Si vibaya kuajiri akili kubwa kutoka nje!

Si vibaya kuajiri akili kubwa kutoka nje!

Napenda tu kuwakumbusha watawala wa Tanzania kuwa mambo yanaposhinda si vibaya kutaka msaada wa kiakili kutoka nchi zilizofanya vizuri.

Nasema hivi kwa maana naona gap kubwa ya uongozi mzuri katika Wizara na sekta nyingi Tanzania. Ukichunguza vizuri utaona mapungufu hayo kwa kweli yanatokana na kutojua, ujinga na 'lack of exposure' (Sijui utaiitaje hii) ushamba?

Si haramu kuwaajiri watu kutoka nje wakaziba pengo hilo angalau kwa muda hadi hapo tutakapokuwa na weledi sisi wenyewe, badala ya kujifunza kutokana na makosa....hili huchukua muda mrefu na husabisha hasara kubwa.

Ni wazi kabisa katika elimu, fedha, ustawi wa jamii, mipango miji, biashara, ardhi, benki.....Tanzania inahitajia akili kubwa. Katika Wizara na sekta chini ya Wizara hizo mambo ni ovyo ovyo.

Nitakumbusha tu, hata nchi zilizoendelea sana kama Marekani huazima 'akili kubwa' katika sekta zake. Ukienda NASA huko kumejaa kila aina ya watu kutoka India, Misri, Urusi nk.
Sekta ya Afya Uingereza, NHS, ukiwafukuza madokta kutoka India, Sudan, Nigeria.....hii leo, sekta nzima itaanguka! Mfano wa karibu ni Rwanda.

Nani walioendeleza Rwanda hadi kuwa na satalaiti yake yenyewe (jambo ambalo viongozi tulio nao hata hawajui umuhimu wake!) na mipango miji mizuri ya kuvutia? Ni wataalamu ambao Rwanda iliwakusanya kutoka nchi mbali mbali kutoka Uganda, Kenya, DRC na hata Tanzania.

Vyuo vikuu vya Rwanda hata vinadiriki kuwaajiri Wazungu kuwa wakuu wa chuo. Sisi tumeshikilia uzalendo njaa, hata uraia pacha hatuutaki! Pum..fu kabisa.

Hebu waajirini Wanyarwanda wale wale walioweka plan za miji yao, muone. Hebu mwajiri Waziri wa elimu wa Botswana aliyestaafu uone elimu inakuwaje Tanzania?

Hebu mwajiri Waziiri wa zamani wa fedha wa Kenya aliyeufanya uchumi wa Kenya kuondoka kwenye GDP ya USD 80b mwaka 2015 wakati huo ukifukuzana na wa Tanzania GDP USD 65 b, hadi leo ambapo uchumi wa Kenya umeushinda hata ule wa Ethiopia kwa ku click GDP USD 120 b, katika kipindi cha miaka 10 tu!, Wakati ule wa Tanzania uko hapo hapo!

Tanzania haitaukaribia tena uchumi wa Kenya, kama tuna Mawaziri hawa wa akili za tozo!

Ajabu ya Tanzania: twakubali kuajiri 'akili kubwa kutoka nje' katika jambo moja tu: mpira! Ila mambo ya maana...uzalendo wetu watuzuia!
Haya si mambo ya aibu wala kukosa uzalendo: ni ujanja, kwa kusoma kwa yule aliyekupita!
Uwa nikiiangali serikali yetu,kiukwel nina akili kubwa kuliko wengi wao... ukweli usiopingika asilimia kubwa ya Watanzania bado ni wajinga au uwezo wa kufikiri ni mdogo ila wanatembelea bahati na uwezo wa waliowatangulia
 
Nakubali sana hoja hii. Lakini kuleta 'akili kubwa' pia kwaweza kuchangia mabadiliko katika sekta nyingine, hata uongozi. Kinachotakikana ni 'critical mass' ya hizo 'akili kubwa' ndipo wananchi waone kuna haja ya kubadilisha.
Si lazima 'critical mass'. Ni zile sehemu muhimu kwa uchumi na maendeleo. Tena kwa muda mfupi mpaka wenyewe tuchukue. Vietnam ilifanya hivyo na sasa uchumi wa Vietnam ni mara tatu ya wa Tanzania at USD 261 billion, wakati ule wa Tanzania ni USD 61 Billion!
Wajua mwaka 1972 uchumi wa Tanzania uikuwa USD 5 billion na ule wa Vietnam USD 3.5 billion?
Tanzania iliwahi kuipa Vietnam ruzuku ya bure ya dola 1 million mwaka 1975!
 
Kuna maeneo mengine kuajiri toka soko la ajira la kimataifa si kukosa uzalendo. Mbona Kuna wakati Emirates( airline) waliajiri Muingreza kama CEO. Nissan ya Japan ilikuwa na CEO Mlebanon. Makocha wa soka n.k. Air Tz kmf. ikipata CEO mahiri huenda ikapona.
 
