna Mawaziri hawa wa akili za tozo!

Ajabu ya Tanzania: twakubali kuajiri 'akili kubwa kutoka nje' katika jambo moja tu: mpira! Ila mambo ya maana...uzalendo wetu watuzuia!
Haya si mambo ya aibu wala kukosa uzalendo: ni ujanja, kwa kusoma kwa yule aliyekuzidi!
 
Napenda tu kuwakumbusha watawala wa Tanzania kuwa mambo yanaposhinda si vibaya kutaka msaada wa kiakili kutoka nchi zilizofanya vizuri.

Nasema hivi kwa maana naona gap kubwa ya uongozi mzuri katika Wizara na sekta nyingi Tanzania. Ukichunguza vizuri utaona mapungufu hayo kwa kweli yanatokana na kutojua, ujinga na 'lack of exposure' (Sijui utaiitaje hii) ushamba?

Si haramu kuwaajiri watu kutoka nje wakaziba pengo hilo angalau kwa muda hadi hapo tutakapokuwa na weledi sisi wenyewe, badala ya kujifunza kutokana na makosa....hili huchukua muda mrefu na husabisha hasara kubwa.

Ni wazi kabisa katika elimu, fedha, ustawi wa jamii, mipango miji, biashara, ardhi, benki.....Tanzania inahitajia akili kubwa. Katika Wizara na sekta chini ya Wizara hizo mambo ni ovyo ovyo.

Nitakumbusha tu, hata nchi zilizoendelea sana kama Marekani huazima 'akili kubwa' katika sekta zake. Ukienda NASA huko kumejaa kila aina ya watu kutoka India, Misri, Urusi nk.
Sekta ya Afya Uingereza, NHS, ukiwafukuza madokta kutoka India, Sudan, Nigeria.....hii leo, sekta nzima itaanguka! Mfano wa karibu ni Rwanda.

Nani walioendeleza Rwanda hadi kuwa na satalaiti yake yenyewe (jambo ambalo viongozi tulio nao hata hawajui umuhimu wake!) na mipango miji mizuri ya kuvutia? Ni wataalamu ambao Rwanda iliwakusanya kutoka nchi mbali mbali kutoka Uganda, Kenya, DRC na hata Tanzania.

Vyuo vikuu vya Rwanda hata vinadiriki kuwaajiri Wazungu kuwa wakuu wa chuo. Sisi tumeshikilia uzalendo njaa, hata uraia pacha hatuutaki! Pum..fu kabisa.

Hebu waajirini Wanyarwanda wale wale walioweka plan za miji yao, muone. Hebu mwajiri Waziri wa elimu wa Botswana aliyestaafu uone elimu inakuwaje Tanzania?

Hebu mwajiri Waziiri wa zamani wa fedha wa Kenya aliyeufanya uchumi wa Kenya kuondoka kwenye GDP ya USD 80b mwaka 2015 wakati huo ukifukuzana na wa Tanzania GDP USD 65 b, hadi leo ambapo uchumi wa Kenya umeushinda hata ule wa Ethiopia kwa ku click GDP USD 120 b, katika kipindi cha miaka 10 tu!, Wakati ule wa Tanzania uko hapo hapo!

Tanzania haitaukaribia tena uchumi wa Kenya, kama tuna Mawaziri hawa wa akili za tozo!

Ajabu ya Tanzania: twakubali kuajiri 'akili kubwa kutoka nje' katika jambo moja tu: mpira! Ila mambo ya maana...uzalendo wetu watuzuia!
Haya si mambo ya aibu wala kukosa uzalendo: ni ujanja, kwa kusoma kwa yule aliyekupita!
Hatuna cha kujifunza Rwanda bali tuna mengi ya kuwafunza kwa sasa na tuliwafunza sana toka Kagame aingie mwaka 1994 baada ya kumuua Habyarimana. Rwanda inayotawaliwa kimabavu huku kiongozi wake akiua wakosoaji kimya kimya popote walipo na kuwekeza kwenye PR ya akina Tony Blair haina cha kutufunza

Ni upuuuzi kufananisha hivyo "vimafanikio vya Rwanda" na nchi ya Tanzania. At most linganisha Rwanda na mkoa wa Mwanza.

Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
 
Watu wenye uwezo wapo wengi tu hapa nchini.

Ila watawala wameshatengeneza circle yao ambayo kama haumo humo kamwe huwezi pata nafasi hata uwe na akili kama Isack Newton.