Kuna maeneo mengine kuajiri toka soko la ajira la kimataifa si kukosa uzalendo. Mbona Kuna wakati Emirates( airline) waliajiri Muingreza kama CEO. Nissan ya Japan ilikuwa na CEO Mlebanon. Makocha wa soka n.k. Air Tz kmf. ikipata CEO mahiri huenda ikapona.
Hapo umesema. Air Tanzaia inataka CEO aliyefanya kazi hiyo akaleta ufanisi katika shirika ambalo lilikuwa linakufa. Kwa lugha ya Kiingereza mtu mwenye track record. Alas! Tanzania sharti kuu ni uwe mkereketwa wa CCM!
 
Umewakilisha nilichokuwa nakiwaza japo mimi nilifikiri ata baadhi ya position kubwa za kiserikali sema ndio vile haiwezekani..
 
Haya ndiyo niyasemayo ndugu. Ukiwa Tanzania bila kutoka ndio unakuwa na dhana hizi. Nani kakuambia kuwa mtu akiwa raia hawezi kuhatarisha usalama wa taifa? On the contrary, wengi waliotoa siri za nchi si wengine bali raia wenyewe.
Sio waliotoa siri za nchi hii. Sema waliouza utu wa nchi hii ni watanzania wenyewe. Matanzania karibu yote ninayoyaona mtaani na yaliyomo serikalini na kwenye siasa ni matanzania mepesi sana kununulika. Wawe wasomi wasiwe wasomi yaani ni taabu tupu.

Though sidhani kama solution ya kupiga hatua za kimaendeleo ni lazima kuazima kutoka nje. Miaka mitano ya utawala wa Magufuli ilituonesha kwamba watu hao hao mafala wakipata uongozi bora kutoka juu wanaweza kufanya kitu. Solution ni uongozi bora kutoka juu.
 
Wakuu nimesoma aya kwa aya. Mstari kwa mstari. Point ziko njema. Nimezifupisha nazo ni
*Mifumo mibovu
*viongozi kukosa exposure
*Kujuana kiitikadi kisiasa ili kupewa uongozi
*Wabongo tuna akili finyu
*Madhara ya ujamaa (huu ulifeli na haukutakiwa uwepo)
*Elimu mbovu


Nyingine nitazipandisha kadri ya muda
 
Kwa hiyo hiyo broadband wanaoewa bure? Mbona nyie watu mna mawazo so mediocre? Tanzania iko kwenye top 10 big economies in GDP terms in Africa ikiwa ni pamoja na Nigeria, SA, Egypt, Algeria, Morocco, Kenya, Ethiopia, Ghana na Angola. Sasa hawa Rwanda mnataka watufundishe nini sisi? Labda Udikteta, wizi w madini ya DRC na kuua wapinzani
FB_IMG_1658076356227.jpg
 
January 2025

Dr. Kaberuka recounts his regrets in joining a Western school of governance after leaving the AfDB



View: https://m.youtube.com/watch?v=MdFP8Ichj-8
Dkt. Kaberuka ni mwanataaluma tajwa katika masuala ya benki, biashara ya kimataifa na maendeleo na huduma ya serikali . Raia wa Rwanda, alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango ya Uchumi wa nchi hiyo kati ya 1997 na 2005. Dk. Kaberuka alisoma katika shule na vyuo vikuu vya Tanzania na Uingereza
 
17 January 2025
Prof. Rwigamba Balinda : A lifelong commitment to shaping Africa's future leaders through education

View: https://m.youtube.com/watch?v=j74C8KliK6Q
Profesa Rwigamba Bal8inda alizaliwa Oktoba 1948 huko Masisi, zamani Zaire (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo), mapito ya Prof. Balinda yanaonesha ufafanuzi wa kweli wa ustahimilivu, na hadithi yake inaonyesha kwamba ikiwa unafuatilia jambo ambalo una shauku nalo - hakuna shaka unaweza kufanikiwa. Haijalishi ni changamoto gani unakutana nazo njiani.

Baba yake alihama kutoka Rwanda hadi Zaire mwaka 1935 kutafuta ardhi kwa ajili ya kundi lake kubwa la ng'ombe - na ndivyo ambayo walivyoishi kwa shughuli za ufugaji huko Masisi, eneo katika Mkoa wa sasa wa jimbo la Kivu Kaskazini Congo DR, na hatimaye kuendelea na elimu yake huko.

Anaposimulia hadithi yake, Prof. Balinda anazungumza kana kwamba ni jana. Katika umri wake, labda mtu angefikiria kuwa hajali sana maelezo, lakini msomi huyo mwenye uzoefu ana akili kubwa na kumbukumbu kali, akikumbuka kila tarehe, mwezi, na mwaka ambao alipata kufanya hatua za mapito ya kimaisha akikua katika nyakati tofauti.

Source: The New Times Rwanda
 
Hatuna cha kujifunza Rwanda bali tuna mengi ya kuwafunza kwa sasa na tuliwafunza sana toka Kagame aingie mwaka 1994 baada ya kumuua Habyarimana. Rwanda inayotawaliwa kimabavu huku kiongozi wake akiua wakosoaji kimya kimya popote walipo na kuwekeza kwenye PR ya akina Tony Blair haina cha kutufunza

Ni upuuuzi kufananisha hivyo "vimafanikio vya Rwanda" na nchi ya Tanzania. At most linganisha Rwanda na mkoa wa Mwanza.

Usitumalizie Bando kwa hoja kama hizi
Na karibia yote jamaa kasema uongo, eti GDP ya Kenya inaizidi ya Ethiopia,
 
Nakuunga mkono, ni hatari sana kuwapa watu wasio na exposure madaraka.
Ndio maana wakiteuana tunaona kama vile wametoka mbinguni wanaleta miujiza wakati wapo miaka yote walewale recycling washibe upya wakishapungukiwa kiuchumi!
 
CEO wa Tanzania Railways Corporation ndugu Masanja Kungu Kadogosa anaburuzwa na viongozi wote wa chama dola tawala wa ngazi zote.

Kiasi mkurugenzi mkuu Shirika la Reli Tanzania hawezi kutumia muda mwingi katika kusimamia utendaji wa shirika, rasilimali watu, rolling stock (mabehewa) / vichwa vya treni, ufundi, reli ya mkoloni MGR na miradi yake ya SGR. Muda mwingi anautumia katika matukio ya kisiasa.

Reli ya Mkoloni MGR Kigoma hadi Dar es Salaam haipewi uzito unaostahili

View: https://m.youtube.com/watch?v=_PkRDvMWgzg

CCM SIMIYU WATOA TAMKO ZITO - NI KUHUSU RAIS SAMIA na DK NCHIMBI - MAMIA WAFURIKA

View: https://m.youtube.com/watch?v=RWjm_z1kQbM
...Wanachama na viongozi wa chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Simiyu, serikali na shirika la Reli leo wamejitokeza kwa wingi katika mkutano wa kutoa tamko la kuunga mkono maamuzi ya mkutano mkuu wa dharura wa kumchagua Rais Dkt. Samia kuwa mgombea Urais katika uchaguzi mkuu mwaka huu...

Masanja Kungu Kadogosa. Chief Executive Officer. Tanzania Railways Corporation....

1737852176840.jpeg

Picha maktaba : Masanja Kungu Kadogosa mkurugenzi mkuu wa Shirika la Reli Tanzania - TRC
 
Muscat, Oman
Taarifa za kundi la makampuni tanzu ya Mohammed Al Barwani Group 16 January 2025


View: https://m.youtube.com/watch?v=yt_baHZndAM
kuanza kuchimba madini ya Shaba, kitalu kipya cha petrol na gas , hoteli mpya, jengo jipya la kistratejia ... kifaa kipya cha operesheni ya uchimbaji mafuta, Gulf Drilling, gesi LNG ...
Source : MBG Family

Mohammed Al Barwani, founder of the Oman-based diversified group MB Holding Company, discusses his group's first global investments in China, Indonesia and Hungary, and how the group learned from these early opportunistic investments...


View: https://m.youtube.com/watch?v=zmhwydIIh_Y



Mohammed Al Barwani stori za alipokulia na ndoto zake tangu akiwa kisiwani Zanzibar na mwendelezo wa umuhimu wa kuthamini kazi za mikono kuboreshwa zaidi na zaidi na uwekezaji katika rasilimali hii muhimu yaani ujuzi endelevu kwa matokeo makubwa kutokea ikiwemo bidhaa na huduma bora ...anafafanua CEO Dr. Mohammed Al Barwani


View: https://m.youtube.com/watch?v=_hEy9ALkaRI

Discover insights into the exclusive interview with Dr Barwani and Paris Baloumis on Oceanco by Dr Julia Riedmeier for the Monaco Yachting Report (MYR) of Robb Report Monaco & Côte d’Azur.

View: https://m.youtube.com/watch?v=yZVlCGHAMV0
Special thanks to Dr. Mohammed Al Barwani Paris Baloumis, Usama Barwani Dr Julia Riedmeier, Robb Report Monaco & Côte d’AzurMB Holdings
 
Naunga mkono hoja. Ukienda Marekani utabaini, experts wengi are not of US origin. Huyu katoka Siberia, yule India, huyu Brazil, yule Nigeria etc. Wako makini sana kwenye talent acquisition. Tunaweza kufanya hivyo kwa manufaa mapana ya nchi yetu. Watu wetu wengi sio weledi na ndio maana hatupati matokeo mazuri sana ukilinganisha na vyanzo tulivyonavyo. Pia tuachane na siasa za hovyo.​
 
Back
Top Bottom