Hua wanasema wakwetu huyo. Kama wewe sio wakwao. Sahau.

Ndio maana mtu anaiba hapa wanamwamishia kule.
 
Hatuna cha kujifunza Rwanda bali tuna mengi ya kuwafunza kwa sasa na tuliwafunza sana toka Kagame aingie mwaka 1994 baada ya kumuua Habyarimana. Rwanda inayotawaliwa kimabavu huku kiongozi wake akiua wakosoaji kimya kimya popote walipo na kuwekeza kwenye PR ya akina Tony Blair haina cha kutufunza

Ni upuuuzi kufananisha hivyo "vimafanikio vya Rwanda" na nchi ya Tanzania. At most linganisha Rwanda na mkoa wa Mwanza.

Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
Sasa swali la msingi kwanini mwanza sio nzuri na yenye kupendeza km rwanda km zipo sawa
 
Hatuna cha kujifunza Rwanda bali tuna mengi ya kuwafunza kwa sasa na tuliwafunza sana toka Kagame aingie mwaka 1994 baada ya kumuua Habyarimana. Rwanda inayotawaliwa kimabavu huku kiongozi wake akiua wakosoaji kimya kimya popote walipo na kuwekeza kwenye PR ya akina Tony Blair haina cha kutufunza

Ni upuuuzi kufananisha hivyo "vimafanikio vya Rwanda" na nchi ya Tanzania. At most linganisha Rwanda na mkoa wa Mwanza.

Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
Chief unalopendekeza ni wazo zuri sana ila watanzania tulio wengi bado tuna mitizamo ya kijima sana! Na hili kuanzia wananchi hadi viongozi wetu

Kwa kifupi watanzania tulio wengi hatupendi mabadiliko na tunachukia pale mabadiliko yanatuchallenge kifikra

Hii inapelekea kuwa na matatizo yaleyale kila siku bila kupata suluhisho la kudumu
Tunakuwa km tumestuck vile na kukubaliana na hali jinsi ilivyo.
 
Waziri anatoka kijijini anaingia chuo KiKUU akimaliza kwa Kua Alipata Ufaulu mkubwa anapelekwa serikalini anagombea ubunge na anakua waziri

Hakuna exposure at all , waziri kama huyo ni Mzigo Hawezi kuleta ubunifu na akili za Darasani sio akili za Maisha
 
Sasa swali la msingi kwanini mwanza sio nzuri na yenye kupendeza km rwanda km zipo sawa
Ubaya wa Mwanza uko wapi? Au unalinganisha kale kapicha ka mtaa mmoja wa Kigali wenye maghorofa na barabara ukadhani Rwanda yote iko vile?
 
Waziri anatoka kijijini anaingia chuo KiKUU akimaliza kwa Kua Alipata Ufaulu mkubwa anapelekwa serikalini anagombea ubunge na anakua waziri

Hakuna exposure at all , waziri kama huyo ni Mzigo Hawezi kuleta ubunifu na akili za Darasani sio akili za Maisha

Nakuunga mkono, ni hatari sana kuwapa watu wasio na exposure madaraka.
 
Hakuna mahala duniani somasoma waliwahi kuleta mabadiriko na maendeleo maana ni non-risk taker, waoga, too much theory nk.

Wahuni ndio chachu ya maendeleo duniani asikudanganye mtu.

Kama hujawahi kuwa mtundu utotoni, ujanani na mhuni uzeeni tambua tu huwezi leta mabadiriko wala impact kwenye jamii.
 
Si kwamba Taifa hili la watu milioni 60 halina vichwa wa kuendesha Taifa na likasogea la hasha. Tatzio ni SERA na mpango mkakati ambao hata ukiamua kuwaajiri hao uliowataja bado hawataweza kuperform ilivyo kwa kuwa bado watahitajika wafanye yale matakwa ya wakubwa.

Kwa sisi Watanzania system ina wenyewe na inahitaji ujuane na mtu ili upate nafasi, vivyo hivyo ili uende sawa sawa na system inabidi uwe mwabudu wa maelekezo ya mtu mmoja jambo hili ndilo linalofanya Watanzania wengi ambao wanaonekana wana akili na uwezo kukimbilia nchi za wenzetu.Tuanze kubadilisha Sera kwanza kisha mengine yatafuata.

Kingine ambacho sikubaliani nawe katika kuwaajiri foreigners katika sekta nyeti ni kutokana na usalama wa Taifa letu pendwa la Jamuhuri. Labda tukubali kwanza wawe raia wa nchi hii ndipo tuwape nafasi au tuwapeleke hawa waliopo kwenda kujifunza na kujinoa zaidi pamoja na kupata exposure.

Suala la Uraia Pacha pia sikubaliani nalo lakini kama Taifa tunaweza kuanzisha mfumo wa hadhi maalum kwa waliowahi kuwa raia wa Tanzania.
 
Hatuna cha kujifunza Rwanda bali tuna mengi ya kuwafunza kwa sasa na tuliwafunza sana toka Kagame aingie mwaka 1994 baada ya kumuua Habyarimana. Rwanda inayotawaliwa kimabavu huku kiongozi wake akiua wakosoaji kimya kimya popote walipo na kuwekeza kwenye PR ya akina Tony Blair haina cha kutufunza

Ni upuuuzi kufananisha hivyo "vimafanikio vya Rwanda" na nchi ya Tanzania. At most linganisha Rwanda na mkoa wa Mwanza.

Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
Hizi ndizo akili za kipumbafu..leo hii rwanda wana mipango miji safi wewe tz una nini katika hili..leo hii rwanda wana assemble magari na simu..hadi waziri wako aliomba kuanza kuagiza magari toka huko..wewe tz njaa una nini..jifunze ku appreciate..nw rwanda currency iko juu ya tz currency halafu unajisifia ujinga.

#MaendeleoHayanaChama
 
tunaweza kuwalaumu hawa ndugu zetu kiukweli tukaona wanafanya makusudi kumbe tatizo akili ndogo kichwani

Tupunguze pia matumizi ya ugali na wali kupita kiasi.
Unashauri tule nini?

#MaendeleoHayanaChama
 
Si kwamba Taifa hili la watu milioni 60 halina vichwa wa kuendesha Taifa na likasogea la hasha. Tatzio ni SERA na mpango mkakati ambao hata ukiamua kuwaajiri hao uliowataja bado hawataweza kuperform ilivyo kwa kuwa bado watahitajika wafanye yale matakwa ya wakubwa.

Kwa sisi Watanzania system ina wenyewe na inahitaji ujuane na mtu ili upate nafasi, vivyo hivyo ili uende sawa sawa na system inabidi uwe mwabudu wa maelekezo ya mtu mmoja jambo hili ndilo linalofanya Watanzania wengi ambao wanaonekana wana akili na uwezo kukimbilia nchi za wenzetu.Tuanze kubadilisha Sera kwanza kisha mengine yatafuata.

Kingine ambacho sikubaliani nawe katika kuwaajiri foreigners katika sekta nyeti ni kutokana na usalama wa Taifa letu pendwa la Jamuhuri. Labda tukubali kwanza wawe raia wa nchi hii ndipo tuwape nafasi au tuwapeleke hawa waliopo kwenda kujifunza na kujinoa zaidi pamoja na kupata exposure.

Suala la Uraia Pacha pia sikubaliani nalo lakini kama Taifa tunaweza kuanzisha mfumo wa hadhi maalum kwa waliowahi kuwa raia wa Tanzania.
Haya ndiyo niyasemayo ndugu. Ukiwa Tanzania bila kutoka ndio unakuwa na dhana hizi. Nani kakuambia kuwa mtu akiwa raia hawezi kuhatarisha usalama wa taifa? On the contrary, wengi waliotoa siri za nchi si wengine bali raia wenyewe.
 
Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
Kwa akili hizi utaendelea kuwa na changamoto ya bando! Maskini, hujui kuwa watu wengi duniani hawana taabu tena na mambo hayo ya bando, wanatumia wifi au high speed broadband! Nenda Kenya, 70% ya wananchi wana wifi ndani. Tanzania sidhani hata 10% wanafika. Kwao internet ni bando tu, wifi iko maofisini pekee! Si haya ndiyo niyasemayo hapa?
 
Ubaya wa Mwanza uko wapi? Au unalinganisha kale kapicha ka mtaa mmoja wa Kigali wenye maghorofa na barabara ukadhani Rwanda yote iko vile?
Hujafika rwanda sikulaum ...ila rwanda ipo very organized licha ya kuwa na milima mingi. Kingine ni usafi wenzetu wamejitahidi sana kutunza mazingira.
 
Back
Top Bottom